Mike Tyson Aenda Makka Kuhiji

Tuesday, July 06, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Bingwa wa dunia wa zamani wa ndondi, Mike Tyson ambaye alibadili dini kuwa muislamu alipokuwa jela kwenye miaka ya 1990 yupo nchini Saudi Arabia kwaajili ya hija ndogo.
Bingwa wa dunia wa zamani wa ngumi za uzito wa juu, Mike Tyson anatembelea miji mitakatifu ya waislamu Makka na Madina kwaajili ya kuhiji.

Tyson ambaye alikuwa bingwa dunia kuanzia mwaka 1986 hadi 1990, aliwasili Madina siku ya ijumaa akiwa na maafisa wa umoja wa Daa'wa wa Kanada kwaajili ya Umrah ambayo ni hija ndogo.

Baada ya kutoka Madina, Tyson ataenda Makka na gazeti la Okaz la Saudia limeripoti kuwa Tyson ana mpango wa kutembelea pia miji mingine ya Saudia.

Tyson mwenye umri wa miaka 44 alibadili dini kuwa muislamu wakati alipokuwa jela akitumikia kifungo cha miaka 10 jela kwa kumbaka mrembo wa Marekani mwaka 1991. Hata hivyo alitumikia miaka mitatu jela na kuachiwa huru.

Baada ya kutoka jela alijaribu kurudi tena kwenye ngumi lakini hakuweza kulirudia taji lake na mwishoe aliachana na ndondi mwaka 2005.

source nifahamishe

Mama Amuua Mtoto Wake na Kuliuza Sikio Lake Kwa Mganga

Tuesday, July 06, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mama mmoja nchini Zimbabwe amemuua mtoto wake wa miezi 18 na kisha kulikata sikio lake moja na kumuuzia sikio hilo mganga wa nchini Msumbuji kwa dola 20.
Christine Hofisi mwenye umri wa miaka 21 anayeishi katika kitongoji cha Chipinge nchini Zimbabwe karibu na mpaka wa nchini Msumbiji, alimuua mtoto wake mchanga wa kiume mwenye umri wa miaka 18 na kisha kulikata sikio lake la kushoto na kumuuzia mganga anayeishi nchini Msumbiji.

Mwili wa mtoto huyo aliyepewa jina la Edmore uligunduliwa na majirani kwenye kichaka kilichopo karibu na nyumba ya mwanamke huyo.

Christine aliliuza sikio la mtoto wake kwa dola 20 kwa mganga anayeishi karibu na mpaka nchini Msumbiji anayeitwa Maheza.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Christine alipewa dola 10 na dola 10 zilizobaki aliahidiwa kulipwa baadae.

Mganga Maheza anatafutwa na polisi akituhumiwa kwa mauji ya watu wengine kadhaa baada ya mafuvu 11 ya binadamu kukutwa ndani ya nyumba yake.

Polisi nchini Zimbabwe wamesema kuwa wanamhoji Christine kwa mauaji ya mtoto wake na wataenda nchini Msumbiji kushirikikiana na maafisa wa Msumbiji kumsaka mganga Maheza.


source nifahamishe

Ajiua Baada ya Brazil Kufungwa na Kutolewa Kombe la Dunia

Sunday, July 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Kipigo cha Brazil jana toka kwa Uholanzi kimepelekea kijana mmoja nchini Haiti ajiue mwenyewe kwa kujigongesha kwenye gari lililokuwa spidi.
Kijana mmoja nchini Haiti kutokana na huzuni za Brazil kufungwa na Uholanzi na kutupwa nje ya kombe la dunia, amejiua mwenyewe kwa kujigongesha kwenye gari.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 18 alifariki hapo hapo kwenye eneo la tukio katika kitongoji cha Nerette kilichopo nje kidogo ya mji mkuu wa Haiti.

Brazil ilitandikwa na Uholanzi mabao 2-1 kwenye mechi ya robo fainali na kutupwa nje ya kombe la dunia.

Nchini Haiti, Brazil ina washabiki wengi na Brazil ilipokuwa ikishinda mechi zake za kombe la dunia, watu walikuwa wakimiminika mitaani kushangilia.

Hali ilikuwa tofauti kidogo jana kutokana na kipigo hicho cha Brazil ambacho kimekiweka kibarua cha kocha wa Brazil, Dunga matatani.

source nifahamishe

antivirus song-song of MR. Two a.k.a sugu.wmv

Saturday, July 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Waziri Mkuu Mwanamke Afunga Ndoa na Mwanamke Mwenzie

Thursday, July 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Baada ya bunge la Iceland kuipitisha sheria ya kuruhusu watu wa jinsia moja kuoana, waziri mkuu wa Iceland ambaye ni mwanamke amefunga ndoa na mwanamke mwenzake.
Waziri mkuu wa Iceland, bi Johanna Sigurdardottir amefunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi ambaye pia ni mwanamke.

Siku chache baada ya bunge la Iceland kupitisha sheria ya kuruhusu watu wa jinsia moja kuoana, bi Johanna amefunga ndoa na mpenzi wake Jonina Leosdottir.

Bi Johanna amekuwa akiishi na Jonina kwa muda mrefu na walifunga ndoa juzi jumapili.

Sheria ya kuruhusu wanaume kuoa wanaume wenzao na wanawake kuoa wanawake wenzao ilipitishwa juni 11 mwaka huu bila ya upingamizi wowote.

Bi Johanna mwenye umri wa miaka 66 alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Iceland mwaka jana baada ya migomo iliyosababishwa na kutetereka kwa uchumi kupelekea serikali iliyokuwepo kuondolewa madarakani.

Bi Johanna ndiye waziri mkuu wa kwanza barani ulaya kujitangaza wazi kuwa yeye ni msagaji. Ndoa yake inaonekana itakuwa ni changamoto kwa jumuiya zinazounga mkono ndoa za jinsia moja.


source nifahamishe

Mji wa Luanda Angola Ndio Mji Wenye Maisha Ghali Afrika

Thursday, July 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mji wa Luanda nchini Angola ndio mji ambao gharama za maisha ni kubwa kuliko miji yote barani Afrika, kwa duniani mji huo unashika nafasi ya tatu baada ya miji ya Tokyo, Japan na Oslo, Norway.
Kwa mujibu wa takwimu za gharama za maisha katika miji mbalimbali duniani kwa mwaka huu wa 2010 zilizotolewa na ECA International, mji wa Luanda nchini Angola unashika nafasi ya tatu duniani kwa gharama za maisha.

Katika takwimu za mwaka jana, mji wa Luanda ndio uliokuwa ukishika nafasi ya kwanza mbele ya miji mingi mikubwa duniani.

Katika takwimu za mwaka huu, mji wa Tokyo Japan unashika nafasi ya kwanza ukifuatiwa na mji wa Oslo, Norway.

Mjini Luanda nchini Angola, chakula cha mchana katika mgahawa wa saizi ya kati, kinagharimu dola 47, kopo moja la bia ni dola 1.62, kilo moja ya mchele ni dola 4.73 na dazani moja ya mayai hugharimu dola 4.75. Ukitaka kwenda sinema na mpenzi wako basi jiandae kutoa dola 13 kwa kichwa kimoja.

ECA imetoa listi ya miji 65 duniani ambayo ndiyo inayoonekana ina gharama kubwa za maisha kwa kuangalia gharama za chakula, nguo, vifaa vya umeme na burudani.

Katika listi ya miji 65 iliyolewa mji wa New York unashika nafasi ya 29 wakati jiji la Dar es Salaam limeshindwa kuingia kwenye orodha hiyo.

Chini ni orodha ya miji iliyomo kwenye top 10.

1:Tokyo
2:Oslo
3:Luanda
4:Nagoya
5:Yokohama
6:Stavanger
7:Kobe
8:Copenhagen
9:Geneva
10:Zurich



source nifahamishe

Amuua Mtoto Wake Kwa Hasira za Marekani Kufungwa na Ghana

Thursday, July 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja nchini Marekani anashikiliwa na polisi baada ya kumpiga mpaka kumuua mtoto wake aliyekuwa akilia sana wakati yeye akiangalia mechi ya kombe la dunia kati ya Marekani na Ghana ambayo Marekani ilifungwa 2-1 na kuliaga kombe la dunia.
Hector Castro mwenye umri wa miaka 28 alimpiga sana na kisha kumuua kwa kumziba pumzi mtoto wake wa kambo wa kike mwenye umri wa miaka miwili.

Baada ya kumuua mtoto huyo ili kuficha ukweli, Castro aliididimiza bisibisi kwenye shingo ya mtoto huyo ili kufanya kifo cha mtoto huyo kionekane kuwa ni cha ajali.

Castro aliita ambulansi akidai mtoto wake amepata ajali wakati akicheza na bisibisi imezama kwenye shingo yake.

Hata hivyo mchezo wake uligundulika muda mfupi baada ya madaktari waliokuja na ambulansi kugundua kuwa mtoto huyo alifariki kutokana kupigwa na kuvunjwa mbavu kadhaa na wala si bisibisi.

Castro alitiwa mbaroni kwa tukio hilo lililotokea jumamosi wakati wa mechi ya kuwania kuingia robo fainali kati ya Marekani na Ghana.

Castro alijitetea kuwa alishikwa na hasira kutokana na mtoto huyo kulia sana bila kunyamaza wakati yeye akiangalia mechi hiyo ya Marekani na Ghana ambayo iliisha kwa Marekani kufungwa mabao 2-1.

Kutokana na umri mdogo wa mtoto aliyeuliwa, Castro huenda akahukumiwa adhabu ya kifo iwapo atapatikana na hatia.
source nifahamishe