Osama Bin Laden Atishia Usalama Kombe la Dunia

Wednesday, April 14, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kundi la Al-Qaeda linaloongozwa na Osama Bin Laden limetishia usalama kwenye kombe la dunia nchini Afrika kwa kuahidi kufanya shambulizi la kigaidi litakaloua mamia ya watu wakati wa mechi kati ya Marekani na Uingereza.
Kundi la Al-Qaeda limetishia kuwaua mamia ya watu watakaohudhuria mechi kati ya Marekani na Uingereza kwenye kombe la dunia nchini Afrika Kusini mwezi juni mwaka huu.

Kundi linalojiita Al-Qaeda in the Islamic Maghreb, limetoa taarifa kwenye website likisema kuwa watu wa kujitoa mhanga wakiwa na mabomu ambayo si rahisi kugundulika kwenye mitambo ya ulinzi, wako tayari kujilipua kwenye mechi kati ya Uingereza na Marekani kwenye uwanja wa Rustenburg juni 12 mwaka huu.

Kundi hilo liliweka taarifa hiyo kwenye tovuti inayoitwa "Mushtaqun Lel Jannah" (Njia ya kuelekea peponi).

"Al-Qaeda watakuwepo kwenye mechi za kombe la dunia", ilisema taarifa hiyo ya Al-Qaeda.

"Litakuwa ni jambo la kufurahisha sana wakati wa mechi kati ya Marekani na Uingereza ikirushwa live kwenye luninga wakati sauti ya mlipuko itakaposikika kwenye majukwaa na kuugeuza uwanja mzima juu chini", iliendelea kusema taarifa hiyo ya Al-Qaeda.

Uingereza na Marekani zipo kwenye kundi moja la C pamoja na Algeria na watapimana ubavu juni 12 kwenye uwanja wa King Bafokeng mjini Rustenburg unaochukua watazamaji 44,500.

Maafisa wa Marekani wamesema kuwa vitisho hivyo vya Al-Qaeda vinachukuliwa kwa uangalifu mkubwa katika kuhakikisha usalama kwenye fainali hizo za kombe la dunia zitakazochukua mwezi mmoja.

Maafisa wa usalama wa Uingereza wamekataa kusema chochote.

Mwezi oktoba mwaka jana, maafisa wa usalama wa Afrika Kusini walisema kuwa wamefanikiwa kulizima jaribio la shambulizi la kigaidi lililokuwa limepangwa lifanyike wakati wa fainali hizo.

Iliripotiwa kuwa maafisa wa Afrika Kusini kwa kushirikiana na maafisa wa Marekani walifanikiwa kuwatia mbaroni watu wanaodaiwa kuwa ni wanachama wa Al-Qaeda nchini Somalia na Msumbiji ambao walikuwa wakijiandaa kufanya shambulizi wakati wa fainali za kombe la dunia.

Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa jumla ya polisi 44,000 watalinda usalama kwenye fainali hizo.

source nifahamishe

Mwanaume Mwenye Bahati Mbaya Kuliko Wote Uingereza

Wednesday, April 14, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mkulima wa nchini Uingereza Mick Wilary ambaye anadaiwa kuwa ndiye mtu mwenye bahati mbaya kuliko wote nchini Uingereza kutokana na ajali kibao zinazomkumba, amepata ajali kwa mara nyingine tena iliyoivunja miguu yake yote miwili.
Mick Wilary, mwenye umri wa miaka 58 anadaiwa kuwa ndiye mtu ambaye hana tabasamu kutokana na bahati mbaya zinazomkumba na kumfanya akumbwe na ajali mbaya zinazoyatia maisha yake hatarini.

Mick ameishakumbwa na ajali mbaya zaidi ya 30 na ajali hizo zimepelekea kuvunjika kwa mifupa ya viungo vyake 15.

Katika tukio la hivi karibuni, Mick anaendelea kupatiwa matibabu hospitalini baada ya miguu yake kupondwa na tingatinga.

Katika tukio hilo dereva wa tingatinga akiliendesha tingatinga hilo modeli ya JCB bila ya kuwa mwangalifu, alimgonga Mick na kumbamiza ukutani.

Katika tukio hilo mguu wa kushoto wa Mick ulivunjika na kupinda kuelekea mabegani wakati mguu wake wa kulia ulijeruhiwa na kugeuka ukiangalia nyuma.

Hata hivyo pamoja na ajali hiyo mbaya ya kutisha, madaktari katika hospitali ya Newcastle wamefanikiwa kuiokoa miguu yake na wamesema kuwa ndani ya miezi sita Mick ataweza tena kuitumia miguu yake kutembea.

Ajali ya kuvunjika kwa miguu yake imetokea ikiwa ni miezi michache baada ya kuvunjika kwa enka za miguu yake yote miwili baada ya kuteleza na kuanguka chini alipokanyaga kiazi mviringo.

Miongoni mwa ajali mbaya zilizowahi kumkumba Mick ni kupasuka kwa fuvu la kichwa chake kwenye sakafu alipopigwa mweleka na paka.

Mick pia ameishawahi kuvunjika mbavu, shingo na mikono katika mfululizo wa ajali mbaya zinazoendelea kumkumba ambazo zimeifanya sura yake ikose tabasamu wakati wote.


source nifahamishe

Azinduka Toka Kwenye Koma na Kuanza Kuzungumza Kijerumani

Wednesday, April 14, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Msichana mmoja wa nchini Croatia amewashangaza watu wengi baada ya kuzinduka toka kwenye koma baada ya kupoteza fahamu kwa masaa kadhaa akiwa ameisahau kabisa lugha yake halisi na kuanza kubonga kijerumani kama vile alizaliwa nacho.
Msichana huyo ambaye alipoteza fahamu kwa masaa 24 wiki mbili zilizopita, amewaacha madaktari wakiumiza vichwa kutokana na hali aliyo nayo.

Msichana huyo alizinduka akiwa ameisahau kabisa lugha yake ya Croatia na kuanza kuzungumza kijerumani fasaha kama vile alizaliwa nacho.

Wazazi wake walisema kuwa msichana huyo alikuwa akijifunza kijerumani shuleni na pia akiangalia shoo za kijerumani kwenye luninga lakini kijerumani kilikuwa hakipandi kabisa akishindwa hata kuziunga sentesi kifasaha.

"Huwezi kujua ukizinduka toka kwenye koma ubongo utakuwa katika hali gani", alinukuliwa mkurugenzi wa hospitali ya KB Hospital ambayo msichana huyo alikuwa amelazwa.

Madaktari kadhaa wamejaribu kumfanyia uchunguzi msichana huyo lakini wameshindwa kujua chanzo cha hali iliyomtokea.

source nifahamishe

Ukimfumania Mumeo na Kondomu Mpongeze'

Wednesday, April 14, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mkufunzi mmoja ambaye ni nguli wa kuwafunda akina dada wakati wa Kitchen Party amewataka akina dada ambao wanakwenda kuolewa kufahamu vizuri jinsi ya kuutumia mwiko wa kupikia kwenye chungu ili kuzidumisha ndoa zao na pia wasiwe na ghadhabu wanapokuta kondomu kwenye mifuko ya suruali ya waume zao.
Nguli huyo maarufu jijini Dar es Salaa kwa masuala ya Kitchen Party [Jina Kapuni] alikuwa akitoa mafunzo katika sherehe mojawapo iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, hivi karibuni.

"Katika ndoa kuna mengi yanayojitokeza mbali na kufanya kazi za nyumbani, unaweza kukuta katika suruali ya mume wako ndani ya mfuko amesahau Kondomu ukiona hivyo mpongeze mume wako maana anakujali pia usichukie wewe iweke vizuri na ikiwezekana pindi anaposafiri nenda dukani kamwongezee boksi nyingine ,mfungie kwenye begi lake", alisema kungwi huyo.

Kungwi huyo alimwambia pia bibi harusi kuwa ukiona mwanamke mwenzako jirani yako amekuja kwako kukwambia kwamba mume wako ana uhusiano na mwanamke mwingine basi mchukulie mwanamke huyo kuwa anataka kuharibu ndoa yako.

Mambo yako ya ndani usimwambie mtu mwingine zaidi ya mume wako maana ukisema mume wako anakojoa kitandani atakayechekwa ni wewe mwenyewe", alimalizia kusema mama huyo.

Alisema pia kuwa wengi wa wasichana wanapoolewa huwa hawajui maana ya huu mwiko ambao alikuwa ameushikilia akimwelezea bibi harusi mtarajiwa jina tunalihifadhi.

Alisema utakuta akina mama watu wazima ambao tayari wameolewa wanakuwa wanachanganya mwiko katika vyungu mbalimbali jambo ambalo halitakiwi mwiko unatakiwa kuingia katika chungu kimoja tu ni cha mme wako ambaye amekuoa na si vinginevyo.

"Mwiko ukitumika katika vyungu vingi hupoteza ladha" alisema nguli huyo.

Alifafanua kuwa wengi wa akina mama walioolewa wamekuwa wakithubutu kwenda nje ya ndoa zoa na hivyo miili yao kuingiliwa na miiko zaidi ya mmoja ambapo hasara yake ni kuambukizwa magonjwa.

source nifahamishe

Bi Harusi Mwenye Umri wa Miaka 13 Achanwa Sehemu za Siri, Afariki

Sunday, April 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Msichana mwenye umri wa miaka 13 wa nchini Yemen amefariki dunia kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye sehemu zake za siri siku nne baada ya wazazi wake kumuozesha kwa mwanaume mwenye umri wa miaka 23.
Tamaduni za wanaume nchini Yemen kuoa wasichana wenye umri mdogo zimezidi kupigwa na vita na makundi ya kutetea haki za binadamu baada ya msichana mwenye umri wa miaka 13 kufariki katika siku ya nne ya ndoa yake.

Msichana huyo kutoka katika mji wa Hajja, kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa Yemen, Sanaa, alifariki tarehe mbili mwezi huu ikiwa ni siku ya nne tu baada ya kuozeshwa kwa mwanaume mwenye umri wa miaka 23, alisema Majed al-Madhaji, msemaji wa taasisi ya kutetea haki za wanawake nchini Yemen inayojulikana kama Sisters Arab Forum for Human Rights.

Ripoti ya daktari katika hospitali ya Al-Thawra Hospital ilionyesha kuwa msichana huyo alifariki kutokana na kupoteza damu nyingi sana baada ya kuchanika kwa sehemu zake za siri.
Mume wa msichana huyo amekamatwa na anashikiliwa na polisi.

Taarifa za makundi ya kutetea haki za binadamu zilisema kwamba msichana huyo aliozeshwa baada ya makubaliano kufikiwa baina ya kaka wa marehemu na mume wa marehemu kuwa kila mmoja amuoe dada wa mwenzake ili kupunguza gharama za mahari.

Taarifa zinasema kuwa desturi hiyo ya marafiki kuozeshana madada hufanyika sana nchini Yemen ambako hali ya maisha ni ngumu sana kutokana na kuyumbayumba kwa uchumi. Familia masikini hushindwa kukataa kuwatoa binti zao wakati watu wenye pesa wanapoahidi kutoa mahari kubwa.

Kwa mujibu wa takwimu za wizara ya mambo ya jamii, zaidi ya robo ya wanawake wa Yemen huolewa wakiwa na umri chini ya miaka 15 kutokana na taratibu za kitamaduni kuamini kuwa mwanamke akiolewa akiwa na umri mdogo hunyooka na kuwa mke bora, atazaa watoto wengi na pia ataepukana na hadaa za wanaume.

source nifahamishe

Amuua Mkewe Kwa Kuchati Online na Mwanaume

Sunday, April 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja nchini Jordan anashikiliwa na polisi baada ya kumuua mkewe miezi sita baaa ya ndoa yao akidai kuwa alimfumania akichat online na mwanaume mwingine.
Mtuhumiwa alimkaba koo mkewe mwenye umri wa miaka 37 kabla ya kukipasua kwa nyundo kichwa chake na kisha kujaribu kuutupa mwili wake”, alisema msemaji wa polisi.

“Alijaribu kuuchoma moto mwili wake lakini alishindwa. Alidai kuwa mkewe alikuwa na tabia mbaya ya kuchat na mwanaume kwenye internet”, aliendelea kusema msemaji huyo wa polisi.

Mtuhumiwa huyo ambaye ana umri wa miaka 30 anashikiliwa na polisi na anakabiliwa na adhabu ya kifo.

”Baada ya mauaji alitoa taarifa kwa wakwe zake kuwa mkewe amepotea na hajui alipo wakati huo huo watu wengine wawili walienda kutoa taarifa polisi”, alisema msemaji wa polisi.

Lakini hata hivyo kutokana na taarifa zake za utatanishi polisi walimhisi yeye ndiye aliyefanya mauaji ya mkewe.

Baada ya kubanwa sana na polisi mwanaume huyo aliamua kukiri kumuua mkewe akisema kuwa alikuwa hapendi tabia ya mkewe kuchat na mwanaume kwenye internet.

source nifahamishe

Ndege Yadondoka Rais Wa Poland Afariki

Sunday, April 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais wa Poland, Lech Kaczynski pamoja na mkewe na maafisa wa jeshi na serikali wamefariki dunia baada ya ndege iliyokuwa imebeba abiria 132 kuanguka karibu na uwanja wa ndege nchini Urusi.
Rais Lech Kaczynski wa Poland amefariki dunia kufuatia ajali mbaya ya ndege iliyotokea leo baada ya ndege yake kuanguka kwenye miti karibu na uwanja wa ndege wa Smolensk nchini Urusi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, abiria waote 132 waliokuwemo kwenye ndege hiyo wamefariki dunia.

Miongoni mwa wwaliofariki katika ajali hiyo ni mke wa rais huyo, Maria, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Andrzej Kremer, Mkuu wa majeshi ya Poland, Franciszek Gagor, na Gavana wa Benki Kuu ya nchi hiyo, Slawomir Skrzypek.

Pia katika orodha ya watu waliofariki kutokana na ajali hiyo ya ndege ni wabunge wa Poland na wanahistoria kadhaa.

Rais huyo wa Poland pamoja na ujumbe wake walikuwa wakielekea katika mji wa Katyn karibu na Smolensk kuhudhuria kumbukumbu ya mauaji ya wafungwa wa vita wa Urusi na Poland waliouawa wakati wa utawala wa kisovieti.

Kufuatia kifo hicho, Spika wa bunge la Poland, Bronislaw Komorowski, anachukua madaraka ya nchi hiyo.

Rais Kaczynsk na mkewe ambao wote wamefariki katika ajali hiyo wameacha mtoto mmoja wa kike, Marta.

source nifahamishe