Chris Brown Adaiwa Kujiliza Jukwaani

Tuesday, June 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Nyota wa muziki wa Pop wa Marekani, Chris Brown aliangua kilio jukwaani wakati wa shoo ya kumkumbuka mfalme wa muziki wa Pop, Michael Jackson.
Akipanda jukwaani kufanya shoo yake ya kwanza kubwa baada ya kuingia matatani kwa kumpiga mpenzi wake zamani, Rihanna, Chris Brown aliangua kilio jukwaani wakati akiimba nyimbo ya Michael Jackson.

Brown alipanda jukwaani kufanya shoo ya kumuenzi Michael Jackson wakati wa tamasha la kutoa tuzo za muziki za Black Entertainment Television.

Brown alianza kwa kuwachengua watazamaji kwa shoo ya dansi akiigiza staili mbalimbali za Michael Jackson.

Alipoanza kuimba wimbo wa Michael Jackson "Man In The Mirror" uliotamba sana mwaka 1988, Chris Brown alianza kuangua kilio jukwaani na kushindwa kuendelea kuimba hali iliyopelekea watu waliohudhuria shoo hiyo kuungana naye kuimba nyimbo hiyo.

Pamoja na hisia alizozionyesha jukwaani kuhusiana na kifo cha Michael Jackson, Chris Brown amekumbwa na tuhuma kuwa alizuga kujiliza jukwaani ili watu waanze kumsapoti tena baada ya kashfa ya kumpiga Rihanna mwaka jana.

Chris Brown kutokana na kumpiga Rihanna alipoteza washabiki wengi na baadhi ya wadhamini wake na alihukumiwa kufanya kazi za kuitumikia jamii kwa miezi sita.

Maoni mengi katika tovuti ya MTV.com yalimponda Chris Brown kwa kuonyesha hisia za uongo ili kupata huruma za watu.

Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kama hisia za Chris Brown zilikuwa za kweli au la.


source nifahamishe

Baada ya uthibitisho akabidhiwa mtoto

Tuesday, June 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

HOSPITALI ya Wilaya ya Ilala Amana ya Dar es Salaam, imemkabidhi Martin [35] mtoto Alphonce Martin aliyekuwa akilelewa hapo kwa takribani siku 11 baada ya uthibitisho wa kina kuwa ni mwanae halali
Martin Melicyori mkazi wa Pugu Kinyamwezi, akifuatana na ndugu zake aliweza kukabidhiwa mtoto huyo kwa kuwasilisha barua ya Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa anapoishi kuthibitisha kuwa ni mwanae na kufafanua maswali aliyopewa hospitalini hapo.

Mbali na kuwasilisha maelezo hayo pia aliweza kutoa ushahidi mwengine mbalimbali ikiwemo picha mbalimbali na kufafanua vizuri maswali aliyokuwa akihojiwa.

Martin alidai kwa kweli hakuwa na habari kabisa kama mkewe alifikishwa hospitalini hapo kwa kuwa siku ya mwisho mkewe alimuaga kwenda kutafuta huduma za uzazi wa mpango akiwa na jirani yake.

Alisema kuwa majira ya jioni jirani yake huyo alifika nyumbani kwake na kumuulizia mke wake kama alikuwa amerudi na kumshanga kwa kuwa waliondoka wote na kutoa taarifa kituo cha polisi.

Alisema alijitahidi kufika hospitali mbalimbali hadi Muhimbili na kuambiwa hakuna jina la la mgonjwa kama huyo na hadi juzi walipoona taarifa hiyo kwenye gazeti.

KAtika maelezo yake alisema kuwa Alphonce ni motto wake wa tatu kuzaliwa kati ya watoto watatu ikiwa ni pamoja na Sweet (9) na Samson (4.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dk. Meshark Shimwela, baada ya kuridhika na maelezo hayo pia ndugu hao waliruhusiwa kuja kuchukua mwili wa marehemu ambao ulikuwa umehifadhiwa hospitalini hapo ilipowasiliana na uongozi wa hospitali hiyo ulidai kuwa mwili huo utachukuliwa leo kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika Tabata.

11 Wafariki Wakiangalia Kombe la Dunia

Tuesday, June 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Watu 11 wamefariki nchini Senegal na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya jengo walilojazana kuangalia mpira kuporomoka.
Polisi nchini Senegal wamesema kuwa watu 11 wamefariki dunia wakiangalia mechi ya kombe la dunia wakati jengo walilokuwemo lilipobomoka na kuwafunika.

Kundi kubwa la watu lilikusanyika kwenye nyumba ya mkuu wa kampuni ya umeme katika mji wa Matam kaskazini mwa Senegal ili kuangalia mechi ya kombe la dunia.

Polisi walisema kuwa jengo hilo lilibomoka wakati wakati wa mechi ya jumamosi mchana kati ya Uruguay na Korea.

Senegal haikufanikiwa kufuzu kushiriki fainali za kombe la dunia lakini fainali za kombe za dunia zinazoendelea nchini Afrika Kusini zimekuwa zikifuatiliwa kwa ukaribu sana nchini humo.

Mamia ya watu walimiminika mitaani jumamosi usiku kushangilia ushindi wa Ghana wa mabao 2-1 dhidi ya Marekani.

Ghana ndio wawakilishi pekee wa Afrika waliobaki kwenye kombe la dunia na wataingia uwanjani ijumaa kumenyana na Uruguay ili kuwania tiketi ya nusu fainali.

source nifahamishe

Afukua Maiti Toka Kaburini na Kufanya nayo Mapenzi

Tuesday, June 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kijana mwenye umri wa miaka 20 wa nchi ya kusini mwa Amerika ya Guyana amewashangaza watu wengi kwa kitendo chake cha kufukua maiti ya bibi wa miaka 75 na kisha kufanya nayo mapenzi.
Kijana huyo aliyetajwa kwa jina la Roopram Bacchus ambaye hufanya kazi ya kuokota taka, alipandishwa kizimbani ijumaa kujibu mashtaka yanayomkabili.

Bacchus alikiri mashtaka aliyofunguliwa ya kufanya mapenzi na maiti.

Kijana huyo alikiri kulifukua kaburi la bibi mwenye umri wa miaka 75 na kisha kufanya mapenzi na maiti yake.

Bacchus alijitetea kuwa ana matatizo ya kupenda sana pombe ambayo ndiyo iliyompelekea akafanya kitendo hicho.

Jaji aliamuru afanyiwe uchunguzi wa akili zake na alimuamuru alipe faini ya dola 200 za Kimarekani. Atatupwa jela mwaka mmoja kama akishindwa kulipa faini hiyo.

Kamanda wa polisi wa eneo hilo, Steve Merai alisema kuwa Bacchus alilifukua kaburi la bibi huyo siku moja baada ya bibi huyo kuzikwa.

"Bacchus alilivunja jeneza, aliitoa maiti toka kwenye jeneza na alifanya nayo mapenzi", alisema kamanda huyo wa polisi.

Kamanda huyo wa polisi aliongeza kuwa Bacchus na familia ya bibi huyo walikuwa ni majirani.


source nifahamishe

Mashindano ya Maimamu 'Imamu star' Yaanza Malaysia

Saturday, June 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kuna mashindano mengi yameibuka duniani kutafuta vipaji kama vile Pop Star, Bongo Star Search na mengineyo lakini huko nchini Malaysia yameanza mashindano ya aina yake kutafuta imamu bora.
aada ya mashindano ya Popstar, American Idol, The X Factor na mengineyo kuibuka sehemu mbalimbali duniani, mashindano ya kwanza ya aina yake yameanza nchini Malaysia yakienda kwa jina la "Imam Star".

Mashindano hayo ambayo nchini Malaysia yanajulikana kwa jina la "Imam Muda", yanawashindanisha vijana wa kiislamu ili kumpata imamu bora kati yao.

Vijana wenye umri kati ya miaka 19-27 wamewekwa nyumba moja ambapo kwa kipindi cha miezi mitatu na watakuwa wakishindana kumpata imamu bora kati yao.

Vijana hao watashindana kusoma azana, kusalisha, kutoa khutba, kuosha maiti na kuongoza mazishi.

Maiti zitakazotumika katika mashindano hayo ni maiti zilizopo monchwari ambazo hazijatambuliwa na ndugu zao.

Mshindi wa mashindano hayo hatapewa zawadi ya pesa kama yalivyo mashindano mengine. Atapewa schorlaship ya kusoma mambo ya dini katika chuo kikuu cha al-Madinah University cha nchini Saudi Arabia. Mshindi pia atapewa kazi ya kusalisha misikiti mikubwa ya mjini Kuala Lumpur na pia atakuwa akilipiwa gharama zote za kuhiji Makka.

Mashindano hayo yamekuwa gumzo nchini Malaysia yakivunja rekodi ya watazamaji. Yamebakiza mwezi mmoja kuisha.

source nifahamishe

'Michael Jackson Asingefariki Kama Angekuwa Muislamu'

Thursday, June 24, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Katika kuadhimisha mwaka mmoja tangia alipofariki, kaka yake Michael Jackson, amesema kuwa anaamini kaka yake angekuwa hai hadi leo kama angebadili dini kuwa muislamu.
Akiongea na shirika la habari la Uingereza la BBC katika mahojiano ambayo yatarushwa hewani leo, kaka yake Michael Jackson, Jermaine Jackson amesema kuwa anaamini kaka yake angekuwa hai hadi leo hii kama angefanikiwa kubadili dini kuwa muislamu.

Jermaine alisema kuwa kama Michael angebadili dini kuwa muislamu basi maisha yake yangebadilika na asingekuwa na maisha ambayo yalipelekea kifo chake.

"Naamini kama Michael angekuwa muislamu, angekuwa hai hadi leo, nasema hivi kwasababu nyingi sana", alisema Jermaine ambaye yeye alibadili dini kuwa muislamu miaka mingi sana iliyopita.

"Sababu ni kwamba mtu unapokuwa muislamu na ukafahamu kwa asilimia 100 sababu ya wewe kuwepo duniani na sababu ya watu waliokuzunguka kuwepo duniani, basi maisha hubadilika na kuwa mazuri", alisema Jermaine.

Jermaine aliongeza kuwa alimnunulia Michael vitabu vingi vya kiislamu toka Saudi Arabia na Bahrain.

"Alisoma vitabu vingi vya kiislamu", alisema Jermaine na kuongeza kuwa Michael hakuwa akiupinga uislamu.

"Walinzi wake wote walikuwa waislamu kwa kuwa aliuamini Uislamu, aliwaamini kwakuwa waislamu hujaribu kuwa watu wazuri kadri wawezavyo, si kwaajili ya Michael Jackson bali kwaajili ya Mungu".

"Wakati unapozungukwa na watu kama hawa unajua kwamba Mwenyezimungu atakulinda", alimalizia kusema Jermaine.

Michael Jackson alifariki akiwa na umri wa miaka 50, juni 25 mwaka jana kutokana na shambulizi la moyo lililotokana na matumizi makubwa ya madawa ya kupunguza maumivu.

Washabiki wake wanajiandaa kuadhimisha mwaka mmoja wa kifo chake siku ya ijumaa kwa kufanya shughuli mbalimbali za kukumbuka kazi zake za muziki.

source nifahamishe

Achomwa Kisu Kwa Kulalamikikia Miguno ya Ngono ya Jirani

Thursday, June 24, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanaume mmoja nchini Marekani amechomwa kisu na jirani yake baada ya kulalamikia sauti kali za ngono anazozitoa anapofanya mapenzi na mpenzi wake.
Mwanaume mwenye umri wa miaka 40 aliyejulikana kwa jina la Russell Willis Shepherd Jr. amefunguliwa mashtaka ya kumshambulia jirani yake mwenye umri wa miaka 58 ambaye alikuwa akilalamika miguno ya kimahaba aliyokuwa akiitoa.

Katika tukio hilo lililotokea South Carolina nchini Marekani, jirani wa Russel alirudi nyumbani kwake na kumkuta Russel akitoa sauti kali wakati akifanya mapenzi na mpenzi wake mwenye umri wa miaka 39.

Kuepuka kelele hizo aliamua kwenda nje kuvuta sigara, aliporudi na kukuta kelele hizo zikiwa ndio zimepamba moto, aliamua kumgongea mlango Russel na kumwambia apunguze kelele za ngono anazozitoa.

Russel alikasirishwa na kitendo hicho, alichukua kisu na kuanza kumshambulia jirani yake huyo mpaka alipofanikiwa kuchoropoka na kuomba msaada toka kwa jirani.

Russel almefunguliwa mashtaka ya kufanya shambulizi la kudhuru mwili na ametupwa jela akisubiri kufikishwa mahakamani.

source nifahamishe