Dawa ya Babu inawezekana kuwa katika mfumo wa vidonge -WHO

Thursday, May 05, 2011 / Posted by ishak / comments (1)


Foleni ya kupewa kikombe cha babu

UTAFITI unaoendelea kufanyika wa dawa ya Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa kijiji cha Samunge umebainika kuwa dawa inatibu maradhi sugu na Shirika la Afya Duniani [who] Kuikubali dawa hiyo
Hayo yamebainishwa na Askofu wa Kanisa la KKKT na kubainisha kuwa shirika hilo limekubali kuwa dawa hiyo inatibu maradhi sugu kama ilivyobainishwa awali katika utafiti wa kina walioufanya.

Imesemekana kuwa dawa hiyo inawezekana kuwa katika mfumo wa vidonge na chupa.

Shirika la Afya Duniani WHO ambalo lilituma wataalamu wake kuichunguza dawa ya babu, limebainisha hilo na kulifanyia kazi mikakati hiyo ya kuweka dawa hiyo katika mifumo hiyo na si kikombe pekee kama ilivyozoeleka, alisema Askofu huyo.

Pia dawa hiyo imethibitishwa na taasisi ya TMF na kubainisha kuwa dawa hiyo inatibu maradhi sugu.

Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa TMF, Marwa Gonzaga jijini Dar es Salaam.

Alisema wakati wakiendelea na utafiti huo walibaini kuwa tiba hiyo ni mchanganyiko wa mizizi ya miti shamba ya aina mbili ambayo ni kisayansi unafahamika kama Carissa Spinarum na mti wa Ntuntwa.

Tayari dawa ya babu imeshajizolea sifa ndani na nje ya nchi ambapo watu wameendelea kumiminika kijijini hapo kunywa dawa hiyo.

Hata hivyo taarifa zilizopatikana baadae zimesema kuwa babu amekataa dawa yake kufanyiwa mabadiliko yoyote kwakuwa Mungu hapendi.

Babu alisema kuwa kwakuwa dawa hiyo ni ya miujiza alioteshwa na Mungu, masharti aliyopewa na mungu kwenye ndoto yake hayaruhusu dawa hiyo ifanyiwe mabadiliko yoyote yale. Labda kama ataoteshwa ndoto nyingine ya kupewa ruhusa kufanya hivyo.

source nifahamishe

Wakristo Wamsalie Osama

Thursday, May 05, 2011 / Posted by ishak / comments (0)



Kardinali Albert Vanhoye

Wakristo inabidi wasali kumuombea makazi mema peponi Osama bin Laden ingawa alikuwa ni adui wao kwakuwa kutoa msamaha ndio mafundisho ya biblia.
Ingawa Osama alikuwa ni adui wa wakristo, wakristo inabidi wasimame kusali na kumuombea makazi mema Osama bin Laden.

Hayo yalisemwa na kardinali Albert Vanhoye mwenye umri wa miaka 87 wa kanisa katoliki nchini Italia ambaye alisema kuwa mafundisho ya biblia yanafundisha kusameheana.

"Mimi nimeusalia mwili wa Osama bin Laden, inatubidi tumuombee dua njema kama tulivyowaombea wahanga wa shambulio la septemba 11, hivyo ndivyo Yesu anavyowafundisha wakristo", alisema Kardinali Vanhoye.

"Yesu ametutaka tuwasamahe maadui zetu, tunaposali huwa tunasema "Baba, tusamehe kwa yale tuliyoyatenda kama vile tulivyowasamehe watu kwa yale waliyotutendea".

"Sala hii haiwezi kukubalika kama bado tutaendelea kuweka chuki kwa maadui zatu", alisema Kardinali Vanhoye, ambaye alichaguliwa kuwa Kardinali na Pope Benedict XVI mwaka 2006.

Kardinali Vanhoye anatambulika sana kwa mafundisho yake kuhusiana na biblia.


source nifahamishe

Binti wa Osama bin Laden Akiri Baba Yake Ameuliwa

Thursday, May 05, 2011 / Posted by ishak / comments (0)


Osama bin Laden

Mtoto wa kike wa Osama bin Laden amesema kuwa baba yake alikamatwa akiwa hai kabla ya kuuliwa kwa kupigwa risasi mbele yake na wanajeshi wa kikosi maalumu cha Marekani.
Televisheni ya Al-Arabiya iliwanukuu maafisa usalama wa ngazi za juu wa Pakistan wakisema kuwa binti huyo wa Osama mwenye umri wa miaka 12, aliwaambia kuwa baba yake aliuliwa mbele ya familia yake na kisha mwili wake kuburuzwa hadi kwenye helikopta ya Marekani.

Mwili wa mtoto wa kiume wa Osama nao ulichukuliwa na wanajeshi wa Marekani na kupakizwa kwenye helikopta.

Televisheni ya Al-Arabiya iliwanukuu maafisa usalama wa Pakistan wakisema kuwa watoto sita wa Osama bin Laden, mmoja wa wake zake na mwanamke mmoja toka Yemen ambaye inasemekana alikuwa daktari wake walisafirishwa hadi kwenye mji wa Rawalpindi karibu na mji wa Islamabad, kupatiwa matibabu kwenye hospitali ya jeshi.

"Hivi sasa wanapatiwa matibabu kwenye hospitali ya jeshi ya Rawalpindi" alisema mmoja wa Maafisa usalama wa Pakistan na kuongeza kuwa mke wa Osama bin Laden aliwaambia kuwa wamekuwa wakiishi Abbottabad kwenye nyumba hiyo kwa miezi sita sasa.

Afisa mwingine wa ngazi za juu wa Pakistan alisema kuwa baadhi ya taarifa zilizotolewa na Marekani kuhusiana na kukamatwa na kuuliwa kwa Osama hazina ukweli ndani yake.

"Hakuna hata risasi moja iliyopigwa toka kwenye nyumba ya Osama, ndege yao ya kivita ilipata matatizo ya kiufundi angani na ilianguka kwenye eneo la tukio".

Maafisa usalama wa Pakistan walisema kuwa hawakukuta silaha yoyote wala mabomu wakati walipofanya msako wa nguvu ndani ya nyumba ya Osama baada ya maiti yake kuchukuliwa na Marekani.

Uchunguzi wa kwanza ulifanyika jumatatu na jumanne walirudia kufanya msako kwenye nyumba hiyo yenye vyumba 13. Walichokuta ndani ya nyumba ya Osama ni nyati wawili, ng'ombe mmoja na kuku wapatao 150.

"Kulikuwa hakuna handaki wala sehemu maalumu ya kujificha ndani ya nyumba hiyo, ndio maana sielewi kwanini mtu anayetafutwa kuliko watu wote duniani alienda kuishi pale", alisema afisa huyo wa Usalama wa Pakistan.


source nifahamishe