Siri ya Mapenzi ya Michelle Obama

Wednesday, February 16, 2011 / Posted by ishak /

Katika kusherehekea siku ya wapendanao duniani, mke wa rais wa Marekani, Michelle Obama amewapa wapendanao siri ya mapenzi kuwa ni 'Si kwa wapenzi kununiana na kuwa siriasi muda wote bali ni kuchekeshana na kupeana matabasamu wakati wote.
Michelle Obama amesema kuwa siri kubwa ya mapenzi ndani ya nyumba ni kuchekeana na mpenzi wako hivyo kudumisha furaha wakati wote.

Michelle Obama amesema kuwa amekuwa akiitumia njia hiyo kuyadumisha mapenzi kati yake na rais Barack Obama na kwa kweli amefanikiwa katika hilo.

Ingawa ndoa yao imekumbwa na misukosuko mingi ya kimaisha na harakati za kisiasa, ndoa hiyo imetimiza miaka 19 sasa.

Bi Obama alisema kuwa siri kubwa ya kudumu kwa mapenzi ndani ya ndoa yao ni kuchekeshana na kupeana matabasamu wakati wote.

Katika kusherehekea siku ya wapendanao Valentine Day, Bi Obama alisema anatarajia mzee Obama atazama mfukoni na kumnunulia zawadi ya mkufu au hereni za dhahabu.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment