Pinda aguswa na sakata la Jerry

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


WAZIRI MKUU Mizengo Pinda, ameliagiza Jeshi la polisi nchini kufanya uchunguzi haraka iwezekanavyo ili suala hilo liweze kujulikana kama ni la fufikishwa mahakamani ama la ili haki iweze kutendeka kwa kuwa suala hilo limeigusa jamii iliyokubwa nchini
Pinda amemuagiza Mkuu wa Jeshi hilo IGP Said Mwema na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kufanya uchunguzi wa kina bila kuvihusisha vyombo vya habari ili kuweza kumaliza sakata hilo.

Waziri Pinda alitoa agizo hilo jana wakati alipokuwa akijibu maswali ya papo kwa papo bungeni Dodoma.

Pinda ambaye ni kiongozi wa kwanza wa ngazi za juu wa serikali kuingilia kati ametaka suala hilo lishughulikiwe mara moja tuhuma za mwanahabari huyo ambalo kwa sasa limekuwa gumzo la jiji.

Agizo la Waziri Mkuu lilitokana na swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), aliyehoji jitihada zinazofanywa na serikali katika kushughulikia suala hilo.

Katika swali lake la msingi, Hamad Rashid alisema waandishi wengi duniani wanapofuatilia mambo mazito, hupatwa na misukusosuko mikubwa na kuhoji kama yaliyompata Muro ni mojawapo ya misukosuko ya aina hiyo.

Akijibu swali hilo, Pinda alisema tayari amekwishazungumza na Masha na IGP Mwema ambao wameahidi kulifuatilia jambo hilo kwa haraka na binafsi asingependa jambo hilo kuendelea kuleta utata kutokana na kuwepo na kauli nyingi za watu mbalimbali kuhusu suala husika.

Pia alisema “Mimi pia sipendi suala hili lichukue muda mrefu maana linaweza kuleta hisia tofauti miongoni mwa jamii,” alisema Pinda.

Alisema kila binadamu anao upungufu wake, hivyo kuna uwezekano wa tuhuma dhidi ya Muro zikawa za kweli au la kwani pande zote mbili, akiwemo Muro na polisi wamekuwa wakikimbilia katika vyombo vya habari na kutoa taarifa zinazotatanisha.

source nifahamishe

Mafundi wafa kwa kufunikwa na kifusi Dar

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MAFUNDI UJENZI wawili wakazi wa Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam, wamekufa papo hapo baada ya kufunikwa na kifusi cha mchanga walichokichimba kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi
Taarifa hiyo ilitolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, na kusema tukio hilo lilitokea juzi huko Pugu Bagdad.

Shilogile amesema kuwa, mafundi hao James Katenga (27) na Adamu Mtolela (30), walikutwa na umauti huo wakati wakiendelea na uchimbaji mchanga kwenye moja ya machimbo yaliyopo eneo hilo.

Amesema mafundi hao walikutwa na wenzi wao ambao walikuwa wanahusika katika ujenzi na kuwakuta wameshapoteza maisha na kutoa tarifa kituo cha polisi.

Katika tukio jingine la ajali lililotokea jijini Dar es Salaam, mtu mmoja amekufa dunia papohapo na mwenzake kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari.

Amesema mtu aliyefariki alitambulika kwa jina la Mussa Issah (24) ambaye alikuwa akiendesha pikipiki na aliyejeruhiwa alikuwa ni abiria wake aliyetambuliwa kwa jina la Gidimash Geofrey 22 .

Amesema waligongwa vibaya na gari dogo aina ya Audi Saloon eneo la Brush huko barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Liberatus Sabas, alisema ajali hiyo ilitokea juzi eneo hilo wakati gari hilo lenye namba za usajili T 357 ASE likiendeshwa na Magreth Lega (34).

Amesema gari hilo lilikuwa alikitokea eneo la Kamata kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati dereva wa pikipiki hiyo yenye namba za usajili T 391 AYU alikuwa akitokea Tazara kuelekea Kamata.

Amesema Geofrey amelazwa hospitali ya Temeke.

source nifahamishe

Afikishwa kortini kwa kuua wanawe

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MOSES CHIPAMA [45] anayedaiwa kuwaua watoto wake wawili katika mazingira ya kutatanisha jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kujibu shitaka hilo la mauaji.
Shata hilo lilifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Rose Kangwa, wakati upande wa mashitaka ulikuwa ukiongozwa na Inspekta Dustan Kombe.

Kombe alidai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na mashitaka mawili ya mauaji ya watoto wake.

Katika shitaka la kwanza mshtakiwa alikamatwa Januari 25, mwaka huu, majira ya saa 5:55 usiku eneo la Tuangoma kwa Saku baada ya kumuua mtoto wake, Patrick Moses (16), aliyekuwa akisoma darasa la saba Shule ya Msingi Tuangoma.

Katika shitaka la pili, ilidaiwa kuwa mshtakiwa huyo alimuua mtoto wake mwingine, Sety Moses (12), aliyekuwa akisoma darasa la nne katika Shule ya Msingi ya Olympio.

Hata hivyo mshitakiwa alirudishwa rumande kwa kuwa hakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Hakimu aliamuru arudishwe rumande na kusubiri tarawtibu za kimahakama zifanyike na atakwenda kujibu shitaka hilo mahakama kuu, Kesi hiyo itarudishwa tena mahakamani hapo Februari 18, mwaka huu.

Katika hali ya kushangaza mshitakiwa huyo alianza kuwarushia mawe waandishi wa habari waliokuwa ndani ya mahakama kusikiliza shauri hilo huku akiwarushia viatu kwa kukataa kuandikwa na na kupigwa picha.

Alipoona viatu vyote viwili alivyovaa viliisha alivua fulana aliyovaa na ulijifunika sura ili wanahabari wasiweze kupata sura ili wasiweze kuianika magazetini.

Kutokana na fujo zake hizo maaskari magereza walilazimika kumtuliza mshitakiwa huyo kwa virungu na kuacha kuwatukana matusi wanahabari.


source nifahamishe

Msichana Azikwa Hai Kwa Kosa la Kuwa na Rafiki wa Kiume

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (1)


Msichana mwenye umri wa miaka 16 amezikwa hai na ndugu zake nchini Uturuki kwa kosa la kuwa na rafiki wa kiume hivyo kudaiwa ameiletea aibu familia yake.
Msichana mwenye umri wa miaka 16 wa nchini Uturuki amezikwa hai na ndugu zake baada ya kushutumiwa kuwa ameitia aibu familia yake kwa kuwa na marafiki wa kiume.

Baada ya kupewa taarifa ya tukio hilo, polisi walifanikiwa kuupata mwili wa msichana huyo aliyetambulika kwa jina la Medine Memi siku 40 baada ya kutangazwa kuwa ametoweka.

Mwili wa Medine ulikutwa katika mji wa Adiyaman umekalishwa kitako kwenye shimo la mita 2 huku mikono yake ikiwa imefungwa na kamba.

Baada ya maiti yake kufanyiwa vipimo kadhaa iligundulika kuwa kwenye tumbo lake na mapafu kulikuwa na kiasi cha mchanga hivyo kumaanisha kuwa alizikwa akiwa hai, taarifa ya wataalamu wa makosa ya jinai ilisema.

"Matokeo ya uchunguzi wa maiti yake yanasikitisha sana, msichana ambaye hakuwa na mchubuko hata mmoja kwenye mwili wake na wala hakuwa na kiasi chochote cha sumu kwenye damu yake, alikuwa hai na mwenye kujitambua wakati alipozikwa hai", alisema mtaalamu mmoja ambaye hakutaka kusema jina lake.

Baba yake Medine na babu yake, wametiwa mbaroni na kutupwa jela wakati uchunguzi wa mauaji yake ukiendelea.

Shirika la habari la Anatolia la Uturuki liliripoti kuwa baba yake Meline alisema katika ushahidi wake polisi kuwa familia yake haikuwa ikifurahia kumuona Medine akiwa na marafiki wa kiume.

Mauaji hayo yanayoitwa "Mauaji ya kulinda heshima" hufanyika sana kusini mashariki mwa Uturuki katika maeneo yenye Wakurdi wengi.

Serikali ya Uturuki imekuwa ikijaribu kuyakomesha mauaji hayo ya kulinda heshima bila mfanikio yoyote.

Wanawake wanaobakwa au wanaopata ujauzito kabla ya kuolewa huuliwa na familia zao katika kile kinachodaiwa kusafisha nuksi na fedheha wanazoziletea familia zao.

source nifahamishe

Binti wa Miaka 12 Arudi Kwa Mumewe wa Miaka 80

Friday, February 05, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Binti mwenye umri wa miaka 12 wa nchini Saudi Arabia ambaye alimkimbia mumewe mwenye umri wa miaka 80 baada ya kufungishwa ndoa kinguvu na baba yake, amekubali kurudi kwa mumewe na kuyaondoa madai ya talaka aliyofungua mahakamani.
Msichana mwenye umri wa miaka 12 wa nchini Saudi Arabia ambaye kwa kushirikiana na mama yake alifungua kesi mahakamani kudai talaka toka kwa mumewe mwenye umri wa miaka 80 ameamua kuyaondoa madai yake ya talaka na kurudi kwa mumewe.

Msichana huyo aliozeshwa kinguvu na baba yake ambaye alichukua mahari ya dola 22,670 toka kwa babu huyo.

Binti huyo ambaye jina lake limewekwa kapuni, alikuwa akiishi na baba yake baada ya ndoa ya baba yake na mama yake kuvunjika.

Binti huyo na mama yake waliifuta kesi ya madai ya talaka waliyoifungua katika kitongoji cha Buraidah katika mji wa Al-Qasim.

"Nimeikubali ndoa iliyofungwa na sina kipingamizi chochote", alisikika akisema binti huyo na kuongeza "Nafanya hivi kwaajili ya heshima ya baba yangu na kumtimizia ndoto yake".

Bila ya kueleza sababu za kubadilisha uamuzi wake ghafla, binti huyo aliiambia mahakama kuwa ndoa hiyo ilifungwa kwa hiari yake.

Ndoa ya binti huyo na babu mwenye umri wa miaka 80 ilizua mtafaruku mkubwa sana duniani baada ya mama wa binti huyo kufungua kesi mahakamani kuipinga ndoa hiyo huku akidai binti yake amebakwa.

Wakati taasisi za kutetea haki za watoto zikijiandaa kumtetea mahakamani, binti huyo amezivunja moyo taasisi hizo na kukubali kurudi kwa mumewe.

source nifahamishe

Wanne wa familia moja wateketea kwa moto wa jenereta

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

WATU wanne wa familia moja wamekufa kwa moto baada ya jenereta lililokuwa limefungiwa katika moja ya chumba ndani ya nyumba hiyo kupasuka na kuwaka moto
Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa kuamka leo, huko maeneo ya Kibwenzini Zanzibar wakati watu hao wakiwa wamelala ndani humo.

Ilidaiwa kuwa jenereta hilo liliripuka majira ya saa 11 za alfajiri na kuzua moto uliosababisha vifo hivyo.

Ilidaiwa kuwa familia hiyo ilinunua jenereta hilo kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kutokana na kukosekana kwa umeme visiwani Zanzibar.

Katika ajali hiyo waliopoteza maisha walitajwa kuwa ni Safia Shabani, Ahmed Shaban na mtoto ambaye hakuweza kupatikana jina lake, akiwemo na msichana wa kazi Sikudhani Nasorro.

Hadi habari hii inarushwa hewani, kamanda wa Polisi wa wilaya husika hakuweza kupatikana kuongelea juu ya tukio hilo juhudi zaidi zinafanyika ili kuweza kupata maelezo yake.

source nifahamishe

Mwanafunzi Aiuza Bikira Yake Kwa Dola 32,000

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi mmoja wa nchini New Zealand ameinadi bikira yake kwa dola 31,900 kwa mwanaume asiyemfahamu ili aweze kupata pesa za kulipia gharama za masomo yake ya chuo kikuu.
Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 19 aliinadi bikira yake kwenye mtandao wa www.ineed.co.nz baada ya kukabiliwa na ukata wa pesa.

Mwanafunzi huyo anayejiita "Unigirl" alijitambulisha kuwa yeye ni mrembo mwenye kuvutia, yuko fiti na mwenye afya njema.

Zaidi ya watu 1,000 walijaribu kuinunua bikira yake lakini mwanaume mmoja ambaye hakutajwa jina lake aliibuka mshindi baada ya kuweka dau kubwa la dola 31,900. (Takribani Tsh. Milioni 42).

"Nawashukuru watu wote zaidi ya 30,000 waliolitembelea tangazo langu, na zaidi ya watu 1,200 walioweka madau yao kuinunua bikira yangu", alisema mwanafunzi huyo.

"Dau lililoshinda ni kubwa sana kuliko hata nilivyotarajia".

Mwanafunzi huyo alisema kuwa hajawahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na pesa atakazopata atazitumia kulipia masomo yake.

Mwanafunzi huyo aliendelea kusema kuwa ili mradi masuala ya afya yake yatapewa kipaumbele hana hiana kumtunuku bikira yake mwanaume yoyote yule bila kubagua kabila wala umri ilimradi apate pesa za kulipia masomo yake.

Mmiliki wa tovuti iliyotumika kuinadi bikira hiyo, Ross MacKenzie, alisema kuwa tangazo la mwanafunzi huyo lilikuwa ni halali kisheria na hakuna sheria yoyote iliyovunjwa.

Mwanafunzi huyo aligoma kufanya mahojiano na waandishi wa habari lakini MacKenzie, aliliambia gazeti la Waikato Times kuwa ameruhusiwa kutaja kiasi cha dau lililoshinda bila kutoa maelezo ya ziada.

Matukio ya wanawake kuzinadi bikira zao kwenye internet yaliibuka kwa kasi baada ya mwanafunzi wa Marekani Natalie Dylan ,22, kuinadi bikira yake na kupata mteja aliyeweka dau la dola milioni 3.7.

Natalie naye wakati anainadi bikira yake alitoa sababu kama hizi kuwa anatafuta pesa za kulipia masomo yake.

Mwezi mei mwaka jana nchini Ujerumani, mwanamke mmoja toka Romania, Alina Percea, 18, aliinadi bikira yake kwa matumaini ya kuingiza mamilioni kama Natalie lakini aliambulia euro 10,000 tu toka kwa mfanyabiashara wa Italia mwenye umri wa miaka 45 aliyeshinda katika mnada huo.

Mbali ya kupata dau dogo, Alina alipata hasara zaidi baada ya maafisa kodi wa Ujerumani kuzikata kodi pesa alizopata kwa kuinadi bikira yake akiambiwa kuwa alichofanya ni sawa na wanachofanya makahaba ambao nao wanalipa kodi kwa shughuli zao.

Alina alibakia na karibia nusu ya pesa alizopata baada ya makato ya kodi kufanyika.

source nifahamishe

Ajali za Kujitakia...

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Daktari wa nchini Slovenia aliyepigania mahakamani kwa miaka minne arudishiwe mbwa wake watatu ambao walikuwa wakiwang'ata watu, amefariki dunia baada ya kung'atwa na kujeruhiwa vibaya sana na mbwa hao.
Daktari huyo mwenye umri wa miaka 52 alipigania kwa miaka minne mahakamani kabla ya kushinda kesi na kurudishiwa mbwa wake ambao alinyang'anywa kutokana na matukio ya mbwa hao kuwang'ata watu.

Daktari huyo alikutwa jana akiwa amefariki kwenye bustani ya nyumba yake baada ya kung'atwa na kujeruhiwa vibaya na mbwa wake watatu aina ya "Bullmastiff".

Hadi polisi wanawasili kwenye nyumba yake katika mji mkuu wa Slovenia, Ljubljana, daktari huyo alikuwa ameishafariki lakini mbwa hao walikuwa wakiendelea kumshambulia.

Polisi walimpiga risasi na kumuua mbwa mmoja na kufanikiwa kuwaweka chini ya ulinzi mbwa wengine wawili.

Mbwa hao walitumia muda mrefu sana kwenye jela za polisi wakati kesi hiyo iliyochukua miaka minne ikiendelea. Mbwa hao walitengwa na kuwekwa kwenye vyumba maalumu vyenye ulinzi mkali baada ya kumshambulia afisa aliyekuwa akiwahudumia.

Lakini baada ya kumalizika kwa hukumu iliyochukua masaa 11, mwezi juni mwaka jana, daktari huyo alishinda kesi na kukabidhiwa mbwa wake.

"Mbwa watatu wamemshambulia na kumuua mmiliki wao jana", alisema msemaji wa polisi Maja Adlesic.

Habari za kuuliwa kwa daktari huyo zimesababisha mjadala mkubwa nchini Slovenia huku chama cha upinzani kikimtaka waziri wa kilimo ajiuzulu kwa kushindwa kuzuia mbwa hao wasirejeshwe kwa mmiliki wao.

Polisi walikataa kutoa maelezo zaidi wala kulitaja jina la daktari huyo.

source nifahamishe

Rais Zuma Akiri Kumzalisha Mwanamke Nje ya Ndoa

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amekiri kuwasaliti wake zake watatu na kuzaa na mwanamke mwingine nje ya ndoa.
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amezithibitisha taarifa za vyombo vya habari kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti wa rafiki yake na amemzalisha mtoto wa kike.

Katika taarifa iliyotolewa na ofisi ya Zuma jana, Zuma amekiri kuwasaliti wake zake watatu na mchumba wake anayetegemea kumuoa hivi karibuni.

Mbali na kukiri uhusiano huo, rais Zuma amepinga vikali tuhuma kuwa anaonyesha mfano mbaya wakati harakati za kupambana na ukimwi zikiendelea nchini Afrika Kusini.

Asilimia 10 ya raia wa Afrika Kusini wanaishi na virusi vya ukimwi.

Vyombo vya habari vya Afrika Kusini viliripoti wiki hii kuwa Rais Zuma mwenye umri wa miaka 67 amezaa na binti wa rafiki yake wa karibu ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Gazeti la Sunday Times la Afrika Kusini liliripoti kuwa Zuma alizisaliti ndoa zake na kuzaa na Sonono Khoza ambaye ni binti wa Irvin Khoza, mmiliki wa timu ya Orlando Pirates.

Sonono mwenye umri wa miaka 39 alijifungua mtoto wa rais Zuma mwezi oktoba mwaka jana.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, baba yake Sonono alielezea kuhuzunishwa sana na kitendo cha Zuma kumtia mimba binti yake.

Khoza aliiambia familia yake kuwa anahisi amesalitiwa na Zuma ambaye alikuwa akimchukulia kama rafiki yake wa karibu sana.

source nifahamishe

Jerry aumiza vichwa vya wabunge, wengi wahisi kasukiwa tuhuma

Thursday, February 04, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Baadhi ya wabunge waliozungumza na NIFAHAMISHE walisema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi dhidi ya Muro ni cha uonevu, huku wengine wakitaka sheria ichukue mkondo mara moja
Mbunge mmoja kwa tiketi ya CCM), aliyezungumza na NIFAHAMISHE aliyeomba kutotajwa jina alisema, suala la Muro kukamatwa kwa tuhuma za rushwa ni majungu kwani amekamatwa siku chache baada ya kuibua uovu unaofanywa na Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani aliowanasa wakipokea rushwa kutoka kwa madereva wa magari makubwa.

“Katika hali ya kawaida, hata mtu asiyejua sheria kutokana na maelezo yanayotolewa na jeshi la polisi dhidi ya Muro binafsi hayaeleweki kwani yanachanganya sana, hali inayoonyesha kwamba mashitaka ya mwanahabari huyo maarufu nchini aliyejipatia sifa kubwa kwa kufichua ufisadi nchini kwa sasa yamepikwa kumkomoa,” alisema mbunge huyo akionekena kukerwa na jambo hilo.

Amesema kama ni suala la rushwa hilo ni jambo la TAKUKURU wangeweka mitego yao na kumkamata na sio kama hivyo walivyopanga

“Inauma sana kuona mtu muhimu kama Jerry anatiwa mbaroni wakati amesaidia sana umma wa Tanzania hadi kupewa Tuzo ya Mwanahabari Bora kwa kuibua na kufichua mambo yaliyokuwa yakitendeka kwa kificho na hasa ndani ya Jeshi la Polisi na katika sekta nyingine muhimu nchini", alimalizia kusema mbunge huyo.

Kwa upande wa Mbunge maarufu anayewika nchini kwa kukosoa ufisadi, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela (CCM), alisema suala hili liangaliwe kwa undani ili kubaini ukweli uliojificha ndani yake.

Alisema ni vema ufanyike uchunguzi huru ambao hautaegemea upande wowote ili haki iweze kutendeka kwa kuwa watanzania wamekuwa hawataki kuambiwa ukweli.

Aidha, wabunge wengine waliotoa maoni yao walionyesha wasiwasi na kutaka kesi hiyo ipelekwe mahakamani mapema kama ilivyo kwa kesi nyingine badala ya kuendelea kuiweka mikononi mwa polisi kwa muda mrefu.

Hatahivyo jeshi la polisi nchini linasuasua kumfikisha mwanahabari huyo mahakamani kwa madai kuwa hadi wapate uthibitisho kutoka kwa wakili wa serikali.

source nifahamishe

Sigara Yamlipukia Mdomoni na Kumng'oa Meno Sita

Wednesday, February 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Indonesia ameapa kutokurudia tena kuvuta sigara baada ya sigara aliyokuwa akivuta kumlipukia mdomoni katika mazingira yasiyoeleweka na kusababisha meno yake sita yang'oke.
Andi Susanto mwenye umri wa miaka 31, anapatiwa matibabu hivi sasa kufuatia tukio la kupoteza meno yake sita ya mbele baada ya sigara kumlipukia mdomoni.

Akihojiwa na televisheni ya Metro TV ya Indonesia akiwa kwenye kitanda chake hospitalini, Andi alisema kuwa haelewi ilikuwaje sigara ikamlipukia mdomoni.

Andi alisema kuwa kampuni iliyozalisha sigara hiyo, inayoitwa PT Nojorono Tobacco Indonesia imekubali kulipa gharama zote za matibabu yake.

"Maafisa wa kampuni wameongea na familia yangu na wamekubali tumalize suala hili nje ya mahakama", alisema Andi.

Sababu ya mlipuko wa sigara hiyo bado haujajulikana na Andi anasema kuwa hakuwa akitafuna wala kuweka mdomoni kitu kingine chochote zaidi ya hiyo sigara.

Andi aliendelea kusema kuwa wakati alipoiwasha na kuanza kuivuta sigara hiyo inayoitwa "Clas Mild" hakuona utofauti wowote katika ladha au harufu lakini ghafla ililipuka na kuuharibu mdomo wake na kusababisha meno yake sita yang'oke.

Andi aliapa kuwa hataendelea kuvuta sigara tena atakaporuhusiwa kurudi nyumbani kwake toka hospitali.

Indonesia ni miongoni mwa nchi zenye biashara kubwa ya sigara na asilimia 60 ya wanaume wa Indonesia wanavuta sigara.

source nifahamishe

Ana Miaka 13 Lakini Anaonekana Kama Bibi wa Miaka 50

Wednesday, February 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Akikuambia kuwa ana umri wa miaka 13 unaweza ukabisha mpaka siku inayofuatia bila kukubali, msichana Zara Hartshorn wa nchini Uingereza aliyepatwa na ugonjwa wa ajabu anashindwa kuufaidi utoto wake kutokana na jinsi watu wanavyomchukulia kuwa yeye ni bibi mwenye umri wa miaka zaidi ya 50
Siku moja Zara Hartshorn alipanda basi la abiria na kutaka kukata tiketi ya watoto lakini dereva wa basi hilo alimuangalia kwa mshangao na kumwambia kuwa asifanye masihara alipe pesa kamili.

Zara aliposema kuwa yeye ni mtoto na ana umri wa miaka 13, dereva huyo ambaye alikuwa ni mzee wa makamo, alicheka sana na kumwambia kama ndio hivyo basi na mimi nina umri wa miaka 21.

Abiria nao waliingia kwenye mjadala huo na kumuunga mkono dereva kuwa Zara anawachezea watu akili kwani anaonekana wazi kuwa yeye ni kikongwe mwenye wajukuu.

Zara kwa aibu alishuka toka kwenye basi hilo na kusubiria basi jingine kwa imani dereva wa basi lifuatalo angeweza kumuelewa kuwa yeye ni mtoto.

Huo ni mkasa mdogo sana kati ya mikasa inayomkumba binti Zara Hartshorn wa Rotherham nchini Uingereza ambaye umri wake halisi ni miaka 13 pamoja na kwamba anaonekana kuwa na umri zaidi ya miaka 50.

Zara anakabiliwa na ugonjwa unaoitwa lipodystrophy ambao humfanya aonekane mzee sana kuliko umri wake huku akiwa na tabia za kitoto kama watoto wenzake.

Mama yake Zara bi Tracey Pollard ilibidi achukue uamuzi wa kumsimamisha masomo Zara kwakuwa alikuwa akitaniwa sana na wenzake akiitwa "Bibi" na kubandikwa majina kadhaa ya fedheha.

Ugonjwa unaomkabili Zara umewahi kuwatokea watu 2,000 tu duniani ambapo tabaka la chini la mafuta la ngozi hutoweka na kuifanya ngozi izeeke kwa spidi ya ajabu sana.

Ugonjwa wa lipodystrophy hauna tiba hivyo Zara ataendelea kuzeeka mapema jinsi anavyozidi kuendelea kukua.

Zara amerithi ugonjwa huo toka kwa mama yake ambaye ni miongoni mwa wagonjwa wachache sana duniani wa ugonjwa huo.

"Nilijuta kumzaa Zara, nilihuzunishwa sana nikifikiria kuwa Zara atapitia matatizo yote yaliyonikumba mimi wakati wa utoto wangu", alisema mama yake Zara.

Zara anaelezea masikitiko yake kutokana na jinsi watu wanavyomchukulia na kumtania kwa kusema kuwa wakati mwingine hukimbilia chumbani kwake na kuanza kulia peke yake.


source nifahamishe

Daktari aliyebaka nje kwa dhamana

Wednesday, February 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

DAKTARI wa Hospital ya Marie Stopes tawi la Mwenge jijini Dar es Salaam, Paul Andrew (34), anayekabiliwa na tuhuma za kumbaka mgonjwa, amefikishwa mahakamani na kuachiliwa kwa dhamana.
Daktari huyo ambaye ni mkazi wa Sinza, jijini Dar es Salaam, amefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kujibu shtaka hilo la ubakaji mbele ya Hakimu Suzan Kihawa.

Mwendesha Mashitaka Inspekta wa Polisi, Nassor Sisiwayah, alidai mbele ya Hakimu huyo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 26, mwaka huu, majira ya saa 7:00 mchana eneo Mwenge katika hospitali ya Marie Stopes.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa akiwa ni daktari wa hospitali hiyo, alitumia nafasi hiyo kumbaka mlalamikaji, Judith Keleth (30) bila idhini yake wakati akijitayarisha kumfanyia kipimo cha uchunguzi wa mimba cha Ultra Sound.

Hata hivyo, mshtakiwa alikana shitaka hilo na yupo nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti aliyopewa.

Hakimu alimtaka Dokta Paul awe na wadhamini wawili ambao kila mmoja anatakiwa kusaini hundi la shilingi 500,000 kila mmoja.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Machi 9 mwaka huu.


source nifahamishe

Hausigeli aanguka kutoka ghorofani na kufa

Wednesday, February 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MSICHANA wa kazi za ndani aliyefahamika kwa jina moja la Modiwa anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 na 25, mkazi wa Kariakoo Mtaa wa Livingstone amekufa baada ya kuteleza kutoka kwenye ghorofani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile amesema kuwa, ajali hiyo imetokea jana saa 3 usiku, huko Kariakoo Mtaa wa Livingstone.

Maelezo ya Shilogile yalisema kuwa, msichana huyo alikuwa ni mfanyakazi nyumbani kwa Hassan.

Alisema kuwa msichana huyo aliteleza kutoka ghorofa ya nne kisha kuanguka chini na kufa papo hapo.

Maiti imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo..

source nifahamishe

Paka Anayedaiwa Kuwa na Uwezo wa Kunusa Kifo Kabla Hakijatokea

Wednesday, February 03, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Ukimuona ni paka wa kawaida ambaye hana tofauti yoyote na paka wengine lakini inasemwa kuwa ana uwezo wa kuwatambua wagonjwa wanaokaribia kufariki hospitalini na hadi sasa imesemwa kuwa ameishafanikiwa kuvinusa vifo vya wagonjwa 50 kabla hata havijatokea
Paka anayejulikana kwa jina la Oscar hujisogeza na kukaa karibu na kitanda cha mgonjwa aliyebakiza muda mchache kufariki.

Iwapo ndugu wa mgonjwa huyo watamfukuza paka huyo nje ya chumba cha mgonjwa wao na kumfungia mlango, basi paka huyo hugoma kuondoka na huanza kuukwaruza mlango kwa nguvu aking'ang'ania kuingia ndani.

Paka Oscar ambaye huishi katika nyumba moja ya kutunza wagonjwa wazee iliyopo kwenye mji wa Province katika jimbo la Rhode Island nchini Marekani hupenda kuzungukazunguka toka chumba kimoja hadi kingine katika nyumba hiyo.

Inadaiwa kuwa Paka Oscar huwa hapendi kutumia muda wake pamoja na vikongwe katika nyumba hiyo isipokuwa wale tu ambao wanakaribia kufariki.

Tabia ya paka huyo ambaye hivi sasa ana umri wa miaka mitano, iligunduliwa mwaka 2007 na manesi wa nyumba hiyo ambao kwa jinsi walivyo na uhakika na uwezo wa paka Oscar huwataarifu familia ya mgonjwa anayezungukiwa sana na paka huyo kuwa mambo yanaelekea kuwa mabaya.

Katika kuonyesha uwezo wa paka huyo, siku moja manesi walimchukua paka huyo na kumweka kwenye kitanda cha mgonjwa ambaye waliamini atafariki dakika yoyote ile, lakini paka huyo alichoropoka na kukimbilia chumba cha pili yake.

Uamuzi wa paka Oscar ulijionyesha siku hiyo hiyo kwa mgonjwa wa chumba cha pili kufariki siku hiyo hiyo jioni wakati mgonjwa wa chumba cha kwanza aliendelea kuishi kwa angalau siku mbili kabla ya kufariki paka Oscar akiwa amerudi pembeni ya kitanda chake.

Wataalamu hivi sasa wanamfanyia uchunguzi paka huyo ambaye alianza kulelewa kwenye hospitali hiyo tangia alipokuwa kichanga.

Mmmoja wa wanasayansi anayemfanyia uchunguzi paka huyo, Dr David Dosa, ameelezea mshangao wake kwa uwezo wa paka huyo kutabiri bila kukosea vifo vya wagonjwa 50 katika kipindi cha miaka mitano.

Dokta Dosa anasema kuwa hakuna maelezo yoyote ya kisayansi kuelezea tabia ya paka huyo.

Katika tukio jingine, mwanaume mmoja aliyetajwa kwa jina la Richards aliamua kukaa pembeni ya kitanda cha mama yake muda wote baada ya madaktari kumwambia kuwa mama yake aliyekuwa mgonjwa mahututi angefariki muda wowote ule.

Richard bila kupumzika alikaa pembeni ya kitanda cha mama yake kwa siku tatu mfululizo lakini mama yake hakufariki.

Madaktari walimshauri Richard aende nyumbani kwake akapumzike kidogo kabla ya kurudi baadae. Richard kwa shingo upande alikubali kuondoka kwenda kwake kupumzika.

Muda mfupi baada ya kuondoka, mama yake alifariki. Hakufariki akiwa peke yake bali Oscar alikuwa pembeni yake.

source nifahamishe

Mashine ya Kuwatawadhisha Waislamu Yavumbuliwa nchini Malaysia

Tuesday, February 02, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kampuni moja nchini Malaysia imevumbua mashine ambayo itakuwa ikiwatawadhisha waislamu kabla ya sala ambayo inatumia maji kiasi cha lita 1.3 tu.
Mshine hiyo imevumbuliwa na kampuni ya nchini Malaysia ya AACE Technologies kwaajili ya kuwasaidia waislamu kutia udhu bila kutumia maji mengi.

Mashine hiyo inatumia misingi yote ya sheria za kiislamu katika kutawadha na imepitishwa na serikali ya Malaysia kutumia kuwatawadhisha watu.

Mashine hiyo yenye urefu wa mita 1.65 inayojulikana kama "The Auto Wudu Washer" inatumia mabomba yenye sensor kumtawadhisha mtu mmoja katika hali ya kusimama kwa kutumia lita 1.3 tu.

Mashine hiyo itasaidia kupunguza upotevu wa maji wakati wa kutawadha ambapo kawaida bomba huachwa wazi muda wote wakati wa kutia udhu, alisema mwenyekiti wa AACE, Anthony Gomez.

Kuna waislamu zaidi ya bilioni 1.7 duniani ambapo asilimia kubwa ya waislamu wapo Afrika na mashariki ya kati ambako kuna uhaba wa maji.

Mashine hiyo imepokelewa vizuri katika nchi tajiri za kiarabu ambazo zimeelezea mpango wa kuzinunua mashine hizo.

Mashine hizo mbali ya kumtawadhisha mtu, humwezesha mtu anayetawadha kusikiliza quran huku akitawadhishwa.

"Wakati wa Hija, watu milioni 2 hutumia lita milioni 50 za maji kwa siku moja kwaajili ya udhu, kwa kutumia mashine hizi wangeweza kuokoa lita milioni 40 kwa siku", alisema Gomez.

Dubai ina mpango wa kunua mashine hizo na kuzitumia kwenye viwanja vyake vya ndege kwaajili ya misikiti iliyopo kwenye viwanja hivyo.

source nifahamishe

Mwanamke Ajilipua nchini Iraq na Kuua Watu 54

Tuesday, February 02, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke aliyekuwa ameficha mabomu ndani ya nguo zake, amejilipua katika mkusanyiko wa waumini wa kiislamu wa dhehebu la shia nchini Iraq na kupelekea vifo vya watu 54 na wengine 117 kujeruhiwa.
Mwanamke huyo akiwa ameyaficha mabomu kwenye nguo zake alifanikiwa kuingia kwenye hema la wanawake na watoto na kujilipua.

Jumla ya watu 54 wameishafariki kutokana na shambulio hilo na wengine 117 wamejeruhiwa.

Tukio hilo lilitokea wakati waumini wa Shia walipoweka kambi ya muda ya mapumziko kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea mji wa Karbala uliopo kilomita 110 toka Baghdad.

Asilimia kubwa ya watu waliofariki na waliojeruhiwa ni akina mama na watoto ambao walikuwa kwenye hema moja na mwanamke huyo.

Maelfu ya waumini wa Shia walikuwa wakiandamana wakitembea kuelekea kwenye mji wa Karbala kwaajili ya ibada za Shia za kuomboleza kifo cha mjukuu wa mtume Muhammad (s.a.w), Hussein ambaye alifariki kwenye karne ya 7 katika vita vya Karbala.

Maelfu ya waumini wa Shia toka nchi mbali mbali duniani walijumuika katika ibada hiyo.

Tukio la kujilipua la mwanamke huyo limetokea huku walinzi 30,000 wa Iraq wakishiriki kuimarisha usalama kwenye ibada hizo.

Hata hivyo waumini wa Sunni wanye kupingana na Shia wamekuwa wakifanikiwa kujipenyeza na kusabababisha maafa kila mwaka wakati wa mkusanyiko wa ibada hizo.

source nifahamishe

Kibonge wa Dunia Apungua Kilo 127,Lakini Bado Anaongoza

Tuesday, February 02, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mtu mnene kuliko wote duniani amepungua kilo 127 baada ya kufanyiwa operesheni ya kuokoa maisha yake lakini bado ameendelea kutambulika kama mtu mnene kuliko wote duniani kwa kilo zake 311 zilizobaki.
Baada ya kupungua kilo 127, Mtu mnene kuliko wote duniani, Muingereza Paul Mason hivi sasa ana uzito wa kilo 311 na ameendelea kushikilia taji la unene duniani.

Mason mwenye umri wa miaka 48, alitumia mwisho wa wiki kwenye kitanda cha kitengo maalumu cha hospitali baada ya kufanyiwa operesheni kubwa ya kumzuia kuendelea kunenepa na kuondolewa kwa mafuta kwenye tumbo lake.

Katika operesheni hiyo tumbo la Mason lilipasuliwa na kutengenezwa kisehemu kidogo kama pochi kwaajili ya kuhifadhi chakula chake.

Kwa maana hiyo chakula chake chote hivi sasa kitaenda kwenye hicho kipochi na hivyo kumfanya awe anakula kiasi kidogo sana cha chakula.

Wiki iliyopita madaktari walimuingiza Mason kwenye diet ya nguvu ya kuupunguza unene wake ili aweze kuwa fiti kwaajili ya operesheni.

Mason ameelezea nia yake ya kupunguza uzito wake zaidi ili aweze kuendesha gari.

Mwaka 2002 kutokana na unene wa Mason, Zimamoto iliwabidi waubomoe ukuta wa chumba chake na kisha kutumia forklift ili kuweza kumbeba na kumwingiza kwenye ambulansi kumwahisha hospitali kwaajili ya operesheni ya hernia.

Wakati huo alikuwa na uzito wa kilo 355, aliwaambia madaktari kuwa anataka kupunguza uzito wake lakini alianza kula sana ili kuvunja rekodi ya dunia awe mtu mnene kuliko wote duniani.

Hatimaye mwaka jana alifanikiwa kuvunja rekodi hiyo kwa kufikisha uzito wa kilo 444 na kumfunika kibonge wa dunia wa wakati huo toka Mexico, Manuel Uribe ambaye aliamua kupunguza uzito wake ili aweze kumuoa mpenzi wake.

source nifahamishe

Uvaaji Wako wa Suruali Hudhihirisha Umri Wako

Tuesday, February 02, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti uliofanyika hivi karibuni, uvaaji wa suruali wa mwanaume huendana na umri alio nao, wakati vijana wengi hushusha suruali zao chini ya makalio wanaume wanaoanza kuzeeka huzipandisha suruali zao juu ya kiuno.
Utafiti uliofanywa na watafiti wa Uingereza umedhihirisha kuwa kuna uhusiano wa uvaaji wa suruali wa mwanaume na umri wake.

Paul Baldwin, mkurugenzi wa nguo za kiume katika duka kubwa la nguo na vipodozi la Debenhams, la nchini Uingereza ambalo liliendesha utafiti huo, alisema kuwa kuna uhusiano wa mkubwa kati ya uvaaji wa suruali wa mwanaume na umri wake.

Watoto chini ya miaka 12 kawaida huvaa suruali zao kwenye usawa wa kiuno kwakuwa kwa umri huo hununuliwa nguo na wazazi wao na wakati mwingine kuvalishwa na wazazi wao.

Wanapofikisha umri wa kati ya miaka 16 na 26 huanza kuwaiga waimbaji wa Hip Hop wa Marekani na kuanza kuvaa suruali zao chini ya makalio. (kata K).

Mwanaume anapokuwa na umri kati ya miaka 27 na 39 huanza kuvaa suruali kwa jinsi inavyotakiwa iwe usawa wa kiuno. Miongoni mwa sababu zinachongia kumfanya mwanaume aanze kubadilika ni masuala ya kazi au kuoa.

Mwanaume anapofikisha umri wa miaka 45, kama vile dalili ya kuanza kwa uzee, suruali nayo huanza kupanda juu na kuvaliwa nchi mbili juu ya kiuno. Suruali huendelea kupandishwa juu ya kiuno na kufikia inchi 5 mwanaume anapofikisha umri wa miaka 57.

Kuanzia umri wa miaka 65, kiuno cha mwanaume huanza kunywea ndani na hivyo kuifanya suruali ianze kushushwa chini taratibu hadi kufikia usawa wa inchi moja tu juu ya kiuno mwanaume anapofikisha umri wa miaka 75.

Utafiti huu ulifanywa kwa kushirikisha jumla ya wanaume 1,000.


source nifahamishe

Daktari mbaroni kwa kudaiwa kubaka mgonjwa

Tuesday, February 02, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

DAKTARI wa Hospitali ya Marie Stoppers iliyopo Mwenge, jijini Dar es Salaam, Paul Andrew ametiwa mbaroni kwa tuhuma za kudaiwa kumbaka mgonjwa aliyefika hospitalini hapo wakati akimpatia matibabu
Ilidaiwa kuwa mgonjwa huyo alifika hospitalini juzi, majira ya jioni kwa lengo la kupatiwa matibabu wakati alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa tumbo na alifika kwa ajili apatiwe uchunguzi wa kina ili tatizo lake liweze kugundulika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga alithibitisha kuwa mgonjwa huyo alifika hospitalini hapo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kina wa tumbo llilokuwa likimsumbua.

Alisema alipofika hapo alikutana na daktari huyo aliyetambulika kama Dk. Andrew na alimwandikia afanyiwe kipimo cha Utra Sound ili aweze kugundulika tatizo lake.

Kalinga alisema alithibitisha tukio hilo kwa mujibu wa maelezo ya mgonjwa

Alisema baada ya mgonjwa huyo kuingia katika chumba cha kufanyiwa kipimo hicho ndipo daktari huyo alimpa kitu kilichomfanya alale kwa muda na nguvu ya dawa ilipokwisha alishtuka na kumkuta daktari huyo akiendelea kumbaka.

Alisema mgonjwa huyo alipozinduka na kujikuta akibakwa na daktari huyo alijinasua na alitoka nje na kukimbilia Kituo cha Polisi Mabatini kilichopo Kijitonyama na kufungua jalada lenye namba RB/KJN/123/552/10.

Alisema mgonjwa huyo aliongozana na askari wa kituo hicho hadi hospitalini na kumkamata mtuhumiwa aliyekuwa bado yupo eneo hilo.

Kamanda Kalinga alizidi kutoa maelezo hayo kuwa, kutokana na maelezod ya utatanishi wa mgonjwa huyo ilibidi jeshi hilo apelekwe kufanyiwa vipimo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kubaini kama kweli alifanyiwa unyama huo.

Baada ya vipimo kufanyika iligundulika alifanywa na mtuhumiwa anashikiliwa na polisi

source nifahamishe

Jerry Muro na sakata lake la rushwa..............

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia Mtangazaji wa Shirika la Habari Tanzania (TBC) Jerry Muro (pichani juu kulia) kwa tuhuma za kudai fedha kwa njia ya vitisho.

Muro anadaiwa kumtisha aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo Michael Wage ambaye hivi karibuni alisimamishwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa tuhuma za ubadhilifu pamoja na viongozi wengine wa Halmahauri ya Wilaya Bagamoyo.

Akithibitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo Suleimani Kova alikiri jeshi lake kumshikilia Muro na kuwa alimtishia Wage kuwa yeye ni Ofisa wa Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) na kumtaka atoe fedha Sh milioni 10.

“Polisi inamhoji Muro dhidi ya tuhuma hizo na mahojiano yakikamilika taratibu za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na maelezo zaidi nitayatoa kesho wakati wa mazungumzo yangu na waandishi wa habari” Kova alisema.

Aidha blogu ya Watu ilimwona Bingwa huyo wa Tuzo za Uandishi wa Habari 2009 Tanzania akiwa polisi na mkononi ameshikilia bahasha tatu pamoja na kamera ya Video.

Ilipomhoji juu ya kuhusika na tuhuma hizo alikana na kudai kushangazwa kuwekwa chini ya ulinzi kwa madai kuwa alipigiwa simu na mtu kupewa taarifa kuwa kuna kazi katika Hoteli ya City Garden.

“Kaka nilitaarifiwa tu kama ujuavyo kazi zetu kuwa kuna kazi City Garden niakaamua kwenda, lakini baada ya kufika tu nilishangaa nawekwa chini ya ulinzi na askari kanzu ambao ndiyo walionifikisha kituoni hapa bila ya kunitajia kosa lanmgu. ” alilonga Muro.

Kwa upande wake Wage alidai kuwa mtuhumiwa anatumiwa na watu wengine ambapo juzi alimpandisha katika gari lake na kumfunga pingu kisha kumtaka atoe Sh milioni 10 na kwa kuthibitisha kuwa alikuwa ndani ya gari hilo alidai kuacha miwani yake yenye mikanda myeusi.

Polisi ilipomhoji Muro kama anazo pingu alikiri kumiliki pingu pamoja na bastola ambapo baada upekuzi katika gari lake lenye namba za usajili T 545 BEH polisi walikuta pingu hizo pamoja miwani iliyosemwa na mlalamikaji.

Muro ameibuka kuwa mtangazaji mahari kwa mwaka 2009 hadi kujinyakulia tuzo ya Mwandishi bora wa mwaka kupitia vipindi vyake vya Televisheni vya USIKU WA HABARI vinavyorushwa katika kituo cha TBC1 kila siku na kabla ya kuhamia hapo alikuwa kituo cha ITV na aliendesha kipindi cha RIPOTI MAALUM.

Miongoni mwa mambo aliyokuwa akirusha katika vipindi hivyo ni pamoja na rushwa, matumizi mabaya ya madaraka pamoja na ukiukwaji wa sheria.

Polisi ni wahanga wakuu katika vipindi hivyo kwani mara mbili amewatoa Polisi Usalama barabarani wakiomba na kupokea rushwa hadharani kutoka kwa madereva wa malori na mabasi ya mikoani.

Serikali ya mseto yapitishwa Z'bar

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

HATIMAE Baraza la Wawakilishi Zanzibar limeidhiria hoja ya kuundwa kwa serikali ya kitaifa kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa 2010.

Hoja hiyo liyowasilishwa na kiongozi wa kambi ya upinzani Abubakar Khamis Bakari na inayotaka kuundwa kwa serikali hiyo ili kujenga umoja na maridhiano kwa Wazanzibari ambayo wamekuwa katika migogoro ya kisiasa kwa muda mrefu.

Wajumbe wa baraza hilo wote kwa sauti moja walikubaliana na suala hilo kwa kuridhia baaada ya Baraza la Wawakilishi kuwasilisha mapendekezo ya hoja binafsi ya Chama cha wananchi CUF na kujadiliwa na Mwakilishi huyo wa Jimbo la Mgogoni Pemba.

Hata hivyo kabla ya kufanyika kwa mabadiliko hayo CUF walikubali kufanya mabadiliko katika hoja zake kadhaa baada ya wajumbe wa CCM kutaka kufanyiwa mabadiko hayo ya hoja yake.

"Marekebisho ya sheria ya uchaguzi, hatua ya kutaka ridhaa ya wananchi kwa njia ya kura ya maoni, na maekebisho ya katiba endapo wananchi wataridhia uanzishwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa, yote hayo yafanywe kabla ya uchaguzi mkuu wa 2010," ilisema kipengele hicho ambacho kimekubaliwa na wote.

Katibu wa baraza la Wawakilishi, Ibrahim Mzee akisoma vipengele vilivyoridhiwa na baraza hilo alisema ni pamoja na kukubaliwa kuundwa kwa kamati ya wajumbe sita ambao watasimamia suala hilo watatu wataotoka upinzani na serikalini.

Aidha Baraza hilo alisema limekubali suala la wakuu wa mikoa waendelee kuwa wanasiasa, lakini bado wateuliwe na rais kwa kufuata uwiano wa kura za rais za vyama viliomo kwenye Baraza kwa vyama vya siasa vilivyomo humo ama waondolewe kabisa katika vyama vya siasa ili wasiwe wateuliwa wa Rais.

Nafasi ya makamu wa rais ambayo ilikuwa na utata kidogo baada baadhi ya wajumbe kuwa na wasi wasi nayo juu ya mfumo utakaotumika kuunda nafasi hiyo bila ya kuingilia vipengele vya katiba vya muungano.

Hoja hizo zilizuka baada ya wajumbe hao kuuliza iwapo nafasi hiyo ikaleta utata wa kisheria katika katiba ya muungano kwa kuwa tayari nafasi hiyo imetajwa katika nafasi ya muungano na haitawezekana kuwa makamu wa pili kutoka Zanzibar.

Hoja nyingine kuhusu suala hilo kuwepo utata pindi rais aliteteuliwa pamoja na wateuliwa wengine wakiwewa pingamizi kwa mujibu wa tume ya uchaguzi je nafasi hiyo itaweza kupatikana hivi ambapo upande wa upinzani wanapendekeza suala hilo lipelekwe kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi kwa ajili ya kuteuliwa kwa mujbu w akura.

Akijibu hoja hizo Bakari amesema haoni haja ya kuw ana wasi wasi huo kwa kuwa suala hilo litaingizwa katika mapendekezo ya marekebisho ya katiba na baadae kuwasilishwa katika kikao cha baraza la wawakilishi jambo ambalo litawapa nafasi ya ya kutoa maoni yao juu ya uendeshaji wa suala hilo.

Hata hivyo suala la hoja ya makamu wa raias wa muungano Bakari alisema hakuna utata wowote kwa kuwa huyo atakuwa ni makamu wa rais wa Zanzibar kama vilivyo afasi nyengine za mawaziri wa Zanzibar.

Awali jana wawakilishi hao walionekana kuzungumza lugha laini tofauti ya siku ya kwanza katika kuchangia hoja binafsi iliyowasilishwa na kiongozi wa kambi ya upinzani Abubakar Kahmis Bakari.

Wakichangia hoja hiyo wajumbe mbali mbali kutoka CCM na CUF walionekana kutumia busara zaidi kuliko katika michango yao tofauti kabisa na siku ya mwanzo waipokuwa wakichangia hoja hiyo kwa kuwa zaidi upande wa CCM walionekana kusimamia hoja ya Butiama zaidi kuliko kukubaliana na hoja hiyo.

Ingawa baadhi ya wajumbe wao tokea kuanza mjadala huo walionekana kulainika mapema na kuwataka wenzao watumie hekima na busara zaidi katika michango kama walivyoelekezwa na Spika wa baraza hilo, Pandu Ameir Kificho kuwataka kuwa makini zaidi na michago yao ili kujenga na kuepukana na jazba ambazo zimezoeleka katika vikao vya baraza hilo.

Mwakilishi wa jimbo la Muyuni (CCM) Ramadhani Nyonje Pandu aliwahimiza wajumbe wenzake kuona umuhimu wa hoja hiyo na kuwataka waiunge mkono na kuacha kuvutana kwani hoja hiyo ikiwachwa itaweza kusababisha matatizo makubwa nchini.

"Napenda kwa mara ya kwanza nimsifu na kumpongeza maalim Seif kwa kukomaa kwake kisiasa na ukomavu wake wa kutaka mazungumzo ya kujenga umoja, mashirikiano na utulivu katika nchi yetu," alisema Pandu.

Mwenyekiti wa baraza la wawakilishi Ali Mzee Ali (CCM) naye aliunga mkono hoja na kuwataka wajumbe wenzake waungane kwani ni kitu kizuri kilichoanzishwa na ni muhimu sana kwa kuwaunganisha Wazanzibari ambao wamekuwa katika mazungumzo na hakuna haja yoyote ya kuikata hoja hiyo ambayo lengo lake ni kuwaunganisha Wazanzibari.

"Nakuombeni sana hoja hii tuipitishe kwa ..furaha na tusiwe na pingamizi hapana pahala mazuri kama hapa serikali ya shirikisho, umoja wa kitaifa ni mhimili mkuu katika nchi na Rais Karume yeye ndio kisiwa cha amani na utulivu jina lake Amani na anapenda amani na amani ndio hii tayari,"alisema.

Mwakilishi wa jimbo la Mkanyageni (CUF), Haji Faki Shaali alisema suala la kura ya maoni linatia hofu kutokana na historia kuwepo na shaka juu ya suala hilo kwa kuwa mara nyingi kura hizo huwa hazipigwi kwa haki na inavyotakiwa na ndio maana baadhi ya watu wengine huwa hawalitaki maana linaweza kusababisha mivutano kama ile ya uchaguzi ambayo mara huwagawa wananchi.

Mwakilishi aliyeteuliwa na rais, Juma Duni Haji (CUF) alisema haiwezekani kwa Wazanzibari kila baada ya miaka mitano kwanza wapigane na wauane ndio wapate rais kwanza jambo ambalo alisema wananchi wanapaswa kulikataa suala hilo kwani linaleta hasara kubwa katika jamii.

Alisema ni vizuri kutatarishwa kwa mazingira mazuri ili kuelekea uchaguzi mkuu na bila ya hivyo ni hatari kuingia katika uchaguzi kauli ambayo iliungwa mkono na waziri wa maji, ujenzi, nishati na ardhi, Mansoor Yussuf Himid ambaye kwa upande wake alisema hakuna haja ya kukimbilia uchaguzi wakati mazingira ni mabaya.

Mwakilishi wa Gando (CUF), Said Ali Mbarouk akichangia hoja hiyo alisema mawaziri wapatikane kwa kura na ukifanywa utaratibu wa wingi wa viti huenda vyama vidogo vikateketea na kupotea kabisa kwani chama kupata asilimia 10 ya kura za rais halafu kukiwacha nje haitakuwa vyema tutakuwa na vitakavyopata asilimia 5 na 10 na kupendekeza kwamba vile viti viwili vya upinzani wapewe wao maana wakiwekwa nje watakuwa ni waangalizi katika suala la demokrasia jambo ambalo sio zuri.

source mwananchi

BEBE COOL AVUNJWA MIGUU KWA RISASI

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)



Mwanamuziki mashuhuri wa reggae nchini Uganda, Bebe Cool a.k.a Moses Sali, akiingizwa katika hospitali ya Nsambya jijini Kampala baada ya kupigwa risasi katika klabu moja jijini humo.

Kwa mujibu wa mtandao wa gazeti la The Monitor toleo la mchana huu, risasi hizo zimevunja miguu yote miwili, amesema Daktari Mratibu wa hospitali hiyo, Dk. Martin Nsubuga.

Habari zinasema risasi zilirindima katika klabu ya Effendys katika maeneo ya Centenary Park, na kwamba kuna utata wa sababu zilizopelekea purukushani hilo. Inasemekana watu wengine watatu ikiwa ni pamoja na mabaunsa wa Bebe Cool na askari wa kikosi maalum pia walijeruhiwa.

source globalpublisher

Misri Yaibanjua Ghana na Kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

Manchester Yaizamisha Arsenal 3-1

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Manchester United imepunguza pengo la pointi kati yake na vinara wa ligi ya Uingereza, Chelsea kwa kuibanjua Arsenal magoli 3-1 kwenye uwanja wake wa Emirates.

Winga wa Manchester United toka Ureno, NANI ndiye aliyekuwa mwiba mkali kwa mabeki wa Arsenal katika mechi ya leo.

Katika dakika ya 35, Nani baada ya kuwaramba chenga wachezaji watatu wa Arsenal alimimina majaro kati lakini kipa wa Arsenal, Manuel Almunia, aliusindika mpira huo kwenye nyavu zake katika harakati za kuuokoa.

Dakika nne baadae Nani tena alimpa pasi nzuri sana Wayne Rooney ambaye hakufanya ajizi kuiandikia Manchester goli la pili ambalo lilikuwa ni goli lake la 100 katika ligi ya Uingereza.

Mkorea Park Ji-Sung alipigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Arsenal kwenye dakika ya 52 baada ya kuambaa na mpira karibia nusu ya uwanja na kuachia shuti lililojaa kwenye ubavu wa kulia wa nyavu za Arsenal.

Wakati washabiki wa Arsenal wakianza kutoka uwanjani dakika 15 kabla ya mechi kuisha, Thomas Vermaelen aliipatia Arsenal goli la kufutia machozi kwenye dakika ya 80.

Akiongea baada ya kichapo hicho, kocha wa Arsenal, Arsene Wenger aliwataka wachezaji wake kukusanya nguvu zao tena na kulipa kisasi kwa kuilaza Chelsea watakapokutana siku ya jumapili.


source nifahamishe

Akamatwa na Kimada, Apigwa Faini ya Nyati Wanne

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mahakama ya kikabila ya nchini Malaysia imeamuaru mwanaume aliyefumaniwa na mkewe akiishi na kimada, alipe faini ya nyati wanne na nguruwe mmoja.
Mahakama ya kikabila katika jimbo la Sabah katika kisiwa cha Borneo nchini Malaysia imemuamuru mwanaume pamoja na kimada wake walipe faini ya nyati wanne na nguruwe mmoja kwa kuishi kinyumba bila kuoana.

Kwa mujibu wa gazeti la The Star la nchini Malaysia, mwanaume huyo na kimada wake walipatikana na hatia ya kuishi pamoja bila kuoana.

Mke wa mwanaume huyo, alipeleka malalamiko kwenye mahakama ya kikabila ya mji wa Penampang akisema kuwa mumewe amekuwa akiisaliti ndoa yake na kwenda kuishi pamoja na kimada huyo.

Jaji William Sampil alisema kuwa mahakama imepata ushahidi wa kutosha kumtia hatiani mwanaume huyo na kimada wake pamoja na kujitetea kwao kuwa wao ni marafiki tu.

Jaji huyo aliamuru mwanaume huyo na kimada wake walipe fidia ya nyati wanne na nguruwe mmoja pamoja na pesa taslimu sawa na dola 600.

Taarifa ya mahakama haikuweka wazi kama nyati hao wanatakiwa kutolewa wakiwa hai au la.

Utawala wa kikabila unachukua asilimia moja tu ya watu wote milioni 28 wa nchini Malaysia.

source nifahamishe

Kufanya Operesheni Ili Afanane na Supastaa wa Marekani

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Ili kumfanya mpenzi wake wa zamani amrudie tena, mwanamke mmoja wa nchini China anafanya operesheni ya kuubadilisha mwili wake ili afanane na nyota wa Marekani, Jessica Alba.
Mwanamke mwenye umri wa miaka 21 aliyejitambulisha kwa jina la Xiaoqing wa nchini China ameamua kufanya operesheni ya kuubadilisha mwili wake ili afananane na mcheza sinema wa Marekani, Jessica Alba.

Mwanamke huyo aliliambia gazeti la Shanghai Daily kuwa ameishakutana na madaktari wa operesheni za urembo wa mjini Shanghai ambao wamemuahidi watamfanyia operesheni hiyo bure.

Xiaoqing aliliambia gazeti hilo kuwa atafanya operesheni za kuubadilisha mwili wake ili afanane na Jessica Alba kwakuwa mpenzi wake wa zamani anampenda sana mcheza sinema huyo hivyo anaamini kuwa atakapofanana naye basi mpenzi wake atamrudia.

Afisa wa hospitali ya Shanghai Time Plastic Surgery Hospital, ambayo Xiaoqing atafanyiwa operesheni zake alisema kuwa Xiaoqing atafanyiwa bure operesheni za kurekebisha kope na nyusi za macho yake pamoja na operesheni ya pua yake ili aweze kufanana na Jessica Alba ambaye alitamba kwenye "Sin City" na "Fantastic Four".

"Hakuna wasiwasi wa malipo, operesheni inawezekana kufanyika", alisema afisa huyo na kuongeza "Inabidi afahamu kuwa hataweza kuirudia sura yake ya zamani baada ya operesheni".

Xiaoqing alisema kuwa mpenzi wake huyo wa zamani anampenda sana Jessica Alba kiasi cha kwamba kwenye ukuta wa chumba chake ameweka picha yake kubwa na hata kwenye simu yake kuna picha za msanii huyo maarufu wa Marekani.

Xiaoqing aliongeza kuwa mpenzi wake huyo alikuwa akimlazimisha ajipodoe kama Alba na alimnunulia wigi ambalo alimtaka alivae wakati wote. Xiaoqing alisema kuwa uhusiano wao ulivunjika baada ya kuamua kulivua wigi hilo na kulitupa.

"Nampenda sana ndio maana nafanya hivi... sitaki kumpoteza ", alimalizia kusema Xiaoqing.

source nifahamishe

Akataliwa Kubadili Dini, Atishia Kujiua

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)

MSICHANA mmoja [24] [jina kapuni] mkazi wa Mikocheni B, mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amejikuta akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kuitaarifu familia yake kuwa atakunywa sumu baada ya kukataliwa na wazazi wake kubadili dini ili aoane na mpenzi wake.
Chanzo chetu cha habari kilisema kuwa kasheshe lilianza baada ya msichana huyo kuwataarifu wazazi wake kuwa amepata mchumba na yuko tayari kubadili dini yake ili aweze kuoana naye.

Lakini wazazi wake walimkatalia kwa kuwa walikuwa wametofautiana kwa imani za kidini.

Wazazi wa msichana huyo waliweka wazi kuwa hawako tayari kuona binti yao akibadili dini ili aone na mpenzi wake huyo.

Msichana huyo alionekana kutoridhika na uamuzi wa wazazi wake hao na baada ya siku chache kupita aliwaambia wazazi wake hao kuwa hataweza kumkosa mpenzi wake huyo aliyempenda kwa moyo wake wote na kwa kuwa hawataki aoane naye basi atakunywa sumu ili aiage dunia.

Kutokana na tamko hilo kikao cha dharura cha familia kiliitishwa na walio wengi katika kikao hicho walitoa tamko kuwa hawako tayari ndugu yao abadili dini.

Msichana huyo naye alitoa tamko mbele ya kikao hicho kuwa atakunywa sumu pamoja na baadhi ya wanafamilia kumsihi asifanye hivyo kwa kuwa angeweza kupata mchumba mwingine wa dni yake.

Msichana huyo aliingia chumbani kwake akitishia kutafuta sumu ili ajiue na kupelekea baadhi ya wanafamilia kwenda kutoa tarifa kituo cha polisi.

Polisi walimkamata msichana huyo na kumpeleka kituoni huku wazazi wake na wanafamilia wengine wakiitisha kikao kingine kujadili sakata hilo.

source nifahamishe

Rais wa Afrika Kusini Amtia Mimba Binti wa Rafiki Yake

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ambaye ana jumla ya wake watatu amemtia mimba binti wa rafiki yake wa karibu.
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amepata mtoto wa 20 baada ya kumtia mimba binti wa rafiki yake wa karibu ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Gazeti la Sunday Times la Afrika Kusini limeripoti leo kuwa Zuma alimpachika ujauzito Sonono Khoza ambaye ni binti wa Irvin Khoza, mmiliki wa timu ya Orlando Pirates.

Sonono mwenye umri wa miaka 39 alijifungua mtoto wa rais Zuma mwenye umri wa miaka 67 mwezi oktoba mwaka jana.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, baba yake Sonono amehuzunishwa sana na kitendo cha Zuma kumtia mimba binti yake.

Khoza aliiambia familia yake kuwa anahisi amesalitiwa na Zuma ambaye alikuwa akimchukulia kama rafiki yake wa karibu sana.

Gazeti hilo liliendelea kusema kuwa mwezi disemba mwaka jana, wawakilishi wa rais Zuma waliitembelea familia ya Khoza katika mji wa Soweto na kujadiliana nao malipo ya kitamaduni ya kumzalisha mwanamke nje ya ndoa (inhlawulo).

Rais Zuma alikutana na Sonono na mama yake mwanzoni mwa mwezi huu kulijadili zaidi suala hilo.

Zuma hivi sasa anaishi na jumla ya wake watatu na amewahi kufunga ndoa jumla ya mara ya tano.

Mtoto wa Sonono amekuwa mtoto wa 20 katika idadi kubwa ya watoto wa rais Zuma.

source nifahamishe