MZEE WA MIAKA 100 AELEZEA SIRI YA MAZOEZI YAKE

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtu huyo, Georgina Easter, amesema siri kubwa ni kula chakula chenye lishe kamili.

"Siri yenyewe ni kuachana na vyakula ambavyo havijengi chochote mwilini,” alisema mwanamke huyo kutoka Chaddesden, Derby, Uingereza.

"Isitoshe huwa ninafanya kazi kwenye bustani yangu, napika chakula changu kila siku. Pia napenda kula maini yaliyokaangwa na vitunguu.”

Mwanamke huyo alizaliwa wakati Mfalme Edward wa Saba wa Uingereza alikuwa anashikilia taji na wakati ambapo ujenzi wa meli maarufu ya Titanic ulikuwa umefikia nusu.

Easter amewazidi kwa wastani wa miaka 30 wenzake ambao anafanya nao mazoezi ya kujiweka katika afya njema.

Freda Notley, 64, mmoja wa watu wanaofanya mazoezi na Georgina, anasema ni vigumu kuamini uwezo ambao bado anao katika mazoezi bibi huyo.

Mfanya mazoezi mwingine, Jean Bell, 71, anamsifia Georgina kwa ukakamavu wake ikiwa ni pamoja na kufanya shughuli zingine nyumbani kwake.

source.globalpublisher

SENEGAL YAWAKARIBISHA WATU WA HAITI

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais Abdoulaye Wade alisema watu wa Haiti ni wana wa Afrika kwani Haiti ilianzishwa na watumwa waliochukuliwa kutoka Afrika na baadhi wakiaminika kutoka Senegal.

“Rais anatoa fursa hiyo kwa watu wa Haiti watakaokubali kwa hiari yao kurejea katika shina lao,” alisema msemaji wa rais, Mamadou Bemba Ndiaye.

Jumanne iliyopita makumi ya maelfu ya watu waliuawa na wengine kukosa makazi baada ya nchi hiyo kukumbwa na tetemeko la ardhi.

Majengo yameteketea na utoaji wa misaada unakwenda taratibu mno huku watu wakiondoka katika mji mkuu wa nchi hiyo, Port-au-Prince, ambao umeharibiwa vibaya.

“Senegal iko tayari kuwapatia ardhi na hata maeneo makubwa zaidi. Hii itategemea ni watu wangapi wa Haiti watakaoamua kuja,” alisema Ndiaye.

source.globalpublish

Tolu wa Dunia Alipokutana na Mtu Mfupi wa Dunia

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtu mrefu kuliko wote duniani na mtu mfupi kuliko wote duniani kwa mara ya kwanza walifanikiwa kukutana mbele ya waandishi wa habari nchini Uturuki.
Wanaume hao wawili wanaoshikilia rekodi za dunia za kitabu cha Guinness, walikutana kwa mara ya kwanza katika ufunguzi wa mashindano ya wazi ya kuvunja rekodi za dunia yaliyofunguliwa nchini Uturuki.

Mturuki Sultan Kosen mwenye umri wa miaka 27 ambaye kwa urefu wake wa mita 2.46 ndiye mtu mrefu kuliko wote duniani alikutana na Mchina He Pingping mwenye umri wa miaka 21 ambaye yeye urefu wake ni sentimeta 74 tu.

"Nilikuwa nikisubiria kwa hamu kukutana na Pingping tangia nilipotambulishwa rasmi kama mtu mrefu kuliko wote duniani, nimefurahi amkuja Uturuki kwenye ufunguzi wa mashindano haya ya Guinness World Records Live,", alisema Kosen.

"Nasubiria kwa hamu kumtembeza auone mji wetu mzuri wa Istanbul".

Mashindano ya The Guinness World Records live yanafanyika katika shopping Mall kubwa kuliko yote barani ulaya la "Forum Istanbul" ambapo wakazi wa Istanbul wanapewa nafasi ya kujitokeza na kujaribu kuandika majina yao kwenye rekodi za dunia.

Baada ya wiki sita katika jiji la Istanbul, mashindano hayo yatahamishiwa katika miji mingine saba ya Uturuki.

Pingping toka China ufupi wake unatokana na ugonjwa unaojulikana kama "Primordial Dwarfism" ambapo kwa mujibu wa baba yake alipozaliwa alikuwa na umbile dogo sana kiasi cha kujaa kwenye viganja vya baba yake.

Kosen kwa upande wake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa pituitary gigantism ambapo alikuwa na uvimbe uliomsababishia aendelee kukua muda wote, Baada ya operesheni kadhaa za kuuondoa uvimbe huo, Kosen aliacha kukua mwaka 2008.

Mbali ya rekodi ya kuwa mtu mrefu kuliko wote duniani, Kosen pia anashikilia rekodi ya dunia ya kuwa na mikono na miguu mikubwa kuliko watu wote duniani.

Chini ni VIDEO na Picha za tukio la kukutana kwa Tolu wa dunia na mtu mfupi kuliko wote duniani.


source nifahamishe

Hali ilivyo Nchini Haiti ni Mfano wa Jahanamu

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Hali iliyopo nchini Haiti baada ya tetemeko kubwa la ardhi inatisha sana hakuna tena utawala wa sheria mwenye nguvu anamuonea mnyonge ili apate chochote cha kukaganga njaa, maiti zimezagaa kila kona kiasi cha kwamba zinatumiwa kama vizuizi vya barabarani.
Jinsi siku zinavyozidi kwenda mbele mamia ya watu wanazidi kufariki kutokana na njaa na maradhi mbali mbali huku maelfu ya watu wakiwa wamezikwa hai chini ya vifusi vya majengo yaliyoporomoka kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililotokea nchini Haiti.

Tetemeko hilo la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 limeuharibu kwa asilimia 90 mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince.

Majengo mengi sana likiwemo jengo la ikulu na jengo la Umoja wa mataifa nchini Haiti yameporomoka na kuwafukia maelfu ya watu.

Hadi sasa jumla ya watu 50,000 wameishatibitishwa kufariki na idadi kamili ya watu waliofariki inakisiwa kuwa zaidi ya watu 200,000.

Maiti zimezagaa kila kona kiasi cha kwamba watu ambao walishindwa kupata msaada ulioletwa na mataifa ya nje waliamua kuzikusanya maiti na kuzijaza barabarani kuonyesha hasira zao.

Wezi nao wameongezeka kila kona, mwizi mmoja ambaye alikamatwa akimuibia mmoja wa wahanga wa tetemeko hilo la ardhi aliuliwa na kisha maiti yake kuburuzwa barabarani kabla ya kuchomwa moto.

Kwa hali iliyopo sasa nchini Haiti, kila mtu anajiangalia mwenyewe. Watu wenye nguvu wamekuwa wakitumia silaha zao kama vile visu na silaha nyinginezo kuwatishia watu wengine ili waweze kuwanyang'anya mali zao.

Misaada toka mataifa mbali mbali duniani imesaidia kuokoa maisha ya baadhi ya watu lakini bado haitoshi na haijawafikia watu wengi kutokana na kuharibika kwa njia zote za mawasiliano.

Hospitali zote zimefurika wagonjwa na maiti zimezagaa pia kila kona kiasi cha kwamba zimekuwa zikikusanywa na kulundikwa pamoja maiti za wanyama vile.

source nifahamishe

Mtoto wa Miaka 11 Aruhusiwa Kuendesha Gari, Aitekeza Familia Yake

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto mwenye umri wa miaka 11 wa nchini Marekani ambaye aliruhusiwa kuendesha gari na wazazi wake, alisababisha ajali iliyosababisha kifo chake, mama yake na dada yake.
Polisi nchini Marekani wanafanya uchunguzi kujua ni kwanini mtoto wa kiume Jose Manuel Silva Covarrubias mwenye umri wa miaka 11 aliruhisiwa kuendesha gari lililopata ajali baada ya dereva hiyo mtoto kushindwa kusimama kwenye mataa.

Gari lililokuwa likiendeswa na mtoto Jose likiwa limembeba mama yake, dada yake na mwanaume mwingine mwenye umri wa miaka 34 liligongwa na gari jingine aina ya Ford baada ya kukatiza kwenye mataa huku taa nyekundu zikiwa zimewaka.

Polisi wanachunguza ilikuwaje Jose aliruhusiwa kuendesha gari aina ya Honda na kupelekea kutokea kwa ajali hiyo katika kitongoji cha Porterville, California.

Polisi wanatarajia kumhoji mtu pekee aliyenusurika katika ajali hiyo rafiki wa familia hiyo, Froylon Gonzalez mwenye umri wa miaka 34 aliyekuwa amekaa siti ya pembeni ya dereva huyo mtoto.

Gonzalez alinusurika kwakuwa alikuwa amevaa mkanda wakati mama wa mtoto huyo Maria Covarrubias, 30 na dada wa mtoto huyo Elizabeth Silva Covarrubias,6, walifariki baada ya kurushwa toka siti za nyuma kwakuwa hawakuwa wamevaa mkanda.

Kaka wa majeruhi aliyenusurika maisha yake alisema kuwa familia hiyo ilikuwa ikitoka kwenye mazoezi ya soka ya Jose na pia alisema kuwa hakuwahi kumuona Jose akiendesha gari kabla ya siku ya ajali hiyo.

source.nifahamishe

Mchezaji Mweusi wa Marekani Abadili Rangi ya Ngozi Yake

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mmarekani mweusi Sammy Sosa ambaye aliwika sana enzi zake kwenye mchezo wa Baseball amebadili rangi ya ngozi yake kutoka nyeusi kuwa nyeupe kama mzungu.
Mchezaji maarufu wa zamani wa Baseball, Sammy Sosa mwenye umri wa miaka 41 amejibadilisha rangi ya ngozi yake kuwa mweupe kama mzungu kwa kutumia krimu za kujichubua.

Sosa alianza kujichubua kuanzia mwaka 2007 na wiki iliyopita alionekana kwenye tuzo za Latin Grammy jijini Las Vegas akiwa hana tena rangi yake nyeusi ya kuonyesha asili yake ya Afrika.

Sosa alionekana mweupe kama mzungu na kwa watu ambao hawamfahamu ni vigumu kuamini alikuwa mweusi 'tii' zamani.

Sosa amesema kuwa nia yake kubadili rangi ya ngozi yake ni kutokana na mapenzi yake mwenyewe na si kumuiga marehemu mfalme wa muziki wa Pop, Michael Jackson.

Sosa amekiri pia kubadilika kwa rangi hakutokani na maradhi yoyote ya ngozi bali ni kutokana na krimu anayoitumia ambayo alisema ataipigia kampeni za kibiashara.

Hivi karibuni idadi ya watu weusi wanaojichubua nchini Marekani ili wakubalike katika soko la wazungu imezidi kuongezeka na wataalamu wa ngozi wanaonya kuwa matumizi ya krimu kujichubua ni hatari kwa afya.

Magonjwa mengi ya ngozi kama vile kansa ya ngozi yamekuwa yakihusishwa na madawa na krimu za kujichubua.

source.nifahamishe

Aibu Yamkumba Mkaguzi wa Silaha wa Umoja wa Mataifa

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mkaguzi wa silaha wa zamani wa Umoja wa Mataifa aliyepewa madaraka wakati huo kuzikagua silaha za aliyekuwa rais wa Iraq, Saddam Hussein amekumbwa na fedheha kubwa ya ngono za watoto ambapo alijipigisha punyeto mbele ya msichana wa miaka 15 na huenda akatupwa jela miaka saba.
Mpelelezi Scott Ritter mwenye umri wa miaka 48 ambaye alikuwa mkaguzi wa silaha wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq kabla ya kujiuzulu mwaka 1998, anakabiliwa na mashtaka ya ngono za watoto baada ya kunaswa akimtongoza msichana mwenye umri wa miaka 15.

Ritter ambaye anaishi na mkewe, bila kufahamu kuwa alikuwa akichunguzwa kuhusiana na ngono za watoto, alikuwa akiwasiliana kwa njia ya internet na msichana aliyejitambulisha kwa jina la Emily mwenye umri wa miaka 15.

Ukweli ni kwamba Emily hakuwa msichana mwenye umri wa miaka 15 bali ni afisa wa polisi Ryan Venneman aliyekuwa akimchunguza Ritter kuhusiana na ngono za watoto kwenye internet.

Ritter alianza kumwagia sera zake Emily kuanzia mwezi februari mwaka jana akitaka kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi.

Katika kipindi cha miezi tisa bila kufahamu kuwa anachunguzwa, Ritter aliendea kumwaga sera zake na kuna wakati alidiriki hata kujipigisha punyeto live huku akijionyesha kwa kutumia webcam.

Jina la Ritter lilisikika sana wakati wa utawala wa rais George Bush alipotakiwa kukagua silaha za sumu nchini Iraq ambazo mpaka Saddam Hussein ananyongwa mwaka 2006 zilikuwa bado hazijapatikana.

Ritter alishawahi kuingia matatani kwa kosa kama hili la kujihusisha na ngono za watoto mwaka 2001 lakini kesi yake ilifutwa baada ya kukosekana ushahidi wa kutosha.

Safari hii maafisa wa polisi wamesema kuwa wana ushahidi wa meseji za simu na webcam kumtia hatiani Ritter.

Ritter amefunguliwa kesi mjini Pennsylvania na kesi yake itaanza kusikilizwa mwezi machi. Iwapo atapatikana na hatia anaweza kutupwa jela miaka saba.

source.nifahamishe