Ukiwa Mchungaji Kanisani Nigeria, Utajiri Nje Nje

Thursday, June 23, 2011 / Posted by ishak /



Mchungaji tajiri kuliko wote Nigeria, Mchungaji David Oyedepo

Uchunguzi uliofanywa nchini Nigeria umebaini kuwa wachunga kondoo wa Bwana nchini humo mbali ya kuhubiri neno la bwana wanatengeneza pesa ya maana kiasi cha kwamba baadhi yao wanamiliki ndege, hoteli na biashara kubwa.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Muandishi wa Nigeria wa jarida la Marekani la masuala ya uchumi, Forbes, wahubiri wa neno la bwana nchini Nigeria wanatengeneza pesa sana kutokana na uchungaji kiasi cha kufanananishwa na matajiri wa biashara ya mafuta.

Mfonobong Nsehe akitoa ripori ya uchunguzi wake alisema kuwa wachungaji wa Nigeria wanaishi maisha ya kifahari na wana miradi mikubwa ya kibiashara.

"Kuhubiri ni biashara inayolipa sana, sawa sawa na biashara ya mafuta", alisema Nsehe.

Utajiri wa wachungaji watano maarufu nchini Nigeria unakadiriwa kufikia dola milioni 200, alisema Nsehe.

Makanisa mengi yameibuka nchini Nigeria na waumini wamekuwa wakiongezeka.

Nsehe alisema kuwa mchungaji tajiri kuliko wote ni Mchungaji David Oyedepo wa kanisa la Living Faith World Outreach Ministry, ambaye utajiri wake ni dola milioni 150.

Mchungaji Oyedepo ndiye anayeshika nafasi ya pili akimiliki ndege nne, kampuni ya uchapishaji, chuo kikuu na shule moja na majumba ya kifahari jijini London na Marekani.

Mchungaji Chris Oyakhilome wa kanisa la Loveworld Ministries ana utajiri unaokadiriwa kuwa kati ya dola milioni 30 na 50. Mchugaji Oyakhilome anamiliki kampuni ya magazeti na majarida, stesheni ya televisheni, hoteli na kampuni ya majumba.

"Wachungaji hawa wanaishi maisha ya kifahari utawaona kwenye ndege zao binafsi na magari ya kifahari", alisema Nsehe.

Wachungaji wengine walioingia kwenye listi ya utajiri ni mchungaji Temitope Joshua Matthew mwenye utajiri kati ya dola milioni 10 na 15, Mchungaji Matthew Ashimolowo dola milioni 6-10, na mchungaji Chris Okotie mwenye utajiri kati ya dola milioni 3-10.

Nsehe aliongeza kuwa wawakilishi wa wachungaji wote isipokuwa mchungaji Ashimolowo, wamethibitisha taarifa ya umiliki wa mali za wachungaji hao.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment