Madaktari Wauza Figo za Watu 109

Saturday, September 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Madaktari watano wa nchini Afrika Kusini wamepandishwa kizimbani kwa kuuza figo za watu 109 katika kipindi cha miaka miwili.
Madaktari watano wa hospitali binafsi kubwa ya nchini Afrika Kusini wamepandishwa kizimbani kwa kuwauzia figo za watu 109 matajiri wa Israel.

Madaktari hao walifanya biashara haramu ya viungo vya binadamu kwa kununua kwa bei rahisi figo za watu maskini toka Israel, Romania na Brazil.

Madaktari hao katika kipindi cha kati ya mwaka 2001 na 2003 walizininua figo 109 na kufanya operesheni kinyume cha sheria kuwapandikiza matajiri wa Israel.

Miongoni mwa waliopandishwa kizimbani ni mkuu wa mtandao wa hospitali kubwa binafsi nchini Afrika Kusini wa Netcare bwana Richard Friedland, lilisema gazeti la The Star.

"Raia wa Israel wanaohitaji figo, waliletwa nchini Afrika Kusini kwaajili ya kupandikizwa figo za watu wengine kwenye hospitali ya St. Augustine iliyopo mjini Durban".

"Mwanzoni walikuwa wakinunua figo toka kwa raia wa Israel lakini baadae waliamua kununua figo za raia wa Brazili na Romania kwakuwa figo zao zilikuwa zikiuzwa kwa bei chee".

Figo ya raia wa Israel ilikuwa ikinunuliwa kwa dola 20,000 wakati figo za Wabrazili na Waromania zilikuwa zikinunuliwa kwa dola 6,000 tu, ilisema taarifa ya mwendesha mashtaka.

source nifahamishe

Wajukuu wa Osama Bin Laden Wafariki

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamama aliyekuwa amejitolea kupandikizwa mimba ya watoto mapacha wa mtoto wa kiongozi wa Al-Qaeda, Osama Bin Laden, amewapoteza watoto hao baada ya mimba yake kuharibika kufuatia kichapo alichopewa mtaani na wanaume wawili ambao hawajajulikana.
Mtoto wa Osama Bina Laden, Omar Bin Laden mwenye umri wa miaka 29 ambaye amemuoa mwanamke wa Kiingereza ambaye alikuwa hana uwezo wa kupata mimba kutokana na umri wake, alimkodisha mwanamke toka mji wa Bristol nchini Uingereza abebe mimba yake.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 anayejulikana kwa jina la Louise Pollard alipoteza mimba hiyo ya watoto wawili mapacha baada ya kushambuliwa na watu wawili wasiojulikana wakati akielekea nyumbani kwake toka kwenye mgahawa mmoja nchini Syria.

Louise ambaye zamani alikuwa akicheza dansi za utupu kwenye klabu za starehe nchni Uingereza, alienda hospitali ambako aliambiwa kuwa watoto wote wawili walioko tumboni mwake wamefariki.

Louise alisema kuwa hajajua sababu ya wanaume hao kumshambulia ingawa alisema kuwa watu wengi wanamfahamu kama mwanamke aliyebeba mimba ya wajukuu wa mkuu wa Al Qaeda, Osama bin Laden.

Mke wa mtoto wa Osama, Zaina mwenye umri wa miaka 54, ambaye awali alikuwa akijulikana kama Jane Felix-Browne alisema kuwa Omar amekumbwa na upungufu wa akili hivyo wameamua kuachana.

Omar na Zaina walipanga kumlipa paundi 10,000 mwanamke huyo baada ya kujifungua watoto hao mapacha.

source nifahamishe

Mtoto Akutwa Kwenye Choo Cha Ndege

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto mchanga wa kiume amekutwa akiwa hai kwenye pipa la taka la kwenye choo cha ndege iliyowasili nchini Philippines ikitokea Bahrain.
Kwa mujibu taarifa zilizotolewa punde baada ndege ya shirika la ndege la Gulf Air kutua mjini Manila, Philippines ikitokea Bahrain, wafanya usafi waliingia kwenye ndege hiyo baada ya abiria wote kushuka na ndipo walipokumbana na tukio wasilolitegemea baada ya kumkuta mtoto mchanga aliyezaliwa muda mfupi uliopita akiwa kwenye pipa la taka la chooni.

Mtoto huyo mchanga wa kiume alikuwa amezungushiwa makaratasi ya chooni akiwa bado hajasafishwa damu toka kwenye mwili wake huku kipande kikubwa cha utambi wa kitovu kiking'inia.

Madaktari waliitwa na kumchunguza mtoto huyo na kutoa taarifa mtoto huyo bado yuko hai na mwenye afya njema.

Mtoto huyo alipewa jina kwa kutumia herufi mbili za GF zinazowakilisha Gulf Air pia herufi hizo ziliwakilisha jina jingine alilopewa la George Francis.

Mtoto huyo wa kiume alisafishwa kwa kutumia maziwa na manesi wa uwanja wa ndege mjini Manila.

Polisi wanafanya uchunguzi kumtafuta mama wa mtoto huyo ambaye aliwashangaza watu kwa jinsi alivyoweza kujifungua mwenyewe ndani ya ndege bila ya kushtukiwa na mtu yeyote.

Kwa mujibu wa polisi wa Manila, mama huyo akipatikana atafunguliwa mashtaka mahakamani.


source nifahamishe

Amtukana Obama, Afungiwa Maisha Kwenda Marekani

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kijana wa Kiingereza ambaye alimtumia rais wa Marekani email ya vitisho na kashfa amefungiwa maisha kuingia Marekani.
Luke Angel alifuatiliwa na polisi wa Marekani na Uingereza baada ya kumtumia email ya vitisho na kashfa rais wa Marekani, Barack Obama na kumfananisha rais huyo wa taifa kubwa duniani na sehemu za siri za kike.

FBI waliichunguza email ya Luke na kisha kuwajulisha polisi wa Uingereza ambao waliendaaa nyumbani kwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 17 anayekaa Silsoe, Bedfordshire.

Luke, ambaye ni mwanafunzi wa sekondari, ameingia kwenye orodha ya watu waliopigwa marufuku kukanyaga ardhi ya Marekani maishani.

Luke aliliambia gazeti moja la Bedfordshire kuwa aliamua kumtumia Obama email hiyo ya kashfa baada ya kuangalia kipindi kwenye luninga kilichokuwa kikizungumzia shambulizi la kigaidi la septemba 11,2001.

"Polisi walikuja nyumbani kwetu na kunipiga picha na kuniambia kuwa nimepigwa marufuku kuingia Marekani", alisema Luke.

"Sijali kupigwa marufuku kuingia Marekani ingawa wazazi wangu hawajafurahia", aliongeza Luke.

Polisi hawana mpango wa kumfikisha mahakamani kijana huyo.

source nifahamishe

Aichana Quran na Biblia na Kuzivutia Sigara Kurasa Zake

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Mwanasheria mmoja wa nchini Australia amezua balaa jingine baada ya kuzichana kurasa za kwenye msahafu na biblia na kuzitumia kurasa hizo kuvutia sigara.
Siku chache baada ya mchungaji wa Marekani kuzua mtafaruku duniani baada ya kutishia kuichoma moto Quran, mwanasheria mmoja wa nchini Australia amezua mtafaruku mwingine kwa kuzichana kurasa za kwenye msahafu na kwenye biblia na kisha kuzitumia kurasa hizo kuvutia sigara.

Mwanasheria huyo aliyejulikana kwa jina la Alex Stewart, aliandaa video ya dakika 12 ambayo aliiweka kwenye YouTube akiwa ameshikilia msahafu na biblia kabla ya kunyofoa kurasa kwenye vitabu hivyo vitakatifu na kuzitumia kuvutia sigara.

Stewart ambaye hana dini alisema katika video hiyo "Hivi ni vitabu tu kama vitabu vingine".

Video yake ilifutwa kwenye YouTube muda mfupi baada ya kuwekwa baada ya watu kuanza kuilaani video hiyo.

Stewart ambaye anafanya kazi kwenye chuo kikuu cha Queensland University of Technology amesimamishwa kazi kwa muda na chuo hicho ambacho kimesema kuwa kimesikitishwa sana na kitendo chake.

"Chuo kikuu kimesikitishwa sana na hakijafurahia kitendo kama hiki kutokea", alisema makamu mkuu wa chuo hicho Peter Coaldrake.

Kitendo cha Stewart kimefuatia tukio la mchungaji Terry Jones wa Florida, Marekani kutishia kuchoma moto misahafu 200 siku ya septemba 11.

Aliahirisha azma yake hiyo kutokana na vitisho toka kwa waislamu na shinikizo kubwa toka kwa serikali ya Marekani.

Hata hivyo wachungaji wawili wa jimbo la Tennessee nchini Marekani, mchungaji Bob Old na msaidizi wake Danny Allen waliichoma moto Quran na kitabu chenye maandishi ya "Muhammad" kwenye ukurasa wake wa mbele.

Mjini Washington, mwanaume mmoja aliichana Quran mbele ya jengo la ikulu ya Marekani na kukiweka kipande cha ukurasa alichokinyofoa kwenye mfuko wa plastiki.

Tukio hilo lilishuhudiwa na watalii waliokuwa maeneo hayo pamoja na polisi wanaolinda usalama eneo hilo ambao hawakuchukua hatua yoyote ili kuepuka kuingilia haki za watu za uhuru wa kujieleza.

source nifahamishe

Aamua Kumuoa Dada Yake

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume wa nchini Ireland ambaye alimpachika mimba dada yake na kuzaa naye mtoto kabla ya kugundua kuwa ni ndugu yake, anafunga ndoa na dada yake huyo mwishoni mwa mwezi huu.
James na Maura, ambao ni kaka na dada ambao wamezaa mtoto mmoja, wanategemea kuvalishana pingu za maisha mwishoni mwa mwezi huu.

Ndugu hao ambao wameamua kubadilisha majina yao halisi ili wasijulikane na jamii, waliangukia kwenye penzi zito bila ya kutambua kuwa wamezaliwa kutokana na baba mmoja.

"Itakuwa ni harusi ndogo, tuna mashahidi wawili tu ambao tunawafahamu vizuri na wanaelewa hali tuliyo nayo", alisema James

"Hatujui kama baba yetu atakuja kwenye harusi au kama mama zetu watahudhuria harusi yetu".

"Mtoto wetu wa kiume anasubiria kwa hamu harusi yetu na anaelewa kinachoendelea, hatujali kuoana mtu na dada yake", aliongeza James.

James na Maura walizaliwa kutokana na baba mmoja na walikuwa wakiishi miji miwili tofauti iliyo mbali kwa kilomita 160.

James na Maura ambao hivi sasa wana umri kati ya miaka 20-28, Walikutana miaka michache iliyopita kwenye ukumbi wa starehe katika mji mwingine wa tatu na kuangukia kwenye penzi zito na walipata mtoto wa kiume miaka miwili baadae.

Waligundua kuwa ni ndugu mwaka jana wakati wa krismasi wakati mama yake James alipomuambia James kuwa baba yake wa kweli siyo mwanaume aliyemlea miaka yote.

Mwezi wa nne mwaka huu walithibitisha kuwa ni mtu na dada yake baada ya vipimo vya DNA kuthibitisha kufanana kwa DNA zao.

James na Maura walielezea jinsi wanavyoisubiria kwa hamu harusi yao pamoja na kwamba wanajua kuwa sheria za nchi haziwaruhusu kufunga ndoa.

Kutokana na kwamba kitambulisho cha James kinaonyesha jina la baba yake kuwa ni Vincent ambalo ni jina la mwanaume aliyemlea, kipingamizi cha kisheria cha kuzuia ndoa yao kinakuwa kimeepukika kwani majina ya baba kwenye vitambulisho vyao yatakuwa tofauti.


source nifahamishe

11 mbaroni sakata la vifo vya watoto Luxury Pub

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

KUFUATIA ripoti maalum iloyoundwa kuchunguza sababu iliyopelekea kutokea kwa vifo vya watoto na kubainika ni uzembe ulisababisha vifo hivyo, watu 11 wanashikiliwa na polisi.
Ripoti hiyo imeonyesha kuwa uzembe mkubwa ulifanyika katika ukumbi huo na kusababisha vifo hivyo.

Akitoa ripoti hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bi. Chiku Galawa alisema, ripoti hiyo imeonesha kuwa uzembe uliofanyika katika ukumbi huo ni kuwa na idadi kubwa ya watu ndani ya ukumbi huo kuliko uwezo wa ukumbi.

Pia mmiliki wa ukumbi huo imegundulika hakuwa na kibali cha kuendesha biashara hiyo ya disco hivyo alikuwa akienda kinyume na sheria za nchi, na aliendesha dico hilo toto hadi majira ya saa 1:50 usiku na kuonekena kukiuka utaratibu uliowekwa.

"Watoto ni haki yao kufurahia sikukuu, lakini mmiliki wa ukumbi huo alikiuka maadili ya watoto, kwanza aliwalundika watoto ukumbini kupit kiasi, pili alipitisha muda maalum" alsiema mkuu huyo

Mmiliki wa ukumbi huo alitambulika kwa jina la Damas Nyingo alikuwa ni mmoja kti ya watu 11 waliokamatwa na majina mengine hayakuekwa bayana hadi upelelezi ukamilike.

Watoto wawili waliweza kupoteza maisha sikukuu ya Idd Pili, katika ukumbi wa Luxury Pub uliopo Temeke, katika makutano ya mtaa wa Madenge na Liwale baada ya umeme kukatika ghafla na kusababisha watoto kukimbia hovyo mlangoni na kukanyagana.

Watoto waliopoteza maisha ktika tukio hilo ni Lilian Sango (8) na Amina Ramadhani (7), wote wakazi wa Temeke na wengine zaidi ya kumi na moja kujeruhiwa.

source nifahamishe

Britney Spears Ashtakiwa Kwa Kumtesa Kingono Mlinzi Wake

Sunday, September 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mlinzi wa zamani wa nyota wa muziki wa Pop wa Marekani, Britney Spears amefungua kesi mahakamani akimshtaki nyota huyo wa muziki kwa kumnyanyasa kijinsia kwa kutembea uchi mbele yake na kufanya mapenzi na mpenzi wake mbele yake.
Mlinzi wa zamani wa nyota wa muziki wa Pop wa Marekani, Britney Spears, Fernando Flores amefungua kesi mahakamani akimtuhumu nyota huyo wa muziki kwa kumnyanyasa kijinsia.

Flores amedai kuwa nyota huyo wa muziki alikuwa akitembea uchi mara kwa mara mbele yake na wakati mwingine alikuwa akifanya mapenzi na mpenzi wake mbele yake.

Mlinzi huyo alisema katika hati alizowasilisha mahakamani mjini Los Angeles kwamba Britney Spears alijaribu mara kwa mara kumvuta kimapenzi na wakati mwingine alimvuta chumbani kwake na kujianika uchi mbele yake.

Mlinzi huyo alisema kuwa kitendo cha Britney Spears kugombana na mumewe wa zamani mbele ya watoto wao kilikuwa kikiumiza hisia zake.

Mlinzi huyo ambaye alifanya kazi kama mlinzi wa Britney Spears kuanzia mwezi february hadi julai mwaka huu, aliilalamikia pia kampuni yake ya ulinzi kwa kutoyatilia mkazo malalamiko yake aliyokuwa akiyapeleka kuhusiana na unyanyasaji wa kijinsia wa Britney Spears.

Wakili wa Britney Spears alikataa kusema chochote kuhusiana na kesi hiyo.

source nifahamishe