Waziri Amla Uroda Malkia, Kuhukumiwa Adhabu ya Kifo

Thursday, August 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Waziri wa Sheria na rafiki wa karibu wa Mfalme Mswati wa Swaziland ametupwa jela na anakabiliwa na adhabu ya kifo baada ya kumla uroda mmoja wa wake wa mfalme Mswati.
Chini ya amri ya mfalme Mswati, waziri wa sheria na rafiki wa karibu wa Mfalme Mswati, Ndumiso Mamba ametupwa jela baada ya kukamatwa kitandani hotelini akimla uroda malkia wake, Nothando Dube, ambaye ni mke wa 12 wa mfalme huyo wa Swaziland.

Malkia Nothando Dube mwenye umri wa miaka 22 amewekwa ya chini ulinzi mkali nyumbani kwa mama mkwe wake huku waziri huyo mkware akiendelea kunyea debe jela.

Waziri Mamba alikamatwa na polisi kitandani akijivinjari na malkia wake kwenye hoteli ya Royal Villas mjini Mbabane.

Wadadisi wa masuala ya kisiasa nchini Swaziland walidai kwamba uhusiano wa kimapenzi kati ya malkia na waziri huyo ulikuwa ukijulikana sana kilichobaki watu walikuwa wakisubiri ushahidi.

Mamba huenda akahukumiwa adhabu ya kifo iwapo atapatikana na hatia.

Mfalme Mswati yuko nchini Taiwan kwa ziara ya kiserikali.

Dube ambaye amezaa watoto wawili na mfalme Mswati aliolewa na Mfalme Mswati akiwa na umri wa miaka 16 baada ya kuonekana kwenye dansi maalumu la kila mwaka la wasichana bikira ambapo wasichana hupita wakiwa wameacha matiti yao nje huku mfalme akijichagulia yupi amuongeze kwenye himaya zake.

Dube huenda akafukuzwa toka kwenye himaya za kifalme iwapo atapatikana na hatia.

source nifahamishe

Aacha Ualimu na kuwa Msanii wa Ngono

Thursday, August 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwalimu mmoja nchini Uingereza ameacha kazi yake ya ualimu wa sekondari na kuamua kuanza kazi mpya ya usanii wa filamu za ngono huku akitumiwa salamu za kutakiwa mafanikio na wanafunzi wake walioziona filamu zake kwenye internet.
Liselle Bailey mwenye umri wa miaka 30 aliacha kazi yake ya ualimu wa sekondari na kuanza kazi mpya kucheza na kuongoza filamu za ngono.

Wanafunzi wa mwalimu huyo waliobahatika kuona filamu zake kwenye internet walipigwa na butwaa lakini hawakusita kumtumia salamu za kumtakia mafanikio kwenye kazi yake hiyo mpya.

Mmoja wa wanafunzi wake aliyeitwa Daniel aliandika "Mwalimu Bailey tunakupenda, nakutakia mafanikio kwenye kazi yako mpya".

Mwanafunzi mwingine aliandika maoni kwenye internet "Mwalimu bora wa kiingereza, umepata kazi bora kuliko zote, hongera".

Mwalimu Bailey alikuwa akifundisha somo la kiingereza na somo la maigizo kwenye shule ya seminari ya Grindon Hall.

"Huu ulikuwa ni uamuzi wangu wa busara", alisema Bailey na kuongeza kuwa katika mwaka mmoja wa fani yake hiyo mpya ameweza kuwa nyota wa kampuni ya Joybear Pictures.


source nifahamishe

Nyota wa Hip Hop Kugombea Urais

Thursday, August 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamuziki maarufu duniani wa muziki wa Hip Hop, wa kundi la Fugees, Wycleaf Jean amejitosa kwenye siasa na atagombea urais wa Haiti katika uchaguzi utakaofanyika novemba.
Baada ya kutesa kwa muda mrefu katika anga ya muziki wa hip hop na miondoko reggae, nyota wa kundi la Fugees la Marekani, Wycleaf Jean ameamua kujitosa kwenye masuala ya siasa na atakuwa miongoni mwa wagombea urais.

Wycleaf ambaye alizaliwa nchini Haiti amesema kuwa atatangaza rasmi kugombea wa urais wa Haiti kesho alhamisi kupitia televisheni ya CNN kwenye kipindi cha Larry King Live.

Uchaguzi wa Haiti utafanyika novemba 28 mwaka huu na rais wa sasa wa Haiti, Rene Preval, hataweza kugombea tena urais kutokana na kumaliza miongo yake kisheria.

Ili aweze aweze kugombea urais Wycleaf anakabiliwa na changamoto ya kuthibitisha kuwa ameishi nchini Haiti kwa miaka mitano na hana uraia wa nchi nyingine yoyote.

Wycleaf alizaliwa nje kidogo ya mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince, lakini alilelewa Brooklyn, New York nchini Marekani.

Wycleaf ana historia ndefu ya kujihusisha na masuala ya kisiasa nchini Haiti na alikuwa miongoni mwa watu walioshiriki kuandaa tamasha la kusaidia wahanga wa tetemeko kubwa la ardhi lililotokea mwezi januari mwaka huu na kuua maelfu ya watu.

source nifahamishe

'Naogopa Kufariki Nisaidieni'

Tuesday, August 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke wa nchini Iran ambaye kutokana na kufanya zinaa alihukumiwa kupigwa mawe hadi atakapofariki, amesema kuwa anaogopa kufariki na anaomba awakumbatie watoto wake kwa mara ya mwisho.
"Kila siku kabla ya kulala huwa nafikiria nani ndio angekuwa wa kwanza kunirushia mawe", alisema Sakineh Mohammadi Ashtiani mwenye umri wa miaka 43 ambaye ni mama wa watoto wawili.

Hivi karibuni adhabu ya kuuliwa kwa kupigwa mawe ya Sakineh ilibadilishwa na kuwa adhabu ya kuuliwa kwa kunyongwa baada ya mashirika ya kutetea haki za binadamu kuishinikiza serikali ya Iran kumwachia huru mwanamke huyo.

Katika ujumbe wake alioutuma kwa watu toka jela aliyofungwa mjini Tabriz, Sakineh aliwashukuru watu waliofanya kampeni ya kutaka aachiwe huru lakini alisema kuwa anaogopa kufariki.

"Siku niliyohukumiwa kuuliwa ni siku ambayo naiona kama nilidondokea kwenye shimo refu lenye giza, nimepoteza fahamu zangu, siku nyingine kabla ya kulala huwa nafikiria nani angekuwa wa kwanza kunipiga mawe na kwa sababu ipi?, Nawaambieni nyote, Naogopa kufariki naomba nisaidieni, naomba niwakumbatie watoto wangu kwa mara ya mwisho", alisema Sakineh.

Sakineh aliendelea kusema kuwa alivunjika sana moyo siku ambayo alicharazwa bakora 99 mbele ya mtoto wake Sajad mwenye umri wa miaka 17.

Sakineh alipatikana na hatia ya kufanya mapenzi nje ya ndoa yake mwaka 2006 na alihukumiwa kuuliwa kwa kupigwa mawe lakini kutokana na kampeni za mashirika ya kutetea haki za binadamu hatimaye serikali ya Iran hivi karibuni iliibadilisha adhabu hiyo na sasa Sakineh atauliwa kwa kunyongwa.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu bado yanaendeleza kampeni za kutaka Sakineh aachiwe huru lakini serikali ya Iran imekuwa ikisisitiza kuwa adhabu iliyotolewa itatekelezwa kama inavyotakiwa.

source nifahamishe

Mwizi ajifanya mzigo ili akombe fedha

Tuesday, August 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu

Sunday, August 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Thomas Beatie ambaye mwaka 2008 alikuwa gumzo duniani akitambulika kama mwanaume wa kwanza duniani kupata ujauzito anatarajiwa kujifungua mtoto wa tatu muda wowote kuanzia sasa.
Mwanamke aliyebadilisha jinsia na kuwa mwanaume na kisha kutambulika kama mwanaume wa kwanza duniani kupata ujauzito, anatarajiwa kujifungua mtoto wa tatu.

Thomas Beatie, alijifungua mtoto wake wa kwanza aliyepewa jina la Susan mwezi juni mwaka 2008 na mwaka mmoja baadae alijifungua mtoto mwingine aliyepewa jina la Austin.

"Ameishatimiza muda wake wa kujifungua na ameipita siku aliyotarajiwa kujifungua", alisema mdau mmoja wa karibu na familia hiyo.

Thomas alizaliwa kama mwanamke akijulikana kwa jina la Tracy lakini mwaka 2002 alianza kutumia madawa ya homoni kubadilisha jinsia yake kuwa mwanaume lakini hakufanya operesheni ya kuzibadilisha sehemu zake za siri.

Umbile lake lilibadilika na kufanana na mwanaume huku akifuga madevu ili aonekane kama mwanaume kweli.

Alibadilisha kisheria jinsia yake kuwa mwanaume na jina lake alilibadili kuwa Thomas badala ya Tracy.

Mwaka 2003 alifunga ndoa na mwanamke aliyeitwa Nancy ambaye alikuwa ni mama wa watoto wawili aliyepewa talaka na mumewe.

Baada ya kugundua kuwa Nancy hawezi kupata ujauzito tena kutokana na umri wake, Thomas aliamua kushika ujauzito kwa njia ya upandikizaji ili familia yake iweze kupata mtoto.

Huo ndio ulikuwa mwanzo wa Thomas kujulikana duniani kama mwanaume mjamzito. Alipata mtoto wa kwanza mwaka 2008 na sasa anatarajia kupata mtoto wa tatu.


source nifahamishe

Mama Asiyetaka Watoto Aua Watoto Wake 8 na Kuwafukia

Sunday, August 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja wa nchini Ufaransa ambaye baada ya kujifungua watoto wawili alikuwa hataki tena kupata watoto wengine, hakutaka kutumia kinga wakati wa kujamiiana na alipopata ujauzito aliwaua watoto wake wanane aliowazaa bila ya mumewe kujua.
Mwanamama Dominique Cottrez mwenye umri wa miaka 47 wa mji wa Lille nchini Ufaransa amekuwa gumzo nchini humo baada ya kukiri kuwaua watoto wake wanane aliowazaa bila ya mumewe kugundua.

Dominique anashikiliwa na polisi huku uchunguzi ukiendelea wakati mumewe ameachiwa huru.

Dominique aliwaambia polisi kuwa hakutaka kupata watoto wengine baada ya kuzaa watoto wawili kwa tabu kutokana na unene aliokuwa nao lakini pia hakutaka kutumia kinga wala kuomba ushauri wa madaktari kujizuia kupata ujauzito tena.

Dominique alisema kuwa alipopata ujauzito alikuwa akifanya siri bila ya mumewe kujua na alipojifungua aliviua vichanga vyake na kuvifunga kwenye plastiki kabla ya kuvifukia chini ya ardhi.

Dominique aliwaambia wapelelezi kuwa wakati wa ujauzito alitumia muda mwingi peke yake na alikuwa akijizalisha mwenyewe bila ya msaada wa mtu yoyote.

Vichanga vinane alivyoviua vilizaliwa kati ya mwaka 1987 na 2007.

Ukatili wa Dominique uligundulika baada ya wapangaji kuhamia kwenye nyumba aliyokuwa akiishi awali ambapo maiti za vichanga viwili ziligunduliwa chini ya ardhi kwenye bustani ya nyumba hiyo.

Maiti zingine sita ziligunduliwa kwenye gereji ya nyumba aliyokuwa akiishi na mumewe.

Taarifa zinasema kuwa Dominique na mumewe ni watu waliokuwa wakijulikana na kuheshimika sana kwenye kijiji chao cha Villers-au-Tertre.

Dominique alikuwa akifanya kazi kama nesi wakati mumewe alikuwa akifanya kazi za ujenzi.

Wanakiji na watu wanaomjua Dominique na mumewe wameelezea kupigwa na butwaa na habari hizi kwakuwa Dominique na mumewe walikuwa ni watu wanaopenda kusaidia watu na kujishughulisha katika shughuli mbalimbali za jamii.

Watoto wawili wa mwanzo wa Dominique ambao hivi sasa wana umri wa miaka 21 na 22, nao wameelezea kusikitishwa na habari hizi wakisema kuwa hawajui ni nini kilichomsibu mama yao mpaka akaamua kufanya ukatili huo.

source nifahamishe

Mapozi ya Bwana na Bi Harusi Yamuua Mpiga Picha

Sunday, August 01, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mpiga picha kwenye harusi nchini Sicily amefariki dunia kwa kupigwa risasi alipowapa bunduki bwana na bi harusi waweke pozi ili awapige picha ya ukumbusho.
Mpiga picha Calogero Scimea mwenye umri wa miaka 45 aliwapa bunduki bwana na bi harusi ili waweke pozi na bunduki hizo ili awapige picha ya ukumbusho.

Scimea alikuwa akipiga picha za harusi ya wapenzi wa tangia utotoni Valentina Anitra, 22, na Ignazio Licodia, 25, wakati alipowaambia watumie bunduki za kuwindia wanyama kuweka pozi.

Mojawapo ya risasi katika bunduki hizo ilifyatuka na kumuua mpiga picha mbele ya bwana na bi harusi pamoja na wazazi wao.

Ajali hiyo ilitokea muda mfupi kabla ya maharusi kwenda kanisani.

Taarifa zilisema mpiga picha huyo alifika kwenye harusi hiyo kuchukua nafasi ya rafiki yake ambaye alishindwa kufika kwenye harusi hiyo kutokana na ugonjwa.

Bunduki zilizotumika wakati wa tukio zilikuwa na vibali halali.

Polisi wanaendelea na uchunguzi.

source nifahamishe