Achaniwa nguo na wapiga debe

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MSICHANA mmoja jina lake halikuweza kupatikana maramoja alijikuta yupo kwenye wakati mgumu baada ya kuchaniwa nguo yake aliyovaa na wahuni na kumuacha na aibu kedekede na akiwa hana la kufanya kwa wakati huo.
Tukio hilo la aibu lilitokea jana majira ya saa 2 usiku, maeneo ya Magomeni Kagera wakati msichana huyo akiwa kituoni hapo akisubiri usafiri.

Wahuni hao walianza kumshambulia kwea maneno dada huyo na msichana huyo kuwajibu jeuri na hivyo wahuni hao waliamua kumchania nguo yake ya isiyo na heshima aliyoivaa.

Msichana huyo alivaa nguo fupi kupita kiasi, alivaa blauzi tu na kuigeuza gauni hivyo kupelekea maungo yake ya mwili kuonekana ambapo wahuni hao waliamua kumfanyia uhuni kumchania ng uo hiyo ili atembee kama alivyozaliwa kabisa.

Wahuni hao walimshika dada huyo na kumchania gauni hilo na kupiga kelele na hakuna hata msamaria mwema mmoja aliyeweza kumsaidia wka wakati huo kwa kuwa hakuna mtu aliyependezwa na uvaaaji wake huo.

Wahuni hao ambao walikuwa zaidi ya wawili walishirikiana kwa pamoja kumshikisha adabu dada huyo na kumuacha akilia kituoni hapo na nguo yake kuichana.

“Tumeanza na wewe leo, na wengine watafuata tunataka mpate adabu si mteembee uchi tu” walisikika wakaka hao

source nifahamishe

Wengine watano wauawa Mara

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

WATU WENGINE watano wameuwa na wengine zaidi ya kumi kujeruhiwa usiku wa kuamkia leo huko Tarime Mkoani Mara.
Watu hao wameuawa usiku wa kuamkia leo kwa kukatwakatwa na mapanga na kupelekea vifo vyao wakati wakiwa katika kusherehekea harusi.

Kamanda wa Polisi Mara, Bw. Constantine amesema kuwa watu hao walikuwa katika harusi kwa mzee Mwita Burure na mauti hayo yaliwakuata hapo.

Amesema kuwa walizuka watu ambao hawakufahamika mara moja waliwavamia katika harusi hiyo na kuua watu na kujeruhi wengine zaidi ya kumi.

Amesema maiti hizo zimehifadhiwa na majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Mkoa kwa matibabu zaidi.

Amsema ucbhunguzi zaidi juu ya tukio hilo linafanyika na kuwakamata waliohusika na tukio hilo la kinyama.

Tukio hili ni la tatu katika wiki mbili hizi mfululizo ambapo inadaiwa ni visasi vinavyolipizwa katika koo mkoani humo kwa kuli[izana kutokana na mauaji ya kinyama yaliyotokea mwezi ulipita kwa kuuawa watu 17 wa familia moja.


source nifahamishe

Kondomu Ndogo Kwaajili ya Watoto Zaingia Madukani

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kampuni kubwa ya kutengeneza kondomu ya Uswizi imetengeneza kondomu ndogo sana kwaajili ya watoto kuanzia umri wa miaka 12 kutokana na kile kinachosemwa kuwa watoto wa siku hizi wanaanza kufanya ngono mapema.
Kondomu hizo zilizopewa jina la "Hotshot" ni maalumu kwa vijana wa kiume wenye umri mdogo kuanzia umri wa miaka 12 hadi miaka 14.

Kondomu hizo zilitengenezwa kufuatia hatua ya makundi ya uzazi wa mpango kusema kuwa vijana wenye umri mdogo hawapati kinga inayotakikana wakati wa kujamiiana.

Ilidaiwa kuwa vijana wa siku hizi wanaanza ngono mapema na hawatumii kinga na wala hawajui jinsi ya kujikinga na magonjwa yanayotokana na ufanyaji wa ngono zisizo salama.

Kondomu hizo zimeingia madukani nchini Uswizi na kuzua maoni tofauti toka kwa wazazi nchini Uswizi.

Taarifa ya utafiti uliofanyika kabla ya kutengenezwa kwa kondomu hizo ilionyesha kuhitajika kwa elimu ya mapema kwa vijana jinsi ya kujikinga na magonjwa ya zinaa pamoja na mimba zisizohitajika.

Msemaji wa kampuni ya Lamprecht AG iliyotengeneza kondomu hizo, alisema kuwa watakapoanza kuuza kondomu hizo nje ya nchi, Uingereza itapewa nafasi kubwa kutokana na idadi kubwa ya mimba za wasichana wenye umri mdogo.

Katika nchi za ulaya Uingereza inaoongoza kwa idadi kubwa ya wasichana wanaopata ujauzito kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.

source nifahamishe

Rihanna Amwaga Radhi Kwenye Bethidei Yake

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Nyota wa muziki wa Marekani Rihanna alisherehekea kutimiza miaka 22 kwa shoo toka kwa mwanamke mcheza ngono ambaye ni mfupi kuliko wanawake wote wanaoshiriki kwenye sinema za ngono.
Rihanna alisherehekea kutimiza miaka 22 kwa sherehe ya "Suprise" iliyoandaliwa na mpenzi wake nyota wa mchezo wa baseball, Matt Kemp.

Katika sherehe hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi mmoja mjini Phoenix, Arizona, shoo maalumu ya dansi la kupagawisha watu ilitolewa na mcheza video za ngono mfupi kuliko wote duniani "Midget" mwenye urefu wa mita 1.1 ambaye ana umri wa miaka 29.

Katika sherehe hiyo Rihanna akiwa amevalia kivazi cha kudatisha alinyanyuka na kujitosa ukumbini na kupagawisha watu kwa mauno yake.

Keki ya Bethidei ya Rihanna ilikuwa katika umbile la maboksi ya viatu katika kukumbushia jinsi Rihanna anavyopenda kununua na kuvaa viatu vya wanamitindo mbali mbali.

source nifahamishe

Madhara ya Mabomu ya Marekani, Watoto wa Ajabu Wazaliwa Iraq

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Madhara ya mabomu ya Marekani nchini Iraq yanajidhirisha kwa idadi kubwa ya watoto wenye vilema na maumbile ya ajabu ajabu kama vile watoto wenye vichwa vitatu kuzaliwa nchini Iraq na kuwafanya maafisa wa Iraq wawashauri wanawake wafunge kizazi.
Marekani inahisiwa kuwa ilitumia mabomu ya kikemikali katika mashambulizi yake ya mabomu nchini Iraq mwaka 2004, hii inatokana na idadi kubwa sana ya watoto wanaozaliwa wakiwa na maumbile ya ajabu ajabu.

Katika mji wa Fallujah ambapo ndipo mabomu mengi ya Marekani yalidondoshwa kuung'oa upinzani wa majeshi ya Saddam, idadi kubwa sana ya watoto wenye matatizo mbali mbali wamekuwa wakizaliwa kiasi cha kuwafanya madaktari wawashauri wanawake wa Fallujah wasizae.

Baadhi ya watoto wamekuwa wakizaliwa wakiwa na matatizo ya akili, wengine matatizo ya moyo huku wengine wakiwa na maumbile yasiyo ya kawaida.

Mwandishi wa BBC, John Simpson, aliyetoa ripoti yake toka Fallujah alikiri kushuhudia idadi kubwa ya watoto wenye maumbile ya ajabu.

Mmoja wa watoto hao alikuwa na vichwa vitatu wakati mwingine alikuwa na jicho moja huku watoto wengi wakiwa na maumbile ya kutisha zaidi.

Idadi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na matatizo ya moyo, ubongo au kupooza upande mmoja ni wengi sana kiasi cha kwamba madaktari wanasema kuwa kila siku watoto watatu wanazaliwa mjini Fallujah wakiwa na kasoro kwenye maumbile yao.

Maafisa wa Iraq wanawashauri wanawake wa Fallujah kuziacha ndoto zao za kuwa na watoto kwani watoto watakaozaliwa watakuwa na maumbile ya ajabu.

Majeshi ya Marekani yaliumiminia mabomu makubwa mji wa Fallujah kiasi cha kwamba nusu ya nyumba zote za Fallujah na misikiti ilibomolewa.

Marekani ilikiri kutumia mabomu hatari ya phosphorus ambayo yamepigwa marufuku duniani kutumika kwenye vita kutokana na uharibifu mkubwa unaotokana na mabomu hayo.

Majeshi ya Marekani yalianza mashambulizi yake mjini Fallujah kuanzia novemba 7 mwaka 2004 na baada ya siku 9 walitangaza kuuteka mji huo.

Wanajeshi 51 wa Marekani walifariki kwenye mashambulizi hayo wakati wanamgambo wa Iraq 1,400 waliuliwa kwenye mashambulizi hayo.

source nifahamishe

Rubani Mwenye Vyeti Feki Aendesha Ndege Kwa Miaka 13

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Maafisa wa Uholanzi wamemkamata rubani feki raia wa Sweden ambaye kwa kutumia vyeti feki vya urubani amekuwa akiendesha ndege za abiria kwa miaka 13 bila kugundulika.
Rubani huyo mwenye umri wa miaka 41 alitiwa mbaroni kwenye uwanja wa ndege wa Schiphol mjini Amsterdam akijiandaa kuirusha ndege ya abiria 101 toka Uholanzi kuelekea Uturuki.

Rubani huyo mwenye makazi yake mjini Milan nchini Italia kwa miaka 13 alitumia vyeti feki na kufanikiwa kuendesha ndege za abiria za mashirika ya ndege ya Uingereza, Italia na Ubelgiji.

Kufuatia taarifa waliyotonywa na maafisa wa Sweden, maafisa wa Uholanzi walimnyanyua rubani huyo toka kwenye kiti cha rubani wakati akijiandaa kuanza safari ya kuelekea Uturuki akiwa na abiria 101 kwenye ndege aina ya Boeing 737.

Taarifa zilisema kuwa rubani huyo aliwahi kuwa na leseni ya kuendesha ndege ndogo ambayo pia ilikuwa imeisha muda wake na alikuwa haruhusiwi kuendesha ndege kubwa.

Wakati anakamatwa rubani huyo ambaye jina lake liliwekwa kapuni alikuwa akiendesha ndege ya shirika la Uturuki la Corendon Airlines.

Rubani huyo amewekwa mahabusu mjini Amsterdam akisubiria kufikishwa mahakamani kwa makosa ya kufoji vyeti na kuendesha ndege bila leseni.

source nifahamishe

Mugabe Kugombea Urais Kwa Mara Nyingine

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 86 amesema yuko tayari kugombea urais kwa mara nyingine kuliongoza taifa la Zimbabwe.
Akiongea na waandishi wa habari mjini Harare, rais Robert Mugabe ambaye anaendelea kuiongoza Zimbabwe kwa miaka 30 sasa, alisema kuwa yuko tayari kugombea tena urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika miaka miwili ijayo.

Mugabe alisema kuwa iwapo chama chake cha ZANU-PF kitampitisha kugombea urais basi atasimama kwa mara nyingine kugombea urais.

Mugabe ambaye alianza kuitawala Zimbabwe tangia ilipopewa uhuru wake kutoka kwa Waingereza mwaka 1980, alishinda uchaguzi wa urais uliopita ingawa kambi ya upinzani iligoma kukubali matokeo ya uchaguzi ikisema kuwa hila zilifanyika.

Hali hiyo ilisababisha mtafaruku nchini Zimbabwe ambapo uchumi wake uliyumba kutokana na vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa na mataifa ya magharibi.

Pesa ya Zimbabwe ilipoteza thamani yake na kuifanya Zimbabwe izitose pesa zake na kuanza kutumia dola za kimarekani na Rand za Afrika Kusini kama mbadala wa pesa zake.

source nifahamishe

Kukopa Harusi Kulipa Matanga

Thursday, March 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini China ambaye alikuwa akisumbuliwa na madeni mengi sana yaliyotokana na tabia yake ya kupenda kucheza kamari amejiua mwenyewe kwa kujilipua kwa bomu ndani ya basi lililokuwa limejaa abiria.
Kwa mujibu wa shirika la habari la China, Xinhua mwanaume huyo alijilipua mwenyewe ili kuepukana na madeni mengi anayodaiwa ambayo alikuwa hana uwezo wa kuyalipa.

Yang Yongshou, 42, ambaye zamani alikuwa muuza madawa ya kulevya kabla ya kuangukia kwenye uchezaji wa kamari, alijilipua kwa bomu aliloliweka chini ya kiti chake kwenye basi la abiria lililokuwa likifanya safari zake katika jimbo la Yunnan lililopo karibu na mpaka wa Vietnam.

"Yang alikuwa hana uwezo wa kulipa yuan 100,000 (Tsh. Milioni 19.8) ambazo alikuwa akidaiwa kwenye kamari", ilisema taarifa ya polisi.

Yang alifariki hapo hapo kutokana na bomu hilo huku abiria wengine 11 wa basi hilo wakipata majeraha mbalimbali.

Tabia ya watu kujilipua kwa mabomu wanapozidiwa na matatizo imekuwa ikiongezeka kwa kasi sana nchini China ambapo sababu kubwa inasemwa kuwa ni uhaba wa kazi na kuongezeka kwa tofauti ya kipato kati ya watu masikini na matajiri.

source nifahamishe

Mtoto wa Miaka 2 Mwenye Kilo 41

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kwa umri ana miaka miwili tu lakini kutokana na unene wake mtoto huyu wa nchini China ana uzito wa kilo 41 na bado anaendelea kunenepa.
Mtoto wa kike Pang Ya wa nchini China ingawa ana umri wa miaka miwili tu ana uzito wa kilo 41.

Uzito wa mtoto Pang ni sawa sawa na uzito wa mwanamke mtu mzima wa nchini China mwenye umbile la wastani.

Wazazi wake wamekuwa wakihangaika kutafuta tiba ya unene wa mtoto Pang ambao unatishia maisha yake.

"Madaktari hawajui nini chanzo cha unene wake hali ambayo inatufanya tuwe na hofu kubwa kuhusiana na maisha yake", alisema baba wa mtoto huyo.

Mtoto Pang ambaye anaishi na wazazi wake katika mji wa Taocun katika jimbo la Shanxi, alizaliwa akiwa na uzito wa kawaida wa kilo 3.6.

Katika takwimu za serikali ya China zilizotolewa hivi karibuni, watu milioni 60 wa nchini humo wanakabiliwa na matatizo ya unene uliokithiri.

source nifahamishe

'Sigara Zimeniua'

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mvuta sigara aliyeteseka miaka mingi kutokana na magonjwa yaliyotokana na uvutaji sigara ametimiziwa matakwa yake kuwa atakapofariki jeneza lake na kaburi lake liweke maneno yanayosema 'Sigara Zimeniua'.
Jeneza la mzee Albert Whittamore lilizungushwa katika mitaa ya mji wake nchini Uingereza huku likiwa limewekewa maneno 'Sigara Zimeniua'.

Mzee Albert aliyefariki mwishoni mwa mwezi uliopita akiwa na umri wa miaka 85, aliacha wosia kuwa atakapofariki kaburi na jeneza lake liwekewe maneno hayo ili kuwaonya vijana wasije wakapoteza maisha yao kama alivyopoteza ya kwake kutokana na magonjwa yaliyotokana na uvutaji sigara.

Mzee Albert aliteseka miaka mingi sana kutokana na matatizo ya mapafu, ugonjwa uliotokana na uvutaji wake uliokithiri wa sigara enzi za ujana wake.

Bango lilitengenezwa na kuwekewa maandishi ya 'Sigara Zimeniua' kabla ya jeneza lake kuzungushwa kwenye mitaa kadhaa ya mji wa Dover uliopo kilomita 160 toka jijini London.

Kwenye kaburi lake nako kuliwekewa bango kama hilo ambalo inasemekana litakaa hapo kwa muda wa wiki moja.

Mzee Albert kabla ya kufariki alikuwa akiwausia vijana kuhusiana na madhara yanayotokana na uvutaji wa sigara.

source nifahamishe

MAZISHI YA KIFAHARI NDANI YA TANZANIA

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


MAZISHI YA ASKARI WA BWANA YESU KRISTO MAJOR NASSON JOHN KITUTA AMBAYE NDIYE MMOJA WA WAANZIRISHI WA JESHI LA WAKOVU HAPA TANZANIA (THE SALVATION ARMY).
MAZISHI YA ASKARI WA BWANA YESU KRISTO MAJOR NASSON JOHN KITUTA AMBAYE NDIYE MMOJA WA WAANZIRISHI WA JESHI LA WAKOVU HAPA TANZANIA (THE SALVATION ARMY)
Azikwa kifahari kama viongozi wa serikali ya Nyerere.

Mmoja wa wanzilishi wa shirika la kikristo la Salvation Army hapa nchini Major Nasson Kititu mwenye umri wa miaka 83 alizaliwa mwaka 1926 june 6 na amefariki dunia tarehe 26 februari katika hospitali ya Mikocheni, na kuzikwa katika shamba lake lililopo Kongowe Dar es Salaam,

Alipata Kujiunga na Jeshi la wokovu mwaka1948 akiwa chunya alifunga ndoa na mke wake 'Maria Kititu' mwaka 1950 katika wilaya ya chunya mkoani mbeya,mwaka wa 1951 aliitikia wito wa kumtumiki mungu kama mchungaji akamua kwenda katika chuo cha uchungaji cha jeshi la wokovu Nairobi.

Baada yakumaliza mafunzo ya uchungaji alianza kazi kama Luteni wa Jeshi la wokovu kanisa la Igunga 1952 hadi 1955

Katika mazishi yake kulikuwa na mvua nyingi ilinyesha kuashiria kuwa alikuwa mtumishi wa mungu mamia ya waumini wakiwemo majirani ndugu jamaa walihudhulia katika mazishi ambayo hakiki yalikuwa kama ya mtu mmoja wa kifahari kabisa na yenye heshima kuu kama mtumishi wa mungu yakiwa yameongozwa na COLONEL HEZEKIEL MAVUNDLA ambaye ni kiongozi wa Mkuu wa makanisa ya Salvation Army Tanzania. ambaye ni raia wa South Africa

source nifahamishe

Sugu Awatuhumu Wamarekani Na Ikulu Dar Kwa Kumuingiza Mjini

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Joseph Mbilinyi a.k.a Mr. II au Sugu ameituhumu taasisi moja ya Marekani na Ofisi ya Rais (Ikulu) ya Tanzania kwa kupora haki yake ya kuandaa tamasha la uzinduzi wa mradi wa kampeni ya kuzuia malaria mwezi uliopita.
Kwa mujibu wa gazeti moja la kila siku, Sugu alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa, tayari amewasilisha malalamiko yake makao makuu ya taasisi hiyo, New York, Marekani kwa kosa la kwenda kinyume na makubaliano ya awali.

Kampeni hiyo ambayo ilizinduliwa Februari 13 kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Jakaya Kikwete, inalenga kuhamasisha jamii kupambana na malaria.

Sugu alisema kilichotokea ni kudhulumiwa wazo lake na Wamarekani hao ambao wameshirikiana na mkurugenzi na maofisa wengine (majina tunayo) wa Tanzania.

Alisema, baada ya kukutana na mmoja wa maofisa hao waliweza kujenga urafiki na alipomtaarifu kuhusu mpango wa asasi yao kutaka kuja nchini kuendesha kampeni kubwa ya kutokomeza malaria, hivyo yeye akamshauri atumie muziki wa Bongo Flava na wasanii wake kufikisha ujumbe.

“Kabla ya hapo, siyo huyu ofisa wala mtu yeyote kutoka kwenye asasi hiyo kule Marekani aliyekuwa akijua lolote kuhusu muziki wa Bongo Flava,” alisema Sugu.

Alisema aliandika mchanganuo na mpango mzima wa namna watakavyotekeleza na kupitishwa na bodi ya asasi hiyo yenye maskani yake Marekani.

Sugu amesema, akiwa katika matayarisho hayo mwaka jana, alilazimika kusitisha masomo yake ya elimu ya juu kwenye chuo alichokitaja kwa jina la Springfield, Massachussetts ili apate muda wa kushughulikia kampeni hiyo ya kutokomeza malaria.

“Kilichotushangaza sisi, baada ya mchakato wote kukamilika na wazo letu kukubalika na bodi ya asasi hiyo kwa miaka miwili, ghafla ulipofika muda muafaka wa kutekeleza mradi huu na kufanya uzinduzi tukajikuta tumeenguliwa,” alisema Sugu.

Mwandishi wa habari hizi alipomtafuta Mkurugenzi mmoja wa Tanzania House of Talent (THT), Rugemalira Mutahaba, alisema hawahusiki kwa lolote kuhusu mradi huo ila yeye alihusika kwa kutoa wasanii, vyombo vya muziki na kusema asihusishwe kwa lolote.

source nifahamishe

Wanafunzi Wasagana Mabwenini, Shule Yafungwa

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Shule moja ya wasichana nchini Afrika Kusini imeyafunga mabweni yake na kuwalazimisha wanafunzi wote waondoke baada ya wanafunzi 27 wa shule hiyo kugundulika wanaendeleza tabia ya usagaji shuleni hapo.
Maafisa wa elimu wa nchini Afrika Kusini wanafanyia uchunguzi ripoti ya kufungwa kwa mabweni ya shule ya sekondari ya wasichana kutokana na tabia ya wanafunzi wa kike kusagana.

Wanafunzi wawili wa kike walikamatwa wakibusiana na wanafunzi wengine kadhaa inasemekana wako kwenye mahusiano ya jinsia moja.

Jumla ya wanafunzi 27 wamefukuzwa shule kutokana na tabia hiyo ya usagaji.

Watetezi wa haki za binadamu nchini Afrika Kusini wamekuja juu wakipinga uamuzi wa shule hiyo kwakuwa mahusiano ya jinsia moja yanaruhusiwa kisheria nchini Afrika Kusini.

Afrika Kusini ndio nchi pekee barani Afrika iliyoruhusu wasagaji na mashoga kujitawala kama katika nchi za barani ulaya na Amerika.

Wanafunzi waliofukuzwa shule katika shule hiyo iliyopo KwaZulu-Natal hawakutajwa majina yao kwa vyombo vya habari na jina la shule hiyo nalo liliwekwa kapuni.

Gazeti la The Star la nchini humo lilisema kwamba wanafunzi ambao walishindwa kurudi majumbani mwao walipewa hifadhi kwenye nyumba zilizo karibu na shule hiyo.

Msemaji wa kitengo cha elimu cha Afrika Kusini, Sihle Mlotshwa alinukuliwa na gazeti hilo pia akisema kuwa shule hiyo haina haki ya kuwafukuza au kuwasimamisha shule wanafunzi kwasababu ya masuala yao ya kijinsia.

source nifahamishe

Wezi Wapora Duka na Kumsahau Mtoto Wao

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Polisi nchini Marekani wanawatafuta wezi waliovamia duka moja la madini na vito vya thamani na kuiba kabla ya kukimbia na kumuacha mtoto wao.
Polisi wa Philadelphia nchini Marekani wanawatafuta wezi wawili walioiba vito vya thamani kwenye duka moja mjini humo kabla ya kukimbia na kumuacha mtoto wa kiume wa miaka minne.

Polisi walisema kuwa mwanaume na mwanamke waliingia kwenye duka la Platinum & Ice Jewelry wakiwa na mtoto na kuomba waonyeshe baadhi ya pete.

Ghafla wezi hao walichukua trei lililokuwa limejaa pete za dhahabu zenye thamani ya jumla ya dola laki moja na kukimbia nalo.

Wezi hao walimburuza mtoto huyo mita chache kabla ya kumtelekeza baada ya mmoja wa wafanyakazi wa duka hilo kuwakimbiza.

Polisi wanaendelea kuwatafuta wezi hao ambao walifanikiwa kutoweka eneo hilo na trei hilo la pete za dhahabu.

Mtoto wao amechukuliwa na kuhifadhiwa kwenye nyumba ya ustawi wa jamii.

source nifahamishe

Matiti ya Bandia Yaokoa Maisha Yake

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alitandikwa risasi ya kifua baada ya kujifanya amefariki, alinusurika maisha yake kutokana na matiti ya bandia aliyoyapandikiza kwa operesheni miaka kadhaa iliyopita.
Lydia Carranza alikuwa kazini kwake kwenye zahanati ya meno mjini California wakati mume wa mfanyakazi mwenzake alipovamia kwenye zahanati hiyo.

Mwanaume huyo alikuwa amebeba bunduki na alifika kwenye zahanati hiyo akiwa na lengo moja tu la kumuua mkewe ambaye alikuwa akidai talaka.

Kaka wa mke wa mwanaume huyo ambaye naye anafanya kazi kwenye zahanati hiyo aliingilia kati akitaka kusuluhisha mambo lakini alitandikwa risasi ya tumbo na mwanaume huyo.

Baada ya hapo mwanaume huyo alimgeukia mkewe na kuanza kumpiga risasi kadhaa mpaka alipohakikisha amemuua.

Ndipo sasa zamu ilipomuangukia Coranza na wafanyakazi wenzake. Coranza alitandikwa risasi kwenye mkono wake wa kulia, alipojifanya amefariki mwanaume huyo alimsogelea na kumtandika risasi nyingine ya kifua.

Coranza ambaye ni mama wa watoto watatu alinusurika maisha yake kutokana na matiti ya bandia ya silicone aliyojipandikiza miaka kadhaa iliyopita kuhimili kishindo kikubwa cha risasi hiyo.

Miaka michache iliyopita Coranza alifanya operesheni ya kuongeza ukubwa wa matiti yake kutoka saizi B hadi saizi D.

"Ana bahati sana, risasi ilibakia milimita chache sana kuufikia moyo wake na ogani zake muhimu, kama angekuwa hajafanya operesheni ya kuongeza matiti, tusingekuwa tunaongea hivi sasa", alisema Dr. Ashkan Ghavami wa zahanati hiyo alipokuwa akiongea na gazeti la Los Angeles Times.

Jaime Paredes, mwanaume aliyefanya mashambulizi hayo ya risasi alikamatwa na anasubiria kupandishwa kizimbani akikabiliwa na mashtaka mbali mbali yakiwemo mashtaka ya mauaji ya mkewe.

source nifahamishe

Obama Atakiwa Aache Kuvuta Sigara

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais Barack Obama wa Marekani ametakiwa aache kuvuta sigara na daktari wake.
Rais Obama ametakiwa na daktari wake aache kabisa kuvuta sigara kwaajili ya afya yake mwenyewe.

Obama aliambiwa hivyo baada ya vipimo vya kwanza vya afya yake tangia alipochaguliwa kuwa rais wa Marekani kuonyesha kuwa ana afya njema sana na yupo fiti kulitumikia taifa lake.

Daktari binafsi wa Obama, Jeffery Kuhlman alisema kuwa vipimo vya afya ya Obama vimeonyesha kuwa Obama atakuwa mwenye afya njema kipindi chote cha urais wake.

Dr. Kuhlman alimshauri Obama aendelee na jitihada zake za kujizuia kuvuta sigara ili aiche kabisa tabia ya kuvuta sigara.

Rais Obama mwenye umri wa miaka 48, amekuwa akijitahidi kujizuia kuvuta sigara mbele za watu na amesema kuwa siku hizi huwa havuti sigara mbele ya familia yake.

Enzi zake kabla ya urais, Obama alikuwa mvutaji mkubwa sana wa sigara na kuna wakati Michelle Obama alinukuliwa na jarida moja la Marekani akielezea kukerwa na uvutaji sigara wa Obama.

Rais Obama alimuahidi mkewe kuwa akishinda urais ataacha kabisa kuvuta sigara lakini alikiri kuwa amekuwa akivuta sigara siku moja moja tangia alipoingia ndani ya ikulu ya Marekani.

Mwaka jana rais Obama alisema kuwa amefanikiwa kujizuia kuvuta sigara kwa asilimia 95.
source nifahamishe

Ajali Ya Ndege Yaizuia The Cranes Kutua Mwanza

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


TIMU ya soka ya taifa ya Uganda, The Uganda Cranes, jana ilishindwa kuwasili jijini Mwanza kama ilivyokuwa imepangwa kutokana na kufungwa kwa Uwanja wa Ndege wa jijini humo kutokana na ajali ya Ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Kwa mujibu wa gazeti moja la kila siku, katika ajali hiyo, watu wote waliokuwamo katika ndege hiyo wakati ikijiandaa kutua ikitokea Dar es Salaam, wamenusurika lakini uwanja ukifungwa kwa sababu za kiusalama zaidi.

Ndege hiyo aina ya Boeing 737 yenye namba SH-Mvz, ilipata ajali hiyo jana majira ya saa 1:45 asubuhi; wakati ikitua tairi zake mbili zilipasuka na kusababisha kuacha njia yake huku injini moja ya kushoto ikiingiliwa maji.

Kwa mujibu wa watu walioshuhudia ajali hiyo, wakati ndege hiyo ikitua uwanjani hapo kulikuwa na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha ghafla kilisikika kishindo kikubwa kilichowashtua.

Akizungumza na gazeti moja la kila siku, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela, alisema kutokana na kufungwa kwa uwanja huo kwa siku ya jana, Uganda Cranes walishindwa kuwasili kama ilivyokuwa imepangwa.

Mwakalebela alisema baada ya ajali hiyo, TFF iliwasiliana na Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) wakiwataka kusitisha safari yao kwa jana ili kuepuka usumbufu hadi leo tayari kwa mechi ya kirafiki itakayopigwa kesho kwenye Uwanja wa CCM- Kirumba.

Alisema pamoja na tatizo hilo, maandalizi ya mechi hiyo yanakwenda vizuri na kusema vijana wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, wamejiandaa vizuri kwa mechi hiyo.

Mwakalebela alisema mechi hiyo ni muhimu zaidi kwa Stars kwa ajili ya kujiandaa na kampeni ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika kwa nyota wa Ligi za Ndani (CHAN).

Stars itaanza kampeni yake dhidi ya Somalia, mechi itakayopigwa Machi 13 kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye jijini Dar es Salaam.

source nifahamishe

Ahadi nyingine ya kurudi umeme Zanzibar yatolewa

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MEDAIWA jana kuwa huduma ya umeme visiwani Zanzibar inatarajiwa kurudi Machi 9 baada ya kukamilika kazi za utengenezaji wa kituo cha kupokea umeme kilichopo Fumba, Mkoa wa Mjini Magharibi
Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Hassan Ali Mbarouk, aliwaambia waandishi wa habari kuwa kutokana na kukamilika kwa matengenezo cha Fumba huduma hiyo itarejea punde na kuwaahidi wananchi wasiwe na wasiwasi huduma hiyo itarejea siku hiyo.

Alisema kazi iliyobakia ni kuunganisha waya za umeme kutoka nchi kavu na baharini na kazi hiyo ya kuunganishwa kwa waya kutoka katika vituo vya Fumba hadi Ras Kiromoni Tanzania Bara itachukua muda wa siku tatu.

Alisema hadi Jumapili ijayo kazi ya matengenezo itakuwa imemalizika na matarajio Machi 8 kutafanyika vipimo vya majaribio na Machi 9 ndiyo huduma hiyo inatarajiwa kuwashwa na kurudi rasmi kwa umeme visiwani humo.

Pia aliweza kuwaambia waandishi wa habari kuwa kuchelewa kwa huduma hiyo kumesababishwa na mafuta yaliyokuwemo ndani ya waya zinazoleta umeme kutokuwa safi na kulazimika kusafishwa kwa muda wa siku tatu.

Wakazi wa visiwani humo wamekosa huduma hiyo ya umeme tangu Desemba mwaka jana, baada ya kutokea hitilafu katika kituo cha kupokea umeme huo kutoka Ras Kiromoni hadi Fumba mjini Unguja

source nifahamishe

Basi la laeketea wka moto Ubungo

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

BASI moja la abiria la kampuni ya Abood jana liliteketea kwa moto lote katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo.

Basi hilo likiwa kituoni hapo lilianza kuweaka moto ghafla na kupelekea mali zote vikiwemo na viti kuteketea kwa moto huo.

Ilidaiwa kuwa chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme iliyotoka katika gari hilo.

Hata hivyo kikosi cha zima moto kilichelkewa kufika eneo la tukio na kukut gari hilo liko katika hatua za mwisho kuteketea

Basi hilo leo lilikuwa linatarajiwa lifanye safari zake kuelekee mkoani Tunduma.

source nifahamishe

Zanzibar kuendelea kuwa gizani

Sunday, February 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Shirika la umeme Zanzibar (ZECO) limesema haifahamiki huduma ya umeme itarejea lini visiwani humu kwa vile mafundi kutoka ulaya wanaendelea na matengenezo katika kituo cha Fumba Zanzibar na Ras Kilomoni, Tanzania bara.

Hayo yameelezwa na meneja wa shirika hilo, Hassan Ali Mbarouk, alipokuwa akizungumza na Nipashe baada ya kutakiwa kueleza ni lini huduma ya umeme inatarajia kurudi. Zanzibar iliingia gizani tangu Desemba 10 mwaka jana.

Awali Waziri wa Maji, Nishati na ardhi Mansour Yusuf Himid, alitangaza kuwa huduma ya umeme Zanzibar ilitarajia kurejea Februari 20 kufuatia kuwasili kwa mafundi toka Afrika Kusini na Ulaya.

Meneja huyo wa Zeco alisema jana kazi ya matengenezo katika kituo cha Ras Kilomoni Tanzania bara imeshafanyika kwa asilimia 98 tangu walipoanza matengenezo hayo.

“Mafundi bado wanaendelea na matengenezo na ni mapema kueleza lini umeme utarejea na kabla ya kufanya hivyo ni lazima nishauriane na wakubwa wangu,” alisema meneja huyo na kuongeza kuwa kazi ya matengenezo inandelea vizuri.

Meneja huyo alisema kazi iliyobakia katika kituo cha Ras Kilomoni Tanzania bara ni kuunganisha bomba maalum katika kituo hicho kinachopokea umeme toka Kidatu kabla ya kusafirishwa Zanzibar kupitia waya uliotandikwa chini ya bahari.

Aidha, alisema kwamba katika kituo cha Fumba, mafundi toka Ulaya na wazalendo wanaendelea kukamilisha kazi ya kuweka viunganishi katika waya huo na kazi hiyo inaendelea vizuri tangu vifaa vilivyokuwa vikisubiriwa kuwasili Zanzibar.

“Lakini siwezi kusema kazi zilizobakia zitakamilika lini na kurejeshwa kwa umeme ispokuwa kazi inaendelea vizuri na karibu vifaa vyote vilivyokuwa vinasubiriwa vimewasili Zanzibar,” alisema meneja huyo.

Hata hivyo habari zilizopatikana toka katika vyanzo vya kuaminika ndani ya shirika hilo, zinaeleza kuwa huenda huduma ya umeme Zanzibar ikarejea Machi 3, mwaka huu.

Meneja huyo aliwataka wananchi waendelee kuwa na subira na baada ya kukamilika kwa matengenezo shirika litawatangazia siku ya kurejea huduma hiyo.

Waya unaopokea umeme toka Tanzania Bara uliozikwa chini ya bahari tayari umemaliza muda wake wa matumizi wa miaka 30 na hiyo ni mara ya 3 kulipuka na kusababisha wananchi kukosa huduma ya umeme.

Waya huo unauwezo wa kupokea megawati 45 za umeme wakati matumizi ya umeme yamefikia megawati 43.7.

Tangu kukosekana kwa huduma ya umeme shirika hilo limekuwa likipata hasara ya sh bilioni 2.2 kila mwezi na viwanda vingi vimelazimika kufungwa kutokana na tatizo la umeme pamoja na baadhi ya hoteli za kitalii Zanzibar.

Awali SMZ ilitangaza huduma ya umeme Zanzibar ingetarajia kurejea leo lakini hali imekuwa tofauti.

Kukosekana kwa huduma ya umeme kumesababisha sherehe za kuzaliwa mtume Mohammed kushindwa kufanyika juzi usiku katika viwanja vya Mnazi Mmoja kama ilivyozoeleka na badala yake zilifanyika kuanzia saa 10 jioni katika msikiti wa mwembe shauri na kuongozwa na Rais wa Zanzibar alhaji Amani Abeid Karume.

Mei Mwaka 2008 wananchi wa Zanzibar walilazimika kukaa bila umeme kwa muda wa mwezi mmoja baada ya waya unaopokea umeme kulipuka katika kituo cha Fumba na serikali kulazimika kuagiza wataalamu kutoka Afrika Kusini na Norway.

source ippmedia

Abby Sykes aamua kuja kivingine

Sunday, February 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

JE, unamfahamu mwanamuziki mkongwe Ibrahim Abdulwaheed Sykes maarufu kama Abby Sykes?

Hili si jina geni miongoni mwa wanamuziki nchini, lakini kama hulifahamu sina shaka jina la msanii wa muziki wa kizazi kipya Dully Sykes utakuwa unalifahamu vyema.

Ni kwamba Ibrahim Abdulwaheed Sykes au Abby Sykes kwa wasiomfahamu ndio baba mzazi wa msanii Dully Sykes.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili hivi karibuni, msanii huyo alisema alianza kujifunza muziki mwaka 1966, kwa kutoroka usiku nyumbani na kwenda disko na kwamba kutokana na kupenda sana muziki ndipo akatumia gita la baba yake mdogo kujifunza.

Anasema baada ya kuanza kuimba kwenye majukwaa, ndipo akakutana na Adamu Kingoni, akiwa kiongozi wa bendi ya Rifters.

Sykes anasema familia yao iliwahi kuunda kundi maarufu lililojulikana kama Shery Merry Marcas, ambalo liliundwa na baba zake kama Abdulwaheed Sykes, Ally Sykes, Balozi Sykes.

Anasema ilipofika mwaka 1970, ndipo akajiunga na bendi hiyo ya Rifters akiwa mpiga gita. Baada ya kukaa muda mrefu katika bendi hiyo, akaamua kujitoa na kujiunga na bendi nyingine ya Kenya iliyoitwa Hold Banjo.

Anasema kipindi hicho alikuwa akipiga karibuni vifaa vyote vya muziki, huku akijifunza kuimba kwa kusikiliza nyimbo za wanamuziki maarufu wa nje akiwemo kama James Brown.

Anasema mwaka 1978 akajipanga na kutoa albamu yake ya kwanza iliyoitwa Mimi na Wewe na kwamba albamu hiyo aliweza kupata fedha kidogo, lakini zaidi fedha zao ilikuwa kwenye matamasha.

Anasema kutokana na kuona muziki haulipi vizuri aliungana na rafiki zake na kuomba kazi katika Meli ya mv Oman. Anasema kipindi hicho, mtu huwezi kuonekana bora, au mjanja bila kuwa baharia au mfanyakazi wa bandari.

Akaamua kuachana na kazi ya muziki, na kuungana na wenzake katika kazi ya ubaharia na kuendelea kujifunza vitu vingi kutoka nchi mbalimbali.

Baada ya safari ya kwanza ya miezi minane kurudi, aliamua kuachana na meli hiyo, na kujiunga na meli nyingine ya Youcht kwa miezi minane mingine.

Akiwa Baharia anasema aliona vitendo vingi vya kiovu vilivyoendelea baharini, lakini kubwa ambalo anashindwa kulisahau, anasema siku moja, wakiwa kwenye safari za nchi ya mashariki ya mbali wakiwa katikati ya maji aliona wamekamatwa Watanzania wanne na Wakenya saba.

Anasema baada ya kufikishwa kwa mkubwa, walitupwa baharini. Hapo ndipo roho ilipomuuma kuona ndugu zake wa Kitanzania na wale Wakenya wakiliwa na papa mbele ya macho yao.

Msanii huyo anasema kuwa alipata taarifa kuwa kuna Mkenya mmoja alipona katika sakata hilo na hadi hii leo akikumbuka wenzake hulia na kuchanganyikiwa. Mwaka 1980 akaamua kuachana na kazi hiyo ya ubaharia na kurudia kazi yake ya muziki.

Mwanamuziki huyo anasema yote hayo yameshapita na hivi sasa amerudi, kama zamani na anatarajia kufanya mapinduzi makubwa ya muziki.

Anasema amejiandaa kuibuka na bendi itakayoundwa na yeye, mwanawe na kuwa ameshajiandaa kutoa albamu yake ya pili ukiachilia ile ya zamani ya mwaka 1978 ya Mimi na Wewe.

Albamu hiyo amerekodia studio ya Dhahabu Record inayomilikiwa na Dully Sykes. Tayari ameshakamilisha kurekodi nyimbo kadhaa na kuzitaja kuwa ni Mchumba Mzuri, Famili Song, Only You, Lalaa akiwashirikisha mwanaye Dully Sykes na Mr Blue.

Anasema mtu ambaye anapenda sana kazi zake, na pindi akiwa sawa basi atamshirikisha katika albamu hiyo ni msanii David Nyika ‘Daz Baba’.

Mkali huyo ana nyimbo kwenye albamu moja ya wanamuziki mchanganyiko ya Urithi, ama Baba na Mwana, ambayo ni ya wasanii maarufu walioimba na watoto zao, kama Nguza Vicking na Papi Kocha, Zahir Ally na Banana Zoro, yeye akiimba wimbo wa Malaika.

source habarileo