Mchezaji wa Manchester City Atupwa Jela

Friday, March 25, 2011 / Posted by ishak /



Kelvin Etuhu

Mshambuliaji wa Manchester City, Kelvin Etuhu ametupwa jela miezi minane kwa kumpiga mtu mtaani na kumvunja taya.
Mshambuliaji wa timu tajiri ya nchini Uingereza Manchester City, Kelvin Etuhu ametupwa jela miezi minane kwa kumpiga mtu mtaani na kumvunja taya lake.

Etuhu ambaye alisomewa mashtaka yake katika mahakama ya mjini Manchester alipatikana na hatia ya kufanya shambulizi la kudhuru mwili na kufanya vurugu.

Etuhu mweye umri wa miaka 22 baada ya kupata ulabu alimshambulia mwanaume mmoja aliyekuwa akizozana naye ndani ya baa mwaka jana, Etuhu alionekana kwenye CCTV akiendelea kumshushia kipigo mwanaume huyo baada ya kumtandika ngumi iliyomdondosha chini.

Etuhu ambaye pia ni mchezaji wa timu ya taifa ya Nigeria, amehukumiwa kwenda jela miezi minane.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment