Ruhsa Kumpiga Mkeo Lakini Usimtoe Alama

Thursday, October 21, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mahakama ya sheria za kiislamu katika falme za kiarabu UAE imeamuru kuwa ni ruhsa mwanaume kumpiga mkewe na watoto wake ili mradi hatasababisha alama za vipigo kwenye miili yao.
Hatua hiyo ya mahakama hiyo inawapa haki za kisheria wanaume kuwaadhibu wake zao na watoto wao iwapo wataenda kinyume na matakwa yao.

Hukumu hiyo ilitolewa na mmoja wa majaji wakuu wa UAE, Falah al Hajeri, ambaye alikuwa akitoa hukumu ya mwanaume aliyepigwa faini sawa na Tsh. 160,000 kwa kumpiga kibao mkewe na kumpiga teke binti yake.

Mwanaume huyo alipatikana na hatia ya kumpiga mkewe kwa nguvu sana kiasi cha kusababisha apasuke mdomo wake na kuvunjika jino lake.

Mwanaume huyo pia alimpiga mateke binti yake mwenye umri wa miaka 23 kiasi cha kupelekea apate michuko na uvimbe kwenye mguu na mkono wake.

Mwanaume huyo ambaye jina lake liliwekwa kapuni, awali alidai alimpiga mkewe na mtoto wake kwa bahati mbaya lakini alipopatikana na hatia alikata rufaa akisema kuwa hata kama alimpiga mkewe na mtoto wake kwa makusudi, anayo haki kwa mujibu wa sheria za kiislamu kutumia nguvu dhidi yao iwapo njia zingine za kuwaadabisha zitakuwa zimefeli.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo, jaji Falah al Hajeri alisema: “Ingawa sheria zinaruhusu waume kuwapiga wake zao, lakini pia wanatakiwa wasivuke mipaka na kusawasababisha alama au makovu wake zao”.

“Kama mume atakiuka misingi ya sheria ya kumuadhibu mke au mtoto wake, basi lazima ahukumiwe kwa mujibu wa sheria”, alisema jaji Hajeri.

Jaji Hajeri alielezea kuwa njia rahisi ya kuangalia kama waume wavunja sheria ya kuwaadhibu wake zao ni kwa kuangalia alama za vipigo kwenye miili ya wake zao.

source nifahamishe

Kaka Yake Obama Aoa Mwanafunzi Aliyemtorosha Kwao

Sunday, October 17, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kaka wa kufikia wa rais wa Marekani, Barack Obama anayeishi nchini Kenya, Malik Obama mwenye umri wa miaka 52 ameongeza mke wa tatu ambaye ni mwanafunzi wa sekondari mwenye umri wa miaka 19 aliyeacha shule na kukimbia kwao.
Kaka wa kufikia wa rais wa Marekani, Barack Obama anayeishi nchini Kenya, Malik Obama ambaye ana wake wawili ameongeza mke wa tatu ambaye ni mwanafunzi wa sekondari aliyekimbia masomo yake.

Mama wa msichana huyo mwenye umri wa miaka 52, alielezea hasira zake baada ya binti yake kuacha masomo ili aolewe na Malik ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 52.

Akiongea na televisheni ya NTV ya Kenya, mama wa msichana huyo anayeitwa Mary Aoko Ouma alisema kuwa binti yake awali alijaribu kufunga ndoa na Malik miaka miwili iliyopita lakini hakumruhusu.

Akiongea na televisheni ya NTV bila ya kujua kuwa anarekodiwa, Malik alithibitisha kufunga ndoa na msichana huyo ingawa hakusema ni lini harusi yao ilifanyika.

Sheria za Kenya zinaruhusu mtu kuoa mke zaidi ya mmoja iwapo vigezo vya kidini au kitamaduni vitatumika.

source nifahamishe