Kaka Yake Obama Aoa Mwanafunzi Aliyemtorosha Kwao

Sunday, October 17, 2010 / Posted by ishak /


Kaka wa kufikia wa rais wa Marekani, Barack Obama anayeishi nchini Kenya, Malik Obama mwenye umri wa miaka 52 ameongeza mke wa tatu ambaye ni mwanafunzi wa sekondari mwenye umri wa miaka 19 aliyeacha shule na kukimbia kwao.
Kaka wa kufikia wa rais wa Marekani, Barack Obama anayeishi nchini Kenya, Malik Obama ambaye ana wake wawili ameongeza mke wa tatu ambaye ni mwanafunzi wa sekondari aliyekimbia masomo yake.

Mama wa msichana huyo mwenye umri wa miaka 52, alielezea hasira zake baada ya binti yake kuacha masomo ili aolewe na Malik ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 52.

Akiongea na televisheni ya NTV ya Kenya, mama wa msichana huyo anayeitwa Mary Aoko Ouma alisema kuwa binti yake awali alijaribu kufunga ndoa na Malik miaka miwili iliyopita lakini hakumruhusu.

Akiongea na televisheni ya NTV bila ya kujua kuwa anarekodiwa, Malik alithibitisha kufunga ndoa na msichana huyo ingawa hakusema ni lini harusi yao ilifanyika.

Sheria za Kenya zinaruhusu mtu kuoa mke zaidi ya mmoja iwapo vigezo vya kidini au kitamaduni vitatumika.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment