Jela Maisha Kwa Kumpachika Mimba Binti wa Miaka 9

Friday, March 25, 2011 / Posted by ishak /


Fede Datilus
Saturday, March 26, 2011 2:42 AM
Mwanaume mmoja wa nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela maisha kwa kumpachika mimba mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 9.
Fede Datilus wa Florida nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela maisha kwa kumpachika mimba msichana mwenye umri wa miaka 9 raia wa Haiti.

Datilus lipatikana na hatia ya kumbaka msichana mwenye umri chini ya miaka 12 kosa ambalo aliadhibiwa kifungo cha maisha.

Datilus alipatikana na hatia ya kosa jingine la kumpachika mimba msichana mwenye umri wa miaka 9 kosa ambalo alihukumiwa kwenda jela miaka mitano.

Msichana aliyepachikwa mimba alikuwa ni raia wa Haiti amabye alihamia Marekani pamoja na wazazi wake miaka miwili iliyopita.

Baba wa msichana huyo aligundua mtoto wake ni mjamzito mwezi machi mwaka jana baada ya kumpeleka kliniki alipokuwa akiumwa.

Msichana huyo ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu za kisheria alifanikiwa kumtambua Datilus kuwa ndiye mwanaume aliyembaka.

Msichana huyo alijifungua salama mwa huu akiwa amefikisha umri wa miaka 10.

Datilus mwenye umri wa miaka 33, alihukumiwa kwenda kuyamalizia maisha yake yaliyobakia jela.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment