Wakristo Wamsalie Osama

Thursday, May 05, 2011 / Posted by ishak /



Kardinali Albert Vanhoye

Wakristo inabidi wasali kumuombea makazi mema peponi Osama bin Laden ingawa alikuwa ni adui wao kwakuwa kutoa msamaha ndio mafundisho ya biblia.
Ingawa Osama alikuwa ni adui wa wakristo, wakristo inabidi wasimame kusali na kumuombea makazi mema Osama bin Laden.

Hayo yalisemwa na kardinali Albert Vanhoye mwenye umri wa miaka 87 wa kanisa katoliki nchini Italia ambaye alisema kuwa mafundisho ya biblia yanafundisha kusameheana.

"Mimi nimeusalia mwili wa Osama bin Laden, inatubidi tumuombee dua njema kama tulivyowaombea wahanga wa shambulio la septemba 11, hivyo ndivyo Yesu anavyowafundisha wakristo", alisema Kardinali Vanhoye.

"Yesu ametutaka tuwasamahe maadui zetu, tunaposali huwa tunasema "Baba, tusamehe kwa yale tuliyoyatenda kama vile tulivyowasamehe watu kwa yale waliyotutendea".

"Sala hii haiwezi kukubalika kama bado tutaendelea kuweka chuki kwa maadui zatu", alisema Kardinali Vanhoye, ambaye alichaguliwa kuwa Kardinali na Pope Benedict XVI mwaka 2006.

Kardinali Vanhoye anatambulika sana kwa mafundisho yake kuhusiana na biblia.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment