Kahaba Ajitamba Kula Uroda na Beckham

Wednesday, September 29, 2010 / Posted by ishak /


Kahaba Irma Nici ameendelea kujitamba kuwa alikula uroda na mcheza soka maarufu wa Uingereza, David Beckham ingawa Beckham anajiandaa kufungua kesi ya madai ya fidia kiasi cha dola milioni 16.
Pamoja na kwamba wanasheria wa mcheza soka maarufu wa Uingereza, David Beckham anayesakata kabumbu nchini Marekani wako kwenye jitihada za kufungua kesi mahakamani kumdai fidia ya dola milioni 16, kahaba anayedai kutembea na Beckham ameibuka na kutamba ana ushahidi wa kuthibitisha madai yake.

Kahaba Irma Nici mwenye asili ya Bosnia amedai kuwa anaweza kuithibitishia mahakama kuwa alilala na nyota huyo wa soka mjini London na mjini New York mnamo mwaka 2007.

Nici amedai kuwa Beckham ana alama za kipekee kwenye sehemu zake nyeti hivyo ajiandae kuvua suruali yake mahakamani ili kuzithibitisha alama hizo.

Nici mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akiwakwepa wanasheria wa Beckham na amekuwa akijificha kwenye hoteli mjini New York.

Beckham mwenye umri wa miaka 35 anamshtaki Nici kutokana na habari iliyotoka kwenye jarida moja la Marekani kuwa Beckham alinunua penzi la kahaba Nici.

Nici aliliambia jarida hilo kuwa alishea kitanda kimoja na Beckham wakati Beckham alipofanya mapenzi yaliyowahusisha wanawake wawili kwa mpigo. Mwanamke wa pili aliyezungumziwa katika habari hiyo bado hajajulikana.

Beckham anamshtaki Nici na jarida hilo kwa kuandika habari za kumpakazia kuwa aliisaliti ndoa yake na Victoria Beckham, 36,

Beckham pia anamshtaki Nici na jarida hilo kwa habari ambayo imemfanya Beckham aonekane aliyatia maisha ya mkewe hatarini kwa kutembea na kahaba.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment