Mwanaume Anayemchezea Simba Sharubu

Friday, September 03, 2010 / Posted by ishak /


Wakati watu wengi duniani hufuga mbwa na paka kwenye majumba yao, jamaa huyu wa nchini Iran yeye ameamua kufanya kitu cha hatari zaidi kwa kumfuga simba na kutembea nae mtaani.
Video ya mwanaume huyo akimuogesha simba kwa kutumia bomba la maji imekuwa maarufu kwenye mitandao mbalimbali duniani.

Katika VIDEO hiyo mwanaume huyo anaonekana akimshikilia simba pembeni ya barabara moja mjini Tehran na kumuogesha kama ambavyo watu huwaogesha mbwa wao.

Mamia ya watu wanaonekana wakiwa wamesimama pembeni wakimuangalia na wengine wakimpiga picha mwanaume huyo akimuogesha simba wake.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment