Kuku Mwenye Hirizi Tatu Atinga Hospitali ya Muhimbili

Wednesday, April 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Kuku mwenye hirizi tatu za rangi tofauti alizua kizaa zaa alipoonekana kwenye maeneo ya hospitali ya Muhimbili na baadae kuingia kwenye madarasa ya chuo kikuu cha Muhimbili.
Kuku huyo mweusi alikuwa amevishwa hirizi zenye rangi tatu tofauti nyeusi, nyekundu na nyeupe.

Alionekana kwenye maeneo ya Chuo Kikuu cha Muhimbili kilichopo kwenye hospitali hiyo kubwa nchini Tanzania.

Kuku huyo aliwafanya walinzi wa eneo hilo wachanganyikiwe wasijue la kufanya baada ya kumshuhudia kuku huyo mweusi akirandaranda kwenye maeneo ya Hospitali ya Muhimbili akiwa na hirizi zake tatu.

Haikujulikana mara moja kuku huyo ni wa nani au alitokea wapi ila mmoja wa walinzi wa Muhimbili alisikika akisema eneo hilo limekuwa na matukio mengi ya aina hii na haifahamiiki ni kwanini inakuwa hivyo.

Hata hivyo walinzi wa Muhimbili hawakupenda kulizungumzia suala la kuku huyo wa ajabu.

Watu waliokusanyika waliamrishwa waondoke kwenye eneo la tukio na walinzi kutakiwa warudi kwenye malindo yao baada ya mmoja wa walinzi kumpiga picha kuku huyo kwaajili ya ushahidi na kumbukumbu ya tukio hilo.


source nifahamishe

Mmasai Ang'oa Toto la Kizungu, Wazazi Wamtenga

Sunday, April 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Binti wa Kiingereza ambaye kutokana na utajiri mkubwa wa baba yake, alizoea maisha ya kifahari akisafiri nchi mbalimbali duniani, ameangukia kwenye penzi la kijana wa kimasai nchini Kenya na kuamua kuolewa naye na kusababisha wazazi wake waamue kumtenga kupinga uamuzi wake huo.
Binti wa Kiingereza Colette Armand mwenye umri wa miaka 24 alizoea kuishi maisha ya kifahari akisafiri nchi mbali mbali na kukaa kwenye hoteli za kifahari.

Hata siku moja hakuwahi kufikiria kwamba siku moja angeangukia kwenye penzi la kijana wa kimasai anayeishi porini ambako hakuna umeme wala maji.

Baba yake Colette ni mfanyabiashara mkubwa na mkurugenzi wa kampuni moja kubwa ya madini ya nchini Uingereza wakati mama yake ni nesi katika hospitali moja nchini humo.

Mkasa wa mapenzi wa Colette ulianza miaka mitatu iliyopita wakati Colette alipoacha masomo yake ya chuo kikuu jijini Paris, Ufaransa na kuamua kuja Afrika kufanya kazi za kujitolea kwenye mashirika ya hisani.

Colette bila ya kumwambia mtu mwingine yeyote zaidi ya mama yake, ndani ya wiki moja aliacha shule na kufunga safari hadi Nairobi, Kenya kufanya kazi ya kujitolea kwenye taasisi ya watoto yatima.

Colette alitokea kupendwa kwenye taasisi hiyo ya yatima kutokana na jinsi alivyokuwa akijitolea kwa moyo wote kuwasaidia watoto yatima.

Colette alijipatia umaarufu wa ghafla baada ya mtoto wa miaka tisa aliyejulikana kwa jina la Mumbe ambaye hakuwahi kuongea hata siku moja kabla ya kuwasili kwa Colette, alipotamka neno la kwanza kumwita Colette "Mama".

Colette alijipatia umaarufu mkubwa kutokana na tukio hilo akihesabika kama mtu mwenye miujiza.

Umaarufu huo ulipelekea chifu wa kimasai Kehmini kukitembelea kituo hicho cha yatima na kumpa mwaliko Colette wa kuitembelea jamii ya wamasai.

"Nilipofika nilionyeshwa kibanda ambacho kilikuwa hakina hata mlango, kulikuwa hakuna umeme wala maji", alisema Colette.

"Usiku sikulala kabisa nikihofia nyoka wataingia ndani na kunigonga, nilikuwa nikisiliza sauti toka kila kona kuhakikisha niko salama", aliongeza Colette.

"Maji ya kuoga nayo yalikuwa ya tabu nilishindwa kuoga kwenye mto kwa kuhofia mamba. Niliamua kuchota maji na kisha kuyachemsha kabla ya kuoga".

"Hata hivyo nilitokea kupenda maisha ya kimasai, wanaume wakiondoka asubuhi kwenda kuwinda wakiacha wanawake wakilea watoto, jioni tulikusanyika pembeni ya moto na kupiga stori", alisema Colette.

Ulikuwa ni wakati huo ndipo Colette alipoangukia kwenye penzi motomoto na kijana wa kimasai Meitkini mwenye umri wa miaka 23.

Colette alimaliza miezi akiishi kwenye boma la wamasai mpaka mwaka 2008 yalipotokea machafuko ya kisiasa nchini Kenya ambapo alishauriwa na maafisa wa umoja wa mataifa arudi kwao kwakuwa maisha yake yatakuwa hatarini kutokana na rangi yake.

Colette alikata shauri atumie muda huo kurudi Uingereza kumalizia masomo yake ingawa kutokana na mapenzi aliyo nayo ilikuwa vigumu kwake kuishi mbali na Meitkini.

Colette alirudi Uingereza na kumalizia masomo yake akiwataarifu pia wazazi wake na ndugu zake uamuzi wake wa kuolewa na mmasai na kuishi kwenye boma la wamasai.

Colette hakueleweka katika familia yake na wazazi wake waliliona suala hilo kama skendo na kuamua kutotaka kulizungumzia kabisa.

Colette ingawa hivi sasa ametengwa na wazazi wake bado ameshikilia msimamo wake wa kuolewa na Meitkini na yupo kwenye hatua ya mwisho ya kumalizia maandalizi ya harusi itakayofanyika siku chache zijazo.

Kuhusiana na suala la mumewe kuongeza mke mwingine kama jadi ya wanaume wa kimasai ilivyo, Colette anasema kuwa yeye hatajali kuwa mke mwenza ingawa anaamini Meitkini hafikirii kuongeza mke mwingine zaidi yake.


source nifahamishe

Ng'ombe Anapobebwa Kwenye Ambulansi....

Sunday, April 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Si jambo geni nchini Tanzania kuona gari la serikali likiwa limebeba majani ya ng'ombe au likifanya shughuli ambayo ipo nje ya matumizi ya kikazi, kali ya yote imetokea nchini Pakistan baada ya daktari kununua ng'ombe kwenye mnada na kumpakiza ng'ombe kwenye ambulansi.
Afisa wa kitengo cha afya nchini Pakistan amesimamishwa kazi baada ya kutumia gari la ambulansi kubebea ng'ombe wake aliyemnunua kwenye mnada wa ng'ombe.

Dr Munir Ahmed, afisa wa kituo cha afya cha kitongoji cha Tanda nchini Pakistan amefukuzwa kazi baada ya kutumia gari la ambulansi kumsafirisha ng'ombe wake aliyemnunua kwenye mnada uliopo kilomita 10 toka mji wa Gujrat.

Askari wa usalama wa barabarani waliisimamisha ambulansi hiyo baada ya kuona ng'ombe akiwa ndani huku maski za oxygen zikining'ia kwenye ambulansi hiyo.

Gazeti la Dawn la nchini Pakistan lilichapisha picha ya ng'ombe huyo akiwa ndani ya ambulansi kwenye sehemu ya nyuma ambayo kawaida wagonjwa hulazwa wakati wakiwahishwa hospitali.

Dr. Munir alisimamishwa kazi muda mfupi baada ya kuchapishwa kwa picha hiyo kwenye gazeti huku uchunguzi zaidi ukifanyika kuhusiana na tukio hilo.


source nifahamishe

Maajabu ya Dunia - 'Mtu Nusu' Apata Mtoto

Sunday, April 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume wa nchini Marekani maarufu kama 'Half Man' ambaye maisha yake yote amekuwa akiishi akiwa na nusu ya mwili wake tu kuanzia kiunoni ametamba kuwa yeye ndiyo baba wa mtoto wa kike aliyezaliwa na mchumba wake ingawa baadhi ya watu hawaamini kama kweli mtoto ni wake wakidai atakuwa kabambikiwa mtoto.
Kenny Easterday mwanaume wa nchini Marekani mwenye umri wa miaka 35 ambaye ana nusu mwili kuanzia kiunoni, anasubiria majibu ya DNA ili kuwathibitishia watu kuwa yeye ndio baba wa mtoto wa kike aliyezaliwa na mpenzi wake Nicky.

Katika documentary mpya itakayorushwa hewani leo kwenye televisheni ya Marekani, Kenny mkazi wa West Virginia anasema kuwa yeye ndiye baba wa mtoto Desiree aliyezaa na mpenzi wake Nicky,33 miaka saba iliyopita.

"Watu wanataka kujua kama Kenny ana sehemu za siri", alisema Nicky katika documentary hiyo itakayorushwa hewani na televisheni ya The Learning Channel (TLC).

"Tunafanya mapenzi kama watu wengine, Kenny ana sehemu za siri kama mwanaume mwingine", aliongeza Nicky.

Kenny alizaliwa akiwa na ugonjwa unaowapata watu wachache sana duniani unaoitwa sacral agenesis ambao huzuia uti wa mgongo kukua kama kawaida.

Madaktari walilazimika kuikata miguu yake miwili iliyojipinda iliyojichomoza kidogo chini ya kiuno chake na kisha kuuchukua mfupa wa ugoko wake na kuutumia kuurefusha uti wa mgongo wake.

Kenny ambaye kutembea kwake ni kwa kutumia mikono anasema kuwa ndoto yake kubwa ilikuwa ni kupata mtoto.

"Nataka niwe na mtoto atakayelibeba jina langu ambaye ataweza kusimama mbele ya watu na kusema 'HUYU NDIYO BABA YANGU'", alisema Kenny.

source nifahamishe

Mamia ya Wakristo Wajipigilia Misumari Kwenye Misalaba

Sunday, April 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mamia ya waumini wa Kikristo nchini Philippines walitumia dakika kadhaa wakiwa kwenye maumivu makali wakati walipoadhimisha siku ya kusulubiwa kwa yesu kwa kupigiliwa misumari ya sentimeta tano kwenye miguu na mikono yao.
Bila ya kutumia ganzi misumari ya sentimeta tano ilipigiliwa kwenye mikono na miguu ya waumini wa Kikristo katika kukumbushia kusulubiwa kwa mkombozi wa wakristo, Yesu Kristo.

Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mary-Jane Mamangun alidai kuwa hakusikia maumivu yoyote wakati misumari ya sentimeta tano ilipokuwa ikipigiliwa kwenye miguu na mikono yake.

Lakini sura yake wakati alipotundikwa msalabani ilionyesha wazi maumivu makali aliyokuwa akiyapata na alilazimika kuwahishwa kwenye hema la matibabu ambapo alipatiwa dawa za kupunguza maumivu.


source nifahamishe