Auanza Mwaka Mpya Vibaya Kwa Operesheni ya Kuongeza Makalio

Saturday, January 01, 2011 / Posted by ishak /


Mwanamke mmoja wa nchini Marekani ambaye alitaka kuingia mwaka 2011 akiwa mrembo zaidi na mwenye makalio makubwa amefariki dunia masaa matatu baada ya kufanyiwa operesheni ya kuongeza makalio.
Mwaka 2011 umeanza vibaya kwa bwana Osvaldo Vargas mkazi wa Florida, Marekani, Amempoteza mke wake ambaye operesheni ya kuongeza urembo na makalio ili aonekane mrembo zaidi mwaka 2011 ilimalizika vibaya na kupelekea kifo chake.

Lidvian Zelaya mwenye umri wa miaka 35 alitaka kuingia mwaka 2011 akiwa mrembo zaidi kwa kuamua kufanya operesheni ya kutoa nyama nyama na mafuta toka kwenye tumbo lake na kuzihamishia kwenye makalio yake ili kuyafanya yawe makubwa zaidi.

Masaa matatu baada ya operesheni hiyo, Lidvian aliwahishwa hospitali akiwa amezidiwa sana na wakati mume wake anawasili hospitali Lidvian alikuwa ameishafariki dunia.

"Amefariki akitafuta urembo, kwangu mimi alikuwa tayari ni mrembo", alisema mume wa Lidvian kwa huzuni.

"Alikuwa ni mrembo, mwenye furaha na aliyependa kudansi, nataka kujua nini kimetokea", alisema bwana Oswaldo wakati akiongea na waandishi wa habari.

"Hatumlaumu yeyote lakini tunataka kujua nini kimesababisha kifo chake", alisema Oswaldo akiwa pamoja na mwanasheria wake.

Lidvian alifanyiwa operesheni kwenye kliniki ya Strax Rejuvenation, ya Florida, hata hivyo kliniki hiyo imesema kuwa sheria zinawabana kusema chochote kuhusiana na kifo cha Lidvian.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment