Pinda aguswa na sakata la Jerry

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


WAZIRI MKUU Mizengo Pinda, ameliagiza Jeshi la polisi nchini kufanya uchunguzi haraka iwezekanavyo ili suala hilo liweze kujulikana kama ni la fufikishwa mahakamani ama la ili haki iweze kutendeka kwa kuwa suala hilo limeigusa jamii iliyokubwa nchini
Pinda amemuagiza Mkuu wa Jeshi hilo IGP Said Mwema na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kufanya uchunguzi wa kina bila kuvihusisha vyombo vya habari ili kuweza kumaliza sakata hilo.

Waziri Pinda alitoa agizo hilo jana wakati alipokuwa akijibu maswali ya papo kwa papo bungeni Dodoma.

Pinda ambaye ni kiongozi wa kwanza wa ngazi za juu wa serikali kuingilia kati ametaka suala hilo lishughulikiwe mara moja tuhuma za mwanahabari huyo ambalo kwa sasa limekuwa gumzo la jiji.

Agizo la Waziri Mkuu lilitokana na swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), aliyehoji jitihada zinazofanywa na serikali katika kushughulikia suala hilo.

Katika swali lake la msingi, Hamad Rashid alisema waandishi wengi duniani wanapofuatilia mambo mazito, hupatwa na misukusosuko mikubwa na kuhoji kama yaliyompata Muro ni mojawapo ya misukosuko ya aina hiyo.

Akijibu swali hilo, Pinda alisema tayari amekwishazungumza na Masha na IGP Mwema ambao wameahidi kulifuatilia jambo hilo kwa haraka na binafsi asingependa jambo hilo kuendelea kuleta utata kutokana na kuwepo na kauli nyingi za watu mbalimbali kuhusu suala husika.

Pia alisema “Mimi pia sipendi suala hili lichukue muda mrefu maana linaweza kuleta hisia tofauti miongoni mwa jamii,” alisema Pinda.

Alisema kila binadamu anao upungufu wake, hivyo kuna uwezekano wa tuhuma dhidi ya Muro zikawa za kweli au la kwani pande zote mbili, akiwemo Muro na polisi wamekuwa wakikimbilia katika vyombo vya habari na kutoa taarifa zinazotatanisha.

source nifahamishe

Mafundi wafa kwa kufunikwa na kifusi Dar

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MAFUNDI UJENZI wawili wakazi wa Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam, wamekufa papo hapo baada ya kufunikwa na kifusi cha mchanga walichokichimba kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi
Taarifa hiyo ilitolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, na kusema tukio hilo lilitokea juzi huko Pugu Bagdad.

Shilogile amesema kuwa, mafundi hao James Katenga (27) na Adamu Mtolela (30), walikutwa na umauti huo wakati wakiendelea na uchimbaji mchanga kwenye moja ya machimbo yaliyopo eneo hilo.

Amesema mafundi hao walikutwa na wenzi wao ambao walikuwa wanahusika katika ujenzi na kuwakuta wameshapoteza maisha na kutoa tarifa kituo cha polisi.

Katika tukio jingine la ajali lililotokea jijini Dar es Salaam, mtu mmoja amekufa dunia papohapo na mwenzake kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari.

Amesema mtu aliyefariki alitambulika kwa jina la Mussa Issah (24) ambaye alikuwa akiendesha pikipiki na aliyejeruhiwa alikuwa ni abiria wake aliyetambuliwa kwa jina la Gidimash Geofrey 22 .

Amesema waligongwa vibaya na gari dogo aina ya Audi Saloon eneo la Brush huko barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Liberatus Sabas, alisema ajali hiyo ilitokea juzi eneo hilo wakati gari hilo lenye namba za usajili T 357 ASE likiendeshwa na Magreth Lega (34).

Amesema gari hilo lilikuwa alikitokea eneo la Kamata kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati dereva wa pikipiki hiyo yenye namba za usajili T 391 AYU alikuwa akitokea Tazara kuelekea Kamata.

Amesema Geofrey amelazwa hospitali ya Temeke.

source nifahamishe

Afikishwa kortini kwa kuua wanawe

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MOSES CHIPAMA [45] anayedaiwa kuwaua watoto wake wawili katika mazingira ya kutatanisha jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kujibu shitaka hilo la mauaji.
Shata hilo lilifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Rose Kangwa, wakati upande wa mashitaka ulikuwa ukiongozwa na Inspekta Dustan Kombe.

Kombe alidai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na mashitaka mawili ya mauaji ya watoto wake.

Katika shitaka la kwanza mshtakiwa alikamatwa Januari 25, mwaka huu, majira ya saa 5:55 usiku eneo la Tuangoma kwa Saku baada ya kumuua mtoto wake, Patrick Moses (16), aliyekuwa akisoma darasa la saba Shule ya Msingi Tuangoma.

Katika shitaka la pili, ilidaiwa kuwa mshtakiwa huyo alimuua mtoto wake mwingine, Sety Moses (12), aliyekuwa akisoma darasa la nne katika Shule ya Msingi ya Olympio.

Hata hivyo mshitakiwa alirudishwa rumande kwa kuwa hakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Hakimu aliamuru arudishwe rumande na kusubiri tarawtibu za kimahakama zifanyike na atakwenda kujibu shitaka hilo mahakama kuu, Kesi hiyo itarudishwa tena mahakamani hapo Februari 18, mwaka huu.

Katika hali ya kushangaza mshitakiwa huyo alianza kuwarushia mawe waandishi wa habari waliokuwa ndani ya mahakama kusikiliza shauri hilo huku akiwarushia viatu kwa kukataa kuandikwa na na kupigwa picha.

Alipoona viatu vyote viwili alivyovaa viliisha alivua fulana aliyovaa na ulijifunika sura ili wanahabari wasiweze kupata sura ili wasiweze kuianika magazetini.

Kutokana na fujo zake hizo maaskari magereza walilazimika kumtuliza mshitakiwa huyo kwa virungu na kuacha kuwatukana matusi wanahabari.


source nifahamishe

Msichana Azikwa Hai Kwa Kosa la Kuwa na Rafiki wa Kiume

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (1)


Msichana mwenye umri wa miaka 16 amezikwa hai na ndugu zake nchini Uturuki kwa kosa la kuwa na rafiki wa kiume hivyo kudaiwa ameiletea aibu familia yake.
Msichana mwenye umri wa miaka 16 wa nchini Uturuki amezikwa hai na ndugu zake baada ya kushutumiwa kuwa ameitia aibu familia yake kwa kuwa na marafiki wa kiume.

Baada ya kupewa taarifa ya tukio hilo, polisi walifanikiwa kuupata mwili wa msichana huyo aliyetambulika kwa jina la Medine Memi siku 40 baada ya kutangazwa kuwa ametoweka.

Mwili wa Medine ulikutwa katika mji wa Adiyaman umekalishwa kitako kwenye shimo la mita 2 huku mikono yake ikiwa imefungwa na kamba.

Baada ya maiti yake kufanyiwa vipimo kadhaa iligundulika kuwa kwenye tumbo lake na mapafu kulikuwa na kiasi cha mchanga hivyo kumaanisha kuwa alizikwa akiwa hai, taarifa ya wataalamu wa makosa ya jinai ilisema.

"Matokeo ya uchunguzi wa maiti yake yanasikitisha sana, msichana ambaye hakuwa na mchubuko hata mmoja kwenye mwili wake na wala hakuwa na kiasi chochote cha sumu kwenye damu yake, alikuwa hai na mwenye kujitambua wakati alipozikwa hai", alisema mtaalamu mmoja ambaye hakutaka kusema jina lake.

Baba yake Medine na babu yake, wametiwa mbaroni na kutupwa jela wakati uchunguzi wa mauaji yake ukiendelea.

Shirika la habari la Anatolia la Uturuki liliripoti kuwa baba yake Meline alisema katika ushahidi wake polisi kuwa familia yake haikuwa ikifurahia kumuona Medine akiwa na marafiki wa kiume.

Mauaji hayo yanayoitwa "Mauaji ya kulinda heshima" hufanyika sana kusini mashariki mwa Uturuki katika maeneo yenye Wakurdi wengi.

Serikali ya Uturuki imekuwa ikijaribu kuyakomesha mauaji hayo ya kulinda heshima bila mfanikio yoyote.

Wanawake wanaobakwa au wanaopata ujauzito kabla ya kuolewa huuliwa na familia zao katika kile kinachodaiwa kusafisha nuksi na fedheha wanazoziletea familia zao.

source nifahamishe

Binti wa Miaka 12 Arudi Kwa Mumewe wa Miaka 80

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Binti mwenye umri wa miaka 12 wa nchini Saudi Arabia ambaye alimkimbia mumewe mwenye umri wa miaka 80 baada ya kufungishwa ndoa kinguvu na baba yake, amekubali kurudi kwa mumewe na kuyaondoa madai ya talaka aliyofungua mahakamani.
Msichana mwenye umri wa miaka 12 wa nchini Saudi Arabia ambaye kwa kushirikiana na mama yake alifungua kesi mahakamani kudai talaka toka kwa mumewe mwenye umri wa miaka 80 ameamua kuyaondoa madai yake ya talaka na kurudi kwa mumewe.

Msichana huyo aliozeshwa kinguvu na baba yake ambaye alichukua mahari ya dola 22,670 toka kwa babu huyo.

Binti huyo ambaye jina lake limewekwa kapuni, alikuwa akiishi na baba yake baada ya ndoa ya baba yake na mama yake kuvunjika.

Binti huyo na mama yake waliifuta kesi ya madai ya talaka waliyoifungua katika kitongoji cha Buraidah katika mji wa Al-Qasim.

"Nimeikubali ndoa iliyofungwa na sina kipingamizi chochote", alisikika akisema binti huyo na kuongeza "Nafanya hivi kwaajili ya heshima ya baba yangu na kumtimizia ndoto yake".

Bila ya kueleza sababu za kubadilisha uamuzi wake ghafla, binti huyo aliiambia mahakama kuwa ndoa hiyo ilifungwa kwa hiari yake.

Ndoa ya binti huyo na babu mwenye umri wa miaka 80 ilizua mtafaruku mkubwa sana duniani baada ya mama wa binti huyo kufungua kesi mahakamani kuipinga ndoa hiyo huku akidai binti yake amebakwa.

Wakati taasisi za kutetea haki za watoto zikijiandaa kumtetea mahakamani, binti huyo amezivunja moyo taasisi hizo na kukubali kurudi kwa mumewe.

source nifahamishe

Wanne wa familia moja wateketea kwa moto wa jenereta

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

WATU wanne wa familia moja wamekufa kwa moto baada ya jenereta lililokuwa limefungiwa katika moja ya chumba ndani ya nyumba hiyo kupasuka na kuwaka moto
Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa kuamka leo, huko maeneo ya Kibwenzini Zanzibar wakati watu hao wakiwa wamelala ndani humo.

Ilidaiwa kuwa jenereta hilo liliripuka majira ya saa 11 za alfajiri na kuzua moto uliosababisha vifo hivyo.

Ilidaiwa kuwa familia hiyo ilinunua jenereta hilo kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kutokana na kukosekana kwa umeme visiwani Zanzibar.

Katika ajali hiyo waliopoteza maisha walitajwa kuwa ni Safia Shabani, Ahmed Shaban na mtoto ambaye hakuweza kupatikana jina lake, akiwemo na msichana wa kazi Sikudhani Nasorro.

Hadi habari hii inarushwa hewani, kamanda wa Polisi wa wilaya husika hakuweza kupatikana kuongelea juu ya tukio hilo juhudi zaidi zinafanyika ili kuweza kupata maelezo yake.

source nifahamishe

Mwanafunzi Aiuza Bikira Yake Kwa Dola 32,000

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi mmoja wa nchini New Zealand ameinadi bikira yake kwa dola 31,900 kwa mwanaume asiyemfahamu ili aweze kupata pesa za kulipia gharama za masomo yake ya chuo kikuu.
Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 19 aliinadi bikira yake kwenye mtandao wa www.ineed.co.nz baada ya kukabiliwa na ukata wa pesa.

Mwanafunzi huyo anayejiita "Unigirl" alijitambulisha kuwa yeye ni mrembo mwenye kuvutia, yuko fiti na mwenye afya njema.

Zaidi ya watu 1,000 walijaribu kuinunua bikira yake lakini mwanaume mmoja ambaye hakutajwa jina lake aliibuka mshindi baada ya kuweka dau kubwa la dola 31,900. (Takribani Tsh. Milioni 42).

"Nawashukuru watu wote zaidi ya 30,000 waliolitembelea tangazo langu, na zaidi ya watu 1,200 walioweka madau yao kuinunua bikira yangu", alisema mwanafunzi huyo.

"Dau lililoshinda ni kubwa sana kuliko hata nilivyotarajia".

Mwanafunzi huyo alisema kuwa hajawahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na pesa atakazopata atazitumia kulipia masomo yake.

Mwanafunzi huyo aliendelea kusema kuwa ili mradi masuala ya afya yake yatapewa kipaumbele hana hiana kumtunuku bikira yake mwanaume yoyote yule bila kubagua kabila wala umri ilimradi apate pesa za kulipia masomo yake.

Mmiliki wa tovuti iliyotumika kuinadi bikira hiyo, Ross MacKenzie, alisema kuwa tangazo la mwanafunzi huyo lilikuwa ni halali kisheria na hakuna sheria yoyote iliyovunjwa.

Mwanafunzi huyo aligoma kufanya mahojiano na waandishi wa habari lakini MacKenzie, aliliambia gazeti la Waikato Times kuwa ameruhusiwa kutaja kiasi cha dau lililoshinda bila kutoa maelezo ya ziada.

Matukio ya wanawake kuzinadi bikira zao kwenye internet yaliibuka kwa kasi baada ya mwanafunzi wa Marekani Natalie Dylan ,22, kuinadi bikira yake na kupata mteja aliyeweka dau la dola milioni 3.7.

Natalie naye wakati anainadi bikira yake alitoa sababu kama hizi kuwa anatafuta pesa za kulipia masomo yake.

Mwezi mei mwaka jana nchini Ujerumani, mwanamke mmoja toka Romania, Alina Percea, 18, aliinadi bikira yake kwa matumaini ya kuingiza mamilioni kama Natalie lakini aliambulia euro 10,000 tu toka kwa mfanyabiashara wa Italia mwenye umri wa miaka 45 aliyeshinda katika mnada huo.

Mbali ya kupata dau dogo, Alina alipata hasara zaidi baada ya maafisa kodi wa Ujerumani kuzikata kodi pesa alizopata kwa kuinadi bikira yake akiambiwa kuwa alichofanya ni sawa na wanachofanya makahaba ambao nao wanalipa kodi kwa shughuli zao.

Alina alibakia na karibia nusu ya pesa alizopata baada ya makato ya kodi kufanyika.

source nifahamishe