Bikira Kuwa Sharti la Kuingia Shule za Sekondari

Friday, October 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Wasichana waliopoteza bikira zao hawatapata nafasi za kujiunga na shule za sekondari za serikali nchini Indonesia iwapo muswada mpya wa sheria wa kuzuia vijana kuanza uzinzi mapema utapitishwa na bunge la nchi hiyo.
Muswada wa sheria umefikishwa bungeni nchini Indonesia ukitaka wasichana waliopoteza bikira zao wasiruhusiwe kujiunga na shule za sekondari nchini humo.

Muswada huo wa sheria umetolewa na mbunge wa jimbo la Jambi nchini humo Babang Bayu Suseno ambaye ameeleza kuwa muswada huo ukipitishwa kuwa sheria utasaidia kuzuia vijana kuanza uzinzi mapema.

Suseno alisema kuwa upatikanaji wa video na picha za ngono na ufahamu mdogo wa masuala ya dini umepelekea vijana kujihusisha na matendo ya ngono mapema.

Mbunge huyo ametaka wanafunzi wa kike wafanyiwe uchunguzi kuthibitisha bikira zao kabla ya kuruhusiwa kuingia shule za sekondari za serikali.

Hata hivyo muswada huo umekumbwa na upinzani mkubwa toka kwa wanasiasa na taasisi za kutetea haki za binadamu.

Imeelezwa kuwa kuwalazimisha wasichana kupima bikira zao itakuwa ni kuwabagua na ni kinyume cha haki za binadamu.

"Njia ya kuzuia uzinzi kwa vijana ni kwa kuwapa elimu ya masuala ya jinsia", alisema Seto Mulyadi, mkuu wa kitengo cha taifa cha kuwalinda watoto na kuongeza "Sio wasichana wote wanaoshiriki kwenye masuala ya ngono wanafanya hivyo kwa kupenda".

"Weka somo maalumu shuleni la kuwafundisha wanafunzi jinsi ya kujilinda lakini sio kuwapima bikira", aliongeza Mulyadi.

Indonesia ni nchi yenye waislamu wengi kuliko wote duniani wapatao milioni 210. Wengi wao wana msimamo wa kati lakini wale wenye msimamo mkali wanahofia kuwa maendeleo ya kasi yanayoambatana na vijana kuiga umagharibi yanapelekea kupungua kwa msimamo wa kidini nchini humo.

Ili muswada huo upitishwe inabidi upewe sapoti ya gavana wa jimbo la Jambi pamoja na waziri wa masuala ya wanawake, lakini viongozi hao wawili ndio waliokuwa wa mwanzo kuupinga muswada huo.

source nifahamishe

Ajiua Baada ya Video Akilawitiwa Kuwekwa Online

Friday, October 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi wa kiume wa nchini Marekani ambaye marafiki zake walirekodi kwa siri video wakati akiingiliwa kinyume cha maumbile na mwanaume mwenzie na kisha kuiweka video hiyo kwenye internet amejiua kwa kujirusha toka kwenye daraja.
Tyler Clementi, Mwanafunzi wa kiume wa mwaka wa kwanza wa chuo kikuu cha Rutgers University cha nchini Marekani mwenye umri wa miaka 18 ambaye alikuwa akifanya ushoga kwa siri, amejiua mwenyewe kwa kujirusha toka kwenye daraja baada ya video yake akiingiliwa kinyume cha maumbile na mwanaume mwingine kurushwa LIVE kwenye internet.

Clementi alijirusha wiki iliyopita toka kwenye daraja la George Washington na kuangukia kwenye mto mkubwa wa Hudson River, last week, maiti yake ilipatikana juzi kwenye mto huo.

Clementi alichukua uamuzi wa kujiua baada ya kugundua marafiki zake aliokuwa akikaa nao chumba kimoja walimrekodi kwa siri wakati akifanya mapenzi na mwanaume mwingine na VIDEO za tukio hilo zilirushwa LIVE kwenye internet kupitia Webcam.

"Kama angekuwa kitandani na mwanamke, haya yote yasingetokea", alisema mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho.

"Kama asingeanikwa LIVE kwenye internet, mambo yake ya ndani yasingeanikwa na leo tungekuwa naye hapa", aliongeza mwanafunzi huyo.

Wanafunzi wawili mmoja wa kiume Dhraun Ravi na mwingine wa kike Molly Wei, ambao wote wana umri wa miaka 18, wamefunguliwa mashtaka ya kuvunja haki za msingi za Clementi.

Mahakama iliambiwa kuwa webcam ilitumika kurusha LIVE tukio la Clementi akiingiliwa na mwanaume mwingine mnamo septemba 19 na Ravi alijaribu kulirusha LIVE tena tukio la pili lililofanyika septemba 21 ambayo ni siku moja kabla ya Clementi kujiua.

Taasisi za kutetea haki za mashoga zimeichachamalia kesi hii zikitaka Ravi na mwenzake wahukumiwe adhabu kali.

Taasisi hizo zimesema kuwa Ravi na mwenzake wameonyesha chuki waliyo nayo kwa mashoga na wasagaji na wameitaka mahakama itoe adhabu kali.

Ravi na mwenzake huenda wakahukumiwa kwenda jela miaka mitano iwapo watapatikana na hatia ya kuingilia undani wa mtu bila ya ridhaa yake.

source nfahamishe

Kahaba Ajitamba Kula Uroda na Beckham

Wednesday, September 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kahaba Irma Nici ameendelea kujitamba kuwa alikula uroda na mcheza soka maarufu wa Uingereza, David Beckham ingawa Beckham anajiandaa kufungua kesi ya madai ya fidia kiasi cha dola milioni 16.
Pamoja na kwamba wanasheria wa mcheza soka maarufu wa Uingereza, David Beckham anayesakata kabumbu nchini Marekani wako kwenye jitihada za kufungua kesi mahakamani kumdai fidia ya dola milioni 16, kahaba anayedai kutembea na Beckham ameibuka na kutamba ana ushahidi wa kuthibitisha madai yake.

Kahaba Irma Nici mwenye asili ya Bosnia amedai kuwa anaweza kuithibitishia mahakama kuwa alilala na nyota huyo wa soka mjini London na mjini New York mnamo mwaka 2007.

Nici amedai kuwa Beckham ana alama za kipekee kwenye sehemu zake nyeti hivyo ajiandae kuvua suruali yake mahakamani ili kuzithibitisha alama hizo.

Nici mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akiwakwepa wanasheria wa Beckham na amekuwa akijificha kwenye hoteli mjini New York.

Beckham mwenye umri wa miaka 35 anamshtaki Nici kutokana na habari iliyotoka kwenye jarida moja la Marekani kuwa Beckham alinunua penzi la kahaba Nici.

Nici aliliambia jarida hilo kuwa alishea kitanda kimoja na Beckham wakati Beckham alipofanya mapenzi yaliyowahusisha wanawake wawili kwa mpigo. Mwanamke wa pili aliyezungumziwa katika habari hiyo bado hajajulikana.

Beckham anamshtaki Nici na jarida hilo kwa kuandika habari za kumpakazia kuwa aliisaliti ndoa yake na Victoria Beckham, 36,

Beckham pia anamshtaki Nici na jarida hilo kwa habari ambayo imemfanya Beckham aonekane aliyatia maisha ya mkewe hatarini kwa kutembea na kahaba.

source nifahamishe