UZURI WA KUMSAMEHE MPENZI WAKO............

Sunday, June 12, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Ni vizuri kusamehe na kusahau ili uweze kuishi maisha ya furaha na amani.

Katika maisha inapotokea kuna mtu amekukera inawezekana akawa ni mwenza wako lakini baadaye akakuomba msamaha kwa kile alichokosea kama kweli umeamua kumsamehe basi ni vizuri kujiepusha kuwa na kinyongo yaani ile hali ya kusamehe huku bado moyoni kile kitu unacho kinakusumbua na wakati mwingine labda unayo nia ya kulipiza kisasi au bado unapenda kuzungumzia makosa ya zamani wakati ulishasamehe haipendezi kuwa na tabia ya kutosahau baada ya kusamehe kwani hata wewe mwenyewe binafsi unakuwa hujitendei haki kwani unajidanganya na pia utaendelea kuuumia kutokana na kushindwa kusahau naamini huwa inakuwa ni vigumu kusahau kulingana na uzito wa kosa lakini kama umeamua kusamehe basi samehe kwa moyo wako wote ili uweze kuwa huru na yule umpendaye .