Watoto Wafariki Wakati Baba na Mama Wakiangalia Kombe la Dunia

Wednesday, June 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Watoto wawili wamefariki dunia nchini Uganda kutokana na moto ulioitekeza nyumba yao wakati wazazi wao walipoenda kwa jirani mwenye televisheni kuangalia kombe la dunia.
Polisi mjini Kampala nchini Uganda wamesema kuwa watoto wawili wamefariki kutokana na moto ulioitekeza nyumba yao wakati wazazi wao walipoenda kuangalia mechi ya kombe la dunia.

Polisi nchini Uganda wamewaonya wazazi kutowaacha watoto wao peke yao ndani ya nyumba wakati wanapoenda kuangalia mechi za kombe la dunia.

Watoto wawili wenye umri wa miaka 8 na 10 walifariki kwa moto katika wilaya ya Kayunga iliyopo magharibi mwa mji wa Kampala.

Afisa wa polisi wa Kayunga, Henry Kolyanga alisema kuwa watoto hao walifariki wakati nyumba waliyokuwa wamelala iliposhika moto.

"Mama na Baba wa watoto hao waliacha mshumaa ukiwaka ndani ya nyumba na walienda kuangalia mechi ya kombe la dunia kwa jirani mwenye televisheni", alisema afisa huyo wa polisi.

"Inasemekana kuwa panya aliugonga mshumaa na mshumaa huo uliangukia kwenye meza na kukiunguza kitambaa cha mezani na kusababisha moto mkubwa ulioitekeza nyumba yote", alimalizia kusema afisa huyo wa polisi.


source nifahamishe

Miaka 10 Jela Kwa Kumuua Dada Yake Aliyepata Mimba Nje ya Ndoa

Tuesday, June 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mahakama nchini Jordan imemuondolea adhabu ya kifo aliyohukumiwa mwanaume aliyemuua dada yake baada ya kugundua amepata mimba kabla ya kuolewa. Mahakama imeamuru mwanaume huyo atumikie kifungo cha miaka 10 jela.
Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 24 alimuua dada yake mwenye umri wa miaka 26 kwa kumchomachoma na kisu tumboni mara 15 baada ya kugundua dada yake huyo amepata ujauzito kabla ya kuolewa.

Awali mahakama ya mjini Amman, Jordan iliamuru mwanaume huyo ahukumiwe adhabu ya kifo lakini jana mahakama iliamuru mwanaume huyo atumikie kifungo cha miaka 10 jela baada ya familia yake kumuombea msamaha mahakamani.

"Alimuua dada yake baada ya dada yake huyo kumwambia kuwa alifanya mapenzi na mwanaume ambaye alisafiri kwenda kufanya kazi nchini Saudi Arabia", alisema afisa wa mahakama ambaye hakutaka kutaja jina lake.

Taarifa ya mahakama ilisema kuwa mauaji hayo yalifanyika mwaka jana katika mji wa Karak wakati huo dada yake alikuwa na mimba ya wiki nne.

Kwa mujibu wa sheria za Jordan, mtu anayeua naye huuliwa lakini kwa mauaji yanayoitwa "Kulinda Heshima ya Familia" adhabu ya kifo huondolewa iwapo familia ya mwanamke aliyeuliwa itaiomba mahakama ipunguze adhabu kwa muuaji.

Wanawake 15 hadi 20 huuliwa kila mwaka nchini Jordan kwa staili hiyo hiyo ya kulinda heshima za familia ingawa serikali ya Jordan inafanya jitihada ya kuiondoa tamaduni hiyo potofu.

source nifahamishe

Marekani Yagundua Hazina ya Utajiri Afghanistan

Tuesday, June 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Marekani imegundua hazina ya madini yenye thamani kubwa nchini Afghanistan ambayo yanakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola trilioni moja.
Msemaji wa Pentagon alisema kuwa utafiti wa wataalamu wa madini wa Marekani umeonyesha kuwa nchini Afghanistan kuna kiasi kikubwa sana cha madini ya thamani tofauti na ilivyokuwa ikijulikana awali.

Thamani ya madini kama vile niobium, lithium, chuma, dhahabu na kobalti ambayo yanapatikana kwa kiasi kikubwa nchini Afghanistan ni zaidi ya dola trilioni moja.

Maafisa wa Marekani waliliambia gazeti la New York Times la Marekani kuwa hazina ya madini yaliyopatikana nchini Afghanistan yanatosha kuubadilisha uchumi wa Afghanistan na kuigeuza Afghanistan kuwa mojawapo ya nchi zinazoongoza kwa uzalishaji wa madini duniani.

Rais wa Afghanistan, Hamid Karzai alisema mwanzoni mwa mwaka huu kuwa kiasi kikubwa cha madini kilichogunduliwa nchini humo kitaifanya Afghanistan itoke kwenye umaskini iwe miongoni mwa nchi tajiri duniani.

Aozeshwa Ng'ombe Aliyembaka, Azimia Wakati wa Harusi

Tuesday, June 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kijana mmoja wa nchini Indonesia ambaye alilazimishwa kumuoa ng'ombe aliyembaka, alizimia wakati wa harusi yake na ng'ombe huyo.
Kijana Ngurah Alit mwenye umri wa miaka 18 alikamatwa kwenye kijiji chake cha Yeh Embang katika kisiwa cha Bali nchini Indonesia, akiwa uchi wa mnyama akifanya mapenzi na ng'ombe.

Alit alijitetea kuwa ng'ombe huyo ndiye aliyemtongoza yeye na kumvutia kufanya naye mapenzi.

Alit alidai kuwa aliamini kuwa ng'ombe huyo alikuwa ni msichana mrembo ambaye alikuwa akimfanyia mitego mbalimbali ili afanye naye mapenzi.

Pamoja na utetezi wake, Alit alilazimishwa amuoe ng'ombe huyo na harusi ya kitamaduni iliandaliwa.

Wakati polisi wakiwaweka waandishi wa habari mbali na eneo la harusi, Alit alizimia kabla ya kukabidhiwa rasmi 'mke' wake.

Hata hivyo Alit aligeuka mjane punde baada ya harusi baada ya bi harusi wake kuzamishwa kwenye bahari kama mojawapo ya imani za kijiji hicho.

Ili kusafishika na kitendo chake, Alit aliogeshwa kwenye ufukwe wa bahari.

Mkuu wa kijiji hicho alisema baada ya harusi hiyo kuwa kijiji sasa kimesafishika baada ya tukio hilo lililoleta aibu kwenye kijiji.


source nifahamishe

Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo

Tuesday, June 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Utafiti uliofanywa kwa miaka 50 ukiwashirikisha watu milioni 3 umeonyesha ufupi ni tatizo na watu wafupi wako kwenye hatari ya kufariki kwa magonjwa ya moyo kulinganisha na watu warefu.
Baada ya miaka 50 ya utafiti wanasayansi wamegundua kuwa ufupi wa mtu ni mojawapo ya sababu zinazochangia watu kupata magonjwa ya moyo.

Utafiti huo ulionyesha kuwa watu wafupi wako kwenye hatari ya asilimia 50 zaidi ya watu warefu kupata magonjwa ya moyo.

Kwa wastani mtu alihesabika mfupi akiwa na urefu wa sentimeta 160.5 wakati mtu alihesabika mrefu alipokuwa na urefu wa sentimeta 173.9.

Utafiti huo ulionyesha usahihi kwa jinsia zote za kike na kiume ingawa kipimo cha urefu wa mwanaume na mwanamke kilikuwa tofauti.

Wanaume wafupi walitajwa kuwa na urefu chini ya sentimeta 165.4 wakati wanaume warefu walikuwa na urefu kuanzia sentimeta 177.5.

Wanawake wafupi walihesabika kuwa na urefu chini ya sentimeta 153 wakati wanawake warefu walikuwa na urefu wa sentimeta 166.4.

Kwa kuwa watu wafupi huwa na mishipa midogo ya damu ya coronary artery, hali hiyo huchangia kuwafanya wawe kwenye nafasi kubwa ya kukumbwa na matatizo ya msukumo wa damu mwilini.

Matokeo ya utafiti huu yalitolewa kwenye jarida la European Heart Journal baada ya kuwashirikisha jumla ya watu milioni 3.

Dr Tuula Paajanen, wa chuo kikuu cha Tampere nchini Finland, aliyeongoza utafiti huo alisema kuwa kwa miaka mingi kumekuwa na mjadala mrefu kuhusiana na urefu wa mtu kuwa mojawapo ya sababu za kupata magonjwa ya moyo.

Dr Paajanen alisema kuwa matokeo ya utafiti huu yanaonyesha kuwa ufupi wa mtu ni sababu inayojitegemea ya mtu kupata magonjwa ya moyo.

Dr Paajanen alisema kuwa mbali ya unene, uzee na kiwango kikubwa cha kolestro, ufupi nao inabidi uongezwe katika sababu zinazochangia matatizo ya moyo.


source nifahamishe

Imamu Mwanamke Anapowasalisha Wanaume

Sunday, June 13, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Mwanamama wa Kanada Raheel Raza kama ilivyotarajiwa jana aliweka rekodi kwa kuwa mwanamke wa kwanza wa kiislamu nchini Uingereza kusalisha sala ya ijumaa. Raheel aliwaambia waumini waliokuwepo msikitini kuwa si dhambi katika uislamu mwanamke kusalisha wanaume.
Mwandishi wa habari wa Kanada ambaye pia mwanaharakati wa kupigania usawa wa kijinsia katika dini ya kiislamu, Raheel Raza jana aliweka rekodi ya kuwa imamu mwanamke wa kwanza nchini Uingereza.

"Nilikuwa mwanamke wa kwanza kuwa imamu nchini Kanada, mwanamke kusalisha wanaume si dhambi, hata mtume wetu ametoa ruhusa ingawa baadhi ya maimamu wanakubali na wengine wanaona si sahihi ni makosa", alisema Rahel.

"Mimi kabla ya kutoa uamuzi wangu nilifanya utafiti na nimegundua kuwa ni sahihi na hamna kosa lolote".

"Nimetumiwa email nyingi za vitisho vya kuuliwa ili nisirudie tena kuwa imamu, hata hivyo mimi uimamu sio kazi yangu, nimekuja hapa baada ya kuitwa na watu", alisema Rahel.

Naye kiongozi wa kituo cha waislamu cha Oxford, Dr. Taj Hargey, ambaye ndiye aliyemualika Rahel kuja kusalisha katika kituo chao, alisema kuwa wanawake kuongoza misikiti si suala la kujadili.

"Hakuna aya katika Quran inayokataza wanawake kusalisha au kuongoza misikiti, katika uislamu wanaume na wanawake ni sawa. Kama katika misikiti hakuna usawa wa jinsia basi katika jamii pia hakutakuwa na usawa", alisema.

"Huenda ikawa ni vigumu kuwa na imamu mwanamke nchini Saudi Arabia au Pakistan lakini haimanishi kuwa ni makosa kuwepo sehemu zingine", aliongeza Dr. Taj Hargey.

Dr. Taj Hargey alisema kuwa sala ya jana haikukumbana na vipingamizi vyovyote hivyo inamaanisha kuwa watu wanaanza kuelewa na kukubali taratibu taratibu.

"Inabidi turudie kufanya hivi mara nyingi ili watu wazoee", alisema Dr. Taj Hargey

source nifahamishe

Hatimaye Sio Mungu Tena..

Sunday, June 13, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto aliyezaliwa nchini India akiwa na mikono minne na miguu minne ambaye alikuwa akiabudiwa kama mungu amepoteza uungu wake baada ya kufanyiwa operesheni kuondoa mikono na miguu iliyozidi.
Deepak Paswan, 7, alizaliwa katika sehemu za watu masikini nchini India akiwa ameungana na pacha wake kwenye tumbo. Alikuwa na miguu minne na mikono minne lakini kichwa kimoja.

Waumini wa dini ya Hindu katika kijiji chake kilichopo kwenye jimbo la Bihar walikuwa wakimtembelea nyumbani kwake wakimuabudu kama Mungu wa Kihindu anayeitwa Vishnu.

Familia yake haikufurahia jinsi mamia ya watu walivyokuwa wakienda nyumbani kwao kwaajili ya kumuabudu mtoto huyo na waliomba msaada kwa watu ili mtoto huyo afanyiwe upasuaji.

Hatimaye maombi yao yalikubaliwa mei 30 mwaka huu na hospitali moja katika mji wa Bangalore ilikubali kulipa gharama zote za kumfanyia operesheni mtoto huyo.

Baada ya operesheni ngumu ya masaa manne, madaktari walifanikiwa kuondoa viungo vilivyozidi toka kwenye mwili wa mtoto huyo.

Deepak akitambulishwa mbele ya waandishi wa habari, alionekana kufurahia hali yake mpya ambayo imempotezea sifa yake ya uungu ambayo waumini wa Hindu walimpa.

"Siku zote tulitaka afanyiwe operesheni ili atenganishwe na pacha wake aliyejiunga tumboni mwake ili kuepuka watu kumfanya mtoto wetu chombo cha ibada", alisema baba wa mtoto huyo Viresh Paswan.

"Hatimaye ndoto yangu imetimia sasa tutafanya sherehe tutakaporudi kijijini kwetu", alisema Paswan.

source nifahamishe