Uzio wa Hoteli ya kitalii wabomolewa ni siku tatu toka izinduliwe na R

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak /


UZIO WA HOTELI ya kitalii iitwayo Snow Crest ya jijini Arusha, imebomolewa uzio uliozunguka hoteli hiyo na kuharibu miundombinu mizima ya mawasiliano hotelini hapo baada ya kudaiwa kuwa umejengwa kwenye eneo la hifadhi.
Ukuta huo ulibomolewa jana majira ya saa 11:30 za asubuhi, na Wakala wa barabara nchini [TANROADS] kwa kudai uzio huo umejengwa kimakosa na umezidi eneo la hifadhi ya taifa.

Hatua hiyo ya Tanroads imekuja ni baada ya siku tatu toka Rais wa nchi, Jakaya Kikwete kwenda kuzindua hoteli hiyo ya kitalii mjini humo Ijumaa wa wiki iliyopita.

Meneja wa Hoteli hiyo Bw. Mark Digira aliwaambia vyombo vya habari kuwa Kutokana na kuvunjwa kwa ukuta huo imeharibu hadhi ya hoteli hiyo ambayo I imejengwa kwa mabilioni ya fedha.

Na kusema kuwa labda kuna hujuma maana kama kungekuwa na kasoro hizo wakala wa barabara wangezuia toka hoteli hiyo inajengwa lakini amewsema wao hawakupata kibali chochote kutoka kwenye taasisi hiuyo iliyoashiria wasijenge eneo hilo na ingekuwa hivyo wasingeweza kufanyia hivyo.

Amesema hoteli hiyo iligharamia kiasi cha shilingi bilioni 8 za kitanzania kujenga hoteli hiyo ya kitalii iliyozinduliwa na Rais Kikwete.

Wakizungumza na vyombo vya habari ene o la tukio, wakala hao wa barabara walisema sababu iliyofanya ibomoe uzio huo ni Kutokana kujengwa na kuchota mita 22 na nusu ya hifadhi ya taifa.

Wamesema hiyo ndiyo sababu kubwa iliyofanya uzio huo ubomolewe kwa kuwa walimega eno hilo ambalo haliwahusu kwen yeujenzi huo wa hoteli.
Hoteli hiyo ya Snow Crest ipo mijini Arusha kwenye barabara iendayo Moshi Arusha.

HAta hivyo wadau mbalimbali wakiwemo na wakazi wa mjini humo kitendo cha Tanroads kimechukuliwa ni sawa na kumdharau rais Kikwete aliyekwenda kuzindua hoteli hiyo.

source.nifahamishe.com

0 comments:

Post a Comment