Jogoo Mwenye Hasira Amuua Mmiliki Wake

Tuesday, January 25, 2011 / Posted by ishak / comments (0)


Jogoo mwenye hasira amelipa kisasi kwa kumuua mmiliki wake aliyekuwa akimlazimisha aingie ulingoni kupigana na jogoo mwenzake katika kamari ya kupiganisha kuku nchini India.
Jogoo huyo kwa kutumia viwembe vilivyokuwa vimefungwa kwenye miguu yake wakati wa kupiganishwa na jogoo mwingine, alimrukia mmiliki wake na kulirarua koromeo lake na kupelekea kifo chake hapo hapo.

Taarifa zilisema kuwa jogoo huyo alimuua mmiliki wake aliyetambulika kwa jina la Singrai Soren ambaye alikuwa akimlazimisha jogoo huyo arudi tena ulingoni kupambana na jogoo mwingine baada ya kushinda pambano lake la kwanza.

Taarifa zaidi zilisema kuwa kwa kawaida jogoo hupumzishwa kwa zaidi ya lisaa limoja kabla ya kupambanishwa na jogoo mwingine.

Lakini Soren kwa tamaa ya kujiingizia pesa nyingi kila jogoo wake anaposhinda alimlazimisha jogoo huyo arudi tena ulingoni ndani ya dakika chache na ndipo jogoo huyo alipomaliza hasira zake kwa kulirarua koromeo lake.

Katika kamari hiyo ya kupiganisha kuku, mmiliki wa kuku anayeshinda hupewa zawadi ya pesa sawa na TSh. 60,000/= pamoja na kupewa kuku aliyeuliwa kwenye pambano hilo kama kitoweo.

Maafisa wa polisi katika kijiji cha Mohanpur, Bengal wameanza msako wa kumtafuta jogoo huyo aliyeshinda mapambano manne hadi sasa ili waweze kumvua viwembe alivyovalishwa kwenye pambano lake la kwanza kabla hajamrarua mtu mwingine.

source nifahamishe

Ajilipua ndani ya Uwanja wa Ndege na Kuua Watu 35

Tuesday, January 25, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Mtu mmoja amejitoa mhanga kwa kujilipua na bomu ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Moscow nchini Urusi na kupelekea vifo vya jumla ya watu 35 na kujeruhiwa kwa watu zaidi ya 100.
Ilikuwa ni hali ya kutisha kwenye uwanja wa ndege mkubwa kuliko yote nchini Urusi wa Domodedovo Airport uliopo kusini mwa mji mkuu wa nchini hiyo Moscow.

Muda mfupi baada ya mtu mmoja kujilipua ndani ya uwanja wa ndege huo kwenye sehemu ya kupokea abiria wanaowasili ilikuwa haijulikani yupi yupo hai au yupi amefariki kutokana na mazingira ya kutisha iliyojitokeza.

Rais wa Urusi Dmitry Medvedev aliitisha kikao cha ghafla ambapo alisema kuwa tukio hilo lililotokea leo jumatatu kuwa ni la kigaidi na kuagiza ulinzi mkali kwenye viwanja vya ndege na stesheni za treni.

"Leo saa kumi na nusu (kwa saa za Urusi), mlipuko umetokea kwenye uwanja wa ndege wa Domodedovo Airport,", ilisema taarifa ya kikosi cha upelelezi cha Urusi.

Maafisa wa Urusi walisema kuwa mlipuko huo ulitokea kwenye eneo la kuchukulia mizigo kwenye sehemu ya kupokea abiria wanaowasili.

Watu 35 wamefariki na wengine 130 wamejeruhiwa katika mlipuko huo ambapo 20 kati yao hali zao ni mbaya sana.

Polisi wa Urusi wameanzisha uchunguzi wa mlipuko huo ambapo taarifa za awali zimeonyesha kuwa kuna mtu alijitoa mhanga kwa kujilipua mwenyewe ndani ya uwanja huo wa ndege.

source nifahamishe

Tamaa ya Umaarufu Yapelekea Aiage Dunia

Sunday, January 23, 2011 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke nyota wa filamu za ngono wa nchini Ujerumani ambaye alijipatia umaarufu mkubwa baada ya kushiriki 'Big Brother Germany' amefariki dunia baada ya operesheni ya sita ya kurekebisha matiti yake ili jina lake liendelee kutamba kwenye vyombo vya habari.
Carolin Berger mwenye umri wa miaka 23 ambaye alijipatia umaarufu mkubwa kutokana na ushiriki wake kwenye mashindano ya "Big Brother Germany", amefariki dunia kutokana na matatizo ya kiafya aliyopata baada ya operesheni ya sita ya kuongeza ukubwa wa matiti yake.

Carolin ambaye awali alikuwa akishiriki kwenye sinema za ngono akijulikana kwa jina la Cora kabla ya kushiriki kwenye mashindano ya Big Brother alitaka jina lake liendelee kutamba kwenye vyombo vya habari.

Carolin alifariki juzi muda mfupi baada ya kumalizika kwa operesheni yake ya sita ya kuongeza ukubwa wa matiti yake.

Carolin aliongeza ukubwa wa matiti yake toka saizi 34F hadi 34G.

Alikumbwa na mashambulio ya moyo mara mbili, presha ilishuka ghafla na ubongo wake ulipata madhara makubwa na mwishoe aliiaga dunia.

Daktari aliyemfanyia operesheni hiyo anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi.


source nifahamishe