Babu Nyota wa Video za Ngono

Saturday, October 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Babu mwenye umri wa miaka 76 wa nchini Japan alikuwa akitoka nyumbani kwake kila siku asubuhi akiwa ameuramba suti akiaga anaenda kazini lakini siri yake imegundulika kuwa babu huyo alikuwa akitoka nyumbani kwake asubuhi ili kwenda kushiriki video za ngono.
baada ya kustaafu kazi yake ya uwakala wa kampuni ya utalii, babu Shigeo Tokuda, mwenye umri wa miaka 76 alikuwa akiiaga familia yake aubuhi kuwa anaenda kazini.

Familia yake haikuwa ikijua babu Tokuda alikuwa akienda wapi na alikuwa akifanya kazi gani mpaka hivi karibuni ilipogundulika kuwa babu Tokuda ndiye mwanaume mzee kuliko wote nchini Japan anayeshiriki kwenye video za ngono.

Tokuda aligundulika kuwa ni nyota wa video za ngono baada ya binti yake mwenye umri wa miaka 35 kusoma jarida ambalo lilikuwa likimuelezea babu Tokuda kama mfalme wa filamu za kiutu uzima.

Baada ya kuona familia yake imegundua kazi yake mpya anayoifanya, Tokuda aliamua kuweka wazi kwa kutoboa siri zote.

Tokuda alisema kuwa alipokuwa na umri wa miaka 60, alikutana na mtengenezaji wa filamu za ngono wakati akiwa dukani akinunua DVD ya ngono. Huo ndio ukawa mwanzo wa yeye kujiingiza kwenye filamu za ngono.

Hadi sasa Tokuda ameishashiriki jumla ya filamu 350 za ngono na amekuwa akilipwa kiasi cha dola 500 kila siku.

Tokuda ambaye ana mjukuu mmoja alisema kuwa mkewe ameiridhia kazi yake mpya ingawa binti yake alishtushwa sana alipogundua kuwa yeye ni nyota wa video za ngono.


source nifahamishe