Babu wa Miaka 83 Amuua Mkewe Kwa Kumshindilia Bisibisi Kichwani

Wednesday, December 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Babu mwanablogu mzee wa nchini Taiwan mwenye umri wa miaka 83 amemuua mkewe mwenye umri wa miaka 80 kwa kumshindilia bisibisi kichwani na kisha kuweka maelezo jinsi alivyofanya mauaji hayo kwenye blogu yake.
Babu Wang Ching-hsi mwenye umri wa miaka 83 wa nchini Taiwan kutokana na huruma yake aliamua kuyamaliza maisha ya mkewe mgonjwa wa kansa kwa kuizamisha bisibisi kwenye kichwa chake.

Kabla ya kufanya mauaji hayo, Babu Wang aliandika kwenye blogu yake kuwa hali ya mkewe imezidi kuwa mbaya na amepoteza hamu ya kuendelea kuishi duniani.

Babu Wang alimpa mkewe dawa za usingi na alipopitiwa na usingizi alimuua kwa kuizamisha bisibisi kwenye fuvu lake la kichwa.

Kwa mujibu wa magazeti ya Taiwan, Wang alipiga simu polisi kuwapa taarifa kuwa amemuua mkewe na alikaa nje ya nyumba yake akiwasubiri polisi wafike.

"Kwanini nimemuua mke wangu?, majibu yote yapo kwenye blogu yangu", alisema Wang akiwaambia waandishi wa habari wakati akiingizwa kwenye karandinga la polisi.

Kwa mujibu wa taarifa zilitolewa, Wang alikubaliana na mkewe miaka kumi iliyopita kuwa kila mmoja wao afariki kwa amani muda utakapofika.

Katika makubaliano hayo, Wang alimwambia mkewe, "Muda utakapofika nitakuua".

Kumekuwa na mjadala mkubwa nchini Taiwan kuhusiana na haki ya mtu aliyechoka kuishi kusitisha maisha yake.

Mwezi juni mwaka huu, baraza la kutunga sheria la Taiwan lilipitisha sheria ya kuwaruhusu wagonjwa na ndugu wa mgonjwa aliyekuwa mahututi kwa magonjwa yaliyofikia kikomo, kusitisha kuwapa dawa au huduma za kurefusha maisha yao ili kuwaepusha na mateso wanayopata.


source nifahamishe

Jela Miaka Mitano Kwa Kusoma Email ya Mkewe

Wednesday, December 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani ambaye alifungua email ya mkewe na kugundua kuwa mkewe alikuwa akifanya mapenzi nje ya ndoa, anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela.
Leon Walker mwenye umri wa miaka 33 mkazi wa Michigan nchini Marekani anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela kwa kufungua na kusoma email za mkewe.

Leon alifungua email ya mkewe, Clara Walker, kwa kutumia kompyuta waliyokuwa wakiitumia pamoja nyumbani kwao.

Kwa kutumia password yake, Leon alifungua akaunti ya Gmail ya mkewe na alisoma email zake ambapo aligundua kuwa mkewe alikuwa akitembea nje ya ndoa.

Mkewe alikasirika baada ya siri hiyo kufichuka na aliamua kufungua kesi ya madai ya talaka ambapo pia alimfungulia Leon mashtaka ya kusoma email zake.

"Hii ni kesi ya kustaajabisha, hakuna sheria inayoweka wazi suala kama hili", alisema mwanasheria Frederick Lane.

Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa hii ni mara ya kwanza sheria dhidi ya wizi wa nyaraka za siri kwenye masuala ya kibiashara inatumika kwenye masuala ya kifamilia.

Baadhi ya wanasheria wanasema kuwa huenda Leon akahukumiwa kwenda jela miaka mitano iwapo atapatikana na hatia ya kutumia password ya mkewe kusoma email zake.

Leon akiongea na waandishi wa habari alisema kuwa alichungulia email za mkewe ili aweze kujua chanzo cha mkewe kuwatelekeza watoto wao.

Kesi ya Leon itaanza kusikilizwa februari 7 mwakani.

source nifahamishe

SIRI ZA MTANDAO WA WIKILEAKS: aliyemhoji Dk Hoseah ni jasusi aliyebobea

Wednesday, December 22, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

WAKATI wananchi wakimkosoa mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah kupinga taarifa ya Wikileaks iliyovujisha mazungumzo yake na ofisa wa ubalozi wa Marekani, imebainika kuwa Mmarekani huyo amepikwa "kijasusi" katika masuala ya usalama wa taifa, uhusiano wa kimataifa, jeshi na ni ofisa mwandamizi.

Ofisa huyo, D. Purnell Delly alipeleka taarifa ya mazungumzo nchini Marekani akiripoti kuwa DK Hoseah amemwambia kuwa Rais Jakaya Kikwete hayuko tayari kuachia sheria ichukue mkondo wake katika kuwashtaki vigogo wanaojihusisha na rushwa.

Dk Hoseah, ambaye kwenye taarifa hiyo anadai kutishiwa maisha kiasi cha kufikiria kuikimbia nchi, amekiri kuongea na ofisa huyo lakini akadai kuwa ofisa huyo alimkariri tofauti na alivyosema.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Dk Hoseah amefafanua kuwa alichokisema ni kwamba Rais Kikwete hayuko tayari kuidhinisha vigogo wanaojihusisha na rushwa kufikishwa mahakamani bila ya kuwa na ushahidi wa kutosha dhidi yao.

Ubalozi wa Marekani umekataa kuzungumzia taarifa hizo za mawasiliano zilizovujishwa na mtandao wa Wikileaks ukisema kuwa hauna maelezo yoyote, kwa mujibu wa mkurugenzi wa kitengo cha mahusiano ya jamii cha ubalozi huo, Ilya D. Levin.

Ikulu ya Dar es salaam nayo haikutaka kuzungumzia suala hilo baada ya Mwananchi kuwasiliana na mwandishi wake, Premmy Kibanga.

Lakini Mwananchi imebaini kuwa ofisa huyo ni mzoefu katika kazi na amepitia mafunzo mbalimbali kiasi cha kumfanya aaminiwe na taifa hilo kubwa kufanya kazi hiyo inayofanana na ya kijasusi kwenye nchi tofauti, baadhi zikiwa ni zile zenye matatizo ya amani.

Taarifa ya Delly kwenda Ikulu ya Marekani ilivujishwa na mtandao wa wikileaks ambao umepata umaarufu mkubwa kwa kutoa siri za serikali mbalimbali duniani.

D. Delly alikuwa mkuu wa ujumbe wa wanadiplomasia wa Marekani kwenye Ofisi za ubalozi jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 9, mwaka 2005.

Kabla ya kuja Dar es Salaam kufanya kazi hiyo ya diplomasia, alikuwa msaidizi maalumu wa katibu msaidizi wa masuala ya Afrika kwenye Idara ya Serikali ya Marekani jijini Washington. Alipata nafasi hiyo baada ya kutumikia cheo cha naibu mkuu wa ujumbe wa Marekani jijini Khartoum, Sudan.

Delly alijiunga na idara hiyo mwaka 1983. Awali alikuwa mshauri wa mambo ya siasa na uchumi wa Copenhagen; naibu mshauri wa masuala ya Uchumi jijini Ankara, Uturuki na ofisa katika dawati maalumu nchini Sri Lanka.

Pia alifanya kazi hizo katika miji ya Edinburgh na El Salvador wakati wa vita na akajizolea heshima kubwa na hivyo kutunukiwa tuzo ya ujasiri na utumishi uliotukuka.

Dk Hoseah alieleza kuwa alikaririwa vibaya na ofisa huyo, lakini taarifa zinaonyesha kuwa Delly, ambaye anatokea Jimbo la Virginia, ni mtaalamu wa lugha akiwa amepata shahada yake ya kwanza katika Fasihi ya Lugha ya Kirusi kwenye Chuo Kikuu cha Dartmouth na shahada ya uzamili ya fasihi katika Chuo Kikuu cha Chicago.

Pia Mmarekani huyo alisomea Sheria za Kimataifa kwenye Chuo cha William na Mary, na shahada ya Uzamili ya Usalama wa Kimataifa na Uandaaji wa Mikakati ya Kijeshi katika chuo cha Newport, Rhode Island ambako wanafundishwa askari wa majini.

Chuo cha US Naval alichosomea Delly, ambaye alikuwa mwanachama na mwalimu wa vikosi vya ulinzi vya mwambao wa Marekani, kina kazi ya kuzalisha viongozi wa kuandaa Mikakati ya kijeshi na namna ya kuitekeleza.

Chuo hicho hutoa programu za fani za kijeshi zinazokwenda na wakati, usahihi, mahususi na zinazotekelezeka kwa idadi kubwa ya maofisa wa kijeshi wa Marekani, askari waajiriwa wa majini, waajiriwa raia ndani ya serikali ya Marekani na hata katika taasisi zisizo za kiserikali (NGOs), pamoja na maofisa wa kimataifa.

Chuo hicho hutarajia kupata kundi la viongozi wenye sifa ya uaminifu na kujiamini katika kila jukumu lao na wenye akili za kiutendaji na kimkakati, wenye tafakuri tunduwizi, uwezo mkubwa katika kuunganisha mambo na wapiganaji katika vita.

Mtaala wa chuo umegawika katika kozi kuu tatu za masomo; mikakati na sera, usalama wa taifa katika kufanya maamuzi na namna ya kuunganisha operesheni za kijeshi.

Kozi ya Mikakati na Sera imewekwa kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi kufikiria kulingana na mikakati kuhusu nadharia za kijeshi kuanzia mwanzo wa vita katika bahari kati ya Athens na Sparta hadi sasa. Lengo ni kuweka uhusiano kati ya Malengo ya Taifa kisiasa na namna ambayo mbinu zake za jeshi zinakuwa mahususi kutumika ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa (Ushindi).

Kozi ya pili ya Usalama wa Taifa katika Maamuzi imewekwa kwa ajili ya kuwasaidia watendaji wakuu katika jeshi na wananchi kukabiliana na hoja za kisiasa, kiuchumi, na kijeshi katika kufanya maamuzi sahihi kwenye masuala ya Usalama wa Taifa.

Kozi ya tatu ya kuunganisha operesheni za kijeshi inawasaidia wakuu wa taasisi za kijeshi kutafsiri mikakati ya kijeshi na hasa ya kikanda katika vita vya majini.

Karibu nusu ya wanafunzi wanaotoka Marekani ni maofisa kutoka jeshi, vikosi vya anga, majini, ulinzi wa mwambao na katika meli na kampuni na wakala wa ulinzi binafsi.

Uzoefu huo wa kazi na elimu kubwa ya ofisa huyo wa Marekani ulimfanya mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba kutokuwa na wasiwasi na ripoti ya Delly kwenda Ikulu ya Marekani.

“Delly hana sababu ya kumzulia Hoseah. Ni mzoefu na anajiamini katika kazi zake; haya ya kusema kwamba nimenukuliwa vibaya, ni ujanja ujanja wa kulindana tu,” alisema Profesa Lipumba ambaye alisomea shahada yake ya uzamili, akijikita katika uchumi kwenye Chuo Kikuu cha nchini Marekani.

“Yale yaliyoandikwa katika mtandao wa Wikileaks na baadaye kuchapishwa katika gazeti la The Guardian la Uingereza ni ya kweli ya Dk Hoseah na yale ya kukanusha ni ya kulindana.”

Prof Lipumba alidai kuwa ni kweli Rais Kikwete hayuko tayari hata siku moja kuona rais wa serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa au waziri mkuu wake, Frederick Sumaye wakisimamishwa mahakamani kujibu tuhuma za ufisadi.

Alisema mambo hayo yanafanana kabisa na yaliyoandikwa katika gazeti hilo mwaka 2007 kwamba Hoseah anatembea na mlinzi mwenye silaha kutokana na kuhofia usalama wake.

“Jambo la msingi ambalo tunaliona hapa ni kwamba tuna udhaifu mkubwa katika uongozi na viongozi hawana utashi na ujasiri wa kupambana na rushwa... Hoseah na hata Kikwete hawawezi kupambana,” alisemai.

“Fedha ile (dola 12.4 milioni alizolipwa Shailesh Vithlani katika ununuzi wa rada) haina mjadala kuwa ni rushwa, ni rushwa ambayo alilipwa Vithlani kifisadi kufanikisha zabuni ya uuzaji wa rada kwa serikali ya Tanzania.”

Wakili wa siku nyingi nchini, Profesa Abdallah Safari alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa taarifa iliyotolewa na mtandao huo ni ukweli.

"Kuamini utetezi wa Dk Hoseah ni vigumu kutokana na mwenendo wake," alisema Profesa Safari. "Alijaribu kumsafisha (mwanasheria na mbunge wa Bariadi Magharibi) Andrew Chenge katika kashfa ya rada.
“Amekuwa akitofautiana na ripoti mbalimbali mpaka za bunge kama ile ya Richmond. Kwa hiyo CCM ni watu wasioaminika na serikali yao... wana mambo yao bwana.”

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally alitazama suala hilo katika sura tatu, akielezea sura ya kwqanza kuwa ni nchi za Kiafrika kuanzisha taasisi zisizo huru na zinazoendeshwa kwa kutegemea msaada wa wahisani, akitoa mfano wa Takukuru.

“Hata ukisoma hiyo taarifa kwa umakini kwenye mtandao, utona kabisa kuwa Dk Hoseah alikuwa anajipendekeza kwa ajili ya kulinda ufadhili,” alisema Bashiru.

Alisema endapo Takukuru ingekuwa ni taasisi huru na inayojitegemea kwa kila kitu, basi kusingekuwa na sababu ya mkurugenzi wake kuzungumza na Wamarekani.

Katika mtazamo wake wa pili, Bashiru alisema wasomi, wanahabari na wanasiasa wana kazi kubwa ya kuangalia lengo la mtandao huo kufichua habari kama hizo zinzolihusu bara la Afrika na Asia.

“Lazima tujiulize kwa nini hizi siri zinafichuliwa wakati huu/ kwa nini Marekani na nchi kama Uganda, Iraq na Tanzania; kwa nini hakuna siri za Marekani na nchi nyingine tajiri kusema ni jinsi gani wanavyopanga kutugandamiza,” alisema Bashiru.

Kwa sura ya tatu, Bashiru alisema inakuwa vigumu kwa sasa kuangalia hatima ya mapambano ya rushwa, akisema ni lazima mtu ajitoe mhanga katika vita ya rushwa na kwamba kama hakuna dhamira ya kweli, huwezi kupambana.

“Dk Hoseah amekanusha baadhi ya mambo kwa hiyo labda tusubiri wamarekani wenyewe watuambie kama wamemlisha maneno, lakini kweli kwenye mapambano ya rushwa lazima mambo ya kutishiana maisha yawepo kwa sababu yanahusu watu wazito,” alisema Bashiru.

Mkurugenzi mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali ya kukuza demokrasia nchini Agenda Participation 2000, Moses Kulaba alisema mtandao huo umefungua macho ya Watanzania.

Alisema siri zilizofichuliwa zimekuwa uthibitisho wa masuala ambayo Watanzania walikuwa wakiyawaza kwa muda mrefu.

“Mimi mwenyewe nimeusoma ule mtandao, bado kuna mengi ni mapema mno kwa Dk Hoseah kuanza kukanusha,” alisema Kulaba.

Hussein Kauli
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo cha Uchumi, Adolf Mkenda alimtaka Dk Hoseah ajiuzulu iwapo ni kweli alimuelezea Rais Kikwete kuwa hapendi vita dhidi ya rushwa.

Mkenda alisema kitendo cha Dk Hoseah kueleza mambo ya ndani kwa maofisa wa ubalozi wa Marekani wakati anajua yeye anawajibika kwa serikali ni ukiukwaji wa maadili ya kazi yake na hivyo anapaswa kuwajibika kwa kujiuzulu.

“Ni jambo la ajabu sana kwa Dk Hoseah kufanya kitendo hicho, kama taarifa hizi ni za kweli inabidi ajiuzulu mwenyewe kwani hafai kuendelea kuiongoza Takukuru” alisema Mkenda na kuongeza kuwa iwapo atajiwajibisha, serikali haina budi kumchukulia hatua.

Mkenda pia alieleza kuwa kama Rais Kikwete hapendi sheria ichukue mkondo wake katika vita dhidi ya rushwa, amekiuka katiba.


source mwananchi

Thamani ya Shilingi ya Tanzania yapanda

Sunday, December 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Thamani ya Shilingi ya Tanzania imepanda mfululizo kwa muda wote wa wiki mbili zilizopita tokea Desemba 3 Mwaka huu ukilinganisha na Dola ya Kimarekani.
Kwa mujibu wa takwimu zinazotolewa kila siku na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kiwango cha kubadilisha fedha Desemba 2, kilikuwa Shilingi 1,487.55 kwa Dola moja, lakini Desemba 3, kilishuka na kufikia Shilingi1,485.23 upungufu wa shilingi 2.32.
Hadi kufikia Desemba 10, Dola ilibadilishwa kwa shilingi 1,477.22, pungufu kwa shilingi 8.01 ikilinganishwa na kiwango cha ubadilishanaji wa shilingi kwa dola wa Desemba 3 uliokuwa shilingi 1,485.23.
Kuanzia Desemba 13 hadi jana thamani ya Shilingi ilipanda kwa kasi kubwa ambapo Desemba 13 dola ya Kimarekani ilibadilishwa kwa Shilingi1,466.23, Desemba 14 ilibadilishwa kwa Shilingi 1,455.72, Desemba 15 ilibadilishwa kwa Shilingi 1,443.39 na jana dola ilibadilishwa kwa Shilingi1,432.42.
Hivyo takwimu hizi za Bot zinamaanisha kuwa thamani ya fedha yetu imeimarika ukilinganisha na dola ya Kimarekani kwa kipindi hiki cha wiki mbili zilizopita.
Kupanda huku kwa thamani ya shilingi mfululizo unakinzana na namna ilivyoporomoka kwa haraka mwanzoni mwa Agosti wakati harakati za uchaguzi zilipoanza hadi kura zilipopigwa na kuendelea hivyo hadi mwanzoni mwa mwezi huu.

source nipashe

ray ,kanumba watua kigali ................

Thursday, December 16, 2010 / Posted by ishak / comments (0)





kama unavyowaona katika kiwanja cha ndege walipowasili na pia wakitembezwa katika mji wa kigali na kupokewa na mashabiki wa film za kibogo...............


source newtimes

Maalim Seif ataka kusaidiwa mzigo

Sunday, December 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


KATIKA hali inayoashiria kuelemewa na mzigo wa majukumu, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, amekiomba chama chake, kumtafuta mtu wa kumsaidia katika nafasi hiyo, wakati kikisubiri uchaguzi wake.

Rai hiyo imekuja huku Katibu Mkuu Msaidizi wa CUF, Juma Haji Duni, akiwa ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya na Utabibu katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

Uteuzi huo umefanywa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.

Maalim Seif alitoa kauli hiyo mbele ya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipimba katika kikao cha Baraza Kuu la chama hicho, kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho, mtendaji huyo wa CUF pia alilitaka baraza kujipanga kwa uchaguzi mkuu ujao.

Maalim Seif alisema mtu atakayepata nafasi hiyo ya kumsaidia kwa muda lazima atambue kuwa nafasi hiyo itakuwa bado mikononi mwake (Seif) hadi atakapoyaachia rasmi majukumu ya umakamu wa Rais wa Zanzibar.

"Katibu mkuu atakayepata nafasi ya kuteuliwa, ajue yeye si Katibu Mkuu wa CUF, katibu mkuu nitabaki kuwa ni mimi hadi nitakapoiachia nafasi hii rasmi kwa kufuata utaratibu,"alisema Maalim Seif.

Alimuomba mwenyekiti kwa kushirikiana na baraza, kumsaidia katika kumtafuta au kumpendekeza mtu atakayemsaidia katika nafasi hiyo.

Katika kikao hicho, kiongozi huyo pia alimshukuru Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Dk Shein kwa kuweka uwiano mzuri katika uteuzi wa Baraza la Mawaziri na kwamba uteuzi huo, utaleta mabadiliko makubwa kwa wananchi wa Zanzibar.

Alisema CUF imepata mafanikio makubwa katika uteuzi huo kwa kuwa umepata nafasi ya kuongoza nchi na kwamba kwa sasa Zanzibar inaongozwa na vyama vya CCM na CUF tofauti na miaka ya nyuma ambapo nchi ilikuwa ikiongozwa na chama kimoja.

"Chama chetu ni miongoni mwa vyama viwili vinavyoongoza serikali, kwa hiyo tujivunie ushindi wetu kwani tumetimiza malengo ya CUF ya kushika madaraka ya nchi, tangu tukiunde tumejaribu mara tatu tukashindwa lakini mwaka huu tumeweza,"alisema.

Hata hivyo, alisema ushindi huo ni changamoto kwa CUF na kwamba wote waliopata uongozi wanapaswa kubeba majukumu na kuhakikisha kuwa wanawatumikia wananchi bila kubagua.

Alisema uteuzi wa mawaziri nane kutoka chama hicho ni mkubwa sana hasa ikizingatiwa kuwa Rais Dk Shein, alikuwa na uwezo wa kufanya lolote katika uteuzi huo.

"Mimi ni Makamu wa Kwanza wa Rais, nitamsaidia Rais wangu kufanya kazi kwa bidii kwa kushirikiana na mawaziri wote bila kuangalia kama ni wa CCM au CUF, nina hakika sote kwa pamoja tutaleta mabadiloko,"alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CUF (Lipumba) alimpongeza Maalim Seif kwa kuonyesha ukomavu wa siasa wakati wa kusubiri matokeo ya kura na baada ya kutangazwa kwa kutoa hotuba ya kihistoria tofauti na matarajio ya watu weng.

Alisema baadhi ya waty walidhani kuwa kauli yake ingeleta maafa.

"Tunampongeza kwa kuhakikisha kuwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar yanakuwa mbele badala ya maslahi binafsi kuchukua nafasi. Pia tunampongeza Dk Shein kwa ushirikiano aliotuonyesha katika kuunda baraza lake la mawaziri," alisema.

Alifafanua kuwa mafanikio ya CUF ni matokeo ya maridhiano mazuri yaliyofanywa na Katibu mkuu wa chama na Rais mstaafu wa Zanzibar, Abeid Amani Karume.


Alisema kuwa CUF imefungua njia, ili kwa pamoja wannchi wa Zanzibar, waweze kutatua matatizo yao na kuondokana na umaskini.

source mwananchi

Zitto adai amelishwa sumu

Sunday, December 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ambaye jana aliruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam alikolazwa kwa matibabu ya tumbo amedai kuwa matatizo hayo aliyapata baada ya kula chakula chenye sumu.“Namshukuru Mungu naendelea vizuri na nimesharuhusiwa kutoka hospitali, madaktari wameniambia ilikuwa food poisoning (chakula chenye sumu),” alisema Zitto.

Zitto ambaye hakuweza kueleza chakula hicho alikuwa wapi na kina sumu ya aina gani, alisema kuwa baada ya kugundua tatizo hilo, madaktari walimtaka kuwa makini na vyakula anavyokula.

“Sumu gani nimekula na ni wapi, mimi nadhani sio story (habari). Cha msingi kwa sasa naendelea vizuri na nimetakiwa kuwa makini na vyakula ninavyokula,” alisema Zitto.

Hata hivyo, kauli hiyo ya Zitto inapingana na madaktari wake waliosema kuwa mbunge huyo kupitia tiketi ya Chadema, alikuwa anasumbuliwa na mchafuko wa kawaida wa tumbo.

“Alikuwa anasumbuliwa na Gastro enteritis (mchafuko wa tumbo), tatizo hili linaweza kusababishwa na bacteria, virusi katika chakula, au kama chakula hakijapikwa vizuri,” alisema Dk Mustafa Bapumia.

Zitto alilazwa hospitalini hapo tangu Disemba 9 mwaka huu saa 3:00 usiku, baada ya kutoka kwenye mkutano wa ndani wa chama chake uliofanyika Bagamoyo mkoani Pwani ambako alivuliwa cheo cha Naibu Kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni.

Kuhusu hatua ya chama hicho kumvua Zitto wadhifa wake wa unaibu kiongozi wa upinzani bungeni, alisema kwa sasa bado hawezi kuzungumzia suala hilo kwa sababu hajapata taarifa rasmi kutoka chama chake mbali na kusoma suala hilo kwenye vyombo vya habari.

Hata hivyo, alieleza hakuwahi kuomba kupewa wadhifa huo, kwa hiyo endapo watu waliomwona anafaa kufanya kazi na kumpa wadhifa huo, wakiamua kumnyang’anya siyo tatizo kubwa kwake.

“Kwa sasa nadhani suala la afya yangu ndiyo muhimu zaidi. Ngoja kwanza nitoke hapa na afya yangu iimarike na kama kutakuwa kuna sababu ya mimi kuzungumza nitazungumza,” alisema Zitto:

“Lakini ikumbukwe kuwa mimi sikuwahi kuomba wadhifa huu…, kwa hiyo kama watu walionipa wameamua kunibadilishia, mimi sidhani kama kuna tatizo.”

Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe aliupolizwa na Mwananchi Jumapili juu ya Zitto kuvuliwa uongozi bungeni alisema kuwa chama kitatoa taarifa baadaye.

Katika hatua nyingine Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Amur Arfi aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam, amesafirishwa kwenda India kwa matibabu zaidi.

Arfi aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa madaktari waliokuwa wakimtibu wamemwambia kuwa mfuko wake wa nyongo una mawe hivyo anahitaji kufanyiwa upasuaji.

“Nilikuja hapa kwa sababu nilikuwa nasumbuliwa na maumivu makali ya tumbo, nilitoka Mpanda Disemba 2, mwaka huu kuja kwenye semina lakini kutokana na maumivu ya tumbo nilienda Hospitali ya Regency na baada ya kupigwa ultrasound nilielezwa kuwa nina tatizo la uvimbe kwenye maini,” alisema Arfi.

Alisema alivyokwenda katika Hospitali ya Aga Khan alielezwa kuwa ana tatizo jingine la mawe kwenye mfuko wa nyongo na kuwa inabidi afanyiwe upasuaji.

“Naishukuru serikali kupitia ofisi ya Bunge kunipeleka India kwa matitabu zaidi,” alisema Arfi.

Hata hivyo, alisema bado hajaelezwa hospitali anayokwenda kutibiwa na kuwa, taarifa zote hizo anazo muuguzi wa serikali atakayesafiri naye.
Wakati huohuo, Mtangazaji wa Televisheni ya Channel Ten, Cyprian Musiba, anadaiwa kuwekewa sumu kwenye chakula na kufanya alazwe hospitalini kwa matibabu.

Musiba alilazwa katika kituo cha Afya cha Ebrahim Haji kilichopo jijini Dar es Salaam juzi mchana akiwa hajitambui.

Mmoja wa madaktari wa hospitali hiyo, Dk Ramadhani Ali aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa Musiba alifikishwa katika hospitali hiyo akiwa anasumbuliwa na tumbo lakini, baada ya kupata matibabu, afya yake iliimarika na jana mchana aliruhusiwa kutoka hospitalini.

“Anaendelea vizuri kwa kweli na amesharuhusiwa” alisema Dk Ali huku akisita kueleza tatizo la lililokuwa linamsumbua Musiba.

Mke wa Musiba ambaye hakujitambulisha alisema kuwa kabla ya Musiba kuruhusiwa mmoja wa madaktari wa HospitaliI hiyo waliwaeleza kuwa Musiba alikula sumu iliyokuwa katika chakula.

“Tumeruhusiwa muda si mrefu ila daktari amesema Musiba alijisikia vibaya kwa kuwa alikuwa amekula sumu iliyokuwa katika chakula,”alisema mke wa Musiba.

Musiba ambaye mara nyingi hutangaza habari za michezo na burudani aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa juzi hali yake ilikuwa mbaya na kuongeza kuwa alipelekwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya matibabu.

“Hali yangu ilikuwa mbaya sana nilikuwa wa kufa tu ndugu yangu, ila namshukuru mungu naendelea vizuri, ila daktari hapa hospitali amenieleza kuwa nilikula sum,” alisema Musiba.

Habari zaidi zilidai kuwa Musiba alianza kupata matatizo ya tumbo saa kadhaa baada ya kula chakula katika hoteli moja iliyopo karibu na ofisi za Channel Ten

source mwananchi

Barafu inatabiriwa kuongezeka UK...........

Sunday, December 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



HALI ILIVYO UINGEREZA SASA

Kitabu cha Mafunzo ya Wizi

Tuesday, November 30, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwizi wa nchini Japan ambaye kutokana na kufanya wizi kwa mwaka alikuwa akijiingizia kiasi cha pesa sawa na Tsh. Milioni 540 ametoa kitabu cha kuelezea jinsi ya kuiba kwenye majumba ya watu bila kugundulika, kitabu hicho kimekuwa gumzo nchini Japan na kinanuliwa kwa wingi.
Mwizi wa nchini Japan, Hajime Karasuyama kutokana na utaalamu wake wa kuiba kwenye majumba ya watu, ametoa kitabu kinachoelezea jinsi ya kuiba kwa ustadi mkubwa bila ya kugundulika.

Kitabu chake kinachoenda kwa jina la "Kazi: Mwizi, Kipato Kwa mwaka: Yen Milioni 30", kimekuwa gumzo nchini Japan na kimekuwa kikinunuliwa kama njugu.

Wachapishaji wa kitabu hicho Futabasha Publishing wamesema kuwa nakala za mwanzo za kitabu hicho zipatazo 10,000 zimenunuliwa zote ndani ya siku 10 baada ya kitabu hicho kuzinduliwa.

Katika kitabu hicho, Karasuyama anaelezea jinsi ya kufungua vitasa vya milango ya aina yoyote ile kwa muda mfupi na bila ya ufunguo na jinsi ya kuvunja madirisha ya vioo bila ya kusababisha kelele.

Karasuyama ameelezea pia jinsi alivyokuwa akitumia lensi kuangalia ndani ya nyumba kwa kupitia kwenye tundu la funguo.

Mbali ya wizi wa majumbani, Karasuyama pia amelezea pia njia za kufanya utapeli na kuwaacha watu kwenye mataa.

Karasuyama alisema kuwa kutokana na wizi alikuwa akijiingizia kitita kinono kwa mwaka zaidi ya Tsh. Milioni 540.

"Tunapoingia ndani ya nyumba, sisi wezi huwa tunajua wapi watu huficha pesa zao", alisema Karasuyama alipokuwa akiongea na jarida la Shukan Taishu kuhusiana na kitabu chake ambacho kimeambatanisha maneno ya "Usijaribu kuniiga" kwenye ukurasa wake wa kwanza.

Wachapishaji wa kitabu hicho kinachouzwa Yen 1,200 sawa na Tsh. 20,000 wamekanusha madai kuwa kuchapishwa kwa kitabu hicho kutapelekea baadhi ya watu kugeuka wezi kwa kuiga staili za wizi za Karasuyama.

Wachapishaji hao wamesema kuwa kitabu cha Karasuyama kitawawezesha watu kujifunza njia zinazotumiwa na wezi hivyo kuweza kuzilinda vyema nyumba zao.

source nifahamishe

Siri za Marekani Zaanikwa

Tuesday, November 30, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Pamoja na serikali ya Marekani kuionya tovuti maarufu ya kutoboa siri zilizoficha ya WikiLeaks kutoziweka nyaraka zake za siri hadharani kwa kuwa maisha ya watu wengi yatakuwa hatarini, tovuti hiyo imezitoa nyaraka hizo za siri na kuiweka hadharani sura halisi ya Marekani.
Nyaraka za siri za Marekani zipatazo 250,000 zimeanza kuwekwa hadharani pamoja na serikali ya Marekani kuionya tovuti ya WikiLeaks kuwa inavunja sheria na inayaweka maisha ya watu wengi hatarini.

Tovuti ya WikiLeaks ambayo imebobea kwa kutoboa siri za ndani za masuala mbalimbali duniani ilikabiliwa na mashambulizi ya hackers ambao waliifanya tovuti hiyo ishindwe kupatikana online.

Hata hivyo nyaraka hizo za siri zimewekwa hadharani kama ilivyopangwa kwa kutumia magazeti ya The Guardian la Uingereza, gazeti la New York Times la Marekani, Der Spiegel la Ujerumani, El Pais la Hispania na gazeti la Le Monde la Ufaransa.

Nyaraka hizo za siri huenda zikaharibu uhusiano wa Marekani na baadhi ya viongozi wa nchi mbalimbali duniani ambao Marekani iliwapachika majina mbalimbali ya kuwakashifu.

Miongoni mwa nyaraka hizo za siri hizo ni mazungumzo ya siri kati ya Mfalme Abdullah wa Saudi Arabia ambaye mara nyingi sana alikuwa akiishinikiza Marekani ipigane vita na Iran ili kuziteketeza silaha zake za nyuklia.

Taarifa hizo ziliendelea kusema kuwa Mfalme huyo wa Saudia aliishinikiza Marekani iiwekee Iran vikwazo vikali vya kiuchumi na kuwapiga marufuku viongozi wake kusafiri kimataifa.

Nyaraka hizo ziliendelea kusema kuwa Mfalme Abdullah aliungwa mkono na Mfalme wa Bahrain, Hamad ibn Isa Al Khalifa na Mtawala wa Abu Dhabi, Sheikh Mohammad bin Zayed ambao nao waliitaka Marekani iiteketeze Iran.

WikiLeaks pia ilitoa nyaraka ambazo zilisema kuwa Marekani kwa kuwatumia maafisa wake kinyume cha sheria iliwapeleleza viongozi wa baraza la Umoja wa Mataifa na hata kufikia kuchukua kwa siri alama za mboni ya jicho na alama za vidole za katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon.

Marekani pia ilifuatilia simu walizokuwa wakipiga, fax, email na tovuti walizokuwa wakizitembelea.

Miongoni mwa majina ya kashfa waliyopachikwa viongozi wa serikali mbalimbali duniani, Marekani ilimuita Rais Mugabe wa Zimbabwe kuwa ni "Kichaa Mzee", kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi ameitwa "Mtu wa Ajabu Asiyeeleweka", wakati rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad amefananishwa na Hitler.

Nyaraka nyinginezo zilielezea jinsi Marekani ilivyokuwa ikizishinikiza baadhi ya nchi ziwachukue wafungwa wa kigaidi wa jela ya Guantanamo Bay. Nchi ya Slovenia ililazimishwa imchukue mfungwa mmoja wa Guantanamo Bay iwapo inataka kukutana na Rais Obama.

Nyaraka zaidi za siri zinazoonyesha jinsi Marekani ilivyokuwa ikivunja sheria za kimataifa zinaendelea kuchapishwa.

siurce nifahamishe

Obama Achanika Mdomo

Sunday, November 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais wa Marekani, Barack Obama ameshonwa nyuzi 12 kwenye mdomo wake baada ya kupigwa kiwiko kwenye mdomo wake wakati akicheza mpira wa kikapu pamoja na ndugu na jamaa zake wa karibu.
Obama alikuwa akicheza mpira wa kikapu pamoja na ndugu na jamaa kwenye kambi ya jeshi la Marekani ya Fort McNair mjini Washington, wakati kwa bahati mbaya mcheza wa timu pinzani aliporusha kiwiko chake na kumtandika Obama mdomoni.

Msemaji wa ikulu ya Marekani alisema kuwa Obama alipasuka mdomo na alipatiwa matibabu na madaktari wa ikulu.

Hata hivyo taarifa ya ikulu ya Marekani haikusema ni nani ndiye aliyempasua Obama mdomo wake kwa kiwiko.


source nifahamishe

Bill Gates

Saturday, November 20, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Top row: Steve Wood (left), Bob Wallace, Jim Lane. Middle row: Bob O'Rear, Bob Greenberg, Marc McDonald, Gordon Letwin. Bottom row: Bill Gates, Andrea Lewis, Marla Wood, Paul Allen. December 7, 1978.
Gates has donated the proceeds of both books to non-profit organizations that support the use of technology in education and skills development

William (Bill) H. Gates is chairman of Microsoft Corporation, the worldwide leader in software, services and solutions that help people and businesses realize their full potential. Microsoft had revenues of US$51.12 billion for the fiscal year ending June 2007, and employs more than 78,000 people in 105 countries and regions.

On June 15, 2006, Microsoft announced that effective July 2008 Gates will transition out of a day-to-day role in the company to spend more time on his global health and education work at the Bill & Melinda Gates Foundation. After July 2008 Gates will continue to serve as Microsoft’s chairman and an advisor on key development projects. The two-year transition process is to ensure that there is a smooth and orderly transfer of Gates’ daily responsibilities. Effective June 2006, Ray Ozzie has assumed Gates’ previous title as chief software architect and is working side by side with Gates on all technical architecture and product oversight responsibilities at Microsoft. Craig Mundie has assumed the new title of chief research and strategy officer at Microsoft and is working closely with Gates to assume his responsibility for the company’s research and incubation efforts.

Born on Oct. 28, 1955, Gates grew up in Seattle with his two sisters. Their father, William H. Gates II, is a Seattle attorney. Their late mother, Mary Gates, was a schoolteacher, University of Washington regent, and chairwoman of United Way International.

Gates attended public elementary school and the private Lakeside School. There, he discovered his interest in software and began programming computers at age 13.

In 1973, Gates entered Harvard University as a freshman, where he lived down the hall from Steve Ballmer, now Microsoft's chief executive officer. While at Harvard, Gates developed a version of the programming language BASIC for the first microcomputer - the MITS Altair.

In his junior year, Gates left Harvard to devote his energies to Microsoft, a company he had begun in 1975 with his childhood friend Paul Allen. Guided by a belief that the computer would be a valuable tool on every office desktop and in every home, they began developing software for personal computers. Gates' foresight and his vision for personal computing have been central to the success of Microsoft and the software industry.

Under Gates' leadership, Microsoft's mission has been to continually advance and improve software technology, and to make it easier, more cost-effective and more enjoyable for people to use computers. The company is committed to a long-term view, reflected in its investment of approximately $7.1 billion on research and development in the 2007 fiscal year.

In 1999, Gates wrote Business @ the Speed of Thought, a book that shows how computer technology can solve business problems in fundamentally new ways. The book was published in 25 languages and is available in more than 60 countries. Business @ the Speed of Thought has received wide critical acclaim, and was listed on the best-seller lists of the New York Times, USA Today, the Wall Street Journal and Amazon.com. Gates' previous book, The Road Ahead, published in 1995, held the No. 1 spot on the New York Times' bestseller list for seven weeks.



In addition to his love of computers and software, Gates founded Corbis, which is developing one of the world's largest resources of visual information - a comprehensive digital archive of art and photography from public and private collections around the globe. He is also a member of the board of directors of Berkshire Hathaway Inc., which invests in companies engaged in diverse business activities.

Philanthropy is also important to Gates. He and his wife, Melinda, have endowed a foundation with more than $28.8 billion (as of January 2005) to support philanthropic initiatives in the areas of global health and learning, with the hope that in the 21st century, advances in these critical areas will be available for all people. The Bill and Melinda Gates Foundation has committed more than $3.6 billion to organizations working in global health; more than $2 billion to improve learning opportunities, including the Gates Library Initiative to bring computers, Internet Access and training to public libraries in low-income communities in the United States and Canada; more than $477 million to community projects in the Pacific Northwest; and more than $488 million to special projects and annual giving campaigns.

Gates was married on Jan. 1, 1994, to Melinda French Gates. They have three children. Gates is an avid reader, and enjoys playing golf and bridge.

Ray apata na yeye gari lake...........

Friday, November 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)






hii ndio gari anayoitumia msanii Ray katika shughuli za kurecord movie zake....nawatakia mafanikio mema

RIYAMA ALLY KUSHUKA NA FILAMU YA DNA

Saturday, November 13, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


MUIGIZAJI bora wa kike kupitia tuzo za Risasi Award 2005/ 2006 Riyama Ally yupo location akirekodi filamu inayokwenda kwa jina la DNA, msanii huyu mahiri katika kuigiza filamu za kusikitisha amekuwa kivutio pale anapocheza katika filamu za uzuni, ameiambia filamucentral kuwa kwa sasa anatarajia kuwashika wapenzi wa filamu hapa nchini.

“Unajua siku hizi watazamaji ni werevu kwa hiyo unapocheza lazima uhakikishe unafikia viwango vya juu ili uendelee kuongeza wapenzi wa filamu zako unazocheza, maana wasanii tupo wengi kwa sasa kwa hiyo ukimpoteza mtazamaji mmoja kumrudisha ni kazi, kazi yoyote nitakayoshiriki lazima nipige msuri wa nguvu”
Alisema mwanadada huyo.
Filamu ya DNA inaandaliwa na kampuni ya Sam Enterprises ya jijini Dar filamu hii ambayo ipo katika hatua za mwisho katika uhariri imeongozwa na Seleman Abass Mkangara na kushirikisha nyota wengine kibao.

Aidha Riyama amesema kuwa vile vile yupo katika maandalizi ya filamu zake mpya mbili ambazo anatarajia kuanza kurekodi wakati wowote kuanzia sasa, Riyama ni muigizaji mtunzi na mtayarishaji pia, filamu alizotayarisha ni pamoja na filamu iliyofanya vinzuri soko ya Mwasu.

source filamucentral

film za maigizo zinalipa kweli kweli...............

Saturday, November 13, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




Katika Kuonyesha kuwa ni wazi kwamba Tasnia ya filamu Tanzania inakua na kwamba ni muhimu kuwekeza katika tasnia hii, Leo tumemkuta Steven Kanumba akiwa na Gari lake ambalo ni mahususi kwa ajili ya Production na masuala yote ya utayarishaji wa filamu zake.

Kanumba katikati ya mwaka huu alifungua rasmi kampuni yake na kuweka ofisi katika mitaa ya sinza, Hii kweli inavutia na inakupa fikra kwamba kama huyu anafanya hivi ni kwa sababu gani? Je ni kwamba wadau wanamkubali na kumuwezesha!!!? BIG UP Kanumba, tunamatumani tutaona wengine mkirasimisha utendaji wenu wa kazi.

liverpool once again................

Sunday, November 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Liverpool continued their recent resurgence as Fernando Torres scored both goals in a 2-0 victory over leaders Chelsea at Anfield.

Ili Kumlinda Obama, Nazi Zaangushwa Toka Kwenye Minazi India

Saturday, November 06, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Ili kumlinda rais wa Marekani Barack Obama anayefanya ziara yake nchini India, serikali ya India imeamua kuangua nazi zote toka kwenye minazi iliyo karibu na majengo ambayo Obama atayatembelea.
Katika kujiandaa kumpokea kwa mara ya kwanza rais wa Marekani, Barack Obama, serikali ya India imeangua nazi zote toka kwenye minazi iliyopo karibu na majengo ambayo Obama atayatembelea mjini Mumbai.

Obama anawasili leo jumamosi nchini India katika hatua yake ya kwanza ya ziara zake katika bara la Asia.

Pamoja na ulinzi mkali kuwekwa kama ilivyotegemewa, maafisa wa serikali ya India wameamua pia kuchukua hatua zaidi kwa kumlinda rais huyo wa Marekani hata kwa hatari zitokenazo na mimea.

Nazi zote toka kwenye minazi yote inayolizunguka jengo la ukumbusho la Gandhi zimeangushwa chini ili kumlinda Obama.

Jengo hilo ni mojawapo ya sehemu tano ambazo Obama atazitembelea mjini Mumbai. Katika sehemu zote hizo hatua sawa za ulinzi zimechukuliwa.

"Kwanini tubahatishe?, tumewaagiza maafisa husika kuziangua nazi zote toka kwenye minazi iliyo karibu na jengo hili", alisema mkurugenzi wa jengo la Mani Bhavan ambalo Mahatma Gandhi aliishi wakati wa kupigania uhuru wa India toka kwa Uingereza.

Wiki iliyopita maafisa wa Marekani walilifanyia uchunguzi jengo la Mani Bhavan pamoja na sehemu zingine ambazo Obama atazitembelea.

Obama atazitembelea pia nchi za Indonesia, South Korea, Japan na China katika ziara yake ya siku 10 barani Asia.

source nifahamishe

Mwanamke wa Iran Aliyefanya Mapenzi Nje ya Ndoa Kuuliwa Leo Kwa Mawe

Wednesday, November 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mahakama ya nchini Iran imeruhusu adhabu ya kifo inayomkabili mama wa watoto wa wawili wa nchini Iran ambaye alikamatwa akifanya mapenzi na mwanaume aliyemuua mume wake.
Pamoja na shinikizo kubwa toka nchi za Magharibi na taasisi za kutetea haki za binadamu, Sakineh Mohammadi-Ashtiani huenda akauliwa leo kwa kupigwa mawe kwa mujibu wa vyanzo vya habari.

Mwanaharakati anayemtetea Sakineh alisema kuwa wamepokea taarifa toka kwa mtu anayefanya kazi ndani ya mahakama kuwa Sakineh atauliwa siku ya jumatano.

"Tumepokea taarifa siku tatu zilizopita kuwa Sakineh atauliwa siku ya jumatano", alisema Mina Ahadi, mwanaharakati anayemtetea Sakineh wakati akiongea na shirika la habari la AFP kuhusiana na barua aliyotumiwa na mtu ambaye hakutajwa jina lake.

Mahakama ya mji wa Tabriz ambako Sakineh ametupwa jela imeruhusu adhabu ya kifo inayomkabili Sakineh itekelezwe. Kwa kawaida adhabu za kifo nchini Iran hutekelezwa siku ya jumatano.

Tangu mwezi julai mwaka huu Iran ilikuwa ikisema kuwa adhabu ya kifo kwa kupigwa mawe inayomkabili Sakineh haitafanyika mpaka baada ya kuidhinishwa na mahakama kuu.

Sakine mwenye umri wa miaka 43 ambaye ni mama wa watoto wawili, alihukumiwa adhabu ya kifo na mahakama mbili tofauti mjini Tabriz mwaka 2006.

Adhabu yake ya kwanza ilikuwa ni adhabu ya kifo kwa kunyongwa ambayo baadae ilibadilishwa kuwa kifungo cha miaka 10 jela. Adhabu hiyo ilitokana na Sakineh kutuhumiwa kushiriki kwenye mauaji ya mumewe.

Adhabu ya pili ya kifo ilikuwa ni kuuliwa kwa kupigwa mawe kwa kosa la kufanya mapenzi nje ya ndoa na mwanaume aliyekamatwa kwa mauaji ya mumewe.

source nifahamishe

Makahaba Kuvaa Vizibao Vya Njano Ili Waonekane Vizuri

Thursday, October 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Makahaba wa nchini Hispania wanaowinda wanaume pembeni ya barabara wameanza kuvaa vizibao vya njano vinavyoakisi mwanga ili waweze kuonekana vizuri.
Ili kuepuka faini ya euro 40, makahaba katika mji wa Els Alamus kaskazini mwa Hispania wameanza kufuata masharti ya serikali ya kuvaa vizibao vya njano vinavyoakisi mwanga.

Meya wa mji huo aliamuru makahaba wote wanaosimama pembeni ya barabara kuwinda wanaume wavae vizibao hivyo ili kuwafanya waonekane vizuri na hivyo kuepusha kutokea kwa ajali.

Taarifa ya meya wa mji huo ilisema kuwa baadhi ya makahaba wameanza kuvaa vizibao hivyo baada ya polisi kuanza kuwatoza faini ya euro 40 makahaba wanaosimama pembeni ya barabara kuu kuwinda wateja.

Nchini Hispania kuna jumla ya wanawake laki tatu wanaofanya biashara ya ukahaba. Mwanamke anaruhusiwa kisheria kufanya ukahaba nchini Hispania ingawa kujinufaisha kwa kuwatafutia makahaba wateja ni kinyume cha sheria.

Ni jambo la kawaida katika miji mbalimbali nchini Hispania kuwaona wanawake wanaovaa nguo fupi sana wakiwa wamesimama pembeni ya barabara wakitafuta wanaume.

Utafiti uliofanywa hivi karibuni nchini Hispania ulionyesha kuwa mwanaume mmoja kati ya wanne nchini Hispania ameishawahi kununua penzi toka kwa kahaba.

source nifahamishe

Apata Mimba Sita Nje ya Ndoa, Awaua Watoto na Kuficha Maiti

Thursday, October 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alipata mimba sita nje ya ndoa bila ya mume wake kujua, aliwaua watoto wake na kuzificha maiti zao kwenye sanduku.
Michele Kalina mwenye umri wa miaka 44 mkazi wa Pennsylvania nchini Marekani, alizificha mimba sita alizozipata kwa kufanya mapenzi nje ya ndoa na aliwaua watoto wote waliotokana na mimba hizo na kuzificha maiti zao kwenye masanduku.

Matokeo ya DNA yalionyesha kuwa mifupa ya binadamu iliyokutwa kwenye sandaku lililotiwa kufuli ilikuwa ni mifupa ya watoto watano ambapo wanne kati ya watoto hao walizaliwa wakiwa hai wakati mmoja alizaliwa akiwa tayari ameishafariki.

Kalina na mumewe wa ndoa, Jeffrey walifanikiwa kupata watoto wawili, mmoja wa kike mwenye umri wa miaka 19 na mwingine wa kiume ambaye aifariki dunia mwaka 2003 akiwa na umri wa miaka 13.

Mahakama ilithibitisha kuwa watoto wanne kati ya sita Kalina alizaa na kibuzi chake nje ya ndoa.

Mume wa Kalina na binti yake waligundua mifupa ya watoto wachanga ikiwa imefichwa kwenye maboksi ndani ya sanduku mwezi wa nane mwaka huu ambapo waliripoti polisi na Kalina alitiwa mbaroni.

Mume wa Kalina aliwaambia polisi kuwa ni mara moja tu alihisi mke wake alikuwa mjamzito lakini hakuwa na uhakika.

Mwanaume aliyekuwa akijiiba na Kalina ambaye jina lake liliwekwa kapuni, aliwaambia polisi kuwa Kalina alimwambia kuwa alikuwa na uvimbe tumboni uliolifanya tumbo lake liwe kubwa na uvimbe huo ulikuwa ukimtokea mara kwa mara.

Mwanaume huyo naye alisisitiza kuwa hakugundua kama Kalina alikuwa mjamzito.

Kalina ametupwa jela akikabiliwa na makosa ya mauaji na kuficha maiti za watoto wake.

Kesi ya Kalina itaanza kusikilizwa wiki hii.

source nifahamishe

Mamba Aiangusha Ndege Kongo, 20 Wafariki

Sunday, October 24, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Watu 20 wamepoteza maisha yao nchini Kongo baada ya ndege waliyokuwamo kuanguka toka angani baada ya mamba aliyeingizwa kinyemela ndani ya ndege hiyo kuchoropoka na kuleta kizazaa kikubwa ndani ya ndege.
Abiria aliyetaka kumsafirisha mamba wake kinyemela kwa kumficha mamba huyo ndani ya begi na kuingia nalo ndani ya ndege amesababisha vifo vya watu 20.

Ni mtu mmoja tu kati ya watu 21 waliokuwemo ndani ya ndege huyo ndiye aliyenusurika maisha yake.

Kwa mujibu wa abiria huyo aliyeponea chupu chupu kupoteza maisha yake, mamba huyo aliyekuwa amefichwa ndani ya begi na kuingizwa kinyemela ndani ya ndege nchini Kongo alisababisha mtafaruku mkubwa ndani ya ndege na kupelekea ndege kuanguka.

Mamba huyo alichoropoka toka kwenye begi wakati ndege ndogo ya abiria iliyotengenezwa nchini Czech aina ya Let 410 ilipokuwa angani ikitoka mji wa Kinshasa kuelekea Bandundu.

Ilikuwa ni patashika nguo kuchanika wakati mamba huyo alipoanza kuranda randa ndani ya ndege na kupelekea abiria waviache viti vyao kusalimisha maisha yao.

Wahudumu wa ndani ya ndege walikimbilia ndani ya chumba cha marubani na kufuatiwa na baadhi ya abiria ambao nao waliamua kuitumia nafasi hiyo kusalimisha maisha yao.

Inasemekana kuwa ndege hiyo ilianguka toka angani kutokana na uzito ndani ya ndege kuelemea upande mmoja.

Ndege hiyo iliangukia kwenye nyumba iliyopo maili chache toka kwenye uwanja wa ndege ambao ndege hiyo ilipanga kutua.

Mamba aliyesababisha ajali hiyo alitoka salama salimini toka kwenye mabaki ya ndege hiyo lakini aliuliwa kwa kuchomwachomwa na kisu na watu waliojitokeza kuwaokoa majeruhi wa ajali hiyo.

source nifahamishe

Ruhsa Kumpiga Mkeo Lakini Usimtoe Alama

Thursday, October 21, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mahakama ya sheria za kiislamu katika falme za kiarabu UAE imeamuru kuwa ni ruhsa mwanaume kumpiga mkewe na watoto wake ili mradi hatasababisha alama za vipigo kwenye miili yao.
Hatua hiyo ya mahakama hiyo inawapa haki za kisheria wanaume kuwaadhibu wake zao na watoto wao iwapo wataenda kinyume na matakwa yao.

Hukumu hiyo ilitolewa na mmoja wa majaji wakuu wa UAE, Falah al Hajeri, ambaye alikuwa akitoa hukumu ya mwanaume aliyepigwa faini sawa na Tsh. 160,000 kwa kumpiga kibao mkewe na kumpiga teke binti yake.

Mwanaume huyo alipatikana na hatia ya kumpiga mkewe kwa nguvu sana kiasi cha kusababisha apasuke mdomo wake na kuvunjika jino lake.

Mwanaume huyo pia alimpiga mateke binti yake mwenye umri wa miaka 23 kiasi cha kupelekea apate michuko na uvimbe kwenye mguu na mkono wake.

Mwanaume huyo ambaye jina lake liliwekwa kapuni, awali alidai alimpiga mkewe na mtoto wake kwa bahati mbaya lakini alipopatikana na hatia alikata rufaa akisema kuwa hata kama alimpiga mkewe na mtoto wake kwa makusudi, anayo haki kwa mujibu wa sheria za kiislamu kutumia nguvu dhidi yao iwapo njia zingine za kuwaadabisha zitakuwa zimefeli.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo, jaji Falah al Hajeri alisema: “Ingawa sheria zinaruhusu waume kuwapiga wake zao, lakini pia wanatakiwa wasivuke mipaka na kusawasababisha alama au makovu wake zao”.

“Kama mume atakiuka misingi ya sheria ya kumuadhibu mke au mtoto wake, basi lazima ahukumiwe kwa mujibu wa sheria”, alisema jaji Hajeri.

Jaji Hajeri alielezea kuwa njia rahisi ya kuangalia kama waume wavunja sheria ya kuwaadhibu wake zao ni kwa kuangalia alama za vipigo kwenye miili ya wake zao.

source nifahamishe

Kaka Yake Obama Aoa Mwanafunzi Aliyemtorosha Kwao

Sunday, October 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kaka wa kufikia wa rais wa Marekani, Barack Obama anayeishi nchini Kenya, Malik Obama mwenye umri wa miaka 52 ameongeza mke wa tatu ambaye ni mwanafunzi wa sekondari mwenye umri wa miaka 19 aliyeacha shule na kukimbia kwao.
Kaka wa kufikia wa rais wa Marekani, Barack Obama anayeishi nchini Kenya, Malik Obama ambaye ana wake wawili ameongeza mke wa tatu ambaye ni mwanafunzi wa sekondari aliyekimbia masomo yake.

Mama wa msichana huyo mwenye umri wa miaka 52, alielezea hasira zake baada ya binti yake kuacha masomo ili aolewe na Malik ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 52.

Akiongea na televisheni ya NTV ya Kenya, mama wa msichana huyo anayeitwa Mary Aoko Ouma alisema kuwa binti yake awali alijaribu kufunga ndoa na Malik miaka miwili iliyopita lakini hakumruhusu.

Akiongea na televisheni ya NTV bila ya kujua kuwa anarekodiwa, Malik alithibitisha kufunga ndoa na msichana huyo ingawa hakusema ni lini harusi yao ilifanyika.

Sheria za Kenya zinaruhusu mtu kuoa mke zaidi ya mmoja iwapo vigezo vya kidini au kitamaduni vitatumika.

source nifahamishe

Babu Nyota wa Video za Ngono

Saturday, October 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Babu mwenye umri wa miaka 76 wa nchini Japan alikuwa akitoka nyumbani kwake kila siku asubuhi akiwa ameuramba suti akiaga anaenda kazini lakini siri yake imegundulika kuwa babu huyo alikuwa akitoka nyumbani kwake asubuhi ili kwenda kushiriki video za ngono.
baada ya kustaafu kazi yake ya uwakala wa kampuni ya utalii, babu Shigeo Tokuda, mwenye umri wa miaka 76 alikuwa akiiaga familia yake aubuhi kuwa anaenda kazini.

Familia yake haikuwa ikijua babu Tokuda alikuwa akienda wapi na alikuwa akifanya kazi gani mpaka hivi karibuni ilipogundulika kuwa babu Tokuda ndiye mwanaume mzee kuliko wote nchini Japan anayeshiriki kwenye video za ngono.

Tokuda aligundulika kuwa ni nyota wa video za ngono baada ya binti yake mwenye umri wa miaka 35 kusoma jarida ambalo lilikuwa likimuelezea babu Tokuda kama mfalme wa filamu za kiutu uzima.

Baada ya kuona familia yake imegundua kazi yake mpya anayoifanya, Tokuda aliamua kuweka wazi kwa kutoboa siri zote.

Tokuda alisema kuwa alipokuwa na umri wa miaka 60, alikutana na mtengenezaji wa filamu za ngono wakati akiwa dukani akinunua DVD ya ngono. Huo ndio ukawa mwanzo wa yeye kujiingiza kwenye filamu za ngono.

Hadi sasa Tokuda ameishashiriki jumla ya filamu 350 za ngono na amekuwa akilipwa kiasi cha dola 500 kila siku.

Tokuda ambaye ana mjukuu mmoja alisema kuwa mkewe ameiridhia kazi yake mpya ingawa binti yake alishtushwa sana alipogundua kuwa yeye ni nyota wa video za ngono.


source nifahamishe

Bikira Kuwa Sharti la Kuingia Shule za Sekondari

Friday, October 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Wasichana waliopoteza bikira zao hawatapata nafasi za kujiunga na shule za sekondari za serikali nchini Indonesia iwapo muswada mpya wa sheria wa kuzuia vijana kuanza uzinzi mapema utapitishwa na bunge la nchi hiyo.
Muswada wa sheria umefikishwa bungeni nchini Indonesia ukitaka wasichana waliopoteza bikira zao wasiruhusiwe kujiunga na shule za sekondari nchini humo.

Muswada huo wa sheria umetolewa na mbunge wa jimbo la Jambi nchini humo Babang Bayu Suseno ambaye ameeleza kuwa muswada huo ukipitishwa kuwa sheria utasaidia kuzuia vijana kuanza uzinzi mapema.

Suseno alisema kuwa upatikanaji wa video na picha za ngono na ufahamu mdogo wa masuala ya dini umepelekea vijana kujihusisha na matendo ya ngono mapema.

Mbunge huyo ametaka wanafunzi wa kike wafanyiwe uchunguzi kuthibitisha bikira zao kabla ya kuruhusiwa kuingia shule za sekondari za serikali.

Hata hivyo muswada huo umekumbwa na upinzani mkubwa toka kwa wanasiasa na taasisi za kutetea haki za binadamu.

Imeelezwa kuwa kuwalazimisha wasichana kupima bikira zao itakuwa ni kuwabagua na ni kinyume cha haki za binadamu.

"Njia ya kuzuia uzinzi kwa vijana ni kwa kuwapa elimu ya masuala ya jinsia", alisema Seto Mulyadi, mkuu wa kitengo cha taifa cha kuwalinda watoto na kuongeza "Sio wasichana wote wanaoshiriki kwenye masuala ya ngono wanafanya hivyo kwa kupenda".

"Weka somo maalumu shuleni la kuwafundisha wanafunzi jinsi ya kujilinda lakini sio kuwapima bikira", aliongeza Mulyadi.

Indonesia ni nchi yenye waislamu wengi kuliko wote duniani wapatao milioni 210. Wengi wao wana msimamo wa kati lakini wale wenye msimamo mkali wanahofia kuwa maendeleo ya kasi yanayoambatana na vijana kuiga umagharibi yanapelekea kupungua kwa msimamo wa kidini nchini humo.

Ili muswada huo upitishwe inabidi upewe sapoti ya gavana wa jimbo la Jambi pamoja na waziri wa masuala ya wanawake, lakini viongozi hao wawili ndio waliokuwa wa mwanzo kuupinga muswada huo.

source nifahamishe

Ajiua Baada ya Video Akilawitiwa Kuwekwa Online

Friday, October 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi wa kiume wa nchini Marekani ambaye marafiki zake walirekodi kwa siri video wakati akiingiliwa kinyume cha maumbile na mwanaume mwenzie na kisha kuiweka video hiyo kwenye internet amejiua kwa kujirusha toka kwenye daraja.
Tyler Clementi, Mwanafunzi wa kiume wa mwaka wa kwanza wa chuo kikuu cha Rutgers University cha nchini Marekani mwenye umri wa miaka 18 ambaye alikuwa akifanya ushoga kwa siri, amejiua mwenyewe kwa kujirusha toka kwenye daraja baada ya video yake akiingiliwa kinyume cha maumbile na mwanaume mwingine kurushwa LIVE kwenye internet.

Clementi alijirusha wiki iliyopita toka kwenye daraja la George Washington na kuangukia kwenye mto mkubwa wa Hudson River, last week, maiti yake ilipatikana juzi kwenye mto huo.

Clementi alichukua uamuzi wa kujiua baada ya kugundua marafiki zake aliokuwa akikaa nao chumba kimoja walimrekodi kwa siri wakati akifanya mapenzi na mwanaume mwingine na VIDEO za tukio hilo zilirushwa LIVE kwenye internet kupitia Webcam.

"Kama angekuwa kitandani na mwanamke, haya yote yasingetokea", alisema mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho.

"Kama asingeanikwa LIVE kwenye internet, mambo yake ya ndani yasingeanikwa na leo tungekuwa naye hapa", aliongeza mwanafunzi huyo.

Wanafunzi wawili mmoja wa kiume Dhraun Ravi na mwingine wa kike Molly Wei, ambao wote wana umri wa miaka 18, wamefunguliwa mashtaka ya kuvunja haki za msingi za Clementi.

Mahakama iliambiwa kuwa webcam ilitumika kurusha LIVE tukio la Clementi akiingiliwa na mwanaume mwingine mnamo septemba 19 na Ravi alijaribu kulirusha LIVE tena tukio la pili lililofanyika septemba 21 ambayo ni siku moja kabla ya Clementi kujiua.

Taasisi za kutetea haki za mashoga zimeichachamalia kesi hii zikitaka Ravi na mwenzake wahukumiwe adhabu kali.

Taasisi hizo zimesema kuwa Ravi na mwenzake wameonyesha chuki waliyo nayo kwa mashoga na wasagaji na wameitaka mahakama itoe adhabu kali.

Ravi na mwenzake huenda wakahukumiwa kwenda jela miaka mitano iwapo watapatikana na hatia ya kuingilia undani wa mtu bila ya ridhaa yake.

source nfahamishe

Kahaba Ajitamba Kula Uroda na Beckham

Wednesday, September 29, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kahaba Irma Nici ameendelea kujitamba kuwa alikula uroda na mcheza soka maarufu wa Uingereza, David Beckham ingawa Beckham anajiandaa kufungua kesi ya madai ya fidia kiasi cha dola milioni 16.
Pamoja na kwamba wanasheria wa mcheza soka maarufu wa Uingereza, David Beckham anayesakata kabumbu nchini Marekani wako kwenye jitihada za kufungua kesi mahakamani kumdai fidia ya dola milioni 16, kahaba anayedai kutembea na Beckham ameibuka na kutamba ana ushahidi wa kuthibitisha madai yake.

Kahaba Irma Nici mwenye asili ya Bosnia amedai kuwa anaweza kuithibitishia mahakama kuwa alilala na nyota huyo wa soka mjini London na mjini New York mnamo mwaka 2007.

Nici amedai kuwa Beckham ana alama za kipekee kwenye sehemu zake nyeti hivyo ajiandae kuvua suruali yake mahakamani ili kuzithibitisha alama hizo.

Nici mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akiwakwepa wanasheria wa Beckham na amekuwa akijificha kwenye hoteli mjini New York.

Beckham mwenye umri wa miaka 35 anamshtaki Nici kutokana na habari iliyotoka kwenye jarida moja la Marekani kuwa Beckham alinunua penzi la kahaba Nici.

Nici aliliambia jarida hilo kuwa alishea kitanda kimoja na Beckham wakati Beckham alipofanya mapenzi yaliyowahusisha wanawake wawili kwa mpigo. Mwanamke wa pili aliyezungumziwa katika habari hiyo bado hajajulikana.

Beckham anamshtaki Nici na jarida hilo kwa kuandika habari za kumpakazia kuwa aliisaliti ndoa yake na Victoria Beckham, 36,

Beckham pia anamshtaki Nici na jarida hilo kwa habari ambayo imemfanya Beckham aonekane aliyatia maisha ya mkewe hatarini kwa kutembea na kahaba.

source nifahamishe

Sita Mbaroni Kwa Kuichoma Moto Quran Uingereza

Friday, September 24, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Polisi wa nchini Uingereza wamewatia mbaroni watu sita kwa kueneza chuki katika jamii kwa kuweka VIDEO kwenye YouTube wakionyesha jinsi wanavyoichoma moto Quran na kuipiga mateke.
Polisi wa nchini Uingereza wametoa taarifa wakisema kuwa wamewatia mbaroni watu 6 ambao waliweka video kwenye YouTube wakionyesha jinsi walivyoichoma moto misahafu na kuipiga mateke.

Taarifa ya polisi ilisema kuwa watu wawili walitiwa mbaroni septemba 15 na wengine wanne walitiwa mbaroni juzi jumatano. Wote wako nje kwa dhamana huku uchunguzi ukiendelea.

"Walikamatwa kufuatia tukio la kuchoma moto misahafu miwili katika kitongoji cha Gateshead siku ya septemba 11", alisema msemaji wa polisi.

"Tukio hilo lilirekodiwa na baadae kuwekwa kwenye internet", iliendelea kusema taarifa ya polisi.

Video hiyo ya YouTube iliwaonyesha wanaume walioficha sura zao kwa vitambaa wakipiga kelele za "Septemba 11, siku ya kimataifa ya kuichoma moto Quran" wakitukana na pia wakiimba "Hii ni kwaajili ya vijana wetu waliopo Afghanistan".

Wanaume hao walichukua mafuta ya petroli na kuyamwaga kwenye misahafu miwili na kuichoma moto misahafu hiyo.

Waliendelea kuimba na kupiga kelele wakati misahafu hiyo ikiendelea kuungua kabla ya kuanza kuipiga mateke.

Polisi kwa kushirikiana na uongozi wa kitongoji hicho ulitoa taarifa ya pamoja wakilaani kitendo hicho na kusema kuwa vitendo vilivyoonyeshwa kwenye video hiyo haviwakilishi mawazo ya jamii.

"Jamii yetu imeundwa kwa heshima kwa watu wote na tunaendelea kushirikiana na viongozi wa jumuiya, wakazi na watu wa imani zote ili kudumisha ushirikiano uliopo", ilisema taarifa hiyo.

Kutiwa mbaroni kwa wanaume hao kumekuja zikiwa hazijapita wiki mbili tangu mchngaji wa nchini Marekani, mchungaji Terry Jones alipoahirisha mpango wake wa kuichoma moto misahafu 200 katika kuadhimisha siku ya kuwakumbuka wahanga wa shambulizi la septemba 11, 2001.

source nifahamishe

Madaktari Wauza Figo za Watu 109

Saturday, September 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Madaktari watano wa nchini Afrika Kusini wamepandishwa kizimbani kwa kuuza figo za watu 109 katika kipindi cha miaka miwili.
Madaktari watano wa hospitali binafsi kubwa ya nchini Afrika Kusini wamepandishwa kizimbani kwa kuwauzia figo za watu 109 matajiri wa Israel.

Madaktari hao walifanya biashara haramu ya viungo vya binadamu kwa kununua kwa bei rahisi figo za watu maskini toka Israel, Romania na Brazil.

Madaktari hao katika kipindi cha kati ya mwaka 2001 na 2003 walizininua figo 109 na kufanya operesheni kinyume cha sheria kuwapandikiza matajiri wa Israel.

Miongoni mwa waliopandishwa kizimbani ni mkuu wa mtandao wa hospitali kubwa binafsi nchini Afrika Kusini wa Netcare bwana Richard Friedland, lilisema gazeti la The Star.

"Raia wa Israel wanaohitaji figo, waliletwa nchini Afrika Kusini kwaajili ya kupandikizwa figo za watu wengine kwenye hospitali ya St. Augustine iliyopo mjini Durban".

"Mwanzoni walikuwa wakinunua figo toka kwa raia wa Israel lakini baadae waliamua kununua figo za raia wa Brazili na Romania kwakuwa figo zao zilikuwa zikiuzwa kwa bei chee".

Figo ya raia wa Israel ilikuwa ikinunuliwa kwa dola 20,000 wakati figo za Wabrazili na Waromania zilikuwa zikinunuliwa kwa dola 6,000 tu, ilisema taarifa ya mwendesha mashtaka.

source nifahamishe

Wajukuu wa Osama Bin Laden Wafariki

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamama aliyekuwa amejitolea kupandikizwa mimba ya watoto mapacha wa mtoto wa kiongozi wa Al-Qaeda, Osama Bin Laden, amewapoteza watoto hao baada ya mimba yake kuharibika kufuatia kichapo alichopewa mtaani na wanaume wawili ambao hawajajulikana.
Mtoto wa Osama Bina Laden, Omar Bin Laden mwenye umri wa miaka 29 ambaye amemuoa mwanamke wa Kiingereza ambaye alikuwa hana uwezo wa kupata mimba kutokana na umri wake, alimkodisha mwanamke toka mji wa Bristol nchini Uingereza abebe mimba yake.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 anayejulikana kwa jina la Louise Pollard alipoteza mimba hiyo ya watoto wawili mapacha baada ya kushambuliwa na watu wawili wasiojulikana wakati akielekea nyumbani kwake toka kwenye mgahawa mmoja nchini Syria.

Louise ambaye zamani alikuwa akicheza dansi za utupu kwenye klabu za starehe nchni Uingereza, alienda hospitali ambako aliambiwa kuwa watoto wote wawili walioko tumboni mwake wamefariki.

Louise alisema kuwa hajajua sababu ya wanaume hao kumshambulia ingawa alisema kuwa watu wengi wanamfahamu kama mwanamke aliyebeba mimba ya wajukuu wa mkuu wa Al Qaeda, Osama bin Laden.

Mke wa mtoto wa Osama, Zaina mwenye umri wa miaka 54, ambaye awali alikuwa akijulikana kama Jane Felix-Browne alisema kuwa Omar amekumbwa na upungufu wa akili hivyo wameamua kuachana.

Omar na Zaina walipanga kumlipa paundi 10,000 mwanamke huyo baada ya kujifungua watoto hao mapacha.

source nifahamishe

Mtoto Akutwa Kwenye Choo Cha Ndege

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto mchanga wa kiume amekutwa akiwa hai kwenye pipa la taka la kwenye choo cha ndege iliyowasili nchini Philippines ikitokea Bahrain.
Kwa mujibu taarifa zilizotolewa punde baada ndege ya shirika la ndege la Gulf Air kutua mjini Manila, Philippines ikitokea Bahrain, wafanya usafi waliingia kwenye ndege hiyo baada ya abiria wote kushuka na ndipo walipokumbana na tukio wasilolitegemea baada ya kumkuta mtoto mchanga aliyezaliwa muda mfupi uliopita akiwa kwenye pipa la taka la chooni.

Mtoto huyo mchanga wa kiume alikuwa amezungushiwa makaratasi ya chooni akiwa bado hajasafishwa damu toka kwenye mwili wake huku kipande kikubwa cha utambi wa kitovu kiking'inia.

Madaktari waliitwa na kumchunguza mtoto huyo na kutoa taarifa mtoto huyo bado yuko hai na mwenye afya njema.

Mtoto huyo alipewa jina kwa kutumia herufi mbili za GF zinazowakilisha Gulf Air pia herufi hizo ziliwakilisha jina jingine alilopewa la George Francis.

Mtoto huyo wa kiume alisafishwa kwa kutumia maziwa na manesi wa uwanja wa ndege mjini Manila.

Polisi wanafanya uchunguzi kumtafuta mama wa mtoto huyo ambaye aliwashangaza watu kwa jinsi alivyoweza kujifungua mwenyewe ndani ya ndege bila ya kushtukiwa na mtu yeyote.

Kwa mujibu wa polisi wa Manila, mama huyo akipatikana atafunguliwa mashtaka mahakamani.


source nifahamishe

Amtukana Obama, Afungiwa Maisha Kwenda Marekani

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kijana wa Kiingereza ambaye alimtumia rais wa Marekani email ya vitisho na kashfa amefungiwa maisha kuingia Marekani.
Luke Angel alifuatiliwa na polisi wa Marekani na Uingereza baada ya kumtumia email ya vitisho na kashfa rais wa Marekani, Barack Obama na kumfananisha rais huyo wa taifa kubwa duniani na sehemu za siri za kike.

FBI waliichunguza email ya Luke na kisha kuwajulisha polisi wa Uingereza ambao waliendaaa nyumbani kwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 17 anayekaa Silsoe, Bedfordshire.

Luke, ambaye ni mwanafunzi wa sekondari, ameingia kwenye orodha ya watu waliopigwa marufuku kukanyaga ardhi ya Marekani maishani.

Luke aliliambia gazeti moja la Bedfordshire kuwa aliamua kumtumia Obama email hiyo ya kashfa baada ya kuangalia kipindi kwenye luninga kilichokuwa kikizungumzia shambulizi la kigaidi la septemba 11,2001.

"Polisi walikuja nyumbani kwetu na kunipiga picha na kuniambia kuwa nimepigwa marufuku kuingia Marekani", alisema Luke.

"Sijali kupigwa marufuku kuingia Marekani ingawa wazazi wangu hawajafurahia", aliongeza Luke.

Polisi hawana mpango wa kumfikisha mahakamani kijana huyo.

source nifahamishe

Aichana Quran na Biblia na Kuzivutia Sigara Kurasa Zake

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Mwanasheria mmoja wa nchini Australia amezua balaa jingine baada ya kuzichana kurasa za kwenye msahafu na biblia na kuzitumia kurasa hizo kuvutia sigara.
Siku chache baada ya mchungaji wa Marekani kuzua mtafaruku duniani baada ya kutishia kuichoma moto Quran, mwanasheria mmoja wa nchini Australia amezua mtafaruku mwingine kwa kuzichana kurasa za kwenye msahafu na kwenye biblia na kisha kuzitumia kurasa hizo kuvutia sigara.

Mwanasheria huyo aliyejulikana kwa jina la Alex Stewart, aliandaa video ya dakika 12 ambayo aliiweka kwenye YouTube akiwa ameshikilia msahafu na biblia kabla ya kunyofoa kurasa kwenye vitabu hivyo vitakatifu na kuzitumia kuvutia sigara.

Stewart ambaye hana dini alisema katika video hiyo "Hivi ni vitabu tu kama vitabu vingine".

Video yake ilifutwa kwenye YouTube muda mfupi baada ya kuwekwa baada ya watu kuanza kuilaani video hiyo.

Stewart ambaye anafanya kazi kwenye chuo kikuu cha Queensland University of Technology amesimamishwa kazi kwa muda na chuo hicho ambacho kimesema kuwa kimesikitishwa sana na kitendo chake.

"Chuo kikuu kimesikitishwa sana na hakijafurahia kitendo kama hiki kutokea", alisema makamu mkuu wa chuo hicho Peter Coaldrake.

Kitendo cha Stewart kimefuatia tukio la mchungaji Terry Jones wa Florida, Marekani kutishia kuchoma moto misahafu 200 siku ya septemba 11.

Aliahirisha azma yake hiyo kutokana na vitisho toka kwa waislamu na shinikizo kubwa toka kwa serikali ya Marekani.

Hata hivyo wachungaji wawili wa jimbo la Tennessee nchini Marekani, mchungaji Bob Old na msaidizi wake Danny Allen waliichoma moto Quran na kitabu chenye maandishi ya "Muhammad" kwenye ukurasa wake wa mbele.

Mjini Washington, mwanaume mmoja aliichana Quran mbele ya jengo la ikulu ya Marekani na kukiweka kipande cha ukurasa alichokinyofoa kwenye mfuko wa plastiki.

Tukio hilo lilishuhudiwa na watalii waliokuwa maeneo hayo pamoja na polisi wanaolinda usalama eneo hilo ambao hawakuchukua hatua yoyote ili kuepuka kuingilia haki za watu za uhuru wa kujieleza.

source nifahamishe

Aamua Kumuoa Dada Yake

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume wa nchini Ireland ambaye alimpachika mimba dada yake na kuzaa naye mtoto kabla ya kugundua kuwa ni ndugu yake, anafunga ndoa na dada yake huyo mwishoni mwa mwezi huu.
James na Maura, ambao ni kaka na dada ambao wamezaa mtoto mmoja, wanategemea kuvalishana pingu za maisha mwishoni mwa mwezi huu.

Ndugu hao ambao wameamua kubadilisha majina yao halisi ili wasijulikane na jamii, waliangukia kwenye penzi zito bila ya kutambua kuwa wamezaliwa kutokana na baba mmoja.

"Itakuwa ni harusi ndogo, tuna mashahidi wawili tu ambao tunawafahamu vizuri na wanaelewa hali tuliyo nayo", alisema James

"Hatujui kama baba yetu atakuja kwenye harusi au kama mama zetu watahudhuria harusi yetu".

"Mtoto wetu wa kiume anasubiria kwa hamu harusi yetu na anaelewa kinachoendelea, hatujali kuoana mtu na dada yake", aliongeza James.

James na Maura walizaliwa kutokana na baba mmoja na walikuwa wakiishi miji miwili tofauti iliyo mbali kwa kilomita 160.

James na Maura ambao hivi sasa wana umri kati ya miaka 20-28, Walikutana miaka michache iliyopita kwenye ukumbi wa starehe katika mji mwingine wa tatu na kuangukia kwenye penzi zito na walipata mtoto wa kiume miaka miwili baadae.

Waligundua kuwa ni ndugu mwaka jana wakati wa krismasi wakati mama yake James alipomuambia James kuwa baba yake wa kweli siyo mwanaume aliyemlea miaka yote.

Mwezi wa nne mwaka huu walithibitisha kuwa ni mtu na dada yake baada ya vipimo vya DNA kuthibitisha kufanana kwa DNA zao.

James na Maura walielezea jinsi wanavyoisubiria kwa hamu harusi yao pamoja na kwamba wanajua kuwa sheria za nchi haziwaruhusu kufunga ndoa.

Kutokana na kwamba kitambulisho cha James kinaonyesha jina la baba yake kuwa ni Vincent ambalo ni jina la mwanaume aliyemlea, kipingamizi cha kisheria cha kuzuia ndoa yao kinakuwa kimeepukika kwani majina ya baba kwenye vitambulisho vyao yatakuwa tofauti.


source nifahamishe

11 mbaroni sakata la vifo vya watoto Luxury Pub

Wednesday, September 15, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

KUFUATIA ripoti maalum iloyoundwa kuchunguza sababu iliyopelekea kutokea kwa vifo vya watoto na kubainika ni uzembe ulisababisha vifo hivyo, watu 11 wanashikiliwa na polisi.
Ripoti hiyo imeonyesha kuwa uzembe mkubwa ulifanyika katika ukumbi huo na kusababisha vifo hivyo.

Akitoa ripoti hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bi. Chiku Galawa alisema, ripoti hiyo imeonesha kuwa uzembe uliofanyika katika ukumbi huo ni kuwa na idadi kubwa ya watu ndani ya ukumbi huo kuliko uwezo wa ukumbi.

Pia mmiliki wa ukumbi huo imegundulika hakuwa na kibali cha kuendesha biashara hiyo ya disco hivyo alikuwa akienda kinyume na sheria za nchi, na aliendesha dico hilo toto hadi majira ya saa 1:50 usiku na kuonekena kukiuka utaratibu uliowekwa.

"Watoto ni haki yao kufurahia sikukuu, lakini mmiliki wa ukumbi huo alikiuka maadili ya watoto, kwanza aliwalundika watoto ukumbini kupit kiasi, pili alipitisha muda maalum" alsiema mkuu huyo

Mmiliki wa ukumbi huo alitambulika kwa jina la Damas Nyingo alikuwa ni mmoja kti ya watu 11 waliokamatwa na majina mengine hayakuekwa bayana hadi upelelezi ukamilike.

Watoto wawili waliweza kupoteza maisha sikukuu ya Idd Pili, katika ukumbi wa Luxury Pub uliopo Temeke, katika makutano ya mtaa wa Madenge na Liwale baada ya umeme kukatika ghafla na kusababisha watoto kukimbia hovyo mlangoni na kukanyagana.

Watoto waliopoteza maisha ktika tukio hilo ni Lilian Sango (8) na Amina Ramadhani (7), wote wakazi wa Temeke na wengine zaidi ya kumi na moja kujeruhiwa.

source nifahamishe

Britney Spears Ashtakiwa Kwa Kumtesa Kingono Mlinzi Wake

Sunday, September 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mlinzi wa zamani wa nyota wa muziki wa Pop wa Marekani, Britney Spears amefungua kesi mahakamani akimshtaki nyota huyo wa muziki kwa kumnyanyasa kijinsia kwa kutembea uchi mbele yake na kufanya mapenzi na mpenzi wake mbele yake.
Mlinzi wa zamani wa nyota wa muziki wa Pop wa Marekani, Britney Spears, Fernando Flores amefungua kesi mahakamani akimtuhumu nyota huyo wa muziki kwa kumnyanyasa kijinsia.

Flores amedai kuwa nyota huyo wa muziki alikuwa akitembea uchi mara kwa mara mbele yake na wakati mwingine alikuwa akifanya mapenzi na mpenzi wake mbele yake.

Mlinzi huyo alisema katika hati alizowasilisha mahakamani mjini Los Angeles kwamba Britney Spears alijaribu mara kwa mara kumvuta kimapenzi na wakati mwingine alimvuta chumbani kwake na kujianika uchi mbele yake.

Mlinzi huyo alisema kuwa kitendo cha Britney Spears kugombana na mumewe wa zamani mbele ya watoto wao kilikuwa kikiumiza hisia zake.

Mlinzi huyo ambaye alifanya kazi kama mlinzi wa Britney Spears kuanzia mwezi february hadi julai mwaka huu, aliilalamikia pia kampuni yake ya ulinzi kwa kutoyatilia mkazo malalamiko yake aliyokuwa akiyapeleka kuhusiana na unyanyasaji wa kijinsia wa Britney Spears.

Wakili wa Britney Spears alikataa kusema chochote kuhusiana na kesi hiyo.

source nifahamishe

'Yesu Alikuwa ni Muathirika wa Ukimwi'

Monday, September 06, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mchungaji wa kanisa moja nchini Afrika Kusini amezua zengwe kubwa nchini humo baada ya kudai kuwa Yesu alikuwa muathirika wa virusi vya HIV.
Mchungaji Xola Skosana wa kanisa la Way of Life Church la mjini Capetown, amesababisha mjadala mkubwa nchini humo baada ya kudai kuwa Yesu alikuwa muathirika wa virusi vya HIV vinavyosababisha ukimwi.

Mchungaji Skosana alisema kuwa aliamua kusema hivyo ili kuyafanya makanisa ya Afrika Kusini yaache kukaa kimya linapozungumziwa suala la kuongezeka kwa idadi ya waathirika wa ukimwi.

"Nikiwa kama mchungaji, nina jukumu la kuwajulisha watu juu ya Mungu ambaye huwajali watu na kuwatakia mema, sio ambaye huwadharau na kuwahukumu", alisema mchungaji huyo.

"Wanasema huwezi kumhusisha Yesu na Ukimwi", alisema mchungaji Skosana.

"Lakini Katika sehemu nyingi za Biblia, Yesu anajiweka kama mgonjwa na mtu wa hali ya chini, tukiwatembelea watu ambao ni wagonjwa tunakuwa tumemtembelea yeye, tukiwapuuza wagonjwa tunakuwa tumempuuza yeye", alisema mchungaji Skosana.

Mwezi uliopita, Skosana ambaye alipoteza ndugu zake wawili wa kike kutokana na ukimwi, alijipima ukimwi hadharani mbele ya wafuasi wake, wafuasi wake 100 nao walimuunga mkono na kuamua kujipima ukimwi hadharani.

Hatua yake hiyo ilipongezwa na taasisi za kupambambana na ukimwi nchini Afrika Kusini.

Hata hivyo kauli yake hii imepelekea wakristo nchini Afrika Kusini kumtuhumu kuwa analichafua jina la Yesu.

Mchungaji Skosana, ameyataka makanisa nchini Afrika Kusini kuacha ukimya wao na kuanza kuwausia waumini wao juu ya ugonjwa wa ukimwi.

Kanisa katoliki nchini humo limejiweka mbali na mijadala ya ugonjwa wa ukimwi huku likiendelea kupinga matumizi ya kondomu.

Takribani watu 1,000 wanafariki kila siku kutokana na ukimwi nchini Afrika Kusini.

source nifahamishe