Mtanzania auwawa........

Friday, June 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Takribani mwezi mmoja uliopita kulikuwa na tangazo kwenye blogs na hapa JF kwamba kuna dada yetu mmoja alipotea na akawa anatafutwa na ndugu zake.

Taarifa iliyotolewa kwenye local TV stations za Southern California zinasema kwamba mwili wa huyo dada ulipatikana jana nyuma ya nyumba aliyokuwa akiishi. Ulikuwa umefungwa kwenye mifuko ya plastic na blanket kama takataka.

Mume wa marehemu anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo. Dada huyo alikuja kwa ajili ya kusomea kozi ya Uuguzi na alikuwa anasoma ili awe Registered Nurse. Ameacha watoto 2.

Lilian Mgonjwa alihojiwa na kituo cha TV kutoka makazi yake huko Long Beach. Kama kutakuwa na taarifa za ziada ninatumaini tutaendelea kujulishana

Amzalisha Binti Yake Watoto 7

Friday, June 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Mvuvi wa nchini Brazili ambaye alikuwa akimbaka mtoto wake kwa miaka 16 na kupelekea kuzaa naye watoto 7 ametiwa mbaroni.
Mvuvi toka maeneo ya watu masikini ya Maranhao nchini Brazili ambaye alikuwa akimwingilia kinguvu binti yake kwa miaka 16 ametiwa mbaroni.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Brazili la Estado, polisi walimtia mbaroni Jose Agostinho Bispo Perreira mwenye umri wa miaka 54 baada ya kupewa taarifa na mtu asiyejulikana juu ya mchezo wa mzee huo kula mayai yake mwenyewe.

Taarifa zinasema kuwa Perreira alianza mchezo wa kumuingilia binti yake tangia alipokuwa na umri wa miaka 12.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Perreira alimfungia binti yake huyo kwenye kibanda kilichopo mbali na mji aliokuwa akiishi.

Polisi waliokuwa wakimfanyia uchunguzi Perreira wamegundua kuwa hivi sasa binti yake ana umri wa miaka 28, hajui kusoma wala kuandika na amezaa watoto saba na Perreira.

Mtoto mdogo kuliko wote ana umri wa miezi miwili wakati waliobakia wana umri wa miaka 4, 5, 7, 8 na 12.

Polisi wanasema kuwa Perreira alikuwa akiwagawa kwa familia zingine watoto aliozaa na binti.

Taarifa ya polisi ilisema kuwa mvuvi Perreira alianza kuishi na binti yake baada ya ndoa yake na mkewe kuvunjika.

Perreira alizaa watoto wanne na mkewe huyo. Watoto wake wawili wa kiume na mmoja wa kike walienda kuishi na mama yao mji mwingine.

Hawakuwa na taarifa kuwa baba yao alikuwa akimuingilia kwa nguvu mdogo wao na alizaa naye watoto saba.

source nifahamishe

Bakora 90 na Jela Miezi 4 Kwa Kubusiana Hadharani

Friday, June 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Mahakama nchini Saudi Arabia imemhukumu mwanaume aliyembusu mwanamke hadharani kucharazwa bakora 90 na kwenda jela miezi minne.
Mahakama mjini Riyadh, Saudi Arabia imemhukumu mwanaume aliyembusu mwanamke kwenye shopping mall kwenda jela miezi minne.

Mahakama pia imeamuru mwanaume huyo acharazwe bakora 90 kwa kitendo chake hicho.

Kwa mujibu wa gazeti la kila siku la serikali la Al-Yom, polisi wa kidini wa Saudia walimtia mbaroni mwanaume huyo pamoja na wanawake wawili baada ya kuwaona wakifanya vitendo nje ya maadili mbele ya watu wengine.

Mwanaume huyo ambaye umri wake ni kwenye miaka ya 20, alionekana akiwa amekaa na mwanamke mmoja wakibusiana na kukumbatiana. Haikuelezewa mwanamke wa pili alikuwa akifanya nini wakati huo.

Majina ya wanawake hao na mwanaume huyo hayakutajwa.

Kwa mujibu wa sheria za kiislamu nchini Saudia, ni kosa mwanaume na mwanamke ambao hawana uhusiano wowote (hawajaoana) kuongozana barabarani achilia mbali kukaa pamoja na kuanza kubusiana.

Gazeti la Al-Yom liliripoti kuwa mwanaume huyo atacharazwa bakora 90 kwa mafungu matatu na pia amepigwa marufuku kuingia kwenye shopping mall yoyote nchini humo kwa miaka miwili.

Wanawake aliokamatwa nao watasomewa mashtaka yao katika mahakama nyingine.


source nifahamishe

Mwanamke Kusalisha Sala ya Ijumaa Uingereza Leo

Friday, June 11, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Kwa mara ya kwanza nchini Uingereza sala ya ijumaa ya waislamu itaongozwa na mwanamke anayepigania usawa wa kijinsia katika dini ya kiislamu.
Mwandishi wa habari wa Kanada, Raheel Raza mwenye umri wa miaka 60 atakuwa mwanamke wa kwanza nchini Uingereza kusalisha sala ya ijumaa.

Raheel ambaye alizaliwa muislamu, amekuwa akipigania usawa wa kijinsia katika dini ya kiislamu.

Raheel amealikwa mjini Oxford nchini Uingereza kusalisha sala ya ijumaa katika jumuiya inayoongozwa na kiongozi wa kituo cha waislamu mjini Oxford, Taj Hargey.

Kwa mujibu wa gazeti la Independent, Taj Hargey anadai kuwa yeye ni Imamu anayepigania sala zenye mchanganyiko wa jinsia na pia anapigania wanawake kuwa maimamu.

Raheel ambaye ni mkazi wa mji wa Toronto nchini Kanada, yeye anapigania usawa wa jinsia katika uislamu na anataka wanawake wapewe nafasi za uimamu na uongozi wa misikiti.

Miaka mitano iliyopita, Raheel alitumiwa vitisho vya kuuliwa baada ya kutoa khutba ya sala ya ijumaa ambayo wanawake na wanaume walichanganyika pamoja. Sala hiyo ilifanyika kwenye mojawapo ya vituo vya taasisi yake.

Raheel atakuwa mwanamke wa pili duniani kusalisha sala ya ijumaa lakini pia atakuwa mwanamke wa kwanza muislamu wa kuzaliwa kusalisha sala ya ijumaa.

Mwaka 2008, mwanamke wa kikristo wa Marekani aliyebadili dini kuwa muislamu na kujiita Amina Wadud aliongoza sala ya ijumaa nchini humo. Hata hivyo sala yake ilihudhuriwa na watu pungufu ya 40 kutokana na maandamano ya kumpinga yaliyofanywa na wanawake wa kiislamu.

Taj Hargey amedai kuwa sala ya leo ya ijumaa itakayoongozwa na mwanamama Raheel itahudhuriwa na watu zaidi ya 100 ambapo kama kawaida wanawake na wanaume watachanganyika na kuasali bega kwa bega.

source nifahamishe

Radi Yawatenganisha Kabla Hawajachumbiana

Thursday, June 10, 2010 / Posted by ishak / comments (1)


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani alipanga kumfanyia suprise na kumvalisha pete ya uchumba mpenzi wake juu ya mlima lakini wakiwa nusu ya safari walipigwa na radi na mpenzi wake alifariki hapo hapo.
Richard Butler, 31, wa Knoxville, Tennessee nchini Marekani alimchukua mpenzi wake Bethany Lott na kumpeleka kwenye mlima wa Max Patch Bald uliopo North Carolina.

Richard anasema kuwa alitaka mpenzi wake huyo ambaye ana umri wa miaka 25 afikirie wapo kwenye tripu ya kupanda mlima wakati lengo lake kuu lilikuwa ni kumpigia goti kuomba akubali kuolewa naye na kumvalisha pete ya uchumba ambayo aliificha kwenye mfuko wake wa suruali.

Mvua kubwa zilizoanza kunyesha ghafla hazikuwazuia wapenzi hao kuendelea na safari yao, lakini hali ya hewa ilizidi kuwa mbaya na miungurumo ya radi ilianza kusikika.

Radi tatu zilipiga eneo walilokuwepo na mojawapo ya radi hizo iliwatandika wapenzi hao na kuwarusha mita kadhaa chini.

"Umeiona hiyo?", alisema Richard ambaye wakati huo hakujitambua kuwa ameungua robo tatu ya mwili wake.

Mpenzi wake hakujibu kitu hali iliyomfanya Richard awahi sehemu aliyodondokea kujua kulikoni.

Richard alijaribu kumpa huduma ya kwanza mpenzi wake ambaye alizimia baada ya kupigwa na radi.

Madaktari waliowasili eneo la tukio, walijaribu kila njia kumzindua Bethany kwa muda wa lisaa limoja kabla ya kumpa taarifa Richard kuwa Bethany amefariki.

source nifahamishe

aliyeingia uwanjani apata dhamana

Thursday, June 10, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


SHABIKI namba moja nchini Tanzania wa mchezaji wa timu ya Brazil, Ricardo Kaka, ameachiwa huru kwa kupata dhamana ya jeshi la polisi na suala lake litashughulikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu [TFF
Naggar Ali Kombo alishikiliwa na jeshi la polisi kwa takribani siku tatu kufuatia kitendo cha kuingia uwanjani katika mechi kati ya Brazil na Tanzania iliyofanyika Jumatatu ya wiki hii katika Uwanja mpya wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema, Naggar wamemuachia huru kwa kupata dhamana ya jeshi hilo na dhamana nyingine kutoka kwa baba yake mzazi aliyetambulika kwa jina la Ali Kombo.

Kova alisema baba yake mzazi alijitokeza kumpa dhamana mtoto wake huyo na pia mzazi huyo alimpongeza mwanae huyo kwa kuonesha upenzi wake dhidi ya mchezaji huyo ambaye alikuwa akimpenda kutoka moyoni.

Kova alisema wameamua kumpa dhamana kijana huyo na kuliachia mwenendo mzima wa shauri hilo washughulikie TFF kutokana na kosa lenyewe.

Hivyo Nagaar yuko nje kwa dhamana na TFF limeachiwa kushughulikia mwenendo mzima wa sakata hilo kutokana na kosa lenyewe liko kimichezo zaidi.

Wabunge kupimwa Saratani

Thursday, June 10, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

NAIBU Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda alisema, wanajipanga kuwafanyia vipimo ya saratani wabunge kabla ya kumalizika kwa mkutano huo Julai 16, mwaka huu.


Hatua hiyo imekuja kwa kutaka kuonyesha mfano kwa wananchi wajitokeze kuangalia afaya zao kwa kuwa ugonjwa huo umekuwa ni hatari na kumaliza wananchi walio wengi.

Dk. Kigoda amesema serikali imeandaa mkakati wa kukabiliana na ongezeko la ugonjwa wa saratani nchini kwa kuwa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa ifikapo 2020, theluthi moja ya vifo vyote vitasababishwa na saratani duniani, na zaidi vifo hivyo vitatokea katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.

Amesema hii inatakiwa iwe mfano kwa kuwa wananchi wengi zaidi ya asilimia 80 wamekuwa wakienda hospitalini wakati saratani imewashawatafuna na inakuwa ngumu kutibika.

Amesema saratani ni ugonjwa unaouwa wananchi walio wengi nchini na inaua kuliko ugonjwa wa ukimwi mbao wengi wameonekana kuuogopa kuliko hata saratani ambayo ni hatari zaidi.

source nifahamishe

Baada ya Ajali Mtoto wa Miaka 3 Awa Chapombe na Mvutaji Sigara

Thursday, June 10, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Baada ya kujeruhiwa kwenye ajali ya gari, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu nchini China amekuwa mvutaji sigara na mlevi.
Baada ya kugongwa na gari mwaka jana, mtoto Ya Wen wa nchini China amegeuka kuwa mvutaji sigara sugu na mlevi.

Ajali hiyo imebadilisha kabisa maisha ya Wen kwani siku hizi anapenda kuvaa nguo za kiume na hulia sana wazazi wake wanapokataa kumnunulia nguo za kiume anazozitaka.

Wazazi wake ambao hufanya kazi ya kukusanya taka na kuziuza ili kupata pesa za kujikimu, siku hizi wanalazimika kuzibana bajeti zao ili waweze kumnunulia ulabu na sigara binti yao.

Wen aligongwa na lori mwaka jana, aliwahishwa hospitali ambako alilazwa wiki moja akipatiwa matibabu. Aliruhusiwa kurudi nyumbani lakini alitumia miezi kadhaa kurudia hali yake ya zamani.

Wiki moja baada ya kuruhusiwa kurudi nyumbani toka hospitali, Wen alikutwa na mama yake akiwa amejificha anavuta sigara.

Haukupita muda Wen alianza kuiba sigara za baba yake na pia toka kwenye maduka madogo madogo ya jirani.

Mama yake Wen aliyetajwa kwa jina la Gao, alisema kuwa binti yake amekuwa mvutaji sigara aliyekubuhu na pia amekuwa mlevi.

"Chupa tatu za bia sio tatizo kwake", alisema mama huyo.


source nifahamishe

Tanzania vs Brazil 1-5

Tuesday, June 08, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




wamejitahidi ila ndio ivyo mambo ya mpira,maximo amemaliza kibarua anaingia kocha mpya kutoka Denmark.haya sasa tumsubiri na huyu atafanyeje

byeeeeeeee

Mwalimu Arekodi Video Akimlawiti Mwanafunzi Wake

Monday, June 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Sunday, June 06, 2010 1:53 AM
Mwalimu mmoja wa kiume wa nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela miaka 17 baada ya kurekodi video akimlawiti mwanafunzi wake wa kiume mwenye umri wa miaka 15.
Aliyekuwa mwalimu wa wa shule msingi ya Cedar Lee Middle School ya Virginia, Marekani, Scott Christopher Howe amehukumiwa kwenda jela miaka 17.5 baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mwanafunzi wake wa kiume na pia kurekodi video akifanya kitendo hicho.

Scott mwenye umri wa miaka 34 alirekodi jumla ya video 22 akimlawiti mwanafunzi wake ambaye alikuwa na umri wa miaka 15.

Baadhi ya video hizo zilirekodiwa ndani ya mabafu na madarasa ya shuleni kwake.

Video 9 zilipatikana kwenye laptop ya Scott wakati video zingine 13 zilipatikana kwenye external hard drive.

Polisi walimkamata Scott baada ya kuitwa nyumbani kwake na mwenye nyumba wake ambaye alidai Scott analima bangi ndani ya nyumba yake.

Wakati polisi wakisaka mimea ya bangi ndani ya nyumba yake, waligundua kompyuta yenye kamera iliyoelekezwa kitandani. Walipodadisi vilivyomo kwenye kompyuta hiyo ndipo walipokutana na video za Scott akimlawiti mwanafunzi wake.

Mwanafunzi huyo aliwaambia polisi kuwa alikuwa akifahamu kwamba Scott hurekodi video anapomuingilia kinyume cha maumbile.

Polisi pia waligundua mimea 15 ya bangi ndani ya chumba cha Scott.

Akisomewa hukumu yake jana Scott alihukumiwa kwenda jela miaka 17.5 ingawa upande wa mashtaka ulitaka mahakama itoe adhabu kubwa zaidi.

source nifahamishe

Mke wa Rais Zuma Ala Uroda na Mlinzi Wake

Monday, June 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Familia ya mke wa pili wa rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma imelazimika kumlipa Zuma fidia ya mbuzi mmoja mweupe baada ya kugundulika kuwa mke huyo wa rais Zuma aliisaliti ndoa yake na kula uroda na mlinzi wake. Utata upo kwenye ujauzito alio nao hivi sasa mke huyo wa rais.
Imegundulika kuwa mke wa pili wa rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Nompumelelo Ntuli alifukuzwa toka nyumbani kwa Zuma siku chache kabla ya krismasi baada ya kugundulika alimsaliti Zuma na kutembea nje ya ndoa.

Ntuli alimpa uroda mlinzi wake, Phinda Thomo mkazi wa Dobsonville, Soweto. Mlinzi huyo alijiua mwenyewe baada ya siri kufichuka kuwa ametembea na mke wa rais.

Ntuli ambaye hivi sasa yuko pamoja na Zuma katika safari ya kiserikali nchini India, ana mimba ya mtoto anayetarajiwa kuwa mtoto wa 21 wa Zuma. Hata hivyo maswali mengi yamezuka kuhusiana na ukweli wa baba wa mtoto huyo aliye tumboni mwake.

Taarifa zinasema kuwa Ntuli mwenye umri wa miaka 35 aliamua kufanya hivyo baada ya kukasirishwa na hatua ya Zuma kutangaza kuoa mke wa tatu.

Taarifa zaidi zinasema kwamba Ntuli alimtukana mke wa tatu wa Zuma Tobeka Madiba na pia alitishia kutohudhuria harusi yake iliyofanyika mwezi januari mwaka huu, hata hivyo alibadilisha uamuzi wake na kuhudhuria harusi hiyo lakini alifukuzwa na kurudishwa kwao wakati wa sherehe za kitamaduni za harusi hiyo.

Ntuli alisindikizwa na wazee wa kijadi hadi kwenye nyumba ya familia yake ambapo alikabidhiwa kwa wazazi wake.

Ntuli aliambiwa kuwa kitendo chake cha kuisaliti ndoa yake kimeikasirisha familia ya Zuma na mizimu ya mababu.

Ili kuweka mambo sawa mwezi aprili mwaka huu, familia ya Ntuli ilienda kwa mzee Zuma na kumlipa fidia ya mbuzi mmoja mweupe ambaye alichinjwa siku hiyo hiyo.

Habari za Ntuli kumsaliti Zuma zimeigawanya Afrika Kusini ambapo watu wengi wanampongeza Ntuli wakisema kuwa kama Zuma anazisaliti ndoa zake kwanini wake zake nao wasimsaliti.

Mmoja wa watu waliopiga simu redioni kujadili suala hilo alisema kuwa Zuma ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 68 hayawezi tena mambo ndio maana mke wake ametembea nje.

source nifahamishe