Msanii wa Marekani Awabaka na Kuwazalisha Binti Zake Watoto Sita

Friday, March 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mkurugenzi wa kutengeza video za muziki wa Marekani ambaye alitengeneza video ya wimbo maarufu 'Killing me softly' wa kundi la Fugees ametiwa mbaroni kwa kuwabaka na kuwazalisha watoto sita binti zake watano.
Aswad Ayinde, au maarufu kama Charles McGill ambaye alitengeneza video ya ‘Killing Me Softly,’ ya kundi la Fugees la Marekani ametiwa mbaroni kwa tuhuma za kuwabaka binti zake watano na kuwazalisha watoto sita katika kipindi cha miaka 22 kuanzia mwaka 1980 hadi mwaka 2002.

Ayinde anadaiwa kumwambia mkewe na watoto wake kuwa mwisho wa dunia umekaribia na watakaonusurika ni yeye, wanae na watu wengine walioteuliwa.

Ayinde aliiambia familia yake kuwa ili kulinda kizazi chake damu yake isichafuliwe inabidi afanye nao mapenzi na wazae watoto kutoka kwa damu yake mwenyewe.

Kali zaidi ni kwamba baada ya kuwatia mimba binti zake watatu, aliwazalisha yeye mwenyewe na watoto waliozaliwa hawakusajiliwa majina yao serikalini.

Ayinde anakabiliwa na jumla ya mashtaka 27 ambapo kila binti yake mmoja amemfungulia kesi ya mashtaka matano. Makosa mengine amefunguliwa na mkewe wa zamani.

Mke wa zamani wa Ayinde anayeitwa Beverly ambaye alizaa na Ayinde watoto tisa, alitoa ushahidi wa Ayinde kuwabaka binti zake na alielezea jinsi Ayinde alivyokuwa akimpiga yeye na watoto wake kwa kutumia mbao.

"Nilijua alichokuwa akifanya lakini nilishindwa kusema chochote kwa kuhofia kipigo", alisema mke huyo wa zamani wa Ayinde ambaye alinusurika maisha yake baada ya kufanikiwa kutoroka toka kwenye nyumba ya Ayinde.

Ayinde mwenye umri wa miaka 51 anashikiliwa na polisi na atapandishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwezi ujao.

Enzi zake Ayinde alifanikiwa kuzawadiwa tuzo ya MTV kwa kuitengeneza vizuri sana video ya wimbo wa Fugees.

source facebook

Njaa Mbaya Sana, Wanakijiji Zimbabwe Wamla Tembo

Friday, March 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kweli njaa si mchezo, wanakijiji wa kijiji kimoja nchini Zimbabwe ambacho kimekumbwa na janga la njaa na umaskini, wanakijiji wake walitumia dakika 105 tu kumchuna ngozi tembo aliyekutwa amefariki na kisha kujisevia nyama zake na mwishoe hakuna hata
Ndani ya lisaa limoja na dakika 45 tembo aliyekutwa msituni amefariki, alichunwa ngozi na kisha wanakijiji walianza kujisevia nyama zake na kubakisha mifupa tu ikiwa imezagaa kwenye eneo ambalo tembo huyo alifariki.

Mifupa ya tembo huyo nayo ilipitiwa na wanakijiji wengine siku iliyofuatia na hivyo kufanya eneo alilofariki tembo huyo liwe jeupee bila dalili ya kufariki kwa mnyama yoyote yule.

Tukio hilo lilitokea katika kijiji kimoja nchini Zimbabwe ambapo inasemekana mifupa ya tembo hutumika kutengenezea sabuni.

Tukio la wananchi kujisevia nyama ya mzoga wa tembo huyo halikufanyika kwa utulivu na hali ya vurugu na ngumi zilizuka wakati wanakijiji wakipigania kupata chochote cha kuganga njaa.

Picha za tukio hilo zinaonyesha jinsi hali ngumu ya maisha na njaa inavyowafanya watu wale mpaka mizoga.

source nifahamishe

Jela Mwaka Mmoja Kwa Kumpiga Chabo Mkewe Akioga

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume wa nchini Marekani ambaye alitoboa tundu kwenye ukuta wa bafu lake na kuchukua video kwa siri wakati mkewe akioga amehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja.
Richard Perez mkazi wa Minnesota nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kwa kurekodi video kwa siri wakati mkewe akioga.

Mahakama iliambiwa kuwa Perez alitoboa tundu kwenye ukuta wa bafu lake na kisha kutegesha video kamera ambayo aliitumia kurekodi video za siri wakati mkewe alipokuwa uchi akioga.

Mkewe ambaye alitajwa kwa kifupi kama KP, aliwaita polisi baada ya kukuta video zake akioga kwenye kompyuta iliyopo nyumbani kwao.

Wapenzi hao walikuwa kwenye taratibu za kuivunja ndoa yao wakati video hizo zilipogundulika.

Polisi walizikuta video nne za KP akivua nguo zake na kuingia kwenye bafu kuoga. Pia polisi walifanikiwa kuzipata video kadhaa zilizopigwa na Perez kwenye maeneo ya hadhara ambapo alichukua video za wanawake chini ya sketi zao.

Perez alipatikana na hatia januari mwaka jana kutokana na makosa ya kuchukua video ya mke wake akiwa mtupu akioga bila ya yeye mwenyewe kujua.

"Mke anaweza akawa na masuala binafsi anapokuwa peke yake bafuni na hiyo haimaanishi kuwa kwasababu ya ndoa haki zake za masuala binafsi ndio zipotee", alisema jaji wa kesi hiyo wakati akimhukumu Perez kwenda jela mwaka mmoja.

Perez alikata rufaa lakini juzi mahakama ilitupilia mbali rufaa yake kumuamuru aende jela akatumikie kifungo chake cha mwaka mmoja.


source nifahamishe

Mapenzi Yasababisha Atupwe Jela

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Ujerumani ambaye alitaka kumstaajabisha mpenzi wake kwa kuruka ukuta kuingia nyumbani kwake usiku akiwa amebeba zawadi ya ua la waridi na mvinyo amejikuta akienda jela baada ya mpenzi wake kuita polisi akidhania ameingiliwa na wezi,
Mwanamke mmoja wa nchini Ujerumani huku na hofu kubwa ya maisha yake aliwaita polisi baada ya kuhisi kuna mwizi amevamia nyumbani kwake usiku kwa kuruka ukuta.

Polisi walishangazwa kumuona mwanaume waliyemkamata aliyehisiwa kuwa ni mwizi alikuwa ni mpenzi wa mwanamke huyo akiwa amebeba ua la waridi na mvinyo. Hata hivyo polisi waliamua kumtia mbaroni mwanaume huyo.

"Alikuwa akijaribu kumfanyia suprise mpenzi wake kwa kumpelekea ua na mvinyo saa sita usiku lakini mpango wake ulienda vibaya", alisema msemaji wa polisi.

Polisi walisema kuwa mwanaume huyo alijaribu kukimbia baada ya kuwaona polisi lakini hakufanikiwa kutoroka na alitiwa mbaroni wakati huo huo.

Mwanaume huyo aliamua kuwagaia polisi chupa yake ya mvinyo kama shukurani yake kwa polisi waliomkamata kwa kumchukulia kama rafiki yao na kutompa misukosuko.

source nifahamishe

Katuni Nyingine ya Kumkashifu Mtume Yachapishwa Sweden

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (1)


Mgazeti mengi ya Sweden jana jumatano yaliichapisha katuni nyingine ya kumkashifu mtume Muhammad (S.A.W) katika kuonyesha upinzani wao kwa jaribio la kumuua mchora katuni wa Sweden aliyemchora mtume akiwa na umbile la mbwa.
Mgazeti makubwa ya Sweden jana jumatano yalichapisha katuni ya kumkashifu mtume Muhammad (s.a.w) ambayo ilisababisha waislamu saba wale njama za kumuua mchora katuni aliyeichora katuni hiyo.

Kichwa cha mchora katuni wa Sweden Lars Vilks kimewekewa zawadi ya dola 100,000 na Al-Qaeda kama zawadi kwa mtu atakayemuua mchora katuni huyo.

Waislamu saba walikamatwa juzi nchini Ireland wakidaiwa kula njama za kumuua Vilks ambaye alichora katuni ya mtume akiwa na umbile la mbwa.

Gazeti la Dagens Nyheter la nchini Sweden liliichapisha katuni hiyo iliyosababisha mtafaruku huku ikisema kuwa Lars Vilks hayupo peke yake kwenye mgogoro huu.

"Vitisho vyovyote vya maisha yake kwa upande mmoja ni sawa na kuwatishia maisha raia wote wa Sweden", lilisema gazeti hilo katika sehemu yake ya maoni ya mhariri.

Gazeti liliendelea kwa kuitaka serikali ya Sweden impe Vilks ulinzi wowote unaohitajika.

"Mamlaka husika lazima zichukue hatua dhidi ya shambulio linalotaka kuharibu haki yetu ya msingi ya uhuru wa kujieleza", lilisema gazeti hilo.

Gazeti jingine la Expressen nalo liliichapisha katuni hiyo likisisitiza kuwa ni muhimu kulinda uhuru wa kujieleza ambao unatishiwa amani.

"Jamii lazima ionyeshe kuwa haitatishika na vitisho na kuwa tayari kupigania uhuru wa kujieleza", lilisema gazeti hilo.

Vilks akiongea kuhusiana na jaribio la kumuua alisema kuwa hajatishika na kukamatwa kwa watu saba nchini Ireland waliotaka kumuua.

Vilks aliiambia televisheni ya TV4 kuwa angerudia tena kuichora katuni hiyo iwapo atapata nafasi tena.

Vitisho vya kumuua Vilks vimekwenda sambamba na majaribio kadhaa ya kumuua mchora katuni wa Denmark Kurt Westergaard ambaye mwaka 2005 alichora katuni ya mtume akiwa na bomu kwenye kichwa chake.

"Vitisho dhidi ya Vilks vinasikitisha", alisema Westergaard akiliambia gazeti la Expressen na kuongeza "Nimefurahishwa na ushujaa wake na jinsi alivyoweza kuhimili vitisho".

source nifahamishe

Ruhsa Kujiua Ukitimiza Miaka 70

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Serikali ya Uholanzi inategemea kupitisha sheria yenye utata itakayowaruhusu watu wenye umri kuanzia miaka 70 kujiua wenyewe kwa msaada wa madaktari iwapo watahisi kuwa wametosheka na maisha duniani.
Watu wenye umri zaidi ya miaka 70 wataruhusiwa kujiua kwa kusaidiwa na madaktari iwapo wataona wameishatosheka na maisha yao hapa duniani.

Watu ambao hawana ujuzi wa udaktari watapewa mafunzo jinsi ya kuwasaidia wazee wenye umri zaidi ya miaka 70 kujiua kwa kutumia sindano za simu hospitalini.

Bunge la Uholanzi linatarajia kuujadili muswada wa sheria hiyo baada ya watu wanaoipigia kampeni sheria hiyo kukusanya sahihi za watu 112,500 wanaounga mkono sheria ya kuruhusu watu kujiua.

Watetezi wa sheria hiyo wamesema kuwa kupitishwa kwa sheria hiyo kutawawezesha wazee kuamua kufariki kimya kimya kwa utulivu pindi watakapoona wamechoka kuishi na wanataka kuepukana na pilikapilika za dunia.

Wasaidizi wa madaktari watakaokuwa wakichanganya dawa ya sumu itakayotumika kuwaulia wazee watakaojitokeza.

Hata hivyo mashirika ya kidini yameelezea kupinga kwake kuruhusu watu kujiua eti kwasaabu ya kuyachoka maisha.

source nifahamishe

Mtoto wa Miaka 3 Ajiua Kwa Kujipiga Risasi

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu wa nchini Marekani amefariki dunia baada ya kujipiga risasi ya tumbo wakati alipokuwa akichezea bastola ya kweli ya baba yake akidhania anachezea bastola feki inayotumika kwenye deki ya gemu ya Nintendo Wii.
Mtoto Cheyenne Alexis McKeehan mwenye umri wa miaka mitatu alijipiga risasi ya tumbo kwa kutumia bastola ya baba wake wa kambo aliyoikuta kwenye meza sebuleni.

Mtoto huyo alichukua bastola hiyo ya kweli na kuanza kuichezea akidhani anachezea bastola feki inayotumika kwenye gemu ya Nintendo Wii.

Mama wa mtoto huyo alikuwa amekaa hatua chache na mtoto huyo akitumia kompyuta huku mtoto wake mwingine mwenye umri wa miezi mitatu alikuwa amelala chini kwenye sakafu.

Wachunguzi wa kesi hiyo wamesema kuwa bila shaka mtoto huyo alishindwa kutofautisha bastola ya kweli na bastola feki ya Nintendo Wii.

Mama wa binti huyo, Tina Ann Cronberger mwenye umri wa miaka 32, alisema kuwa binti yake alikuwa mara kwa mara akiitumia bunduki feki kwenye kucheza gemu za Nintendo Wii.

Tukio hilo lilitokea jumapili jioni kwenye kitongoji cha Wilson, Tennesee nchini Marekani wakati baba wa kambo wa mtoto huyo, Douglas Cronberger, 32, alipochukua bunduki yake na kutoka nje alipohisi kuna mwizi ameingia nyumbani kwake.

Baada ya kuizunguka nyumba yake bila ya kumuona mwizi yoyote, alirudi ndani na kuiweka bastola kwenye meza sebuleni na kisha kwenda kulala.

Muda mfupi baadae, Chayenne alijipiga risasi na alipowahishwa hospitalini alifariki njiani.

Haijajulikana kama wazazi wa mtoto huyo watafunguliwa mashtaka au la.

source nifahamishe

Polisi Anapozimeza Pesa za Hongo Alizopokea

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Polisi mmoja wa nchini Urusi ametiwa mbaroni kwa kupokea rushwa na kisha kujaribu kuzimeza noti za pesa alizopokea ili kupoteza ushahidi.
Polisi mmoja wa nchini Urusi ameingia matatani kwa kupokea rushwa ya pesa za Kirusi ruble 2000 sawa na Tsh. 95,000 na kisha kujaribu kuzimeza noti za hongo hiyo ili kupoteza ushahidi.

Afisa wa polisi, Alexei Nikolayev, alichukua rushwa toka kwa dereva aliyemkata kwa makosa ya barabani ili asimchukulie hatua dereva huyo.

Lakini dereva wa gari hilo aliwapa taarifa polisi ambao walimkamata afisa huyo wa polisi wakati akipokea rushwa.

Ili kupoteza ushahidi afisa huyo wa polisi alijifungia kwenye gari la polisi na kuanza kuzitafuna noti za pesa hizo.

Afisa huyo anaendelea kuchunguzwa na atafikishwa mahakamani uchunguzi utakapokamilika.

source nifahamishe

Mwanamke Apata Ajali Akijionyoa Nywele za Sehemu za Siri

Thursday, March 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja wa nchini Marekani huenda akatupwa jela baada ya kuligonga gari jingine alipoamua kuzinyoa nywele zake za sehemu za siri huku akiendesha gari.
Megan Mariah Barnes mwenye umri wa miaka 37 aliamua akiendesha gari kuelekea kwa mpenzu wake kusini mwa Florida, Marekani wakati ajali hiyo ilipotokea, televisheni ta WFOR-TV imeripoti.

Megan aliamua kujiweka sawa kabla hajafika kwa mpenzi wake na kuanza kuzinyoa nywele za sehemu zake za siri huku akiendesha gari huku akiamuachia mumewe wa zamani aliyekuwa kwenye gari hilo awe anabadilisha muelekeo wa usukani.

"Kama nisingekuwepo kwenye eneo la tukio nisingeliamini tukio hili", alisema afisa wa polisi Gary Dunick.

Megan alijitetea kuwa aliamua kujionyoa nywele zake za siri huku akiendesha gari ili awe tayari tayari atakapofika kwa mpenzi wake.

Megan aliligonga lori gari lililokuwa mbele yake wakati huo akiwa kwenye spidi ya kilomita 72 kwa saa.

Siku moja kabla ya tukio hilo, Megan alinyang'anywa leseni yake baada ya kufungiwa kuendesha gari miaka mitano kutokana na makosa ya kuendesha gari huku akiwa amelewa.

Megan huenda akahukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kwa kuendesha gari kizembe, kuendesha gari bila ya leseni, kuendesha gari bila ya bima na kuondoka kwenye eneo la ajali huku akiwa na majeraha.

source nifahamishe

Amchinja Mkewe Kwa Kunyimwa Unyumba Kwa Miaka 21

Tuesday, March 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Ufaransa amemchinja mkewe kwa kutumia kisu kidogo cha jikoni baada ya kukasirishwa na mkewe ambaye aliamua kuitunza bikira yake na kukataa kumpa unyumba kwa miaka 21 ya ndoa yao kwasababu ya alikuwa hataki kupata watoto.
Philippe Cousin mwenye umri wa miaka 53 alimchinja mkewe wa ndoa ya miaka 21 Nicole Cousin mwenye umri wa miaka 47 baada ya Nicole kuendelea kukataa kufanya naye mapenzi kwa kuhofia kupata watoto.

Nicole alikutwa amefariki kwenye nyumba yao katika mji wa Calais kaskazini mwa Ufaransa.

Philippe aliwaambia polisi kuwa mkewe alikataa kufanya naye mapenzi kwa kipindi chote cha ndoa yao akisema kuwa anahofia watoto watakaozaliwa watarithi ugonjwa sugu wa multiple sclerosis (ugonjwa unaosababisha madhara kwenye ubongo na uti wa mgongo) ambao umekua ukimsumbua baba yake Nicole.

Uchunguzi wa maiti ya Nicole ulithibitisha kuwa hadi wakati anafariki Nicole alikuwa kweli ni bikira ingawa alikuwa kwenye ndoa kwa miaka 21.

Siku ya tukio hilo ugomvi ulizuka kati ya Philippe na mkewe ambapo Philippe alichukua kisu na kumwekea mkewe shingoni kabla ya kukikata na kukinyofoa kabisa kichwa chake.

Baada ya tukio hilo Philippe aliwapigia simu polisi na kuwaambia "Samahani kwa kuwasumbua, nimemuua mke wangu".

Phillippe alipandishwa kizimbani jana kwa mauaji hayo aliyoyafanya mwezi aprili mwaka juzi.

Wakili wa Philippe alisema kuwa Philippe alifanya mauaji hayo kutokana na kuchanganyikiwa kimawazo kwa kushindwa kuwa baba.

Philippe ambaye hivi sasa anapatiwa matibabu ya kisaikolojia ndani ya jela huenda akahukumiwa kifungo cha maisha iwapo atapatikana na hatia.

source nifahamishe

Bibi wa China Aota Mapembe Kama Mbuzi

Tuesday, March 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Bibi mwenye umri wa miaka 101 wa nchini China anawashangaza mamia ya watu kutokana na mapembe kama ya mbuzi yanayoendelea kujitokeza kwenye kichwa chake.
Bibi Zhang Ruifang mwenye umri wa miaka 101 wa kijiji cha Linlou katika jimbo la Henan nchini China alianza kuota pembe moja kwenye kichwa chake mwaka jana.

Hadi sasa pembe hilo lililoota kwenye upande wa kushoto wa paji lake la uso limekua na kufikia urefu wa sentimeta sita. Upande wa kulia wa paji lake la uso kuna pembe jingine ambalo ndio kwanza linaanza kujitokeza.

Familia yake imepagawa na mapembe hayo na haijui kwanini yanajitokeza kwenye kichwa chake.

Mtoto wa mwisho wa bibi huyo anayeitwa Zhang Guozheng mwenye umri wa miaka 60 alisema kuwa wakati mapembe hayo yalipoanza kujitokeza mwaka jana hawakujali sana walidhania ni makunjamano ya ngozi tu.

"Lakini siku zilivyozidi kwenda pembe lilijitokeza kwenye kichwa chake na sasa limefikia sentimita sita" alisema Zhang ambaye kaka yao wa kwanza ana umri wa miaka 82.

"Hivi sasa kuna kitu kinajitokeza kwenye upande wa kulia wa paji lake la uso bila shaka ni pembe jingine", aliendelea kusema Zhang.

Madaktari walisema kuwa mapembe hayo yanaweza kuondolewa kwa operesheni lakini sababu ya kujitokeza kwa mapembe hayo bado haijulikani.

source nifahamishe

Mtikila atakwenda jela endapo atashindwa kulipa deni

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala ya jijini Dar es Salaam, imeamuru kunadiwa kwa mali za Mchungaji Mtikila ili kuweza kulipa deni linalomkabili kinyume na hapo atakwnda jela.
Uamuzi huo wa Mahakama umekuja baada ya ombi la kumtaka mchungaji kufungwa jela baada ya kushindwa kulipa deni la silingi milioni 8 analodaiwa.

Hivyo mahakama imeamuru kudainiwa kwa mali zake ili kuweza kufidia kulipa deni hilo na endapo itashindikana ombi la kufungwa kwake litazingatiwa.

Awali Mahakama ya Wilaya ya Ilala iliamua nyumba ya mchungaji huyo iliyopo Mikocheni jijini Dar es salaam iuzwe ili kufidia deni hilo, lakini Hakimu Hakimu Afumwisye Kibona alisitisha uamuzi huo na kuagiza mali zake nyingine ziuzwe kufanikisha malipo ya deni hilo.

Mtikila na mwenzake Mariam Issa wanadaiwa zaidi ya Shilingi milioni 8 na Pascazia Matete ambaye alidai aliwakopesha kwa ajili ya kufanyia biashara.

Matete alishinda kesi namba 78 ya mwaka 2008 aliyoifungua katika Mahakama ya Mwanzo ya Kariakoo mbele ya Hakimu Benjamin Mwakasonda.

Akitoa amri hiyo, Hakimu Kibona alisisitiza kuwa iwapo ombi hilo la kutafuta mali mbadala za Mtikila ziuzwe kwa ajili ya kulipa deni hilo halitafanikiwa, ombi la kumfunga jela litafuatia.

Uamuzi huo wa kumfunga au kutomfunga utatolewa Machi 18, mwaka huu na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Joyce Minde.

Awali baada ya Matete kushinda kesi hiyo kutokana na Mtikila kutohudhuria Mahakamani mara kwa mara, aliiomba mahakama iamuru nyumba ya Mtikila yenye namba MKC/MCB 1135 iliyo kwenye kiwanja namba 237, Kitalu C Mikocheni iuzwe ili alipwe deni lake.

Hata hivyo, ombi la kuuza nyumba hiyo lilishindikana baada ya kampuni ya kimataifa ya Cielmac kuwasilisha pingamizi ikieleza kuwa ilishanunua nyumba hiyo kwenye mnada uliofanywa na benki ya NBC kupitia kampuni ya Comrade Auction Mart $ Court Brokes baada ya Mtikila kushindwa kurejesha mkopo wa Sh15 milioni aliouchukua katika benki hiyo.


source nifahamishe

Serikali yaamuru umeme upitishwe Kanisa la Kakobe

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

HATIMAYE Serikali imeamua kupitisha waya za umeme wa msongo wa kilovolti 132 karibu na Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Serikali imetoa amri hiyo bila kupingwa baada ya kuridhika na taarifa iliyotolewa na kitengo cha utoaji ushauri cha Chuo Kikuu (BICO).

Jana Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja,akizungumza na waandishi wa habari alisema utekelezaji wa mradi huo unatakiwa kufanyika mara moja kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za nchi, kwani ni kwa ajili ya manufaa na ustawi wa taifa.

Alisema serikali imechukua hatua hiyo baada ya kuridhika na utafiti uliofanywa na wataalamu washauri wa BICO, TANESCO na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) umehakikishia serikali kuwa umeme huo hauna madhara kwa wananchi.

“Hivyo TANESCO inatakiwa kuendelea na zoezi la upitishaji wa nguzo za umeme katika eneo hilo” alisema Waziri.
Awali alisema kuwa kuna taarifa zilidai kuwa vipimo vya kupitihsa umeme huio kanisani hapo vilikosewa lakini iliundwa tume kuthibitisha hilo.

Hata hivyo alisema baada ya uchunguzi ilibaini hakuna vipimo vilivyokosewa na maamuzi yalithibitishwa na pande zote mbili kuthibitisha hilo.

Hivyo baada ya kuafikiana na uamuzi huo, Kakobe aliiomba serikali kufikiria kubadilisha laini na kuziweka katikati ya barabara ya Sam Nujoma kwa kuwa bado anaamini kuwepo kwa madhara ya mitambo yake ya televisheni.

Hata hivyo, Waziri Ngeleja alisema serikali haitaweza kupitisha laini hiyo katikati ya badabara, kwani sehemu hiyo kumesimikwa taa za barabarani na pia inakusudiwa kutumika kwa ajili ya mradi wa mabasi yaendayo kasi.

Aliongeza kuwa serikali haiwezi kubadili usanifu wa mradi huo kwa vile hakuna uhakika endapo maombi hayo ya kujenga kituo cha televisheni yatakidhi vigezo vyote ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa masafa.

“Kwa kweli serikali haiwezi kufanya kazi kwa kuhisi, kwani TCRA imethibitisha haijawahi kupokea wala kufanya mchakato wa maombi kutoka kwa kanisa hilo,” alisema Ngeleja.

Alisema BICO katika taarifa yake imeitaka TANESCO kutumia mbinu bora za ujenzi wa laini ya msongo huo, ili kuepukana na kona kali kwenye waya na kutounganisha waya sehemu yoyote kati ya nguzo namba 18 na 19 ambazo ziko kwenye eneo la karibu na kanisa hilo.

Katika taarifa hiyo ya Waziri iliongeza kuwa serikali imetumia shilingi milioni 25 kwa ajili ya kumlipa mshauri mtaalam BICO hadi kukamilika kwa ripoti hiyo ambayo imeweza kuondoa utata uliokuwepo kuhusiana na madai ya kuwepo kwa madhara.

Alisema mradi huo utahakikishwa unamalizika haraka iwezekana kwa kuwa kwa kiasi kikubwa utapunguza kukatika katika kwa umeme kunakosababishwa na uhaba pamoja na uchakavu wa njia za kusafirishia umeme.

Alisema mradi huo unatakwia ukamilike kabla ya Machi 15 mwaka huu, na kusema mrdi huo ukienda kinyume na hapo serikali inaweza ikapata hasara na wafadhili wanaweza wakahitaji fedha zao.

Mgogoro huo ambao ulidumu kwa takribani zaidi ya miezi miwili baina ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO) na kanisa hilo linaloongozwa na Askofu Zakaria Kakobe kubisha kupitisha mradi huo kanisani hapo wka madai unamuathiri.

Na aliamua kutengeneza fulana maalum zinazovaliwa na waumini wa kanisa lake huku wakipiga kambi kanisani hapo kwa saa 24 kwa ajili ya kulinda kukabiliana na wafanyakazi wa TANESCO watakaokwenda kupitisha nguzo hapo.

Katika lindo hilo wafanyakazi wawili wa Tanesco waliweza kujeruhiwa walipofika kanisani hapo kuweka nguzo kupitihsa umeme huo.


source nifahamishe

Mwanafunzi Mahakamani kwa wizi wa Mil.5

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanafunzi Abdallah Miti [18] wa Shule ya Sekondari ya Ari iliyopo Tabata, amefikishwa katika Mahakama ya Ilala ya jijini Dar es Salaam, kujibu tuhuma za wizi wa kuaminika wa Shilingi milioni 5
Mwanafunzi huyo alisomewa mashtaka mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka, Nassoro Katuga mbele ya Hakimu Joyce Minde wa Mahakama hiyo.

Katuga alidai, mtuhumiwa alitenda kosa hilo, Februari 20, mwaka huu katika mtaa wa Garden Ilala jijini Dar es Salaam.

Katuga alidai mwanafunzi huyo aliiba fedha hizo kutoka katika gari namba T 630 aina ya Toyota mali ya Anselem Sigela.
Mtuhumiwa alikana kuhusika na wizi huo na alirudishw rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana aliyopewa.

Ambapo alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika wendye uwezo wa kusaini shilingi milioni 5 mahakamani hapo.

Hivyo kesi hiyo iliahirishwa, itatajwa tena Machi 16, mwaka huu.

source nifahamishe

Noti za Plastiki Kuchukua Nafasi ya Noti za Karatasi

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kidogo kidogo noti za karatasi zinaanza kutoweka duniani na nafasi yake inachukuliwa na noti za plastiki, Kanada imekuwa nchi ya nane duniani kubadilisha pesa zake na kuanza kutumia noti za plastiki.
Noti za karatasi kidogo kidogo zinaelekea kuwa historia na nafasi yake inachukuliwa na noti za plastiki ambazo hazipitishi maji hivyo hata ukizisahau kwenye nguo zako wakati wa kuzifua hazitapata madhara yoyote tofauti na noti za noti za karatasi ambazo huchanika kirahisi zinapolowa maji.

Kanada inakuwa nchi ya nane duniani kubadilisha noti zake na kuanza kutumia noti za plastiki. Kanada itaanza kuziondoa noti za karatasi kidogo kidogo kuanzia mwishoni mwa mwaka ujao.

Noti za plastiki zinatumia plastiki aina ya polymer biaxially-oriented polypropylene (BOPP) na zimeambatanishwa na vionjo vingine vya ulinzi ili kuzifanya noti hizo ziwe si rahisi kufojiwa.

Noti za plastiki hazichaniki wala kuharibika kirahisi hivyo kuziokoa pesa za serikali zinazotumika kuchapisha noti mpya kila baada ya muda.

Faida nyingine ya noti za plastiki ni kwamba hazibebi uchafu mwingi na bakteria kama zilivyo noti za karatasi. Mfano mzuri ni noti za dola ya Kimarekani asilimia kubwa ya noti hizo zina uchafu wa madawa ya kulevya kutokana na kutumiwa zaidi na wauzaji wa madawa ya kulevya.

Australia ndio iliyokuwa nchi ya kwanza kutumia noti za plastiki. Ilianza kutumia noti hizo tangia mwaka 1992.

Nchi zingine zinazotumia noti za plastiki ni Bermuda, Brunei, New Zealand, Papua New Guinea, Romania na Vietnam.

source nifahamishe

Mizimu Iliyowekwa Kwenye Vichupa Yapigwa Mnada

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mizimu miwili iliyokamatwa na kuingizwa kwenye chupa wanapigwa mnada kwenye internet na mamia ya watu wamejitokeza kuinunua mizimu hiyo.
Mwanamke wa nchini New Zealand, Avie Woodbury anawapiga mnada mizimu waliokuwa wakimsumbua kwenye nyumba yake ambao walikamatwa na mchungaji wa kanisa moja nchini humo na kuingizwa kwenye vichupa viwili vidogo.

Avie ameweka tangazo kwenye internet akivipiga mnada vichupa viwili ambavyo anasema vina mizimu iliyokuwa ikimsumbua kwa muda mrefu.

Avie alisema kuwa mizimu hiyo ilikamatwa na kuwekwa kwenye vichupa vidogo vyenye maji matakatifu.

"Maji matakatifu yanawafanya mizimu waishiwe nguvu na kuwafanya walale muda wote", alisema Avie.

Avie ameweka tangazo lake kwenye tovuti ya minada inayoitwa TradeMe. Hadi sasa dau kubwa alilopata ni paundi 1,000.

Avie amedai kuwa tangia mizimu hiyo ilipowekwa kwenye chupa mwezi julai mwaka jana hajapata usumbufu wowote kwenye nyumba yake kama ilivyokuwa zamani.

Mmoja wa mizimu hiyo anadaiwa kupenda kuviangusha vitu na kuzima na kuwasha vitu vya umeme. Mzimu mwingine unadaiwa kupenda kuwatisha watu.

Ili kuizindua mizimu hiyo Avie amesema kuwa ameambiwa kuwa ayamimine maji yaliyomo kwenye vichupa hivyo kwenye dishi na ayaache maji hayo yayeyuke ndani ya nyumba anayotaka mizimu hiyo ikae.

Chupa za mizimu hiyo zimewekewa majina maalumu ili wanunuzi wajue wanamnunua mzimu yupi.

Mnada wa mizimu hiyo umevuta watu wengi na umebakiza siku mbili kabla ya mshindi mwenye dau kubwa kuondoka na vichupa vyenye mizimu hiyo

source nifahamishe

http://www.nifahamishe.com/NewsImages/4193402.jpg

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto aliyezaliwa kabla ya muda wake ambaye alikuwa mwepesi sana kiasi cha kwamba kopo dogo la cocacola lilikuwa zito kulinganisha na uzito wake, amemaliza minane akiwa hai pamoja na hofu ya madaktari kuwa asingeweza kuishi siku nyingi.
Mtoto huyo alizaliwa nchini Ujerumani akiwa na umbile dogo sana na uzito wa gramu 275 tu kiasi cha kwamba aliingia kwenye rekodi za kuwa mtoto wa kiume aliyezaliwa akiwa na uzito mdogo kuliko wote.

Kwa jinsi alivyokuwa na umbile dogo karatasi ya daftari yenye ukubwa wa A4 iliweza kumfunika kuanzia kichwani hadi miguuni.

Uzito wake ulikuwa ni robo tatu ya uzito wa kopo la Cocacola ambalo huwa na uzito wa gramu 350.

Awali madaktari walisema kuwa ni vigumu sana kwa mtoto anayezaliwa akiwa na uzito chini ya gramu 350 kuishi muda mrefu.

Lakini mtoto huyu amefanikiwa kumaliza miezi kadhaa akiwa hai kutokana na matunzo ya kitaalamu aliyokuwa akipewa.

Habari za kuzaliwa kwa mtoto huyo hazikutangazwa kutokana na hali mbaya ya kiafya aliyokuwa nayo wakati alipozaliwa.

Madaktari wameamua kutoa taarifa za kuzaliwa kwa mtoto huyo baada ya kuthibisha sasa kuwa afya yake imekuwa njema na maisha yake hayako hatarini tena.

Mtoto huyo alizaliwa mwezi juni mwaka jana wakati mimba ya mama yake ilipokuwa imetimiza wiki 25.

Alitumia miezi sita akipewa huduma maalumu hospitalini kabla ya wazazi wake kuruhusiwa kuondoka naye mwezi disemba mwaka jana wakati uzito wake ulipoongezeka na kufikia kilo 3.7.

Taarifa ilisema kuwa madaktari wa Ujerumani walizipitia rekodi za watoto wa kiume waliozaliwa kabla ya muda wao katika nchi mbali mbali duniani lakini hakupatikana mtoto hata mmoja aliyezaliwa akiwa na uzito mdogo kama wa mtoto huyo.

source nifahamishe

Makahaba 40,000 Kwenda Afrika Kusini Wakati wa Kombe la Dunia

Monday, March 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Makahaba wapatao 40,000 toka nchi mbalimbali duniani wanatarajiwa kuingia nchini Afrika Kusini wakati wa kombe la dunia litakalofanyika nchini humo baadae mwaka huu.
Wanawake wapatao 40,000 wanatarajiwa kuingia nchini Afrika Kusini kufanya kazi ya ukahaba wakati wa mwezi mmoja wa kombe la dunia ambalo litafanyika baadae mwaka huu nchini humo.

Afrika Kusini inaongeza ulinzi kwenye mipaka yake ili kuzuia wimbi hilo la makahaba ambao wengi wao wanatarajiwa kutoka nchi za ulaya mashariki.

Zaidi ya watu 450,000 toka nchi mbali mbali duniani wanatarajiwa kuingia nchini Afrika Kusini kwaajili ya kombe la dunia.

Akiongea katika kikao na umoja wa mataifa kuhusiana na vita dhidi ya madawa ya kulevya na uhalifu nchini humo, David Bayever, ambaye ni makamu mwenyekiti wa mamlaka ya kupambana na madawa ya kulevya nchini Afrika Kusini alisema kuwa maafisa wa Afrika Kusini wanahofia wimbi kubwa la wanawake wanaotarajiwa kuingia nchini humo kwaajili ya biashara ya ukahaba.

"Tumepewa taarifa na waandaaji wa kombe la dunia kuwa wamepata taarifa kuwa wanawake 40,000 wameajiriwa kuja kufanya ukahaba wakati wa kombe la dunia", alisema.

"Hali inatisha sana kutokana na kwamba asilimia 16 ya idadi ya watu wana maambukizi ya virusi vya ukimwi", alisema.

Bayever alisema kuwa wamehakikishiwa na idara ya uhamiaji kuwa ulinzi utaongezwa kwenye mipaka na ukaguzi wa pasport utaimarishwa.

source nifahamishe

Auliwa Kwasababu ya Picha Kwenye Facebook

Sunday, March 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mwenye wivu aliyekuwa akiishi nchini Trinidad na Tobago alisafiri umbali mrefu hadi Uingereza na kumuua mpenzi wake baada ya kuona picha yake kwenye Facebook akiwa na mwanaume mwingine.
Paul Bristol, 25, alisafiri toka Trinidad and Tobago hadi Uingereza kumfuata mpenzi wake ambaye alipata mpenzi mwingine baada ya kufika Uingereza.

Paul alifanya safari hiyo kutokana na wivu aliokuwa nao baada ya kuona picha ya mpenzi wake huyo kwenye mtandao wa Facebook akiwa na mwanaume mwingine aliyemtambulisha kama mpenzi wake.

Paul alimuua kwa kumchoma choma na kisu Camille Mathurasingh, 27, ndani ya nyumba aliyokuwa akikaa mashariki mwa jiji la London.

Paul ambaye ni fundi wa vifaa vya umeme, alisafiri kwenda Uingereza ndani ya wiki mbili baada ya kuiona picha hiyo kwenye Facebook.

Paul amepandishwa kizimbani nchini Uingereza na alikanusha mashtaka ya mauaji aliyofunguliwa.

Mahakama iliambiwa kuwa Paul na Camille walikuwa wapenzi kwa miaka mitatu nchini Tobago lakini Camille alivyofika Uingereza alipata mpenzi mwingine na kuamua kuuvunja uhusiano wake na Paul kimya kimya.

"Inavyoonekana mpenzi wake alitaka kuuvunja uhusiano wao kimyakimya bila ya kumwambia kuwa amepata mpenzi mwingine", alisema mwendesha mashtaka wa kesi hiyo.

"Aligundua uhusiano wao baada ya kuziona picha zao kwenye Facebook".

Paul alikamatwa na polisi wakati alipokuwa akikimbia baada ya kufanya mauaji huku akiwa na damu usoni na kwenye nguo zake.

Hukumu ya Paul itatolewa baadae mwezi huu.

source nifahamishe.

Mwanamieleka wa Sumo Ainyofoa ATM na Kukimbia Nayo

Sunday, March 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamieleka wa Sumo wa nchini Urusi ametiwa mbaroni baada ya kuinyofoa mashine ya kutolea fedha toka kwenye ukuta wa duka moja nchini humo na kisha kuibeba mabegani na kukimbia nayo.
Mwanamieleka wa mchezo wa Sumo wa nchini Urusi ametiwa mbaroni baada ya kuing'oa mashine ya kutolea fedha toka kwenye ukuta wa duka moja mjini Moscow na kisha kuanza kukimbia nayo.

Polisi wa nchini Urusi walisema kuwa mwanamieleka huyo baada ya kuing'oa mashine hiyo yenye uzito wa kilo 90, aliiweka mabegani na kuanza kukimbia nayo.

Polisi waliendelea kusema kuwa mwanamieleka huyo alifika kwenye eneo la tukio akiwa na wenzake wawili na kuing'oa mashine hiyo iliyokuwa na kiasi cha pesa za kirusi roubles 25,000 sawa na Tsh. Milioni 1.2.

Mfanyakazi wa duka hilo aliyeshuhudia tukio hilo alipiga simu kuwaita polisi ambao waliwahi kufika na kuwakamata washirika wawili wa mwanamieleka huyo.

Mwanamieleka huyo alikamatwa na kushikiliwa na polisi baada ya kukiri kosa lake

source nifahamishe

Polisi Mwanamke Mwenye Pepo la Ngono Asimamishwa Kazi

Sunday, March 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Afisa mmoja wa polisi mwanamke wa nchini Australia amesimamishwa kazi kutokana na usumbufu anaowapa maafisa wa polisi wa kiume kwa kuwabembeleza afanye nao mapenzi.
Afisa wa polisi Jessica Parfrey mwenye umri wa miaka 19, amesimamishwa kazi kutokana na usumbufu anaowapa maafisa wenzake wa kiume kwa kuwataka afanye nao mapenzi.

Ndani ya siku chache za kuanza kazi kama afisa wa polisi wa mjini Sydney nchini Australia, Jessica alimtongoza bosi wake akimwambia kuwa "Kila mtu anajua kuwa unatakiwa uwe na uhusiano wa kimapenzi na mfanyakazi mwenzako".

Mwezi mmoja baada ya kuona bosi wake hana dalili zozote za kukubali, Jessica alimfuata na kumwambia "Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 19, unaonaje tukifanya mapenzi tu, hivi wewe una matatizo gani?"

Mahakama ya mambo ya kazi iliambiwa pia kuwa Jessica alifanya mapenzi na afisa mwingine wa polisi kwenye choo cha baa.

Jessica hakuishia hapo, alimsumbua afisa mwingine mwanaume wa polisi kwa kumpigia simu mara 12 na kumtumia meseji sita kabla ya kumuahidi kumsaidia afisa huyo kwenye mtihani wake wa mambo ya polisi. Jessica alimwambia afisa huyo kuwa kwa kila swali moja atakalopata basi yeye atasaula nguo yake moja. Afisa huyo alikataa dili hilo.

Awali Jessica alisimamishwa kazi mwishoni mwa mwaka 2007 lakini alikata rufaa akisema kuwa matukio ya yeye kuwataka maafisa wenzake yalitokea wakati wakiwa baa nje ya muda wa kazi.

Mahakama ya kazi ya mjini Sydney ilitoa uamuzi wake juzi na kuitupilia mbali rufaa ya Jessica.

Mahakama hiyo iliunga mkono hukumu iliyotolewa awali ya kumfukuza kazi Jessica kwa kukiuka maadili ya kazi na kuwasumbua maafisa wenzake.

source nifahamishe