Dawa ya Babu inawezekana kuwa katika mfumo wa vidonge -WHO

Thursday, May 05, 2011 / Posted by ishak /


Foleni ya kupewa kikombe cha babu

UTAFITI unaoendelea kufanyika wa dawa ya Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa kijiji cha Samunge umebainika kuwa dawa inatibu maradhi sugu na Shirika la Afya Duniani [who] Kuikubali dawa hiyo
Hayo yamebainishwa na Askofu wa Kanisa la KKKT na kubainisha kuwa shirika hilo limekubali kuwa dawa hiyo inatibu maradhi sugu kama ilivyobainishwa awali katika utafiti wa kina walioufanya.

Imesemekana kuwa dawa hiyo inawezekana kuwa katika mfumo wa vidonge na chupa.

Shirika la Afya Duniani WHO ambalo lilituma wataalamu wake kuichunguza dawa ya babu, limebainisha hilo na kulifanyia kazi mikakati hiyo ya kuweka dawa hiyo katika mifumo hiyo na si kikombe pekee kama ilivyozoeleka, alisema Askofu huyo.

Pia dawa hiyo imethibitishwa na taasisi ya TMF na kubainisha kuwa dawa hiyo inatibu maradhi sugu.

Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa TMF, Marwa Gonzaga jijini Dar es Salaam.

Alisema wakati wakiendelea na utafiti huo walibaini kuwa tiba hiyo ni mchanganyiko wa mizizi ya miti shamba ya aina mbili ambayo ni kisayansi unafahamika kama Carissa Spinarum na mti wa Ntuntwa.

Tayari dawa ya babu imeshajizolea sifa ndani na nje ya nchi ambapo watu wameendelea kumiminika kijijini hapo kunywa dawa hiyo.

Hata hivyo taarifa zilizopatikana baadae zimesema kuwa babu amekataa dawa yake kufanyiwa mabadiliko yoyote kwakuwa Mungu hapendi.

Babu alisema kuwa kwakuwa dawa hiyo ni ya miujiza alioteshwa na Mungu, masharti aliyopewa na mungu kwenye ndoto yake hayaruhusu dawa hiyo ifanyiwe mabadiliko yoyote yale. Labda kama ataoteshwa ndoto nyingine ya kupewa ruhusa kufanya hivyo.

source nifahamishe

1 comments:

Comment by emu-three on May 19, 2011 at 3:20 AM

Habari nzuri hiyo mkuu, unajua kuna dawa nyingi za kienyeji nzuri, kama wataziweka katika mfumo wa vidonge itafaaa..!

Post a Comment