Ajirusha Uchi Toka Ghorofa ya 11

Thursday, August 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wakati China ikiendeleza kuombeleza vifo vya mamia ya watu kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo, mwanamke mmoja nchini humo amejaribu kujiua kwa kujirusha toka ghorofa ya 11 huku akiwa uchi wa mnyama.
Kufuatia mzozo na mumewe, mwanamke mmoja wa nchini China alijaribu kusitisha maisha yake kwa kujirusha toka ghorofa ya 11.

Katika tukio hilo lililotokea kwenye jimbo la Anhui nchini humo, mwanamke huyo alisababisha kizaazaa baada ya kuvua nguo zake zote na kupanda kwenye dirisha la nyumba iliyopo ghorofa ya 11 na kutishia kujiua kwa kujirusha chini.

Pamoja na jitihada za zimamoto na majirani kumsihi asijirushe, mwanamke huyo aliamua kujirusha ili kuhitimisha maisha yake.

Hata hivyo maisha ya mwanamke huyo yalinusurika baada ya kuangukia kwenye boya lililowekwa chini na zimamoto. Aliwahishwa hospitali kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Iligundulika kuwa sababu ya mwanamke kujaribu kujiua ni mzozo uliotokea usiku wa siku moja kabla ya tukio hilo.


source nifahamishe

Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500

Monday, August 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Msichana mmoja wa nchini Hungary ambaye aliinadi bikira yake kwenye mtandao ili apate pesa za kuisaidia familia yake, amepata mteja ambaye ameinunua bikira yake sawa na Tsh. Milioni 500.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19 anayejiita "Miss Spring" ameamua kuiuza bikira yake kwa mwanaume raia wa Uingereza ambaye atatoa paundi 200,000.

Msichana huyo alisema kuwa aliamua kuiuza bikira yake ili aweze kulipia gharama za masomo yake na pia aweze kulipa madeni ya mama yake.

"Familia yangu ina madeni na hatuwezi kuyalipa, mama yangu alikopa pesa ambazo alishindwa kuzilipa na kupelekea tupoteze nyumba yetu, nataka nilipe madeni yote", alisema msichana huyo.

"Pesa nilizopata sio nyingi sana kwani nitapoteza nusu yake kwenye kodi", aliongeza msichana huyo.

Msichana huyo alisema kuwa anajiandaa kwenda Uingereza ili aweze kumtunuku bikira yake mdau aliyetoa dau kubwa kuliko wote.

Mnada wa bikira ya msichana huyo ulianzia kwenye mtandao wa Ebay lakini ulimalizikia kwa njia ya email baada ya Ebay kuufutilia mbali mnada huo baada ya kugundua unahusisha uuzaji wa mapenzi.

"Nilikuwa nikiwasiliana na washindi wawili, mmoja raia wa Uingereza na mwingine raia wa Ireland, nimemchagua mwanaume wa Uingereza".

"Wote wanataka kunioa na kuitunza familia yangu lakini kwa sasa sifikirii kuishi maisha ya ndoa", alisema msichana huyo.

source nifahamishe

Nyota wa Uingereza Amhonga Kahaba Paundi 800 Kwa Usiku Mmoja

Monday, August 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Nyota wa Uingereza na timu ya Tottenham Hotspurs, Peter Crouch ameingia kwenye skendo kubwa sana baada ya kumsaliti mchumba wake na kumhonga kahaba paundi 800(Takribani Tsh. Milioni 1.8) kwa usiku mmoja.
Peter Crouch alikuwa kwenye vakesheni nchini Hispania pamoja na mchumba wake mwanamitindo, Abbey Clancy.

Siku mbili baada ya kumaliza vakesheni yake, Crouch alishindwa kujizuia kumsaliti mchumba wake kwa kununua penzi toka kwa kahaba mwenye umri wa miaka 19, anayejiita Monica Mint.

Crouch alimhonga kahaba huyo, paundi 800 ili afanye naye mapenzi mara mbili ndani ya usiku mmoja, mara moja kwenye taksi na baadae hotelini kwake.

Akitoboa siri ya tukio hilo, Monica aliliambia gazeti la News of the World la Uingereza kuwa Crouch hakujivunga hata kidogo kununua penzi lake kwa kiasi kikubwa cha pesa.

"Hakuhofia watu kutuona nyuma ya taksi, alisisitiza tufanye mapenzi ndani ya taksi wakati tukielekea hotelini", alisema Monica.

"Nilikuwa sijui kuwa ana mchumba, bado siamini amenunua penzi langu wakati ana mwanamke mrembo amemuacha nyumbani kwake", alimalizia kusema Monica.

source nifahamishe