Wahindi Walalamikia Ukubwa wa Kondomu

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Utafiti uliofanyika nchini India umeonyesha kuwa wanaume wengi nchini India hawafurahishwi na ukubwa wa kondomu unaotambulika duniani kwakuwa kondomu hizo ni kubwa sana kulinganisha na ukubwa wa nyeti zao.
Utafiti huo uliowashirikisha wanaume 1,000 wa nchini India ulionyesha kuwa kondomu zenye ukubwa unaotambulika kimataifa huwapwaya wanaume wengi wa nchini India.

Utafiti huo uliweka wazi kuwa zaidi ya nusu ya wanaume walioshiriki utafiti huo walikuwa na uume ambao ulikuwa ni mfupi kulinganisha na ukubwa wa kondomu.

Utafiti huo uliofanyika kwa miaka miwili uliweka wazi kuwa asilimia 60 ya wanaume nchini India wana uume wenye urefu kati ya sentimeta tatu hadi tano pungufu ya ukubwa wa kondomu unaotambulika duniani.

Matokeo ya utafiti huu yamepelekea makampuni ya kutengeneza kondomu nchini India yatakiwe kutengeneza kondomu zenye ukubwa tofauti tofauti.

Matokeo ya utafiti huu yametiliwa mkazo kwakuwa India ndiyo nchini inayoongoza duniani kwa idadi kubwa ya watu walioathirika na virusi vya Ukimwi.


source nifahamishe

pata flava na diamond......mbagala.....

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Brazili Kupimana Ubavu na Tanzania Juni 7

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Timu ya soka ya Brazili ikiwa na mastaa wake wote watakaoshiriki kombe la dunia nchini Afrika Kusini, itashuka dimbani kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kupimana ubavu na Tanzania.
Mabingwa wa dunia mara tano, Brazili wametua nchini Afrika Kusini tayari kwaajili ya kombe la dunia litakaloanza kutimua vumbi juni 11.

Wazee wa samba Brazili wakiwa na mastaa wao wote watawasili Tanzania juni 5 na mechi yao dhidi ya Tanzania itafanyika juni 7. Bila shaka hiyo itakuwa mechi ambayo kila mpenzi wa soka Tanzania hatapenda kuikosa.

Brazili katika mechi zake mbili za maandalizi kabla ya kuanza kwa kombe la dunia itacheza na Zimbabwe mjini Harare juni 2 kabla ya kucheza na Tanzania juni 7 jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo ili kufanikisha mechi hizo Tanzania na Zimbabwe zitailipa Brazili mshiko mnene ambao haukuwekwa bayana ingawa inasemekana ni mamilioni ya dola.

Mashirikisho ya soka ya Tanzania na Brazili yamethibitisha kuwepo kwa mechi hiyo juni 7.

Mechi hiyo itakuwa ni fursa pekee ambayo haijawahi kutokea kwa wapenzi wa soka Tanzania kuwaona live mastaa wa Brazili kama vile Kaka, Robinho, Maicon, Lucio, Dani Alves, Elano, Kleberson, Fabiano na wengineo.

Brazili ambayo inajulikana zaidi kwa jina la "Selecao" ipo kwenye kundi la kifo kundi G pamoja na Ureno, Ivory Coast na Korea Kaskazini.

Mechi ya kwanza ya Brazili itakuwa juni 15 ambapo itakiputa na Korea Kaskazini wakati Ivory Coast itachuana na Ureno siku hiyo hiyo.


source nifahamishe

Mama Afanya Mapenzi na Mwanae ili Kumpa Uzoefu wa Mapenzi

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Baba na mama wa mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 9 wa nchini Australia wametupwa rumande kwa kufanya mapenzi na mtoto wao huyo wakidai wanampa elimu na uzoefu wa mapenzi.
Mwanaume mwenye umri wa miaka 57 na mkewe mwenye umri wa miaka 48 wa nchini Australia wametupwa rumande kwa kufanya mapenzi na mtoto wao wa kiume mwenye umri wa miaka 9.

Wazazi wa mtoto huyo ambao ni wafuasi wa kundi la watembea uchi "Nudist" walikuwa wakimpigisha punyeto na kufanya mapenzi na mtoto wao huyo ili kumpa uzoefu wa kimapenzi.

Mamlaka husika zilipewa taarifa juu ya suala hilo baada ya mtoto huyo kumtongoza msichana katika shule yake akimtaka wafanye mapenzi.

Polisi waliwatia mbaroni wazazi wa mtoto huyo novemba 16, 2009 na hawajapewa nafasi ya kumuona mtoto wao tena.

Akiongea mahakamani mjini Sydney jana, baba wa mtoto huyo alikiri makosa mawili ya kumuingilia mtoto wake na makosa mengine ya kumpigisha punyeto, kumshambulia na kuziweka picha na video za vitendo vyake kwenye internet.

Mama yake naye alikiri makosa ya kufanya mapenzi na mwanae na pia kumchua nyeti zake.

Taarifa ya polisi ilisema kuwa mtoto huyo aliwaambia kuwa wazazi wake hutembea uchi wanapokuwa ndani ya nyumba kunapokuwa na hali ya joto.

Baba yake hakuonyesha kujutia vitendo alivyokuwa akimfanyia mwanae na badala yake alidai kuwa anashangaa kwanini amekamatwa wakati alikuwa akimpa elimu ya mapenzi mwanae.

Wazazi wote wawili wa mtoto huyo wamenyimwa dhamana na wametakiwa kutowasiliana na mtoto wao kwa njia yoyote ile mpaka atakapofikisha umri wa utu uzima.

Watapandishwa tena mahakamani juni 4 kujua hatima zao.

source nifahamishe

50 Cent Choka Mbaya, Ukimuona Huwezi Kumtambua

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




Kwa kuiangalia picha yake unaweza usiamini na hata utakapoambiwa hii ni picha ya 50 Cent jinsi alivyo sasa unaweza usiamini, lakini ukweli ni kwamba picha hii ni ya 50 Cent kama alivyo sasa baada ya kupungua kilo 25 ndani ya wiki 9.
Picha mpya za mwanamuziki milionea wa Marekani 50 Cent zimetolewa na kuwafanya watu wabaki midomo wazi kwa jinsi ambavyo imekuwa vigumu kumtambua kwa jinsi alivyopungua kilo 25 ndani ya wiki tisa.

50 Cent amejikondesha kwa kunywa maji na juice pekee ili aweze kuigiza kwenye filamu mpya ambayo jikoni ambayo inamuelezea nyota wa mpira wa miguu ambaye anaugua ugonjwa wa kansa.

50 Cent ambaye ana umri wa miaka 34 amekonda sana na amepungua uzito wake toka kilo 97 hadi kilo 72.

50 Cent amejikondesha ili kuleta uhalisia wa mgonjwa wa kansa katika filamu ya "Things Fall Apart", filamu hiyo 50 Cent ndiye nyota wa filamu na prodyuza msaidizi.

Wakati picha mpya za 50 Cent zilipowekwa kwenye mitandao jana watu wengi waligoma kuamini na kusema kwamba picha hizo ni uzushi tu wa kwenye mitandao.

Lakini 50 Cent ambaye jina lake halisi ni Curtis Jackson alijitokeza na kuthibitisha kuwa picha hizo ni za kweli.

50 Cent alisema kuwa baada ya kumaliza kuigiza kwenye filamu hiyo ataanza kula kama kawaida kurudisha mwili wake wa zamani.

source nifahmishe

Baba na mwanaye wakutana gesti toka kwa orijino komedi

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Orijino komedi na unasemaje !

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)