YUSSUF CHUCHU AZIKWA LEO JIONI

Saturday, June 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)





umati wa watu umejitokeza katka mazishi ya marehemu chuchu ambayo yamefanyika huko mwanakwerekwe

MOLA AMLAZE PEMA PEPONI
AMIN...........

YUSSUF CHUCHU AFARIKI DUNIA..............

Saturday, June 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




MOLA AMSAMEHE MADHAMBI YAKE NA AMPE SAFARI NJEMA NA MAKAZI MEMA PEPONI.......AMIN

George Bush Ajiunga na Facebook

Friday, June 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais wa zamani wa Marekani, George Bush amejiunga na mtandao wa Facebook na kufanikiwa kuwavuta wanachama 65,000 katika muda mfupi, hata hivyo baadhi ya wanachama wake wanalalamika kuwa Bush anayafuta maoni yao wanapomkosoa.
Mtandao wa FACEBOOK umepata mwanachama mwingine ambaye ni rais wa zamani wa Marekani, George W Bush.

Bush alijiunga na mtandao wa Facebook jana na alifanikiwa kupata wanachama zaidi ya 2,000 ndani ya masaa machache. Hadi sasa jumla ya watu 65,000 wamejiunga na ukurasa wa Bush.

Ujumbe wa kwanza katika ukurasa wa Bush uliezea kazi alizofanya Bush tangu alipoondoka madarakani januari 2009.

"Rais Bush ameendelea kuchapa kazi, ametembelea majimbo 20, nchi 8 na ametoa jumla ya hotuba 65 na ameshiriki kikamilifu katika miradi kadhaa ya maendeleo ikiwemo mfuko wa kusaidia Haiti ambao aliuanzisha kwa kushirikiana na rais mstaafu Bill Clinton".

Meseji nyingi zilizoandikwa na wanachama wa Bush ni za kumsifia sana kwa kipindi chake cha urais.

"Mungu akubariki, ahsante kwa uongozi wako wa taifa hili kubwa, tutakumiss sana". alisema jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Matt Thullen.

Hata hivyo baadhi ya wanachama wake walilamika kuwa maoni yao ya kumkosoa Bush yalifutwa.

Ukurasa wa Facebook wa Bush unapatikana kwa linki hii:
facebook.com/georgewbush


source nifahamishe

Afukuzwa Kazi Kwasababu ya Urembo Wake

Friday, June 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja nchini Marekani amefukuzwa kazi kwasababu ni mrembo sana na nguo za kazi anazovaa zinawachengua wafanyakazi wenzake wa kiume.
Debrahlee Lorenzana mama wa mtoto mmoja alikuwa mfanyakazi wa benki ya Citibank lakini umbo lake namba nane na urembo wake ulikuwa ukiwachanganya wafanyakazi wenzake wa kiume kiasi cha kuzorotesha ufanisi wao wa kazi.

Debrahlee mwenye umri wa miaka 33 aliambiwa kwamba nguo za kazini anazovaa kama wafanyakazi wenzake wa kike zinawachengua mabosi wake kiume na wafanyakazi wenzake.

Baada ya malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi wanaume, mabosi wake walimshauri Debrahlee asivae baadhi ya viwalo vya kazini kwakuwa vinamfanya aonekane mrembo zaidi.

Debrahlee alipeleka malalamiko kwenye menejimenti ya benki hiyo akiuliza sababu ya kuzuiwa kuvaa nguo ambazo wafanyakazi wenzake wanaruhusiwa kuvaa.

Katika majibu aliyopewa kufuatia malalamiko yake hayo, Debrahlee aliambiwa kuwa wafanyakazi wenzake wa kike wanaweza wakavaa chochote wakipendacho kwakuwa hawana mvuto.

Aliambiwa pia kwakuwa yeye ana umbile namba nane na ameenda hewani sekunde, asivae viatu vyenye soli ndefu kwakuwa vinalifanya umbile lake lionekane vizuri hivyo kuwachanganya zaidi mameneja wake wanaume.

Baada ya miezi 10 katika benki hiyo, Debrahlee alihamishwa kikazi na kupelekwa kwenye tawi jingine la benki hiyo lakini huko alifukuzwa kazi ndani ya mwezi mmoja akiambiwa kuwa ana ufanisi mdogo.

Debrahlee ameenda mahakamani kupinga kufukuzwa kazi.

source nifahamishe

Nokia Yatoa Simu Zinazochajiwa na Baiskeli

Friday, June 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kampuni kongwe ya simu duniani, Nokia imezitambulisha simu zake mpya za bei chee zenye laini (SIM card) mbili ambazo betri zake huchajiwa na dainamo ya baiskeli.
Simu hizo zilitambulishwa kwa watu jana nchini Kenya ambapo Nokia imesema kuwa imelenga kuziuza kwa bei chee ingawa simu hizo ndio zitakuwa simu za kwanza za Nokia kutumia laini mbili.

Simu hizo pia zina radio na tochi na vionjo vingine vya kawaida.

Simu hizo zinazoitwa Nokia C1-00 zitauzwa kati ya Tsh. 50,000 na Tsh. 90,000 wakati chaja yake itakayotumika kwenye baiskeli itauzwa kuanzia Tsh. 15,000.

Chaja ya simu hiyo inatumia dainamo ya baiskeli hivyo spidi ya mtu kuendesha baiskeli ndivyo betri litakavyojaa chaja nyingi.

Safari ya dakika 10 kwa spidi ya kilomita 10 kwa saa italichaji betri na kukuwezesha kuongea mfululizo dakika 28 au masaa ya 37 ya simu kuwa ON.

Nokia imesema kuwa simu hizo zimelenga zaidi maeneo ya Afrika ambako umeme unapatikana kwa tabu.


source nifahamishe

Mapenzi Yanapozidi..

Friday, June 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Uingereza kwa uchungu aliokuwa nao wa kuondokewa na mpenzi wake, aliamua kuishi na maiti ya mpenzi wake ndani ya nyumba yake akiimwagia pafyumu nyingi sana ili kuzuia harufu isitoke nje.
Gabriel Brown, 54, aliishi na maiti ya mpenzi wake akiiweka kwenye kochi na kuyanyunyuzia pafyumu mabaki yake ya mwili wake ambao uliendelea kuoza ili kuzuia harufu isitoke nje ya nyumba yake.

Gabriel aliishi hivyo kwa takribani miezi 10 hadi alipotiwa mbaroni mwezi disemba mwaka jana baada ya maiti ya mpenzi wake Lynn Warman, 37, ilipokutwa kwenye kochi nyumbani kwake ikiwa imezungukwa na makopo ya pafyumu.

Brown aliwaambia polisi kuwa mpenzi wake alifariki februari 9, 2009 lakini kutokana na majonzi aliyokuwa nayo hakutaka kutoa taarifa polisi.

Brown alishikiliwa na polisi kama mtuhumiwa wa kifo cha mpenzi wake lakini aliachiwa kwa dhamana wakati polisi wakiendelea na uchunguzi.

Wakati polisi wakiendelea na uchunguzi kutafuta ukweli wa kifo cha mpenzi wake, Brown naye alikutwa amefariki baada ya kupoteza damu nyingi wakati alipopata ajali.

Uchunguzi wa maiti ya Lynn ulionyesha kuwa hakuuliwa na alifariki akiwa amekaa kwenye kochi ambalo maiti yake ilikutwa.

Mmoja wa majirani zake alisema: "Brown na Lynn walikuwa wakipendana sana, inasikitisha kusikia kwamba maiti ya Lynn ililala kwenye kochi karibia mwaka huku Brown akiishi nyumba hiyo hiyo".

"Sijui aliwezaje kuishi kwenye harufu mbaya ya maiti iliyoharibika, Natumaini watapumzika kwa amani huko waliko", aliongeza kusema jirani huyo.


source nifahamishe

Shirika la ndege la Oman lazindua safari zake Dar es salaam - Oman

Friday, June 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kuanzia sasa shirika la ndege la Oman litaanza safari zake mfululizo kati ya miji ya muscat na Dar-es-salaam.
Safari hizo zitaanza kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Muscat kila siku ya jumamosi, Jumatatu na Jumatano kwa wiki,Ndege Zitakazo geuza kurudi Muscat Zitaanza safari katika kiwanja cha kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere, Dar-es-salaam na kupitia vituo vingine kuelekea Muscat.Shirika la ndege la Oman linafanya safari zake katika vituo 38 Duniani.

Mkurugenzi mtendaji wa Oman Air Way, Peter Hill Anasema: “Oman Air Way imedhamiria kupanua zaidi wigo wake wa kibiashara kwa kuiongeza Dar es Salaam kwenye safari zake na tutafanya kazi hii kwa bidii bila kuchoka ili kuhakikisha tunatimiza malengo yetu.

Mkurugenzi huyo anasema ‘‘ Tukiwa na historia nzuri ya siku nyingi ya kibiashara baina ya Tanzania na Oman tuna uhakika mkubwa sana wa kuendelea kujenga na kuendeleza uhusiano huu wa nchi hizi mbili kupitia huduma zetu za ndege.

Anasema ikijulikana kwa vivutio vyake vya asili, Dar-es-salaam inatazamiwa kuwa na umaarufu wa safari za kitalii zaidi kutoka duniani kote kulingana na thamani yake, Pia kama sehemu maalum ya kufurahia mapumziko ya likizo kubwa za mwaka.

Huduma zetu katika nchi yenye mvuto wa kipekee Tanzania zitaambatana na wasafiri wenye kutambua vitu vizuri na wenye uchaguzi mzuri wa nchi nzuri za kitalii kama Tanzania.

Dar es salaam ndio mji mkubwa zaidi wa kibiashara katika Tanzania ndiyo maana tunaiunganisha Dar es salaam na Dunia.

Anafafanua kwamba ukiwekwa kama mji wa kitalii na njia kuu ya watalii wanaopitia kwenda kupata mapumziko katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Zanzibar tunaamini kwamba tutakua sehemu ya kukuza utalii nchini Tanzania.


source nifahamishe

Wanaume Waliooana Malawi Waachiwa Huru Baada ya Wafadhili Kupiga Mkwara

Sunday, May 30, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wanaume wawili waliooana nchini Malawi ambao walitupwa jela miaka 14 wiki iliyopita kwa kuvunja sheria na kukiuka maadili ya kiafrika wameachiwa huru baada ya Malawi kuelemewa na shinikizo kubwa la mataifa wafadhili.
Baada ya shinikizo kubwa toka nchi za magharibi, serikali ya Malawi imerudi nyuma katika harakati zake za kupambana na tabia ya ushoga na usagaji kwa kuwaachia huru wanaume wawili waliooana ambao walitupwa jela miaka 14 hivi karibuni.

Steven Monjeza, 26, na "Mkewe" Tiwonge Chimbalanga, 20, walitupwa jela miaka 14 wiki iliyopita baada ya kufunga ndoa na kufanya sherehe iliyohudhuriwa na watu 500.

Mataifa ya magharibi yakidai yanatetea haki za binadamu yalipinga kufungwa kwa Monjeza na mwenzake yakisema kuwa Monjeza na mwenzake hawajafanya kosa lolote zaidi ya kupendana kama wanavyopendana watu wengine.

Serikali ya Uingereza ililaani hukumu iliyotolewa dhidi ya Monjeza na mwenzake ikisema kuwa Malawi imekiuka misingi ya haki za binadamu.

Uingereza ambayo ndiyo mfadhili mkubwa wa Malawi, ilisema kuwa inajadili upya msaada wa paundi milioni 80 ambao Malawi hupewa kila mwaka.

Rais wa Malawi, Bingu wa Mutharika, akiongea na waandishi wa habari leo akiwa pamoja na katibu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, aliagiza Monjeza na mkewe waachiwe huru mara moja.

"Hawa vijana wamefanya kosa dhidi ya utamaduni wetu, dini yetu na sheria zetu lakini hata hivyo nikiwa kama mkuu wa nchi nimewapa msamaha na ninaagiza waachiwe huru bila masharti yoyote", alisema rais Bingu wa Mutharika.

Naye katibu wa Umoja wa Mataifa ambaye alikuwepo kwenye mkutano huo na waandishi wa habari uliofanyika ikulu, alimpongeza rais Bingu wa Mutharika kwa uamuzi wake wa kishujaa wa kulinda haki za binadamu na kuwaachia huru mashoga hao wawili.

source nifahamishe