RIYAMA ALLY KUSHUKA NA FILAMU YA DNA

Saturday, November 13, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


MUIGIZAJI bora wa kike kupitia tuzo za Risasi Award 2005/ 2006 Riyama Ally yupo location akirekodi filamu inayokwenda kwa jina la DNA, msanii huyu mahiri katika kuigiza filamu za kusikitisha amekuwa kivutio pale anapocheza katika filamu za uzuni, ameiambia filamucentral kuwa kwa sasa anatarajia kuwashika wapenzi wa filamu hapa nchini.

“Unajua siku hizi watazamaji ni werevu kwa hiyo unapocheza lazima uhakikishe unafikia viwango vya juu ili uendelee kuongeza wapenzi wa filamu zako unazocheza, maana wasanii tupo wengi kwa sasa kwa hiyo ukimpoteza mtazamaji mmoja kumrudisha ni kazi, kazi yoyote nitakayoshiriki lazima nipige msuri wa nguvu”
Alisema mwanadada huyo.
Filamu ya DNA inaandaliwa na kampuni ya Sam Enterprises ya jijini Dar filamu hii ambayo ipo katika hatua za mwisho katika uhariri imeongozwa na Seleman Abass Mkangara na kushirikisha nyota wengine kibao.

Aidha Riyama amesema kuwa vile vile yupo katika maandalizi ya filamu zake mpya mbili ambazo anatarajia kuanza kurekodi wakati wowote kuanzia sasa, Riyama ni muigizaji mtunzi na mtayarishaji pia, filamu alizotayarisha ni pamoja na filamu iliyofanya vinzuri soko ya Mwasu.

source filamucentral

film za maigizo zinalipa kweli kweli...............

Saturday, November 13, 2010 / Posted by ishak / comments (0)




Katika Kuonyesha kuwa ni wazi kwamba Tasnia ya filamu Tanzania inakua na kwamba ni muhimu kuwekeza katika tasnia hii, Leo tumemkuta Steven Kanumba akiwa na Gari lake ambalo ni mahususi kwa ajili ya Production na masuala yote ya utayarishaji wa filamu zake.

Kanumba katikati ya mwaka huu alifungua rasmi kampuni yake na kuweka ofisi katika mitaa ya sinza, Hii kweli inavutia na inakupa fikra kwamba kama huyu anafanya hivi ni kwa sababu gani? Je ni kwamba wadau wanamkubali na kumuwezesha!!!? BIG UP Kanumba, tunamatumani tutaona wengine mkirasimisha utendaji wenu wa kazi.

liverpool once again................

Sunday, November 07, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Liverpool continued their recent resurgence as Fernando Torres scored both goals in a 2-0 victory over leaders Chelsea at Anfield.