Ajaribu Kumtorosha Mfungwa Kwa Kutumia Begi

Tuesday, July 05, 2011 / Posted by ishak / comments (0)




Mfungwa Juan Ramirez Tijerina akiwa amejificha ndani ya begi akijaribu kutoroka jela Tuesday, July 05, 2011 6:54 PM
Mwanamke mmoja wa nchini Mexico ameingia matatani baada ya jaribio lake la kumtorosha mumewe toka jela kwa kumdumbukiza ndani ya begi na kisha kujaribu kulikokota begi hilo kutokana nalo nje ya jela.
Maafisa jela katika jela ya Chetumal nchini Mexico jana walipigwa na bumbuwazi baada ya kumkamata mwanamke akijaribu kumtorosha mumewe toka jela kwa kumficha ndani ya begi.

Walinzi wa jela hiyo walimuona Maria del Mar Arjona mwenye umri wa miaka 19, akionekana mwenye wasiwasi wakati akitoka nje ya jela huku akilikokota begi ambalo lilionekana limetuna sana.

Walipomsimamisha na kulichunguza begi hilo hawakuamini macho yao walipomuona mfungwa Juan Ramirez Tijerina akiwa amejikunja kama vile mtoto akiwa tumboni mwa mama yake.

Maria aliingia na begi hilo jela wakati alipopewa nafasi ya kumtembelea Juan ambaye anatumikia kifungo chake ndani ya jela hiyo.

Juan alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 20 jela baada ya kutupwa jela mwaka 2007 alipopatikana na hatia ya kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Maria alitiwa mbaroni wakati akisubiri kufikishwa mahakamani.



source nifahamishe

SEMINA YA VITAMBULISHO KWA WAWAKILSHI

Sunday, July 03, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili na Vitambulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana,(kulia) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Sei Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili na Vitambulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana,(kulia) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Sei Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya utambuzi na usajili wa Vitambulisho vya Taifa, Dickson Maina,akizungumza akitoa taarifa kuhusiana na mamlaka ya vitambulisho wakati wa ufunguzi wa Semina kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi iliyofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein
Baadhi ya watendaji wa Mamlaka ya utambuzi na usajili wa vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakisikiliza kwa makini hotuba iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili wa Vitmbulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein akitoa hotuba yake katika ufunguzi wa Semina ya wajumbe hao inayohusu usajili wa vitambulisho vya Taifa,iliyoandaliwa na Mamlaka ya Utambuzi na Usajili vitambulisho vya Taifa,(NIDA) katika ukumbi wa Ocean View Hoteli Kilimani Zanzibar


source othman mapara blog