Wahindi Walalamikia Ukubwa wa Kondomu

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Utafiti uliofanyika nchini India umeonyesha kuwa wanaume wengi nchini India hawafurahishwi na ukubwa wa kondomu unaotambulika duniani kwakuwa kondomu hizo ni kubwa sana kulinganisha na ukubwa wa nyeti zao.
Utafiti huo uliowashirikisha wanaume 1,000 wa nchini India ulionyesha kuwa kondomu zenye ukubwa unaotambulika kimataifa huwapwaya wanaume wengi wa nchini India.

Utafiti huo uliweka wazi kuwa zaidi ya nusu ya wanaume walioshiriki utafiti huo walikuwa na uume ambao ulikuwa ni mfupi kulinganisha na ukubwa wa kondomu.

Utafiti huo uliofanyika kwa miaka miwili uliweka wazi kuwa asilimia 60 ya wanaume nchini India wana uume wenye urefu kati ya sentimeta tatu hadi tano pungufu ya ukubwa wa kondomu unaotambulika duniani.

Matokeo ya utafiti huu yamepelekea makampuni ya kutengeneza kondomu nchini India yatakiwe kutengeneza kondomu zenye ukubwa tofauti tofauti.

Matokeo ya utafiti huu yametiliwa mkazo kwakuwa India ndiyo nchini inayoongoza duniani kwa idadi kubwa ya watu walioathirika na virusi vya Ukimwi.


source nifahamishe

pata flava na diamond......mbagala.....

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Brazili Kupimana Ubavu na Tanzania Juni 7

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Timu ya soka ya Brazili ikiwa na mastaa wake wote watakaoshiriki kombe la dunia nchini Afrika Kusini, itashuka dimbani kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kupimana ubavu na Tanzania.
Mabingwa wa dunia mara tano, Brazili wametua nchini Afrika Kusini tayari kwaajili ya kombe la dunia litakaloanza kutimua vumbi juni 11.

Wazee wa samba Brazili wakiwa na mastaa wao wote watawasili Tanzania juni 5 na mechi yao dhidi ya Tanzania itafanyika juni 7. Bila shaka hiyo itakuwa mechi ambayo kila mpenzi wa soka Tanzania hatapenda kuikosa.

Brazili katika mechi zake mbili za maandalizi kabla ya kuanza kwa kombe la dunia itacheza na Zimbabwe mjini Harare juni 2 kabla ya kucheza na Tanzania juni 7 jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo ili kufanikisha mechi hizo Tanzania na Zimbabwe zitailipa Brazili mshiko mnene ambao haukuwekwa bayana ingawa inasemekana ni mamilioni ya dola.

Mashirikisho ya soka ya Tanzania na Brazili yamethibitisha kuwepo kwa mechi hiyo juni 7.

Mechi hiyo itakuwa ni fursa pekee ambayo haijawahi kutokea kwa wapenzi wa soka Tanzania kuwaona live mastaa wa Brazili kama vile Kaka, Robinho, Maicon, Lucio, Dani Alves, Elano, Kleberson, Fabiano na wengineo.

Brazili ambayo inajulikana zaidi kwa jina la "Selecao" ipo kwenye kundi la kifo kundi G pamoja na Ureno, Ivory Coast na Korea Kaskazini.

Mechi ya kwanza ya Brazili itakuwa juni 15 ambapo itakiputa na Korea Kaskazini wakati Ivory Coast itachuana na Ureno siku hiyo hiyo.


source nifahamishe

Mama Afanya Mapenzi na Mwanae ili Kumpa Uzoefu wa Mapenzi

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Baba na mama wa mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 9 wa nchini Australia wametupwa rumande kwa kufanya mapenzi na mtoto wao huyo wakidai wanampa elimu na uzoefu wa mapenzi.
Mwanaume mwenye umri wa miaka 57 na mkewe mwenye umri wa miaka 48 wa nchini Australia wametupwa rumande kwa kufanya mapenzi na mtoto wao wa kiume mwenye umri wa miaka 9.

Wazazi wa mtoto huyo ambao ni wafuasi wa kundi la watembea uchi "Nudist" walikuwa wakimpigisha punyeto na kufanya mapenzi na mtoto wao huyo ili kumpa uzoefu wa kimapenzi.

Mamlaka husika zilipewa taarifa juu ya suala hilo baada ya mtoto huyo kumtongoza msichana katika shule yake akimtaka wafanye mapenzi.

Polisi waliwatia mbaroni wazazi wa mtoto huyo novemba 16, 2009 na hawajapewa nafasi ya kumuona mtoto wao tena.

Akiongea mahakamani mjini Sydney jana, baba wa mtoto huyo alikiri makosa mawili ya kumuingilia mtoto wake na makosa mengine ya kumpigisha punyeto, kumshambulia na kuziweka picha na video za vitendo vyake kwenye internet.

Mama yake naye alikiri makosa ya kufanya mapenzi na mwanae na pia kumchua nyeti zake.

Taarifa ya polisi ilisema kuwa mtoto huyo aliwaambia kuwa wazazi wake hutembea uchi wanapokuwa ndani ya nyumba kunapokuwa na hali ya joto.

Baba yake hakuonyesha kujutia vitendo alivyokuwa akimfanyia mwanae na badala yake alidai kuwa anashangaa kwanini amekamatwa wakati alikuwa akimpa elimu ya mapenzi mwanae.

Wazazi wote wawili wa mtoto huyo wamenyimwa dhamana na wametakiwa kutowasiliana na mtoto wao kwa njia yoyote ile mpaka atakapofikisha umri wa utu uzima.

Watapandishwa tena mahakamani juni 4 kujua hatima zao.

source nifahamishe

50 Cent Choka Mbaya, Ukimuona Huwezi Kumtambua

Friday, May 28, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




Kwa kuiangalia picha yake unaweza usiamini na hata utakapoambiwa hii ni picha ya 50 Cent jinsi alivyo sasa unaweza usiamini, lakini ukweli ni kwamba picha hii ni ya 50 Cent kama alivyo sasa baada ya kupungua kilo 25 ndani ya wiki 9.
Picha mpya za mwanamuziki milionea wa Marekani 50 Cent zimetolewa na kuwafanya watu wabaki midomo wazi kwa jinsi ambavyo imekuwa vigumu kumtambua kwa jinsi alivyopungua kilo 25 ndani ya wiki tisa.

50 Cent amejikondesha kwa kunywa maji na juice pekee ili aweze kuigiza kwenye filamu mpya ambayo jikoni ambayo inamuelezea nyota wa mpira wa miguu ambaye anaugua ugonjwa wa kansa.

50 Cent ambaye ana umri wa miaka 34 amekonda sana na amepungua uzito wake toka kilo 97 hadi kilo 72.

50 Cent amejikondesha ili kuleta uhalisia wa mgonjwa wa kansa katika filamu ya "Things Fall Apart", filamu hiyo 50 Cent ndiye nyota wa filamu na prodyuza msaidizi.

Wakati picha mpya za 50 Cent zilipowekwa kwenye mitandao jana watu wengi waligoma kuamini na kusema kwamba picha hizo ni uzushi tu wa kwenye mitandao.

Lakini 50 Cent ambaye jina lake halisi ni Curtis Jackson alijitokeza na kuthibitisha kuwa picha hizo ni za kweli.

50 Cent alisema kuwa baada ya kumaliza kuigiza kwenye filamu hiyo ataanza kula kama kawaida kurudisha mwili wake wa zamani.

source nifahmishe

Baba na mwanaye wakutana gesti toka kwa orijino komedi

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Orijino komedi na unasemaje !

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Orijino komedi na mkasa wa madent kugoma

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Mtoto Huyu Anauzwa

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto huyu wa kichina akiwa amefungwa minyororo kwenye mlingoti wa alama za barabarani, anapigwa mnada barabarani na baba yake ambaye ameamua kumuuza ili akatumike kama mtumwa.
Mtoto wa Kichina mwenye umri wa miaka minane akionyesha wazi hofu iliyotanda uso wake, alisimama pembeni ya barabara akiwa amefungwa minyororo na baba yake ambaye alikuwa akijaribu kumuuza mtoto huyo kwa kupiga kelele kama wauza mitumba.

Baba wa mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Yong Tsui aliweka meza ndogo mbele ya mtoto huyo akiandika jina, umri na uwezo wa kufanya kazi wa mtoto wake ambaye aliamua kumuuza kama mtumwa.

Baadhi ya watu waliojitokeza kumnunua mtoto huyo walimuuliza baba yake kiasi cha chakula ambacho mtoto wake anaweza kula, swali hilo liliwakasirisha wasamaria wema ambao walianza kumshushia kipigo baba wa mtoto huyo.

Polisi waliwahi kumuokoa Yong kabla hajauliwa na wakazi wa jimbo la Wuhan, lililopo ukanda wa kati wa China.

Polisi walimchukua mtoto huyo ambaye hivi sasa anapewa matunzo na serikali. Baba wa mtoto huyo aliwaambia polisi kuwa mama wa mtoto wake alifariki miaka mitatu iliyopita na tangu wakati huo amekuwa akipata tabu kumpa matunzo mtoto huyo.

"Hana kazi, nyumba wala pesa, anasema kwamba hakuhitaji pesa kwa kumuuza mtoto wake alikuwa akijaribu kumtafutia maisha bora mtoto wake", alisema mmoja wa maafisa wa polisi.

Yong alisema kwamba alisoma habari ya mtoto wa China, Cheng Jingdan, mwenye umri wa miaka miwili ambaye baba yake alikuwa akimfunga minyororo kwenye mlingoti wakati akiwa kazini kwa kuhofia watu wasimuibe mtoto wake.

Mtoto Cheng alichukuliwa na wasamaria wema na kupewa maisha bora baada ya picha yake akiwa amefungwa kwenye minyororo iliposambazwa kwenye vyombo vya habari.

Yong kwa kujaribu kumuuza mtoto wake alitegemea bahati kama hiyo ingemdondokea na mtoto wake lakini matokeo yake aliokolewa na polisi kutokana na kipigo cha wananchi wenye hasira.


source nifahamishe

Mwanamke Aliyewaingiza Mjini Wanajeshi 11 wa Marekani

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Polisi nchi Marekani wanamtafuta mwanamke aliyewaingiza mjini wanajeshi 11 wa Marekani kwa kufunga nao ndoa na kisha kuwaibia mali zao zote waliposafiri na kumuachia nyumba zao.
Mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Bobbi Ann Finley anaaminika kuwa ni tapeli sugu ambaye amekuwa akiwaingiza mjini wanajeshi wa Marekani kwa takribani miaka 20.

Msako umeanzishwa na polisi kwenye majimbo ya Washington, Nebraska na Texas wakati jeshi la Marekani limemkodisha mpelelezi maalumu kumsaka mwanamke huyo.

Njia yake ya kuwatapeli wanajeshi ni rahisi sana
Hujipeleka kwenye kambi za jeshi la Marekani kuwasaka wanaume waliojaa upweke wa mapenzi ambao wanaandaliwa kwaajili ya kusafirishwa kupelekwa kwenye kambi za Marekani nchini Afghanistan na kwingineko.

Anapofanikiwa kumnasa mwanaume humuongopea kuwa yeye ni binti afisa wa ngazi za juu wa jeshi la Marekani na kwamba ameachiwa urithi mkubwa ambao ataweza kuuchukua iwapo ataolewa.

Baada ya mwanajeshi wa Marekani kuingia mtegoni na kukubali kufunga naye ndoa, Finley huanza maisha ya ndoa na mumewe huyo huku akisubiria kwa hamu siku ambayo mumewe atasafirishwa kwenda nje ya Marekani.

Baada ya mumewe kusafiri, Finley huanza kazi ya kuiba vitu vyote kwenye nyumba na kuzitumia vibaya credit card anazoachiwa. Huhakikisha anawaingiza hasara kubwa kabla ya kutimkia mji mwingine kusaka mwanajeshi mwingine.

Katika miaka yake ya kuwatapeli wanajeshi wa Marekani kuanzia mwaka 1993, Finley amefanikiwa kuwatepeli jumla ya wanajeshi 11 na amezaa watoto tisa na wanajeshi 9 tofauti.

Watoto wake inasemekana wamezagaa katika miji mbalimbali ya Marekani na baadhi yao hawajawahi kuziona sura za baba zao.

Mmojawapo wa wanajeshi aliyelizwa na Finley alikuwa ni Shane Cheeseman, ambaye alikutana na Finley mwaka 1998 kwenye kambi ya jeshi ya Fort Hood mjini Texas.

"Nilifunga naye ndoa jumatatu, ilipofika mwisho wa wiki alikuwa ameishaondoka na ameniacha kwenye deni kubwa sana", alisema Cheeseman alipokuwa akiongea na waandishi wa habari.

Alipotoa taarifa polisi aliambiwa kuwa yeye ni mmojawapo ya wanajeshi wengi walioingizwa mjini na Finley.

Msako mkali unaendelea nchini Marekani kumsaka Finley na taarifa za awali zinasema kwamba jumla ya wanaume 40 wameishajitokeza kuripoti kutapeliwa kwao na Finley.

source nifahamishe

VIDEO - Mtoto wa Miaka Miwili Anayevuta Sigara 40 Kwa Siku

Thursday, May 27, 2010 / Posted by ishak / comments (0)





Alianza kuvuta sigara akiwa na umri wa miezi 18 hivi sasa akiwa na umri wa miaka miwili mtoto mmoja wa nchini Indonesia anavuta sigara 40 kwa siku. Kutokana na tabia yake ya uvutaji sigara hawezi kukimbia na anapata tabu kucheza na wenzake.
Ardi Rizal mtoto mwenye umri wa miaka miwili ambaye amekuwa akivuta sigara 40 kwa siku amekuwa gumzo duniani baada ya video kutolewa ikumuonyesha mtoto huyo jinsi anavyovuta sigara kwa wingi huku akicheza na watoto wenzake.

Ardi alianza kuvuta sigara akiwa na umri wa miezi 18 lakini hivi sasa akiwa na umri wa miaka miwili wazazi wake wanalalamika kuwa amekuwa mvutaji sigara sugu kiasi cha kufanya vurugu kubwa sana anaponyimwa sigara.

"Ardi anaponyimwa sigara huwa mwenye hasira sana na hufanya vurugu na wakati mwingine hujibamiza kichwa chake ukutani", alisema mama yake Diana mwenye umri wa miaka 26.

Kutokana na unene wake na jinsi anavyovuta sigara kwa fujo, Ardi anashindwa kukimbizana na watoto wenzake.

Serikali ya Indonesia iliahidi kuipa familia ya Ardi zawadi ya gari jipya iwapo Ardi ataacha kuvuta sigara. Lakini jitihada zote za kumuachisha Ardi sigara zimegonga mwamba na badala yake Ardi huifanya familia yake itumie takribani Tsh. 8,000 kila siku kwaajili ya kumnunulia sigara.

Baba yake ambaye anafanya kazi ya kuuza samaki, haoni hatari inayomkabili mtoto wake na husema kwamba mtoto wake ana afya njema hana matatizo yoyote.

"Sina wasiwasi wowote kuhusiana na afya yake, Ardi ni mtoto mwenye afya njema", alisema baba yake kuwaambia waandishi wa habari.

Wanawake Watakaovaa Vimini Kuvalishwa Sketi Ndefu

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Serikali ya Indonesia imeandaa sketi ndefu 20,000 kwaajili ya kuwavalisha kinguvu wanawake watakaokamatwa barabarani wakiwa wamevaa vimini au nguo zinazobana.
Kuanzia leo polisi wa kiislamu wa Indonesia wanaingia mitaani kuwasaka wanawake wanaovaa nguo fupi au zinazobana zinazoonyesha maumbile yao, wanawake watakaokamatwa mitaani wakiwa wamevaa hivyo watalazimishwa wavae hapo hapo sketi ndefu zilizotolewa bure na serikali.

Hatua hiyo imefuatia sheria ya kupiga marufuku nguo fupi za wanawake ambayo inaanza kufanya kazi leo katika mojawapo ya majimbo ya nchi hiyo yenye waislamu wengi kuliko nchi zote duniani.

Sheria hiyo imepitishwa katika jimbo la Aceh lililopo kaskazini mwa kisiwa cha Sumatra nchini Indonesia. Vimini, jeans na nguo za kubana ni miongoni mwa nguo za wanawake zilizopigwa marufuku.

Mkuu wa jimbo hilo Ramli Mansur alisema kwamba wanawake watakaosimamishwa na polisi wa sharia, hawatatiwa mbaroni lakini watalazimishwa wavae sketi ndefu zilizotolewa na serikali.

Mansur aliongeza kwamba ataisimamia vyema sheria hiyo kwa kuhofia siku moja ataulizwa na Mungu aliutumiaje uongozi wake katika kusimamia sharia za kiislamu.

source nifahamishe

Kila Anayemiliki Namba ya Simu Hii Hufariki

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Shirika la simu la Mobitel la nchini Bulgaria limeamua kuifuta mojawapo ya namba zake za simu baada ya kugundulika kuwa kila mtu anayeimiliki namba hiyo hufariki baada ya muda mfupi.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Bulgaria, wamiliki wa namba ya simu hii 0888 888 888 hufariki ndani ya kipindi cha muda mfupi.

Shirika la simu la Mobitel la nchini Bulgaria ambalo linaimiliki namba hiyo limeamua kuifutilia mbali namba hiyo baada ya taarifa ya vifo vya wenye kuimiliki namba hiyo.

Mtu wa kwanza kufariki alikuwa ni bosi wa kampuni hiyo kubwa ya simu nchini Bulgaria, Vladimir Grashnov, ambaye alifariki mwaka 2001 kutokana na ugonjwa wa kansa.

Namba hiyo ya simu alipewa mtu mwingine aliyejulikana kwa jina la Konstantin Dimitrov ambaye naye alifariki miaka miwili baadae baada ya kupigwa risasi nchini Uholanzi.

Inasemekana kwamba mabosi wa kundi la Mafia wa Urusi ndio waliopanga mauaji yake baada ya kumuonea wivu kwa jinsi alivyokuwa akisafirisha kwa wingi madawa ya kulevya.

Mfanyabiashara Konstantin Dishliev alipewa namba hiyo baada ya Konstantin kufariki lakini naye alifariki miaka miwili baadae baada ya kupigwa risasi nje ya mgahawa wa vyakula vya kihindi mjini Sofia nchini humo.

Mfanyabiashara huyo inasemekana alikuwa akisafirisha madawa ya kulevya toka nchi za kusini mwa America kuziingiza Bulgaria. Aliuliwa baada ya polisi kuugundua mzigo wake wa madawa ya kulevya ukiwa njiani kuingizwa Bulgaria.

Mobitel wameamua kuifuta namba hiyo baada ya polisi kukumbana nayo mara kadhaa katika upelelezi wao wa baadhi ya vifo vya watu vilivyohusishwa na madawa ya kulevya.

Namba hiyo hivi sasa haipatikani tena na mtu anapojaribu kuipiga hupewa ujumbe "Namba unayopiga haipo kwenye mtandao wetu".

source nifahamishe

Watu 60 Wafariki Kwasababu ya Mtu Mmoja

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Watu 60 wameishafariki nchini Jamaica hadi sasa kufuatia vurugu zilizozuka wakati polisi wa Jamaica walipoanzisha msako wa nyumba kwa nyumba ili kumkamata kiongozi wa kundi la wauzaji wa madawa ya kulevya wa Jamaica ambaye Wamarekani wanataka akamatwe apelekwe nchini Marekani kushtakiwa.
Mamia ya wanajeshi na polisi walivamia magheto ambayo kiongozi wa kundi la wauza madawa ya kulevya wa Jamaica, Christopher Coke au maarufu kama "Dudus" anaaminika kuwa amejificha katika jiji la Kingston.

Vurugu kubwa zilizuka baada ya wananchi wanaomtetea Dudus kuamua kuwashambulia polisi kupinga kukamatwa kwake.

Dudus anatakiwa nchini Marekani kutokana na kujihusisha kwake na biashara za madawa ya kulevya na silaha.

Dudus mwenye umri wa miaka 41 ana wafuasi wengi toka kwenye makazi ya watu maskini wa mjini Kingston ambao wamesema wako tayari kumlinda Dudus kwa gharama yoyote ile.

Dudus ambaye wafuasi wake wanapenda kumwita "rais" hapendi kuvaa nguo za gharama na huwa haonyeshi ufahari anapokuwa kwenye klabu za starehe kama ambavyo mabosi wengine wa makundi ya uuzaji wa madawa ya kulevya hupenda kujionyesha.

Vurugu hizo zimeingia siku ya tatu mfululizo ambapo Dudus hadi sasa hajakamatwa lakini jumla ya watu 60 wameishapoteza maisha yao.

Wafuasi wa Dudus wamekuwa wakirushiana risasi na wanajeshi na polisi kupinga kukamatwa kwake.

Kutokana na vurugu hizo kusambaa maeneo mengi ya mji wa Kingston, shule na biashara nyingi mjini humo zimefungwa.

Mpambano mkubwa wa polisi na wafuasi wa Dudus unaendelea kwenye magheto ya Trenchtown ambako nyota wa muziki wa reggae Bob Marley ndiko alikokulia

source nifahamishe

Kila Nyumba Tanzania Kuwa na Maji ya Uhakika Ifikapo Mwaka 2013

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa kero ya maji nchini inatarajiwa kuisha kabisa ifikapo mwaka 2013.
Hayo aliyasema jana katika ukumbi wa Karimjee katika majumuisho ya ziara yake ya siku moja jijini Dar es Salaam.

Alisema upo mradi mkubwa unaotarajiwa kuanza mapema mwaka huu wa kuvuna maji yaliyoko ardhini katika eneo la Kimbiji ambao ukikamilika mwaka 2013 vyanzo vyote vitakuwa na uwezo wa kutoa maji lita milioni 710 kwa siku ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa upanuzi wa vyanzo vya maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu.

Alisema kwa sasa mahitaji ya maji katika Jiji la Dar es Salaam ni lita milioni 450 lakini zinazopatikana ni lita milioni 300 kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo Ruvu chini na Juu, Mtoni na visima.

Rais Kikwete aliwaagiza watendaji wa halmashauri zote wakishirikiana na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) na Shirika la Majisafi na Majitaka (DAWASCO) na Wizara ya Maji na Umwagiliaji kuondoa kero ya maji katika kipindi cha mpito kwa kuchimba visima vingi virefu na kumaliza kero hiyo ya maji inayowasumbua wananchi.


source nifahamishe

Busu la Mpenzi Lasababisha Awe Kiziwi

Sunday, May 23, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja wa nchini China amekuwa kiziwi sikio moja baada ya kupewa mabusu ya nguvu ya kunyonyana ndimi na mpenzi wake. Vyombo vya habari nchini humo vimekuwa vikiwaonya vijana kupunguza kupeana mabusu ili kuepuka madhara kama hayo yasitokee tena.
Mwanamke huyo anayekisiwa kuwa na umri wa miaka 20 na ushee wa mji wa Zhuhai kwenye jimbo la Guangdong alienda hospitali akiwa hasikii chochote kupitia sikio lake la kushoto, yameripoti magazeti ya China.

Tukio hilo lilitokea baada ya mwanamke huyo kupeana mabusu ya nguvu ya kunyonyana ndimi na mpenzi wake kwa muda mrefu.

Baada ya tukio hilo, makala mbalimbali zimeandikwa kwenye magazeti ya China vijana wakionywa wapunguze tabia ya kunyonyana ndimi sana kuliko kawaida.

"Kunyonyana ndimi kwa kawaida hakuna madhara lakini watu inabidi wawe waangalifu kidogo", liliandika gazeti la China Daily.

"Wakati wa kunyonyana ndimi, presha toka kinywani huisukuma ngoma ya sikio nje na hivyo kusababisha sikio kupoteza usikivu wake" alisema daktari aliyemtibia msichana huyo alipokuwa akitoa maelezo sababu ya msichana huyo kuwa kiziwi sikio moja.

Maelezo zaidi kuhusiana na madhara ya mabusu ya kunyonyana ndimi yaliandikwa kwenye gazeti la Shanghai Daily, ambalo liliandika: "Busu la nguvu husababisha uwiano wa msukumo wa hewa ndani ya masikio kuharibika na hivyo kusabisha ngoma ya sikio kupasuka".

Madaktari wamesema kuwa mwanamke huyo aliyepoteza usikivu sikio moja ataweza kusikia tena kupitia sikio hilo baada ya miezi miwili.

source nifahamishe