Mashindano ya Maimamu 'Imamu star' Yaanza Malaysia

Saturday, June 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kuna mashindano mengi yameibuka duniani kutafuta vipaji kama vile Pop Star, Bongo Star Search na mengineyo lakini huko nchini Malaysia yameanza mashindano ya aina yake kutafuta imamu bora.
aada ya mashindano ya Popstar, American Idol, The X Factor na mengineyo kuibuka sehemu mbalimbali duniani, mashindano ya kwanza ya aina yake yameanza nchini Malaysia yakienda kwa jina la "Imam Star".

Mashindano hayo ambayo nchini Malaysia yanajulikana kwa jina la "Imam Muda", yanawashindanisha vijana wa kiislamu ili kumpata imamu bora kati yao.

Vijana wenye umri kati ya miaka 19-27 wamewekwa nyumba moja ambapo kwa kipindi cha miezi mitatu na watakuwa wakishindana kumpata imamu bora kati yao.

Vijana hao watashindana kusoma azana, kusalisha, kutoa khutba, kuosha maiti na kuongoza mazishi.

Maiti zitakazotumika katika mashindano hayo ni maiti zilizopo monchwari ambazo hazijatambuliwa na ndugu zao.

Mshindi wa mashindano hayo hatapewa zawadi ya pesa kama yalivyo mashindano mengine. Atapewa schorlaship ya kusoma mambo ya dini katika chuo kikuu cha al-Madinah University cha nchini Saudi Arabia. Mshindi pia atapewa kazi ya kusalisha misikiti mikubwa ya mjini Kuala Lumpur na pia atakuwa akilipiwa gharama zote za kuhiji Makka.

Mashindano hayo yamekuwa gumzo nchini Malaysia yakivunja rekodi ya watazamaji. Yamebakiza mwezi mmoja kuisha.

source nifahamishe

'Michael Jackson Asingefariki Kama Angekuwa Muislamu'

Thursday, June 24, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Katika kuadhimisha mwaka mmoja tangia alipofariki, kaka yake Michael Jackson, amesema kuwa anaamini kaka yake angekuwa hai hadi leo kama angebadili dini kuwa muislamu.
Akiongea na shirika la habari la Uingereza la BBC katika mahojiano ambayo yatarushwa hewani leo, kaka yake Michael Jackson, Jermaine Jackson amesema kuwa anaamini kaka yake angekuwa hai hadi leo hii kama angefanikiwa kubadili dini kuwa muislamu.

Jermaine alisema kuwa kama Michael angebadili dini kuwa muislamu basi maisha yake yangebadilika na asingekuwa na maisha ambayo yalipelekea kifo chake.

"Naamini kama Michael angekuwa muislamu, angekuwa hai hadi leo, nasema hivi kwasababu nyingi sana", alisema Jermaine ambaye yeye alibadili dini kuwa muislamu miaka mingi sana iliyopita.

"Sababu ni kwamba mtu unapokuwa muislamu na ukafahamu kwa asilimia 100 sababu ya wewe kuwepo duniani na sababu ya watu waliokuzunguka kuwepo duniani, basi maisha hubadilika na kuwa mazuri", alisema Jermaine.

Jermaine aliongeza kuwa alimnunulia Michael vitabu vingi vya kiislamu toka Saudi Arabia na Bahrain.

"Alisoma vitabu vingi vya kiislamu", alisema Jermaine na kuongeza kuwa Michael hakuwa akiupinga uislamu.

"Walinzi wake wote walikuwa waislamu kwa kuwa aliuamini Uislamu, aliwaamini kwakuwa waislamu hujaribu kuwa watu wazuri kadri wawezavyo, si kwaajili ya Michael Jackson bali kwaajili ya Mungu".

"Wakati unapozungukwa na watu kama hawa unajua kwamba Mwenyezimungu atakulinda", alimalizia kusema Jermaine.

Michael Jackson alifariki akiwa na umri wa miaka 50, juni 25 mwaka jana kutokana na shambulizi la moyo lililotokana na matumizi makubwa ya madawa ya kupunguza maumivu.

Washabiki wake wanajiandaa kuadhimisha mwaka mmoja wa kifo chake siku ya ijumaa kwa kufanya shughuli mbalimbali za kukumbuka kazi zake za muziki.

source nifahamishe

Achomwa Kisu Kwa Kulalamikikia Miguno ya Ngono ya Jirani

Thursday, June 24, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanaume mmoja nchini Marekani amechomwa kisu na jirani yake baada ya kulalamikia sauti kali za ngono anazozitoa anapofanya mapenzi na mpenzi wake.
Mwanaume mwenye umri wa miaka 40 aliyejulikana kwa jina la Russell Willis Shepherd Jr. amefunguliwa mashtaka ya kumshambulia jirani yake mwenye umri wa miaka 58 ambaye alikuwa akilalamika miguno ya kimahaba aliyokuwa akiitoa.

Katika tukio hilo lililotokea South Carolina nchini Marekani, jirani wa Russel alirudi nyumbani kwake na kumkuta Russel akitoa sauti kali wakati akifanya mapenzi na mpenzi wake mwenye umri wa miaka 39.

Kuepuka kelele hizo aliamua kwenda nje kuvuta sigara, aliporudi na kukuta kelele hizo zikiwa ndio zimepamba moto, aliamua kumgongea mlango Russel na kumwambia apunguze kelele za ngono anazozitoa.

Russel alikasirishwa na kitendo hicho, alichukua kisu na kuanza kumshambulia jirani yake huyo mpaka alipofanikiwa kuchoropoka na kuomba msaada toka kwa jirani.

Russel almefunguliwa mashtaka ya kufanya shambulizi la kudhuru mwili na ametupwa jela akisubiri kufikishwa mahakamani.

source nifahamishe

Ili Kupinga Obama Kuwa Rais, Alichoma Moto Kanisa la Watu Weusi

Saturday, June 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani anakabiliwa na kifungo cha miezi 108 jela baada ya kukiri kulichoma moto kanisa la watu weusi ili kupinga Barack Obama kuwa rais mweusi wa Marekani.
Benjamin Haskell, 23, wa Massachusetts nchini Marekani amekiri kosa lake la kulichoma moto kanisa la Wamarekani weusi ili kupinga kuchaguliwa kwa Barack Obama kuwa rais wa kwanza mweusi wa Marekani.

Benjamin alikiri jana kulichoma moto kanisa la Macedonia Church of God in Christ mnamo novemba 5 mwaka 2008, ikiwa ni ndani ya masaa machache baada ya Obama kuchaguliwa kuwa rais.

Benjamin alilimwagia petroli kanisa hilo kabla ya kulipiga kiberiti na kuliteketeza.

"Leo tunatoa ujumbe kuwa watu wanaofanya uhalifu kwa sababu za chuki, watachunguzwa na baadae ya kushtakiwa", alisema Carmen Ortiz mwanasheria mkuu wa Massachusetts.

Benjamin huenda akahukumiwa kwenda jela miezi 108 (miaka 9) baada ya kukiri kosa lake la kuhatarisha maisha ya waumini 300 wa kanisa hilo na kuliharibu jengo la kidini kwasababu ya chuki zake ubaguzi wa rangi.

source nifahamishe

Wivu Wapelekea Amchome Moto Mpenzi Wake

Saturday, June 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kutokana na wivu mwanamke mmoja nchini Marekani alimchoma moto mpenzi wake na kisha kujichoma moto na yeye mwenyewe na kutokana na moto huo nyumba ilishika moto na kupelekea vifo vya watu wengine watatu.
Agnes Bermudez, 50, anatuhumiwa kumuua mpenzi wake William Salazar, 32, katika tukio la kutisha lililotokea siku ya akina baba duniani mwaka 2008.

Agnes ambaye hivi sasa kesi yake inaendelea mahakamani, alimchoma moto mpenzi wake huyo na kisha yeye mwenyewe alijipiga kibiriti.

Agnes hakufariki kutokana na moto aliouanzisha lakini aliungua vibaya sura yake kiasi cha kumfanya asitambulike.

Sababu ya Agnes kumchoma moto mpenzi wake ni wivu wa kimapenzi. Agnes alimshutumu Salazar kuwa anatembea na mwanamke mwingine nje.

Video ya tukio hilo imetolewa mahakamani kama ushahidi wa tukio hilo la kusikitisha.

Video inamuonyesha Agnes na Salazar wakitoka nje ya nyumba yao wakikimbilia kwenye duka lililopo chini ya jengo lao.

Salazar anaonekana akikimbia kuingia ndani ya duka akitafuta maji wakati Agnes alilala chini mbele ya duka hilo huku akiungua na moto.

Wasamaria wema walifanikiwa kuwamwagia maji na kuokoa maisha yao hata hivyo Salazar alifariki siku nne baadae hospitalini.

Moto ulioanzishwa na Agnes ulishika pia nyumba zingine zilizopo kwenye jengo hilo na kupelekea vifo vya watu watatu.

Mke Amuua Mume Kwasababu ya Kombe la Dunia

Saturday, June 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Kombe la dunia linaloendelea nchini Afrika Kusini limekuwa sababu ya kifo cha mwanaume mmoja nchini humo ambaye alifariki baada ya kupigwa na mkewe na watoto wake wakati alipolazimisha kuangalia mechi kwenye TV wakati mkewe na watoto wake walitaka kuangalia nyimbo za dini.
David Makoeya mwenye umri wa miaka 61 hakutaka kuikosa mechi ya jumapili iliyopita kati ya Ujerumani na Australia.

Mke wake na watoto wake wao walitaka kuangalia programu ya nyimbo za dini za kikristo kwenye luninga.

Polisi wanasema kuwa Makoeya alikuwa akigombania remote control na familia yake ili aweze kuangalia mechi ya kombe la dunia.

Familia yake walikataa kubadilisha channel ya mambo ya dini waliyokuwa wakiiangalia na hapo ndipo mzozo ulipoanzia.

"Alisema, Hapana nataka kuangalia mpira", msemaji wa polisi Mothemane Malefo alisema.

Huku akiwa na hasira, Makoeya alinyanyuka na kuelekea kwenye TV ili aweze kubadilisha channel lakini hakufika mbali kwani mkewe na watoto wake walianza kumshushia kipigo.

Mke wa Makoeya mwenye umri wa miaka 68, Francina, akishirikiana na mtoto wake wa kiume Collin mwenye umri wa miaka 36 na binti yake Lebogang mwenye umri wa miaka 23 walimshushia kipigo cha nguvu baba yao.

"Inaonekana walikipigiza kichwa chake kwenye ukuta, walipiga simu polisi baada ya kumjeruhi vibaya sana... wakati polisi wanafika eneo la tukio, Makoeya alikuwa ameishafariki", alisema Malefo.

Mke wa Makoeya na wanae ambao wanaishi kwenye kijiji cha Makweya, walitiwa mbaroni jumapili usiku.

Binti yake aliachiwa kwa dhamana ya dola 200 wakati mkewe na mtoto wake wa kiume wanaendelea kunyea debe rumande.

Ndugu wa familia hiyo wamesikitishwa na kifo cha Makoeya wakisema kuwa Makoeya hakuwa mtu mwenye vurugu alikuwa mtulivu na mwenye furaha kwa familia yake.

Kifo cha Makoeya kimetokea ikiwa ni siku chache baada ya watoto wawili kufariki nchini Uganda kutokana na moto baada ya wazazi wao kuwaacha wakiwa wamelala na kwenda kuangalia mechi ya kombe la dunia.

source nifahamishe

Azamia Jela Baada ya Kuona Maisha Magumu Uraiani

Saturday, June 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Msumbiji ambaye alitoka jela kwa msamaha wa rais baada ya kukaa jela miaka mitano, amevunja ukuta wa fensi ya jela na kurudi gerazani baada ya kuona maisha ya uraiani ni magumu.
Camilo Antonio, 28, aliamua kurudi gerezani mwenyewe baada ya kugundua kuwa hayapendi tena maisha ya uraiani.

Camilo alitumikia miaka mitano jela kati ya 10 aliyohukumiwa kwa kumuua baba yake wa kambo, alitolewa jela baada ya kupewa msamaha wa rais.

Camilo ambaye alitumikia kifungo chake katika jela ya Manica iliyopo ukanda wa kati wa Msumbiji, alishindwa kustahamili maisha magumu ya uraiani na kuamua ni bora arudi jela.

Alishindwa kupata kazi na alikuwa na hofu familia ya baba yake wa kambo ingejaribu kumuua.

Camilo aliamua kuvunja sehemu ya ukuta wa jela ili aweze kuingia ndani. Alikamatwa na kushtakiwa kwa uharibifu wa mali za serikali na alihukumiwa kwenda jela mwaka mmoja.

"Kwajinsi ninavyoona jela kwangu ni sehemu salama kuliko sehemu zote", alisema Camilo kuliambia gazeti la Noticias la nchini Msumbiji.

"Sitaki kuishi jela maisha yangu yote lakini kwa wakati huu jela ni bora kuliko sehemu yoyote ile", alimalizia kusema Camilo.