Urembo Inapotumbukia Nyongo

Friday, November 20, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi mmoja wa kike wa nchini Uingereza ameharibika sura yake kabisa kiasi cha kufanana na UFO (viumbe vinavyosemekana vinaishi angani) baada ya kutumia dawa ya kuzibadilisha rangi nywele zake ziwe nyeusi.
Abigail Colbourne mwenye umri wa miaka 15, alitumia dawa za kupaka za kubadilisha rangi ya nywele kuwa nyeusi za kampuni ya Clairol ili kuzifanya nywele zake ziwe nyeusi lakini ghafla sura yake ilianza kuvimba na macho yake yalivimba kiasi cha kushindwa kuona.

Sura yake iliharibika kabisa kiasi cha kushindwa kutambulika.

Akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza Abigail alisema "Macho yangu yalifunga kutokana na jinsi yalivyovimba na kichwa changu pia kilivimba... nilikuwa natisha sana".

Abigail ambaye ni mkazi wa London alisema kwamba alishindwa kufanya vipimo vya aleji kabla ya kujipaka dawa hizo kama ilivyoshauriwa kwenye paketi ya dawa hizo.

Aliwahishwa hospitali ambako alipatiwa matibabu na uvimbe huo kupungua kidogo. Bado anaendelea na matibabu ya kuirudisha sura yake katika hali yake ya awali.

Mama yake Abigail, Joanna Leech alisema kuwa tukio hilo la kusikitisha lililompata mwanae liwe fundisho kwa wengine wanaotumia dawa kama hizo.

by nifahamishe.com

TOVUTI YA WATU BOMBAA PEKEE

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Tovuti ya watu wazuri pekee yake imekuwa ikipata wanachama wengi hadi sasa ina wanachama 180000 ila imekuwa ikisababisha chembe ya ubaguzi kwa watu wasio na mvuto,hebu tembelea hii mdau

www.beautifulpeople.com

Kikwete anena kuhusu adhabu ya vifo

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Rais Kikwete abadilisha hukumu ya vifo katika kesi 75 ambazo hukumu yake imekuwa kifungo cha maisha

Busta Rymes atawasha moto katika fiesta Dar

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


mwana muziki machachari kwa kufloo atawasha moto katika fiesta ya tarehe 21 novemba,sijui itakuaje wadau nadhani patakuwa hapatoshi

AKON APATA SHAVU KATIKA UFUNGUZI WA KUMBE LA DUNIA

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Akon atapiga shoo ya ufunguzi wa kumbe la dunia kule kwa babu south africa

KOMBE LA DUNIA LILIPOWASILI DAR

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

kombe la mabingwa wa barclays league lilivyotinga dar

Monday, November 16, 2009 / Posted by ishak / comments (0)




watu mbalimbali walivyopiga picha na kombe hilo

MAISHA CLUB JINSI ILIVYOTEKETEA KWA MOTO

Monday, November 16, 2009 / Posted by ishak / comments (0)






Maisha club ilivyoteketea kwa moto,sehemu ya ndani na nje kama jinsi inavyoonekana