Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza

Friday, July 30, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wanawake waliozipoteza bikira zao kwa ngono ambao wanataka kuzirudisha bikira zao kabla ya kuolewa wamezidi kuongezeka nchini Uingereza ambapo operesheni za kurudisha bikira zimekuwa zikifanyika kwa wingi sana siku hizi.
Maelfu ya wanawake nchini Uingereza ambao hutaka waonekane ni bikira kwa waume zao, wamekuwa wakifanya operesheni za kuzirudisha bikira zao.

Idadi ya operesheni za kurudisha au kurekebisha bikira zinazofanyika kwenye mahospitali nchini Uingereza zimeongezeka kwa kasi katika miaka ya karibuni ambapo wanawake wamekuwa wakilipa hadi paundi 4,000 (Takribani Tsh. Milioni 9).

Operesheni hizo zinazotumia muda wa nusu saa huzirudisha tishu za hymen (ngozi inayoziba mlango wa uke) na kumfanya mwanamke awe bikira kwa mara nyingine tena.

Bikira hiyo ya kutengeneza nayo huwa na uwezo wa kuchanika na kutoa damu mwanamke anapojamiiana kwa mara ya kwanza baada ya operesheni hiyo.

Mmoja wa madaktari wa hospitali moja binafsi nchini Uingereza alisema kuwa idadi kubwa ya wanawake wanaoenda kwake ni wanawake wenye asili ya bara la Asia ambao hutaka kuwahakikishia waume zao kuwa hawajawahi kufanya mapenzi kabla ya usiku wa harusi yao.

"Ni jambo la kitamaduni zaidi kuliko kidini, kama mwanamke hatatoa damu kwenye kitambaa cheupe usiku wa harusi yake, basi huonekana ameidhalilisha na kuitia aibu familia yake", alisema daktari huyo.

"Mwanamke huhofia kuwa mumewe anaweza akatoa talaka au kuitolea kashfa familia yake au kumnyanyasa maisha yake yote iwapo atajulikana si bikira", aliongeza daktari huyo.

Daktari huyo aliongeza kuwa wanawake wanaofanya operesheni za kurudisha bikira zao wengi wao hutumia majina na anuani feki ili wasijulikane.

source nifahamishe

Avaa Gauni la Spinachi Kupinga Watu Kula Nyama

Friday, July 30, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamama wa nchini Kenya ambaye anapigania watu waache kula nyama na badala yake wawe wanakula mboga za majani, alikuwa kivutio mitaani alipovaa gauni lililotengenezwa kwa majani ya spinachi.
Michelle Odhiambo alivaa gauni refu lililotengenezwa kwa majani ya spinachi na kupita kwenye mitaa ya Nairobi akipiga kampeni ya kuwahamasisha watu waache kula nyama choma.

Michelle ambaye ni mwanaharakati wa shirika la kutetea haki za wanyama alisema kuwa aliacha kula nyama za aina zote miaka minane iliyopita.

Michelle aliwahimiza wamiliki wa mahoteli waache kupika vyakula vyenye nyama na badala yake watumie mboga za majani.

Hata hivyo kampeni yake ya kupinga ulaji wa nyama inakabiliwa na upinzani mkubwa hasa kwa kuzingatia kuwa mapishi bila nyama huhusishwa na umaskini nchini Kenya. Watu wenye pesa hupenda kujionyesha kwa kula nyama katika vyakula vyao.

Michelle alisema kuwa chakula ambacho hutumiwa kulisha wanyama wanaochinjwa kinaweza kutumiwa kulisha watu wengi.

Michelle pia alihoji tabia ya watu kuwahasi wanyama na kuwachinja bila ya kutumia dawa za kupunguza maumivu.

"Hii ni haki kweli?", aliuliza Michelle.


source nifahamishe

Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe

Wednesday, July 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Wakati wanawake katika nchi za magharibi wanapigania kuwa na matiti makubwa hali ni tofauti nchini Cameroon ambapo akina mama nchini humo wanatumia njia ya kikatili ya kuyapiga pasi matiti ya watoto wao wa kike ili kuwaepusha wasibakwe.
Ili kuwafanya wanaume wakware wasianze kuwanyemelea mabinti zao wanapoanza kupevuka na kupelekea mimba zisizohitajika, akina mama nchini Cameroon wanatumia njia inayosababisha maumivu makali sana ya kuyapiga pasi matiti ya watoto wao wa kike ili yaendelee kuwa madogo wakati wote na hivyo kutowavutia wanaume.

Njia hiyo inayojulikana kama "Breast ironing" hufanyika kwa mawe kuwekwa kwenye moto na kisha mawe hayo kukandamizwa kwenye chuchu ili kuyafanya matiti yasiendelee kuongezeka ukubwa.

Njia hiyo husababisha maumivu makali kwa watoto wa kike na hupelekea baadhi yao wapate vilema vya maisha na wengine washindwe kuwanyonyesha watoto wao wanapokuwa wakubwa.

Utafiti unaonyesha kuwa watoto wa kike nchini Cameroon huanza kupevuka wanapokuwa na umri wa miaka tisa na ni wakati huo huo mama zao huanza kuzipiga pasi chuchu zao ili wasiwavutie wanaume.

Pamoja na njia hiyo kuonekana ya kikatili sana na yenye kuwasababishia maumivu na majeraha watoto wa kike, akina mama nchini Cameroon wanaitetea njia kwa kusema kuwa inawaepusha watoto wao kupata mimba mapema.

source nifahamishe

Orijino komedi na uchawi na wanga

Wednesday, July 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Bomba la Mafuta Lapasuka Dar, Watu Wagombania Mafuta

Monday, July 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Baada ya bomba la mafuta kupasuka baharini nchini Marekani na kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira, bomba la mafuta la TIPA katika bahari ya Hindi limepasuka lakini tofauti na hali ilivyokuwa nchini Marekani Watanzania waligombania kuchota mafuta.
Bomba la mafuta la TIPA na Orexy limepasuka na kusababisha mafuta ya Disel kumwagika katika ufukwe wa Kivukoni na kusababisha shughuli za uoshaji wa samaki kusimama kwa takribani siku nzima.

Akizungumuzia tukio hilo Katibu wa Wizara ya Miundombinu Omary Chande amesema kuwa tatizo lililojitokeza katika bomba hilo la mafuta ni bomba dogo ambalo limepasuka katika mabomba ya Tipa na Orexy ambayo yapo umbali kidogo kutoka katika kivuko cha magogoni.

Baada ya kupata taarifa ya kupasuka kwa mabomba hayo, mafundi wa TIPA walizama ndani ya maji hayo na kuanza kuziba bomba hilo na hatimaye walifanikiwa kuliziba bomba hilo.

Mamia ya vijana wanaojazana maeneo ya feri walikimbilia eneo la tukio ambapo walianza kazi ya kuchota mafuta yaliyokuwa yakielea juu ya maji.

Mafuta yaliyopatikana toka eneo hilo yalikuwa yakiuzwa kwa madereva wa madalala ambapo lita tano kwa kiasi cha shilingi 5,000.

Vijana wasio na ajira ambao mara zote hushinda hapo feri wamesema hii ni neema kwao kwasababu kwa jana pekee wameweza kujipatia kipato kikukbwa ambacho hawakuweza kukitegemea kupata na wanaomba hali hii ingeendelea kutokea kila siku.

Lakini hali ilikuwa tofauti kwa waosha samaki kwani kwa siku ya leo hawakuwa na kazi kutokana na bahari yote kujaa mafuta ya disel ambayo yalikuwa yakinuka kila sehemu.

Katibu Chande alisema kutokana na uharibifu wa mazingira uliotokea, ofisi yake kwa kushirikana na wahusika tayari wameweka dawa kwa ajili ya kudhibiti ukali wa mafuta na kusababisha yasiwe na nguvu yoyote ya kudhuru wananchi.

Pia aliwataka watumiaji wa magari wanaonunua mafuta yaliyochotwa kwenye eneo hilo, wasiyatumie mafuta hayo maana tayari yameshaharibiwa kwa kutumiwa dawa maalumu.

source nifahamishe