Mume Wangu Hataki Kunipiga, Nataka Talaka'

Friday, May 21, 2010 / Posted by ishak / comments (1)


Mwanamke mmoja nchini Iran amemfikisha mumewe mahakamani akidai talaka kwakuwa mume wake hajawahi kumpiga hata siku moja.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 [jina kapuni] alifungua kesi katika mahakama ya masuala ya familia mjini Tehran akilalamika kuwa mumewe hampigi hivyo anataka apewe talaka.

Kwa mujibu wa gazeti moja la kila siku la nchini Iran, mwanamke huyo aliiambia mahakama "Mume wangu ananitumikia na kunitunza vizuri sana lakini mimi nataka awe ananipiga, kama hawezi basi naomba anipe talaka yangu".

Mume wake ambaye ana umri wa miaka 28 alijitetea mahakamani "Mke wangu nampenda sana, sioni sababu ya kumpiga au kutumia maguvu dhidi yake".

Kwakuwa mwanamke huyo alisisitiza kuwa anataka awe anapigwa na mumewe au la apewe talaka, mahakama ilimruhusu mumewe awe anamshushia kipigo mkewe siku moja moja ili kuilinda ndoa yake.

Mumewe kwa shingo upande alikubali na aliahidi kuwa atakuwa akimshushia kipigo mkewe ili kumridhisha.

source nifahamishe

Panya Ndani ya Ikulu ya Obama

Friday, May 21, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Hotuba ya Rais Barack Obama wa Marekani iliingiliwa na kitu asichokitegemea baada ya panya kukatiza mbele yake wakati akitoa hotuba ndani ya ikulu ya Marekani.
Rais Barack Obama alikuwa akitoa hotuba kwenye bustani maarufu ya Rose Garden iliyopo mbele ya ikulu wakati panya alipojitokeza na kukatiza mbele yake toka upande mmoja kwenye upande mwingine.

Wapiga picha waliokuwepo eneo la tukio hawakupitwa na panya huyo na walifanikiwa kuchukua taswira wakati kiumbe hicho kilipokuwa kikipita mbele ya mkuu wa taifa kubwa duniani.

Haijajulikana kama rais Obama alimuona panya huyo au la kwani alielendelea na hotuba yake bila kutetereka.

Taarifa zinasema kwamba panya huyo alionekana pia akipiga misele kabla ya Obama hajaanza kutoa hotuba yake.

source nifahamishe

Wanaume Wanaowasaidia Wake Zao Kazi za Nyumbani Ndoa Zao Hudumu

Thursday, May 20, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wanaume ambao huwasaidia wake zao kazi mbalimbali za nyumbani kama vile kupika, kuosha vyombo na kuwaogesha watoto, ndoa zao hudumu muda mrefu kulinganisha na wale wanaosubiria kufanyiwa kila kitu na wake zao.
Utafiti uliofanywa na watafiti wa chuo cha London School of Economics (LSE) cha Uingereza umeonyesha kuwa wanaume wanaowasaidia wake zao kazi za nyumbani ndoa zao hudumu muda mrefu kulinganisha na wanaume ambao hawependi kuwasaidia kazi za nyumbani wake zao.

Utafiti huo ulisema kuwa ndoa ambazo mke na mume wote wanafanya kazi huwa katika hatari kubwa ya kuvunjika iwapo mume hamsaidii mkewe kazi za nyumbani.

Utafiti huo uliopewa jina la "Men's Unpaid Work and Divorce" ulihusisha familia 3500 za Uingereza.

Matokeo ya utafiti huo yalionyesha kuwa wanaume ambao waliwasaidia wake zao kazi za nyumbani kama vile kwenda sokoni, kuosha vyombo, kupika na kuwaangalia watoto ndoa zao zilionyesha kuwa imara zaidi.

Hata hivyo utafiti huo ulisema kuwa ndoa za watu wa zamani zilidumu sana kwa kuwa mke alikuwa hafanyi kazi akijishughulisha na kazi za nyumbani pekee wakati mume alifanya kazi kutafuta chakula kwaajili ya familia.


source nifahamishe

Arekodi Video Za Binti Yake Akifanya Mapenzi

Thursday, May 20, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mama wa nchini Marekani ambaye alirekodi VIDEO za binti yake mwenye umri wa miaka 16 akiingiliwa kinguvu na mpenzi wake ametupwa jela miaka 58 jela.
Bobbie Jo Geveshausen mwenye umri wa miaka 43 alipenda kurekodi video wakati mpenzi wake Edward D. Shockey alipokuwa akifanya mapenzi na binti yake mwenye umri wa miaka 16 na wakati mwingine alijiunga nao.

Kutokana na tabia yake hiyo, Bobbie atatupwa jela miaka 58 kwa kushiriki kwenye kitendo cha kuingiliwa kinguvu kwa binti yake huku yeye mwenyewe akiwa ndio mchukuaji wa video.

"Ni vigumu kuamini kuwa mama mzazi anafurahia binti yake kubakwa huku akirekodi video", alisema mwendesha mashtaka wa kitongoji cha Platte, Eric Zahnd kabla ya jaji kutoa hukumu jana.

Video za kuingiliwa kinguvu kwa binti yake Bobbie ziligundulika baada ya Edward kumpa kimakosa mpenzi wa binti huyo DVD ambazo zilitakiwa ziwe ni za muziki.

Badala yake DVD hizo zilimuonyesha Edward akimuingilia kinguvu binti huyo ambaye katika baadhi ya matukio ya DVD hizo alionekana wazi kuwa ni mjamzito.

Katika DVD hizo mama yake alionekana pia akishiriki katika baadhi ya matukio ya kuingiliwa kwa binti yake.

DVD hizo zilipelekwa polisi ambapo Edward na Bobbie walitiwa mbaroni muda mfupi baadae.

Wakati Edward alihukumiwa kwenda jela miaka 25, Bobbie alihukumiwa kwenda jela miaka 58 baada ya kukiri makosa matano ya kumuingiza binti yake mwenye umri mdogo kwenye masuala ya ngono na makosa mawili ya kulawitiwa kwa binti yake .

source nifahamishe

Wanaume Waliooana Malawi Watupwa Jela Miaka 14

Thursday, May 20, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wanaume wawili wa nchini Malawi ambao waliiga tamaduni za watu wa magharibi na kuamua kuoana na kufanya sherehe kubwa, wamehukumiwa kwenda jela miaka 14 pamoja na kufanyishwa kazi ngumu.
Akitoa hukumu jaji wa mahakama ya Blantyre, Nyakwawa Usiwa-Usiwa alisema kuwa anatoa hukumu kali ili kuwalinda wananchi na watu wenye tabia kama ya wanaume hao waliooana.

Steven Monjeza, 26, na Tiwonge Chimbalanga, 20, walitupwa jela tangia walipotiwa mbaroni mwezi disemba mwaka jana wakati walipofanya sherehe ya harusi yao.

Kukamatwa kwa Monjeza na “mkewe” Tiwonge Chimbalanga kulisababisha Malawi iingie kwenye mgogoro mkubwa na mataifa ya magharibi ambayo yanatoa msaada kwa Malawi. Uingereza ambayo ndiyo mfadhili mkubwa wa Malawi iliweka wazi kukasirishwa kwake na kesi hiyo lakini haikusitisha misaada yake.

Mahakama ilijaa mamia ya watu na wengine walijaa nje ili kujua hukumu ya Monjeza na mwenzake. Walipotolewa mahakamani kupelekwa jela kuanza kutumikia vifungo vyao, baadhi ya watu walipiga kelele na kuwatupia maneno ya kejeli.

“Mmepata mlichostahili”, “Miaka 14 haitoshi ilibidi mfungwe jela miaka 50”.
Akiongea wakati wa kutoa hukumu, Jaji Usiwa-Usiwa alisema “Nitawapa hukumu ya kutisha ili kuilinda jamii na watu kama nyinyi na iwe mfano kwa wengine”.

Wakili wa washtakiwa aliitaka mahakama itoe adhabu ndogo kwakuwa vitendo vya Monjeza na mwenzake havimdhuru mtu mwingine yeyote.

“Ni watu wawili watu wazima ambao wanafanya mambo yao kwa siri. Hakuna mtu atakayedhurika iwapo wataruhusiwa kurudi kwenye jamii”, alisema wakili huyo.

Nayo taasisi ya kutetea haki za binadamu ya Cedep ya nchini Malawi, ilisema kuwa leo ni siku mbaya sana kwa Malawi.

“Inakuwaje wafungwe miaka 14 eti kwakuwa wanapendana? Hata kama wakifungwa jela miaka 20 jinsia zao haziwezi kubadilika”, mwanaharakati wa taasisi hiyo.

Jaji Usiwa-Usiwa alisema kuwa wanaume hao hawakuonyesha dalili yoyote ya kujutia tabia yao mbaya ya Sodoma na Gomora.

Wakati huo huo Marekani imelaani hukumu iliyotolewa na imesema kuwa hukumu hiyo ni hatua moja nyuma katika kulinda haki za binadamu.


source nifahamishe

Mwalimu Awafundisha Wanafunzi Jinsi ya Kumuua Obama

Wednesday, May 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwalimu wa somo la hisabati wa nchini Marekani anachunguzwa na shirika la ujasusi la Marekani baada ya kutumia mfano wa kumuua rais wa Marekani, Barack Obama kuwaelekeza hesabu wanafunzi wake.
Mwalimu huyo wa mji wa Alabama, alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake somo la hisabati mada ya Jometri (Geometry) wakati alipotumia mfano wa kumuua Obama kuwaelekeza hisabati wanafunzi wake.

Mwalimu huyo ambaye hakutajwa jina lake alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake mistari sambamba na pembe za maumbo mbali mbali wakati alipowaelekeza wanafunzi wake wasimame wapi ili kupata engo nzuri ya kumpiga risasi rais Obama.

"Ukiwa kwenye jengo hili itakubidi ukae kwenye pembe hii ili kuweza kumtungua Obama", alisema mwalimu huyo.

Mwalimu huyo alihojiwa na polisi baada ya mtu mmoja kutoa taarifa kwenye mamlaka husika juu ya tukio hilo.

Taarifa zimesema kuwa mwalimu huyo hakutiwa mbaroni wala kufunguliwa mashtaka mahakamani lakini FBI wanamfanyia uchunguzi.

Uongozi wa shule yake ya Corner High School umesema kuwa hauna mpango wa kumfukuza kazi mwalimu huyo na utamruhusu aendelee na kazi kama kawaida.

source nifahamishe

Mwanasiasa wa Nigeria Akamatwa na kilo 2 za Cocaine Tumboni

Wednesday, May 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanasiasa wa Nigeria ametiwa mbaroni nchini humo baada ya kunaswa uwanja wa ndege akiwa amemeza kilo mbili za madawa ya kulevya aina ya cocaine.
Polisi nchini Nigeria walisema kuwa mwanasiasa huyo aliyegombea ubunge wakati wa uchaguzi uliopita na ambaye pia anagombea ubunge katika uchaguzi ujao, alikamatwa kwenye uwanja wa ndege wa Lagos akiwa amemeza kilo mbili za madawa ya kulevya aina ya cocaine akijaribu kuzisafirisha kuzipeleka Ujerumani.

Mwanasiasa huyo aliyetajwa jina lake kuwa ni Eme Zuru Ayortor aliwaambia maafisa wa polisi kuwa alimeza madawa hayo ya kulevya ili aweze kupata pesa za kupigia kampeni wakati wa uchaguzi.

Polisi walisema kuwa scanners za uwanja wa ndege zilionyesha kete za madawa ya kulevya zikiwa tumboni mwa mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 52.

Polisi walisema kuwa walifanikiwa kuzipata kete 100 za cocaine toka kwenye tumbo lake.

Taarifa zilisema kuwa Ayortor aliwaambia polisi kuwa alihitaji pesa kwakuwa alipoteza pesa nyingi sana wakati wa kampeni za uchaguzi uliopita wa mwaka 2007.

"Kiasi cha madawa ya kulevya alichokibeba tumboni ni kikubwa sana", alisema afisa wa polisi na kuongeza "Tunaamini hii sio mara yake ya kwanza kusafirisha madawa ya kulevya".

Kitaaluma Ayortor, ana shahada ya pharmacy aliyoipata kwenye chuo kikuu cha Wisconsin nchini Marekani.

source nifahamishe

Afariki Kwasababu ya Imani Yake

Wednesday, May 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kijana wa kiingereza ambaye ni muumini wa kanisa la mashahidi wa Yehova amefariki dunia baada ya kukataa kuwekewa damu alipopata ajali mbaya ya gari kwakuwa mafundisho ya dini yake yanakataza watu kuwekewa damu za watu wengine.
Joshua McAuley, 15, alikuwa amesimama mbele ya duka moja mjini Smethwick, West Midlands wakati gari lililopoteza muelekeo lilipomgonga yeye na watu wengine wawili kabla ya kutinga ndani ya duka hilo.

Katika ajali hiyo mbaya Joshua alipata majeraha makubwa tumboni na miguuni na alilazimika kuwahishwa hospitali kwa njia ya helikopta kutokana na hali yake kuwa mbaya sana.

Joshua alipoteza damu nyingi sana kwenye ajali hiyo lakini alikuwa akijitambua wakati alipokuwa akiwahishwa hospitali.

Madaktari walipotaka kumwekea damu, Joshua alikataa na kuwaambia madaktari kuwa dini yake inakataza watu kuwekewa damu za watu wengine.

Joshua aliweka wazi kuwa kanisa lake la mashahidi wa Yehova linakataza watu kuwekewa damu za watu wengine.

Joshua aligoma kata kata kuwekewa damu na kwa kuwa sheria haziruhusu madaktari kuwalazimisha wagonjwa vitu wasivyovitaka, madaktari waliacha kumwekea damu.

Masaa sita baada ya ajali hiyo Joshua alipoteza maisha yake.

Familia ya Joshua imeviomba vyombo vya habari vikae mbali wakati wakiombeleza kifo cha mpendwa wao.

source nifahamishe

Mwanafunzi Ajaribu Kuulipua Ubalozi wa Marekani Dar

Wednesday, May 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi wa shule ya msingi ya Mtambani jijini Dar es Salaam anashikiliwa na polisi baada ya kujaribu kuulipua ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam.
Taarifa zilizopatikana zimesema kuwa mwanafunzi huyo ambaye jina lake limewekwa kapuni, anashikiliwa na polisi na kwenye kituo cha polisi cha Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Mwanafunzi huyo anadaiwa kujaribu kuulipua ubalozi wa Marekani kwa kutumia bomu la mafuta ya taa.

Mwanafunzi huyo alikuwa na mpango wa kulilipua tanki la mafuta ya dizeli la ubalozi huo ambalo wakati wa tukio lilikuwa na zaidi ya lita 1,000.

Mwanafunzi huyo ambaye umri wake unakadiriwa kuwa kati ya miaka 15 na 17 alikamatwa ndani ya ubalozi huo akiwa na dumu lake la lita tano la mafuta ya taa, utambi na kiberiti.

Mwanafunzi huyo aliingia kwenye ubalozi huo jumapili iliyopita nyakati za usiku kwa kupitia mojawapo ya mageti ya ubalozi huo ambapo walinzi wake walikuwa wamepiga mbonji.

Kelele za koki la tanki la mafuta la ubalozi huo wakati mwanafunzi huyo alipokuwa akilifungua ndizo zilizowazindua walinzi hao toka usingizini na kumnasa mwanafunzi huyo akiwa kwenye harakati za kulifungua tanki hilo ili alipige moto lilipuke.

Kijana huyo alipohojiwa na walinzi waliomkamata alikiri kutaka kusababisha mlipuko mkubwa ambao ungesababisha uharibifu mkubwa wa mali na kuhatarisha maisha ya watu.

Mwanafunzi huyo alisema kuwa yeye na wenzake walivutiwa na mafunzo ya Al-Qaeda waliyopewa kwa njia ya Video na walitaka kuyafanyia majaribio kabla ya siku ambayo ilipangwa wafanye shambulio kwenye ubalozi huo.

Ubalozi wa Marekani, Dar umethibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini haukutoa taarifa zaidi kwa kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi.

source nifahamishe

Hasira za Kufumaniwa na Kuachwa Solemba

Wednesday, May 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke wa nchini Kanada ambaye alikuwa akiisaliti ndoa yake hadi mumewe alipogundua kwa kupitia namba zilizopo kwenye bili ya simu, ameifungulia kesi kampuni yake ya simu kwa kupelekea ukware wake ugundulike na anataka alipwe fidia sawa na Tsh. Milioni 800.
Gabriella Nagy, 35, anaidai fidia kampuni yake ya simu kwa kuingilia masuala yake binafsi na kupelekea aachwe na mumewe.

Gabriella anadai fidia sawa na Tsh. Milioni 800 toka kwa kampuni ya simu ya Rogers Wireless baada ya mumewe kugundua kuwa anaisaliti ndoa yake kupitia namba zilizoandikwa kwenye bili yake ya simu.

Katika madai aliyofungua mahakamani, Gabriela alisema kuwa aliitaka kampuni hiyo ya simu imtumie bili yake ya simu kwa jina lake lakini kampuni hiyo iliijumlisha bili ya simu pamoja na bili ya TV na internet na kuzituma kwa jina la mumewe.

Mumewe alipata shauku ya kujua kulikoni alipoona namba moja imepigwa mara nyingi sana kuliko kawaida, alipoipiga namba hiyo aliambiwa na mwanaume aliyepokea kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Gabriela.

Mumewe aliamua kumuacha Gabriela pamoja na watoto wake na kwenda kuishi sehemu nyingine.


"Kinachoniuma sana ni kwamba uhusiano wenyewe ulikuwa umeisha wakati mume wangu alipogundua" alisema Gabriela na kuongeza kuwa aliiamini kampuni ya simu isingemuangusha na kupelekea kuvunjika kwa ndoa yake.

Katika utetezi wake, kampuni hiyo ya simu ilisema kuwa haiwezi kukubali lawama za kuvunjika kwa ndoa ya Gabriela kwasababu ya bili ya simu waliyoituma.

"Kwa vyovyote vile ndoa yao ingevunjika tu kama mumewe angegundua usaliti wake kwa njia nyingine yoyote ile", ilisema taarifa ya utetezi ya kampuni hiyo.

source nifahamishe

Joto la Bangi Lamuua

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume wa nchini Uingereza aliyekuwa akilima bangi ndani ya nyumba yake amefariki kutokana na joto la taa alizoziweka kusaidia mimea ya bangi kukua haraka.
Luke Holmes mwenye umri wa miaka 28, alikutwa amefariki chumbani kwake kutokana na joto lililotoka kwenye shamba lake la haramu la bangi ndani ya nyumba yake iliyopo Halifax, West Yorks.

Luke alifariki baada ya kuzidiwa na joto kali lililotokana na taa alizoziweka kwenye shamba lake la bangi ili kuifanya mimea ya bangi ikue haraka.

Maiti yake iligundulika siku tatu baada ya kufariki kwake baada ya marafiki zake kuzamia nyumbani kwake kupitia mlango wa nyuma.

Nyumba yake ilikuwa na joto kali sana zaidi ya nyuzi joto 40C.

Polisi walipata tabu kidogo kuingia kwenye nyumba yake ambayo ilikuwa na mahema matatu ya mashamba ya bangi ambayo yalikuwa na taa zenye kutoa joto kali sana.

Polisi wamethibitisha kuwa kifo cha Luke kimetokana na joto kutoka kwenye shamba lake la bangi.


source nifahamishe

Kichanga chateketea kwa moto

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

KICHANGA cha siku 25 kimeteketea na moto ulioshika kwenye chumba alichokuwa amelazwa baada ya mama yake kusahau kibatari na kwenda kuteka maji bombani.
.
Alisema chumba hicho kilikuwa cha mpangaji, Mwantoro Haji (30] ambaye aliwasha kibatari na kutoka kuteka maji nje ya nyumba hiyo na nyuma ndipo moto ulizuka ndani ya chumba hicho na kuteketeza kila kitu kilichomo na kusababisha kifo cha kichanga hicho.


source nifahamishe

Mapenzi Ya Mtoto wa Kitanga Yampagawisha, Aitelekeza Familia Yake

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MWANAUME mmoja [40] [jina kapuni] mkazi wa Mabibo Jeshini ,amekiri kuwa amefanyiwa mambo anayohisi ni ya kumpumbaza akili na kujikuta akikimbia familia yake na kuhamia kwa msichana mwenye asili ya kitanga bila kujitambua.
Akiongea na mwandishi wa habari hii kwenye mazungumzo ya urafiki, amekiri kuwa inawezekana amefanyiwa kitu mbaya na msichana ambaye hakumtaja jina na kumsahau mke wake na watoto na kwenda kuhamia kwa dada huyo.

Alidai kuwa alipoanza urafiki na dada huyo miezi minane nyuma alikuwa yupo katika hali ya kawaida, lakini ipipotimia kiezi mitano ya urafiki wao alijikuta akiingia katika penzi zito na dada huyo hali ambayo ilimfanya aanze kusahau kidogokidogo familia yake bila kujitambua.

Alidai kuwa alikuwa akienda kwa dada huyo na kuchelewa kurudi nyumbani kwake, mara alijikuta akishindwa kurudi kabisa nyumbani kwake na kulala hukohuko na kumpigia mke wake simu kuwa alikuwa yuko bize kazini na kurudi kesho yake.

Alisema mbaya zaidi alijiona kama yuko tofauti na kuanza kumuona mke wake kama mtu wa kawaida na kumuona dada huyo kama ni mke wake na kuona kamda kitu cha kawaida.

Kutokana na hali hiyo ya kuzidi kusahau familia yake alidai mke wake alikwenda kuripoti kwa ndugu zake yeye na kuulizwa na kukana kuwa si kweli.

Hivyo kadri siku zilivyozidi kwenda hali ndiyo ilizidi kuongezeka ya kusahau familia yake na mke wake kuwataka baadhi ya ya shemeji zake wafike nyumbani kwake walale ili wathibitishe maneno ambayo alikuwa akiwaambia ya kuwa mume wake alikuwa harudi nyumbani.

Shemeji zake hao walithibitisha tukio hilo na kuanza kulifanyia kazi susala hilo na kumfatilia ndugu yao huyo na kugundua kuwa alikuwa akizuzuliwa na mwanamke huyo.

KWa kuwa alikuwa hajitambui ilibidi ndugu hao wamkanye na kumtaka aachane na mwanamke huyo nay eye kukiri ni kweli alikuwa na mahusiano na huyo dada na kuwambia alikuwa anatamani aondokane na hali hiyo lakini alikuwa anashindwa kujinasua kuachana na huyo dada.

“yaani rafiki yangu inawezekana nimeshalishwa limbwata na yule dada kama watu wanavyosema, yaani nimefikia hatua sirudi nyumbani kwangu hii kali? Alisema kaka huyo kwenye mazungumzo na mwandishi wa habari hii

“Na sitamani kumuacha, nimewaambia ndugu zangu mwenye kujua dawa ya kunifanya nirudi nyumbani kwangu anitafutie anipe ili nisisahau kurudi nyumbani kwangu nikienda kwa yule dada, nampenda mkewangu ila ndio hali imenikuta hii” alidai


source nifahamishe

Wazazi wa watoto ombaomba wa mitaani kusakwa

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

WIZARA ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto imesema ipo katika mikakati ya kuwasaka wazazi wote wanaowatuma watoto wao kwenda kuombaomba barabarani wa lengo la kujipatia pato la siku.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo Dk. Lucy Nkya wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya famuilia.


Alisema kwa sasa serikali iko katika mikakati hiyo kabambe ya kuhakikisha inawatafuta wazazi hao ambao wanasababisha kuwe na ongezeko la watoto wa mitaani nchini kote katika ila pembe hasa mijini.

Alisema licha ya serikali kupanga mikakati hiyo ya kuwachukulia hatua wazazi wanaowatuma watoto kuomba mitaani, pia iko katika mipango ya kujua kuna watoto wangapi mitaani ili watoto hao wasaidiwe.

Alisema inafanya sense maalumu ya kujua idadi ya watoto hao ombaomba ili kuwapeleka katika vituo mbalimbali na haiwezi kutekeleza hayo hadi ijue idadi ya watoto hao.

Alisema serikali inajua kuna baadhi ya familia zinakabiliwa na changamoto kubwa ikiwa ni pamoja na kukosa mahitaji muhimu ya chakula , mavazi, malazi na kupata huduma mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

“ Hivyo tutajaribu kusaidia na serikali haitaweza kusaidia wote ila mkakati uliopo kuwapunguza watoto hao ambao wengine hawana ulazima wa kuwepo mitaani” alsiema


source nifahamishe

Amaliza Shule Akiwa na Umri wa Miaka 94

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Elimu haina mwisho wala umri, hivyo ndivyo alivyothibitisha bibi wa Marekani mwenye umri wa miaka 94 mwenye wajukuu na vitukuu 41 ambaye mwishoni mwa wiki alisherehekea kumaliza elimu ya shahada ya kwanza na kuwa kikongwe wa pili duniani kumaliza elimu ya juu.
Bibi Hazel Soares, mwenye umri wa miaka 94 wa Oakland, Marekani alikuwa miongoni mwa wanafunzi 500 waliotunukiwa shahada mbalimbali za chuo kikuu.

"Imenichukua muda mrefu sana kumaliza digrii kwakuwa nilikuwa bize sana kwenye maisha yangu",alisema Soares ambaye sasa anamiliki digrii ya Art history.

Soares, ana watoto sita na wajukuu na vitukuu wapatao 40, anashika nafasi ya pili duniani kwa kumaliza digrii akiwa na umri mkubwa sana.

Nola Ochs wa Kansas ndiye anayeshikilia rekodi ya kumaliza digrii akiwa na umri mkubwa kuliko watu wote duniani. Alitunukiwa digrii miaka mitatu iliyopita baada ya kumaliza masomo yake kwenye chuo kikuu cha Fort Hays State University wakati huo akiwa na umri wa miaka 95.

source nifahamishe

Aliyeiba Mtoto Toka Kwenye Mimba ya Mwenzake Afungwa Maisha

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alimlaghai mwanamke mjamzito na kumpeleka nyumbani kwake kabla ya kulipasua tumbo lake kwa kisu kwa nia ya kuiba kichanga chake, amehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alikuwa na shauku ya muda mrefu ya kuwa na mtoto, amehukumiwa kwenda jela maisha baada ya kuiba kichanga toka kwenye tumbo la mwanamke mjamzito.

Andrea Curry-Demus, 40, alipatikana na hatia ya kumuua mwanamke mjamzito Kia Johnson, 18 baada ya kulipasua tumbo lake na kisha kuiba kichanga kilichokuwa tumboni mwake na kujifanya yeye ndiye aliyejifungua kichanga hicho.

Curry-Demus akisomewa hukumu yake aliigeukia familia ya Kia na kuwaambia "Naomba mnisamehe".

"Naiomba radhi familia yake", alisema Curry-Demus kabla ya kumgeukia jaji na kusema "Nimekosa".

Mama yake Kia, Darlene Lee, aliridhishwa na hukumu iliyotolewa ya kifungo cha maisha jela akisema kuwa hakutaka Curry-Demus ahukumiwe adhabu ya kifo kwakuwa anataka ateseke kwa uovu alioufanya.

"Nataka ateseke na aione sura ya mwanangu kila siku anapoamka, afikirie kitendo alichofanya".

Hili si tukio la kwanza la Curry-Demus kujaribu kuiba kichanga toka kwenye tumbo la mwanamke mjamzito, miaka 20 iliyopita, Curry-Demus alihukumiwa kwenda jela miaka 10 baada ya kumchoma na kisu tumboni mwanamke mjamzito akiwa
na nia ya kulipasua tumbo lake na kuiba kichanga chake.

Katika tukio la hivi karibuni Curry-Demus aliiongopea familia yake kuwa yeye ni mjamzito baada ya kumlaghai Kia na kujifanya rafiki yake.

Alikuwa akitamba kwa marafiki zake kuwa yeye ni mjamzito akiwaonyesha picha ya Ultrasound aliyoiiba toka kwa Kia na kisha kuibandika jina lake.

Baada ya kutimiza azma yake ya kuiba kichanga cha Kia, aliiambia familia yake kuwa amejifungua mtoto kabla ya muda wake ingawa vipimo vya hospitali havikuonyesha kama aliwahi kuwa mjamzito.

Alitiwa mbaroni baada ya maiti ya Kia kugundulika nyumbani kwake baada ya majirani kulalamikia harufu kali toka nyumbani kwake.

Kichanga alichokiiba kilinusurika maisha yake na kiliwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi.


source nifahamishe

Aunguzwa Vibaya Mkono na Mama wa Kambo Kwa Kudokoa Samaki

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka saba wa wilaya ya Tarime mkoani Mara ameunguzwa vibaya vidole vyote vya mkono wake na mama yake wa kambo baada ya kudokoa samaki aliporudi kutoka shule akiwa na njaa
Polisi wilayani Tarime wamemtaja mtoto huyo kuwa ni Matiko Mwita anayesoma shule ya msingi ya Abainano.

"Mama yake wa kambo alikasirika na kuunguza mkono wake wa kulia kwa moto wa mkaa sababu ikiwa ni kitendo cha mtoto huyo kula kipande cha samaki aliporudi toka shuleni", alisema kamanda msaidizi wa polisi wilaya ya Tarime, Constantine Masawe.

"Nilikuja toka shule na kukuta samaki na ugali lakini mama yangu wa kambo aliponikuta nakula alinuuliza kwanini nakula chakula na ndipo alipoanza kuniunguza na moto mkononi", alisema mtoto Matiko.

Matiko aliungua vibaya vidole vyote vitano vya mkono wake wa kulia kufuatia kitendo hicho cha mama yake wa kambo.

Polisi wanamtafuta mwanamke huyo ambaye alikimbia pamoja na mumewe baada ya suala hilo kufikishwa polisi.

Kamanda Masawe alimtaja mwanamke huyo kuwa ni Pili Mwita mkazi wa kijiji cha Motana wilayani Tarime mkoani Mara.

"Tunamtafuta pia mumewe kwasababu hakutoa taarifa yoyote polisi mpaka mwalimu wake alipomleta mtoto huyo kituo cha polisi".

Mtoto Matiko baada ya kupatiwa matibabu amepelekwa kwenye kituo cha kulea watoto yatima kilichopo kwenye kijiji cha Gamasara nje kidogo ya Tarime.

source nifahamishe

Amuua Mkewe Na Kisha Kuila Maiti Yake

Monday, May 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela miaka 15 baada ya kumuua mkewe kwa kumchoma choma na kisu mara 250 na kisha kula nyama za mapafu yake kabla ya kunywa damu yake mbele ya mtoto wake wa miaka minne.
Mohammad Solaiman alihukumiwa kwenda jela kati ya miaka 15 na kifungo cha maisha kwa kumuua kikatili mkewe Shahida Sultanna ndani ya nyumba yao mjini New York katika tukio lililotokea mwaka 2007.

Binti yao mwenye umri wa miaka minne alikuwa chumba cha pili wakati baba yake alipokuwa akimuua mama yake na alishuhudia kitendo cha baba yake akinywa damu ya mama yake.

"Alichukua maini na mapafu yake na kuyatafuna", alisema dada wa marehemu na kuongeza "Alikunywa damu yake, binti yake ameniambia".

Wakili wa Solaiman, John Scarpa alikanusha madai ya Solaiman kumgeuza asusa mkewe ingawa alikubali kumuua mkewe.

Wakili huyo aliendelea kusema kuwa Solaiman alikuwa akipigwa na kunyanywaswa sana na mkewe na hiyo ndio sababu iliyompelekea kufanya mauaji.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo, jaji Richard Buchter alisema kuwa faili la mshtakiwa halikusema chochote kama alikuwa akinyanywaswa na mkewe.

"Tunachojua ni kwamba, mshtakiwa alimchoma na kisu mkewe usoni, shingoni, tumboni, mgomgoni na kwenye maeneo yake ya siri", jaji Buchter alisema.

"Kuthibitisha kitendo chake cha kikatili alimuonyesha binti yake wa miaka minne mabaki ya mwili wa mama yake", aliongeza jaji Buchter.

Solaiman alihukumiwa kwenda jela kati ya kifungo cha miaka 15 na kifungo cha maisha baada ya kukiri kufanya mauaji hayo.

source nifahamishe

Mwarabu Kuiwakilisha Marekani Mashindano ya Urembo ya Dunia

Monday, May 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mrembo toka Michigan, Rima Fakih ameshinda mashindano ya urembo wa Marekani Miss USA 2010 na kuwa mwarabu wa kwanza kushinda mashindano hayo makubwa ya urembo nchini Marekani.
Rima Fakih Mmarekani mwenye asili ya Lebanon amekuwa Mwarabu-Mmarekani wa kwanza kushinda mashindano ya Miss USA katika historia ya mashindano hayo.

Katika mashindano yaliyofanyika mjini Las Vegas na kuonyeshwa live na televisheni ya NBC, Fakih aliwafunika jumla ya warembo 50 toka majimbo mbalimbali ya Marekani na kutwaa taji la Miss USA 2010.

Fakih mwenye umri wa miaka 24, alitwaa taji la urembo wa Marekani akifuatiwa na Miss Oklahoma aliyeshika nafasi ya pili, Miss Virginia, Miss Colorado na Miss Maine.

Fakih ataiwakilisha Marekani kwenye mashindano ya urembo ya Miss Universe yatakayofanyika baadae mwaka huu.


source nifahamishe

Wanafunzi Wanyonyana Sehemu za Siri Darasani Huku Mwalimu Akichekelea

Sunday, May 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwalimu mmoja wa nchini Marekani anafanyiwa uchunguzi baada ya kuwaachia wanafunzi wake wanyonyane sehemu za siri darasani huku wanafunzi wengine wakichukua video za tukio hilo na kupiga picha.
Televisheni ya KTLA ya Marekani imeripoti kuwa tukio hilo limetokea kwenye shule ya Haydock Intermediate School iliyopo Oxnard, California ambapo mwanafunzi wa kike na wa kiume walinyonyana sehemu za siri darasani mbele ya wanafunzi wenzao waliojaa darasani kwaajili ya kuangalia filamu iliyoandaliwa na mwalimu huyo.

Mwanafunzi wa kiume wa darasa la nane na mwanafunzi wa kike wa darasa la saba ndio waliohusika katika tukio hilo ambalo limewakasirisha wazazi wengi nchini Marekani.

Wanafunzi walichukua video za tukio hilo kwa kutumia simu zao huku wengine wakipiga picha ambapo mwalimu wao alipuuza na hakuchukua hatua yoyote ile kuzuia kitendo hicho kiovu darasani.

Mwalimu huyo amepewa likizo yenye malipo wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.

Wanafunzi waliofanya kitendo hicho hawajachukuliwa hatua yoyote na wanahudhuria shuleni kama kawaida.

Sylvia Ramirez, mmoja wa wazazi ambaye anafanya kazi katika mgahawa wa shule hiyo alisema kuwa ameiona video ya ngono ya wanafunzi hao.

"Inasikitisha sana kuona hawalitilii uzito suala hili, shoo ya ngono inafanyika darasani, inasikitisha sana", alisema Ramirez.

Polisi wanalifanyia uchunguzi tukio hilo baada ya kupewa taarifa.


source nifahamishe

Waislamu Walazimishwa Kula Nguruwe Ili Ziwape Nguvu

Sunday, May 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wanawake watatu wa kiislamu toka nchini Indonesia walilazimishwa na bosi wao katika kiwanda cha nguo nchini Taiwan wale nyama ya nguruwe ili ziwape nguvu na stamina ya kufanya kazi.
Wanawake watatu wa kiislamu ambao ni raia wa Indonesia, walilazimishwa na bosi wao katika kiwanda cha nguo mjini Taipei wale nyama ya nguruwe au la mishahara yao itapunguzwa.

Kwa muda wa miezi saba wanawake hao walilazimishwa na bosi wao kula vyakula vyenye nyama ya nguruwe vilivyokuwa vikigaiwa kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho kwakuwa bosi wa kiwanda hicho alikuwa akiamini kuwa nyama ya nguruwe ingewapa nguvu na stamina ya kufanya kazi wanawake hao.

Bosi wa kiwanda cha nguo cha Shin Hua Hang Fashion Co, Chang Wen-lin amefikishwa mahakamani kwa kuwalazimisha wanawake hao wale nyama ya nguruwe katika kipindi cha ajira yao kuanzia mwezi septemba 2008 hadi April 2009.

Katika jalada la kesi aliyofunguliwa mahakamani, Cheng aliamini kuwa nyama ya
nguruwe ingewapa stamina ya kufanya kazi wanawake hao na alitishia kuwakata mishahara yao iwapo wasingekubali kula nyama hiyo.

Waendesha mashtaka wanataka Chang Wen-Lin ahukumiwe kwenda jela miezi minane.

Wanawake hao walipelekea malalamiko yao kwa taasisi ya kutetea wafanyakazi mjini Taipei ambapo walisema kuwa walifanyishwa kazi nyingi kuliko kawaida katika kipindi cha miezi minane bila ya kulipwa chochote.

Taasisi hiyo ndiyo ililifikisha suala hilo mahakamani kwa niaba ya wanawake hao ambao kutokana na hofu za masuala ya uhamiaji walikuwa wakihofia kurudishwa kwao iwapo wangemchukulia hatua bosi wao.

Wanawake hao hivi sasa wametafutiwa kazi kwenye kampuni nyingine mjini Taipei.

Kuna vibarua takribani 350,000 nchini Taiwan ambapo wengi wao wanatoka Indonesia, Philippines na Vietnam.

Katika ripoti ya mwaka 2009 ya haki za binadamu duniani, tatizo kubwa lililotajwa kuikabili Taiwan lilikuwa ni unyanyasaji wa wafanyakazi makazini.

Ripoti hiyo ilisema kuwa wafanyakazi wengi huogopa kuripoti matatizo yanayowakabili kwa kuhofia kupoteza ajira zao.

source nifahamishe

Mwanaume na Mwanamke Wabakwa Afrika Kusini

Sunday, May 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa mjini Cape Town nchini Afrika Kusini amepandishwa kizimbani kwa kuwabaka wafanyakazi wenzake wawili, mmoja ni mwanaume na mwingine ni mwanamke.
Mwanaume aliyebakwa aliiambia mahakama ya Cape Town kuwa siku ya tukio ambayo kulikuwa na party ya wafanyakazi, alikunywa sana pombe kiasi cha kupitiwa na usingizi.

Mwanaume huyo alisema kuwa alipoamka aliona mambo hayako sawa kwenye maungo yake ya nyuma akihisi hali tofauti.

Mwanaume huyo aliendelea kusema kuwa aligundua kuwa alikuwa amelawitiwa baada ya kurudi kazini siku chache baadae na kusikia wafanyakazi wenzake wakijadili jinsi alivyofanyiwa mchezo mbaya na mwanaume mwenzake.

Mwanaume huyo aliiambia mahakama kuwa aliambiwa na mfanyakazi mwenzake aliyeshuhudia tukio hilo kuwa alimuona mfanyakazi mwenzao akijiandaa kumbaka lakini hakuchukua hatua yoyote.

Mwanaume huyo aliongeza kuwa alienda polisi ambapo alifanyiwa uchunguzi uliothibitisha kuwa aliingiliwa kinyume cha maumbile.

Mwanamke aliyebakwa ni mpenzi wa shuhuda aliyemuona mwanaume akibakwa.

Mwanamke huyo alisema kuwa mtuhumiwa alimkaba koo kwa nguvu na alipozimia mtuhumiwa alimbaka na kumuibia simu yake.

Ripoti ya daktari ilithibitisha kuwa mwanamke huyo alibakwa.

Mtuhumiwa amekanusha madai yote mawili ya ubakaji. Uchunguzi wa kesi hiyo unaendelea.

source nifahamishe

Afariki Baada ya Kuona Maiti za Ajali ya Ndege

Sunday, May 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Afisa mmoja wa Libya amefariki baada ya kuona maiti za ajali ya ndege wakati alipokimbilia kwenye eneo la tukio kutoa msaada.
Afisa huyo ambaye ni mlinzi kwenye uwanja wa ndege alifariki baada ya kuona maiti za watu 102 waliokuwemo kwenye ndege ya Libya ambayo ililipuka wakati wa kutua kwenye uwanja wa ndege wa Tripoli.

Taarifa zinasema kuwa mlinzi huyo alikimbilia kwenye eneo la ajali kwa nia ya kutoa msaada lakini alipofika na kuziona maiti zikiwa zimezagaa kila kona ugonjwa wake wa kisukari ulimzidia na hapo hapo aliiaga dunia.

Taarifa zaidi kuhusiana na kifo chake hazikutolewa ingawa taarifa zilisema kuwa mlinzi huyo alikuwa ni mzee.

Wakati huo huo mtu pekee aliyenusurika kwenye ajali hiyo mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa, Ruben, amesafirishwa leo kurudishwa kwao Uholanzi.

Ruben alikuwa na baba yake, mama yake pamoja na kaka yake mwenye umri wa miaka 11 kwenye ndege hiyo lakini wote walifariki kwenye ajali hiyo.

Ruben na wazazi wake pamoja na kaka yake walikuwa likizo nchini Afrika Kusini kusherehekea ndoa ya wazazi wake kutimiza mwaka mmoja.

Shangazi na mjomba wake toka Uholanzi walikimbilia mjini Tripoli kuwa karibu na mtoto huyo ambaye alikuwa akipatiwa matibabu kutokana na majeraha kadhaa kwenye miguu yake.

Mtoto huyo ameishaambiwa na shangazi yake kuwa wazazi wake na kaka yake wamefariki kwenye ajali hiyo mbaya ya ndege

source nifahamishe

Mshindi wa Tuzo Milionea Akabidhiwa Milioni 100 Zake

Sunday, May 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania imemkabidhi hundi ya shilingi milioni 100 mshindi wa Promosheni ya Tuzo milionea Bw. Bernard John (27) mkazi wa Morogoro.
Bw. Bernard John (27) alikabidhiwa mshiko wake katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwake na kuhudhuriwa na maofisa wa Vodacom ndugu jamaa na marafiki.

Ujumbe wa Vodacom Tanzania uliongozwa na Mkuu wa Uendeshaji wa Vodacom Tanzania Peter Correia ambaye pamoja na mambo mengine alimpongeza mshindi huyo na kumshauri azitumie fedha hizo kuboresha maisha yake.

“Kwa niaba ya Vodacom Tanzania, ninapenda kuchukua fursa hii kukupongeza sana ni furaha iliyoje kuona mwenzetu katika familia kubwa ya Vodacom Tanzania yenye wateja zaidi ya milioni saba anabadilisha maisha yake kwa kuyaboresha,” alisema.

John alishinda kupitia droo kubwa iliyochezeshwa na kampuni hiyo na kuonyeshwa moja kwa moja kupitia kituo cha televisheni cha ITV chini ya usimamizi wa bodi ya michezo ya kubahatisha nchini.

Akiongea katika hafla hiyo, John aliishukuru Vodacom kwa kuanzisha promosheni hiyo ambayo alisema inaboresha maisha ya wateja wa Vodacom.

“Kwakweli ninaipongeza Vodacom Tanzania kwa kuanzisha promosheni hii ambayo imebadilisha kabisa maisha yangu na kuwa yenye matumaini, nitazitumia fedha hizi kwa kujiendeleza zaidi kielimu na manufaa ya familia yangu na jamii yangu inayonizunguka,”alisema.

Promosheni ya Tuzo Milionea kwa mwaka huu, ilianza mapema mwezi Februari lengo likiwa ni kuwarejeshea wateja wa Vodacom sehemu ya kile Vodacom inachokipata na pia kuboresha maisha ya wateja wake.

Correia alifafanua kuwa tangu kuanza kwa promosheni hiyo ambayo imedumu kwa miezi mitatu sasa, wateja wa wameweza kujishindia zawadi mbalimbali zikiwa ni pamoja na muda wa maongezi.

Correia alisema kuwa kupitia Promosheni ya Tuzo Milionea, wateja Saba wa Vodacom walijishindia muda wa maongezi wenye thamani ya sh. 100,000 kupitia droo za kila wiki na hadi mwisho wa promosheni hiyo wateja wetu watajishindia muda wa maongezi wenye thamani ya shilingi milioni tisa.

Aidha aliongeza kuwa Promosheni hii ni mwendelezo wa promosheni ya Tuzo milionea iliyoendeshwa na Vodacom Tanzania kwa mwaka jana.

“Kama mtakumbuka mshindi wa droo kubwa ya mwaka jana alikuwa ni Renatus Mkinga, Mkazi wa Mombasa, Ukonga Jijini Dar es Salaam, ambaye alishinda shilingi milioni 100 na kuboresha maisha yake”.

Akitoa wito kwa wateja wengine kushiriki mara nyingi katika promosheni mbalimbali zinazochezeshwa na kampuni hiyo kwa siku za usoni Bw Correia aliwahakikishia kuwa zitawawezesha kuibuka kidedea na kuboresha maisha yao.

“Tutaendelea kuwekeza ili kuboresha huduma zetu mbalimbali kwa kuwa tunaamini kwamba huduma bora na za uhakika za mawasiliano ni sehemu ya maendeleo, kwani maendeleo ya nchi yoyote yanachangiwa na huduma za mawasiliano zenye uhakika” Alisema.

source nifahamishe