Vurugu zatanda vituo vya mafuta

Wednesday, August 10, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

NewsImages/5866906.jpg

VURUGU, FUJO za hapa na pale zilitawala jana katika vituo mbalimbali viuzavyo mafuta jijini Dar es salaam kutokana na baadhi ya vituo kugoma kuuza mafuta hali iliyofanya kuleta adha kwa watumiaji wa vyombo vya moto
Msongamano mkubwa wa watu waliobeba vidumu mikononi na foleni ya ndefu ya magari vilitawala katika vituo hivyo kusaka nishati hiyo ambapo ilikuwa adimu kupatikana.

Msongamano huo ulioanza mapema jana ulizua tafrani baada ya watu kuanza kugombea huduma hiyo huku kila mmoja akiwa na hofu ya kukosa huduma hiyo.
Hali hiyo imekuja baada ya baadhi ya vituo juzi na jana kugoma kuuza mafuta ya petrol kutokana na Serikali kuamrisha vituo hivyo kuuza bei elekezi iliyopangwa hali iliyofanya kuwa na upungufu wa upatikanaji wa mafuta kama awali.

Vituo vya Bigbon, Lake Oil ndivyo vilionekana kutoa huduma hiyo na watu wengi kukimbilia huko hali iliyofanya mmiliki kuuza mafuta yasiyozidi ya shilingi elfu kumi ili kila mmoja aweze kupata huduma hiyo.

Hali ilikuwa mbaya katika kituo cha Bigbon kilichopo Msimbazi ambapo madereva wa magari na pikipiki kugombania huduma hiyo huku kituo cha Sinza wakigoma kuzia watu wenye vidumu kwa hofu ya kudhani wanakwenda kufanya biashara

Hali hiyo iliwafanya wachanganyikiwe kwa kuwa kuna baadhi ya magari yalizimika njiani na kushindwa kufika kituoni na kufanya fujo kutanda na wengine kutaka kutoa adhabu kwa muuzaji wa mafuta

Serikali ilitangaza mafuta ya petrol yauzwe kwa bei ya Shilingi 2004 na dizeli iuzwe kwa Shilingi1911ambapo wenye vituo walionyehsa kuwatunishia misuli serikali huku serikali nayo kutoa onyo kiuwafutia leseni wale wote wagomao kutoa huduma hiyo

Uchunguzi wa NIFAHAMISHe umebaini jana baadhi ya watu waliuziwa mafuta kwa bei ya zaidi ya shilingi elfutano kutokana na adha hiyo

source nifahamishe

Wanajeshi Wa Kikosi Kilichomuua Osama bin Laden Wauliwa

Wednesday, August 10, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

NewsImages/5870762.jpg

Wanajeshi wa Marekani wapatao 22 toka kikosi cha Seal Team Six kilichotumika kumuua Osama bin Laden wamefariki dunia baada helikopta waliyokuwemo kutunguliwa na makombora ya Taliban nchini Afghanistan.
Jeshi la Marekani limepata pigo kubwa sana la mwaka baada ya kupoteza jumla ya wanajeshi 31 wakiwemo wanajeshi 22 toka kikosi maalumu cha Seal Team Six ambacho wanajeshi wake walitumika katika shambulio la kumuua kiongozi wa Al-Qaeda, Osama bin Laden.

Seal Team Six ni kikosi maalumu cha makomandoo wa Marekani ambacho ndicho kilichotumika kuivamia nyumba ya Osama bin Laden nchini Pakistan na kumuua kiongozi huyo wa Al-Qaeda.

Taarifa iliyotolewa ilisema kwamba helikopta ya kijeshi ya Marekani iliyokuwa imewabeba wanajeshi 31 wa Marekani pamoja na makomandoo saba wa Afghanistan ilitunguliwa na makombora ya wanamgambo wa Taliban.

Kuuliwa kwa wanajeshi wengi wa Marekani ndani ya siku moja ni pigo kubwa sana kwa jeshi la Marekani katika vita hivyo vya Afghanistan ambavyo vimekuwa vikiendelea kwa takribani miaka 10 sasa.

Mmoja wa maafisa wa Marekani ambaye hakutaka kutaja jina lake alisema kwamba helikopta hiyo ya kijeshi ya Marekani ilitunguliwa na Taliban kwenye mji wa Wardak usiku wa siku ya ijumaa.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kwamba helikopta hiyo ilitunguliwa wakati ilipokuwa ikifanya shambulizi kwenye maeneo yanayotawaliwa na Taliban kwenye mji wa Wardak.

"Tulikuwa nyumbani usiku wakati tulipoona helikopta ikitua juu ya paa la jumba la kamanda wa Taliban na mara risasi zilianza kuvurumishwa toka pande zote mbili", alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo Mohammad Saber.

Saber aliongeza kuwa helikopta hiyo iliamua kuondoka toka eneo hilo lakini ghafla ilidondoka chini na kulipuka.

Msemaji wa Taliban, Zabiullah Mujahid alisema kwamba wanamgambo wa Taliban ndio waliyoiangusha helikopta hiyo kwa kombora.

Pia Mujahid alibainisha kuwa wanamgambo wanane wa Taliban waliuliwa wakati wa shambulio hilo.


source nifahamishe

Mwanamke Mwenye Matumbo Mawili ya Uzazi Azaa Mapacha wa Mimba Mbili Tofauti

Wednesday, August 10, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Madaktari wanasema kwamba hali kama hii humtokea mwanamke mmoja tu katika wanawake milioni 50 lakini pamoja na uwezekano huo mdogo sana mwanamke mmoja nchini India aliyekuwa na matumbo mawili ya uzazi alipata mimba mbili kwa wakati tofauti na amejifungua watoto wawili mapacha kwa wakati mmoja.
NewsImages/5874618.jpgRinku Devi alikuwa akijua kuwa ana mimba ya watoto mapacha lakini alikuwa hajui kwamba alikuwa ana matumbo mawili ya uzazi na watoto wake mapacha walikuwa katika matumbo tofauti kutokana na ujauzito ulioingia kwa nyakati tofauti.

Madaktari waliielezea hali aliyo nayo Rinku kuwa inajulikana kama kama "uterus didelphys" au "double uterus" na hutokea kwa mwanamke mmoja tu kati ya wanawake milioni 50.

Rinku ambaye ni mke wa afisa wa jeshi, alijifungua watoto wake mapacha kwenye hospitali iliyopo kaskazini mwa India kwenye mji wa Patna.

Hali aliyokuwa nayo Rinku iligundulika wakati Rinku alipoingia leba baada ya kuzidiwa na uchungu wa uzazi.

Madaktari waligundua kuwa Rinku alikuwa na ujauzito wa watoto mapacha ambao ujauzito wao ulipishana kwa mwezi mmoja.

"Niligundua kuwa nina matumbo mawili ya uzazi wakati nilipokuwa kwenye uchungu wa leba", alisema Rinku mwenye umri wa miaka 28.

Rinku aliwahi kujifungua mtoto wa kiume miaka minne iliyopita na hakukumbana na tatizo lolote.

"Sikujua cha kufanya, nilikuwa kwenye maumivu makali huku nikiogopa, sijawahi kusikia kitu kama hichi", aliendelea kusema Rinku.

Rinku alijifungua watoto wake mapacha kwa njia ya upasuaji kabla ya watoto hao kutimiza miezi tisa. Watoto hao walikuwa na uzito wa kilo mbili na kilo 1.5.

"Kutoka na ripoti za hospitali nilijua alikuwa na mimba ya watoto mapacha lakini nilipogundua ana matumbo mawili tofauti ya uzazi nilishtuka sana, sikuwahi kukutana na hali kama hii", alisema daktari wa Rinku.

Mimba kama hizi huwa ni hatari kwa maisha ya mama na mtoto, huwa kuna uwezekano mkubwa wa mimba kuharibika au watoto kuzaliwa kabla ya muda wao au watoto kuzaliwa wakiwa na uzito mdogo sana, alisema daktari huyo.


source nifahamishe