Mapenzi! Mapenzi! Aifukua Maiti ya Mkewe na Kulala Nayo

Tuesday, December 01, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanaume mmoja wa nchini Vietnam ambaye alikuwa na huzuni ya kuondokewa na mkewe, alifukua kaburi la mkewe na kuichukua maiti ya mkewe na kuanza kulala nayo kitanda kimoja kwa kipindi cha miaka mitano.
Le Van aligubikwa na huzuni kubwa wakati mkewe alipofariki mwaka 2003 kiasi cha kwamba alianza kulala juu ya kaburi lake katika mji wa Quang Nam uliopo ukanda wa kati wa Vietnam.

Gazeti la Vietnamnet liliripoti kuwa Van aliendelea kulala juu ya kaburi la mkewe usiku kwa kipindi cha miezi 20 mpaka alipoanza kuugua kutokana na hali ya hewa ya baridi.

Ili kujikinga na baridi, Van aliamua kutengeneza handaki lililoenda kwenye jeneza lake na kuanza kulala pembeni ya maiti yake.

Watoto wa Van waliligundua handaki hilo na waliamua kumzuia Van kulitembelea kaburi la mkewe.

Mwezi novemba mwaka 2004, Van alilifukua kaburi la mkewe na kuichukua maiti ya mkewe hadi nyumbani kwake.

Van alitumia udongo mfinyazi kuizunguka mifupa ya maiti ya mkewe na kisha aliivalisha maiti hiyo nguo za kike na kisha kuipaka vipodozi.

Van mwenye umri wa miaka 55, baba wa watoto saba, alianza kulala pembeni ya maiti ya mkewe akiikumbatia kuanzia wakati huo hadi leo.

Picha zinazomuonesha Van akiwa pembeni ya maiti ya mkewe zilichapishwa kwenye gazeti la Vietnamnet, ikiwemo picha moja ambayo iliionyesha mifupa ya mkono wa mkewe ikiwa imezungushiwa udongo.

"Mimi ni mtu ninayependa kufanya vitu tofauti.. mimi si mtu wa kawaida", Van alisikika akiliambia gazeti hilo.


source.nifahamishe.com

Auliwa na Mumewe Akisherehekea Kupewa Talaka

Tuesday, December 01, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mama wa watoto wawili wa nchini Uingereza ameuliwa na mumewe baada ya kuandaa sherehe ya kusherehekea kupewa talaka.
Katrina Jones mwenye umri wa miaka 34 aliuwa na mumewe kwa kuchomwa chomwa na kisu masaa machache kabla ya kuanza kwa sherehe aliyoiandaa kusherehekea kupewa talaka.

Mwili wa Katrina ulikutwa ukiwa katika dimbwi la damu ukiwa na majeraha kibao ya kuchomwa na kisu asubuhi ya siku ya jumamosi masaa machache kabla ya wageni waalikwa kuanza kuwasili kwenye sherehe aliyoiandaa "Divorce Party" kusherehea kuvunjika kwa ndoa yake na mumewe.

Mume wake aliyejulikana kwa jina la Brian Jones mwenye umri wa miaka 63 alikamatwa na kushikiliwa na polisi na baadae kufunguliwa mashtaka ya mauaji.

Majirani zake walisema kuwa ndoa ya miaka 9 ya Katrina na Brian ilivunjika mwezi februari mwaka huu.

Siku ya ijumaa Katrina aliweka mabango kwenye madirisha ya nyumba yake katika kitongoji cha Marske, Middlesbrough akiwaalika watu katika sherehe yake ya kuvunjika kwa ndoa yake.

Lakini aliuliwa na mumewe siku iliyofuatia kabla hata ya kuanza kwa sherehe hiyo.

Majirani walimuelezea Brian kuwa ni mtu mwenye vurugu kiasi cha kuogopwa na majirani zake.

Majirani walisema kuwa Katrina aliamua kuachana na mumewe baada ya mapenzi yake kwa mumewe kuisha kutokana na tabia zake.

"Ilikuwa ni vigumu kwake kukubali kuwa ndoa yake na Katrina imevunjika", alisema mmoja wa majirani zake akielezea sababu iliyopelekea Brian kumuua mkewe.

Katrina alikuwa ni mke wa tatu wa Brian baada ya ndoa zake mbili za mwanzo kuvunjika.


source.nifahamishe.com

Matumaini ya Mkenya Kumuoa Mtoto wa Clinton Yaota Mbawa

Tuesday, December 01, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Chelsea Clinton, mtoto wa rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton amekubali posa ya mpenzi wake wa muda mrefu na hivyo kuyafuta kabisa matumaini ya raia wa Kenya ambaye alituma posa ya kumuoa akiahidi kutoa ng'ombe 20 na mbuzi 40.
Awali Mkenya huyo Godwin Kipkemoi Chepkurgor mwenye umri wa miaka 40 alituma posa ya kumuoa Chelsea Clinton, binti wa rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton mwaka 2000 na aliahidi kutoa ng'ombe 20 na mbuzi 40 kama mahari.

Kipkemoi alikumbushia nia yake ya kumuoa Chelsea, wakati mama yake Chelsea ambaye pia ni waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, alipofanya ziara yake nchini Kenya mwaka huu miezi michache iliyopita.

Hillary alimjibu Kipkemoi kuwa Chelsea ni mtu mzima na ana maamuzi yake lakini atamfikishia ujumbe huo.

Matumaini ya Kipkemoi kumuoa Chelsea yamefutika baada ya Chelsea kukubali kuchumbiwa na mpenzi wake wa muda mrefu Marc Mezvinsky.

Mezvinsky ambaye ni mfanyakazi wa benki ya Goldman Sachs alikuwa rafiki wa karibu wa Chelsea tangia utotoni.

Msemaji wa familia ya Clinton alitoa taarifa wiki hii kuwa Chelsea na Mezvinsky walivalishana pete ya uchumba wiki iliyopita.

Kama Chelsea angekubali kuolewa na Kipkemoi angekuwa mke wa pili wa Kipemoi ambaye alifunga ndoa na mwanamke mwingine raia wa Kenya mwaka 2006 baada ya kusubiria majibu ya posa yake ya kumuoa Chelsea kwa miaka sita.

Kipkemoi alidai kuwa mkewe yuko radhi kushea nyumba moja Chelsea Clinton.

Kwa mujibu wa sheria za Kenya, mwanaume anaruhusiwa kuoa zaidi ya mke mmoja.


source.nifahamishe.com