Mfungwa Juan Ramirez Tijerina akiwa amejificha ndani ya begi akijaribu kutoroka jela Tuesday, July 05, 2011 6:54 PM
Mwanamke mmoja wa nchini Mexico ameingia matatani baada ya jaribio lake la kumtorosha mumewe toka jela kwa kumdumbukiza ndani ya begi na kisha kujaribu kulikokota begi hilo kutokana nalo nje ya jela.
Maafisa jela katika jela ya Chetumal nchini Mexico jana walipigwa na bumbuwazi baada ya kumkamata mwanamke akijaribu kumtorosha mumewe toka jela kwa kumficha ndani ya begi.
Walinzi wa jela hiyo walimuona Maria del Mar Arjona mwenye umri wa miaka 19, akionekana mwenye wasiwasi wakati akitoka nje ya jela huku akilikokota begi ambalo lilionekana limetuna sana.
Walipomsimamisha na kulichunguza begi hilo hawakuamini macho yao walipomuona mfungwa Juan Ramirez Tijerina akiwa amejikunja kama vile mtoto akiwa tumboni mwa mama yake.
Maria aliingia na begi hilo jela wakati alipopewa nafasi ya kumtembelea Juan ambaye anatumikia kifungo chake ndani ya jela hiyo.
Juan alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 20 jela baada ya kutupwa jela mwaka 2007 alipopatikana na hatia ya kumiliki silaha kinyume cha sheria.
Maria alitiwa mbaroni wakati akisubiri kufikishwa mahakamani.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili na Vitambulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana,(kulia) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Sei Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili na Vitambulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana,(kulia) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Sei Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho