Ajaribu Kumtorosha Mfungwa Kwa Kutumia Begi

Tuesday, July 05, 2011 / Posted by ishak / comments (0)




Mfungwa Juan Ramirez Tijerina akiwa amejificha ndani ya begi akijaribu kutoroka jela Tuesday, July 05, 2011 6:54 PM
Mwanamke mmoja wa nchini Mexico ameingia matatani baada ya jaribio lake la kumtorosha mumewe toka jela kwa kumdumbukiza ndani ya begi na kisha kujaribu kulikokota begi hilo kutokana nalo nje ya jela.
Maafisa jela katika jela ya Chetumal nchini Mexico jana walipigwa na bumbuwazi baada ya kumkamata mwanamke akijaribu kumtorosha mumewe toka jela kwa kumficha ndani ya begi.

Walinzi wa jela hiyo walimuona Maria del Mar Arjona mwenye umri wa miaka 19, akionekana mwenye wasiwasi wakati akitoka nje ya jela huku akilikokota begi ambalo lilionekana limetuna sana.

Walipomsimamisha na kulichunguza begi hilo hawakuamini macho yao walipomuona mfungwa Juan Ramirez Tijerina akiwa amejikunja kama vile mtoto akiwa tumboni mwa mama yake.

Maria aliingia na begi hilo jela wakati alipopewa nafasi ya kumtembelea Juan ambaye anatumikia kifungo chake ndani ya jela hiyo.

Juan alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 20 jela baada ya kutupwa jela mwaka 2007 alipopatikana na hatia ya kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Maria alitiwa mbaroni wakati akisubiri kufikishwa mahakamani.



source nifahamishe

SEMINA YA VITAMBULISHO KWA WAWAKILSHI

Sunday, July 03, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili na Vitambulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana,(kulia) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Sei Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili na Vitambulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana,(kulia) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Sei Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya utambuzi na usajili wa Vitambulisho vya Taifa, Dickson Maina,akizungumza akitoa taarifa kuhusiana na mamlaka ya vitambulisho wakati wa ufunguzi wa Semina kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi iliyofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein
Baadhi ya watendaji wa Mamlaka ya utambuzi na usajili wa vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakisikiliza kwa makini hotuba iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu Utambuzi wa usajili wa Vitmbulisho vya Taifa,katika ukumbi wa Ocean View Hotel Kilimani Zanzibar jana
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein akitoa hotuba yake katika ufunguzi wa Semina ya wajumbe hao inayohusu usajili wa vitambulisho vya Taifa,iliyoandaliwa na Mamlaka ya Utambuzi na Usajili vitambulisho vya Taifa,(NIDA) katika ukumbi wa Ocean View Hoteli Kilimani Zanzibar


source othman mapara blog

Radi Yaua Wanafunzi 18 Shuleni Uganda

Saturday, July 02, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Radi iliyopiga kwenye shule moja ya msingi nchini Uganda, imewaua watoto 18 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 50.
Radi hiyo iliyopiga kwenye shule ya msingi ya Runyanya katika wilaya ya Kiryandongo magharibi wa jiji la Kampala, imepelekea vifo vya wanafunzi 15 wa kike na watatu wa kiume.

Msemaji wa polisi, Judith Nabakooba alisema kuwa zaidi ya wanafunzi wengine 50 walijeruhiwa na radi hiyo.

“Baadhi ya wanafunzi waliojeruhiwa waliwahishwa hospitali za karibu lakini wanafunzi 15 waliojeruhiwa vibaya sana waliwahishwa kwenye hospitali kuu ya wilaya”, alisema Nabakooba.

Magazeti ya kila siku ya Uganda yaliripoti kuwa wanafunzi wengine 21 katika shule nyingine iliyopo kwenye wilaya ya Zombo, nao walijeruhiwa vibaya baada ya kuunguzwa na radi.

Wakati gazeti la The Daily Monitor likiripoti jumla ya wanafunzi 28 wameishafariki kutokana na radi tangu wiki iliyopita, msemaji wa polisi hakutoa idadi kamili ya wanafunzi waliofariki kutokana na radi katika msimu huu wa mvua zilizoambatana na radi



source nifahamishe

Ukiwa Mchungaji Kanisani Nigeria, Utajiri Nje Nje

Thursday, June 23, 2011 / Posted by ishak / comments (0)



Mchungaji tajiri kuliko wote Nigeria, Mchungaji David Oyedepo

Uchunguzi uliofanywa nchini Nigeria umebaini kuwa wachunga kondoo wa Bwana nchini humo mbali ya kuhubiri neno la bwana wanatengeneza pesa ya maana kiasi cha kwamba baadhi yao wanamiliki ndege, hoteli na biashara kubwa.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Muandishi wa Nigeria wa jarida la Marekani la masuala ya uchumi, Forbes, wahubiri wa neno la bwana nchini Nigeria wanatengeneza pesa sana kutokana na uchungaji kiasi cha kufanananishwa na matajiri wa biashara ya mafuta.

Mfonobong Nsehe akitoa ripori ya uchunguzi wake alisema kuwa wachungaji wa Nigeria wanaishi maisha ya kifahari na wana miradi mikubwa ya kibiashara.

"Kuhubiri ni biashara inayolipa sana, sawa sawa na biashara ya mafuta", alisema Nsehe.

Utajiri wa wachungaji watano maarufu nchini Nigeria unakadiriwa kufikia dola milioni 200, alisema Nsehe.

Makanisa mengi yameibuka nchini Nigeria na waumini wamekuwa wakiongezeka.

Nsehe alisema kuwa mchungaji tajiri kuliko wote ni Mchungaji David Oyedepo wa kanisa la Living Faith World Outreach Ministry, ambaye utajiri wake ni dola milioni 150.

Mchungaji Oyedepo ndiye anayeshika nafasi ya pili akimiliki ndege nne, kampuni ya uchapishaji, chuo kikuu na shule moja na majumba ya kifahari jijini London na Marekani.

Mchungaji Chris Oyakhilome wa kanisa la Loveworld Ministries ana utajiri unaokadiriwa kuwa kati ya dola milioni 30 na 50. Mchugaji Oyakhilome anamiliki kampuni ya magazeti na majarida, stesheni ya televisheni, hoteli na kampuni ya majumba.

"Wachungaji hawa wanaishi maisha ya kifahari utawaona kwenye ndege zao binafsi na magari ya kifahari", alisema Nsehe.

Wachungaji wengine walioingia kwenye listi ya utajiri ni mchungaji Temitope Joshua Matthew mwenye utajiri kati ya dola milioni 10 na 15, Mchungaji Matthew Ashimolowo dola milioni 6-10, na mchungaji Chris Okotie mwenye utajiri kati ya dola milioni 3-10.

Nsehe aliongeza kuwa wawakilishi wa wachungaji wote isipokuwa mchungaji Ashimolowo, wamethibitisha taarifa ya umiliki wa mali za wachungaji hao.


source nifahamishe

Mfanyabiashara maarufu Zanzibar atinga kizimbani

Sunday, June 19, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Mfanyabiashara maarufu mjini Zanzibar Suleyum Mbarak Salim (35) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuiibia Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Sh bilioni 2.7.
Mfanyabiashara huyo, maarufu kama Morgan alisomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu, Amisa Suleima Hemed wa Mahakama ya mkoa mjini Magharibi Unguja jana.
Mwendesha mashtaka wa serikali, Maullid Mkame alisema mshtakiwa huyo anadaiwa kuiibia benki ya watu wa Zanzibar kati ya Machi 12 na Mei 11, 2009.
Alisema kwamba mstakiwa aliiba dola za Marekani 122,000 sawa na sh bilioni 2.7, ikiwa ni mali ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kitendo ambacho ni kinyume na sheria namba 6 kifungu namba 124 (1) (4) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ya mwaka 2004. Mshtakiwa alikana shtaka hilo ambapo wakili anayemtetea Suleiman Salum aliomba mteja wake kupatiwa dhamana kwa vile shtaka alilofunguliwa ni miongoni mwa makosa yenye dhamana na haki yake kwa mujibu wa katiba.
Salum alisema kwamba mshtakiwa hajawahi kuhusishwa na mashtaka yoyote au kutiwa hatiani kwa kosa lolote na kuomba hakimu kumpatia dhamana mteja wake kwa vile ana mali zisizohamishika.
Hata hivyo, mwendesha mashtaka, Maulid Makame alisema kwamba kwa muda mrefu, mshtakiwa huyo alikuwa akisakwa baada ya kuhusishwa na kesi namba 115 inayohusu wizi katika benki hiyo ya Zanzibar iliyofunguiliwa mwaka 2009 na kuwahusisha wafanyakazi wawili wa benki hiyo.
Alisema kitendo cha kumpa dhamana kinaweza kuathiri upelelezi hasa kwa kuzingatia uchunguzi wa suala hilo haujakamilika na mshtakiwa alikuwa anasakwa muda mrefu.
Hata hivyo, Hakimu Amisa alisema atatoa uamuzi juu ya ombi la dhamana Juni 23, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena katika mahakama ya Vuga mjini Zanzibar.



source ippmedia

UZURI WA KUMSAMEHE MPENZI WAKO............

Sunday, June 12, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Ni vizuri kusamehe na kusahau ili uweze kuishi maisha ya furaha na amani.

Katika maisha inapotokea kuna mtu amekukera inawezekana akawa ni mwenza wako lakini baadaye akakuomba msamaha kwa kile alichokosea kama kweli umeamua kumsamehe basi ni vizuri kujiepusha kuwa na kinyongo yaani ile hali ya kusamehe huku bado moyoni kile kitu unacho kinakusumbua na wakati mwingine labda unayo nia ya kulipiza kisasi au bado unapenda kuzungumzia makosa ya zamani wakati ulishasamehe haipendezi kuwa na tabia ya kutosahau baada ya kusamehe kwani hata wewe mwenyewe binafsi unakuwa hujitendei haki kwani unajidanganya na pia utaendelea kuuumia kutokana na kushindwa kusahau naamini huwa inakuwa ni vigumu kusahau kulingana na uzito wa kosa lakini kama umeamua kusamehe basi samehe kwa moyo wako wote ili uweze kuwa huru na yule umpendaye .

MAZINGIRA USIYOTAKIWA KABISA KUANZISHA UHUSIANO KIMAPENZI

Tuesday, June 07, 2011 / Posted by ishak / comments (0)

Wengi kati ya watu ambao hukumbwa na majuto ya “ningejua nisingemkubali” ni wale wanaoanzisha uhusiano wa kimapenzi kwenye mazingita yasiyostahili.
Wataalamu wa mapenzi wanasema, penzi sahihi lazima liambatane na wakati muafaka wa kufanya hivyo. Ukikosea katika kupima mazingira unakuwa kwenye asilimia 80 za kuchagua mtu asiyekufaa maishani mwako.
Leo kwa kutambua umuhimu wa mada hii nimeona niwaletee mazingira ambayo hayafai mtu kuanzisha uhusiano wa kimapenzi, lengo langu likiwa ni kuweka umakini katika kuchagua na kuondoa, kupunguza majuto ya kuumizwa na mapenzi.


KWENYE MGOGORO
Uchunguzi unaonesha kuwa asilimia 60 -70 ya wapenzi huanzisha uhusiano mpya wa kimapenzi nyakati za migogoro baina ya wapendanao kwa lengo la kupoza maumivu.
Msomaji wangu, ni jambo la hatari sana kuanzisha uhusiano kwenye mazingira ya mgogoro kwani utakapofanya hivyo utapoteza umakini na hivyo kujikuta ukijiingiza kwenye uhusiano usiokuwa na faida ya baadaye kwako.

UKIWA NA HISIA KALI
Kama binadamu kamili kuna wakati tunakuwa kwenye msukumo mkubwa wa hisia za kimapenzi, kila umuonaye anaweza kukushawishi si kwa sababu anakufaa lakini njaa ya penzi isiyohitaji kuchagua itakuwa inakusukuma kujishibisha hata kwa maganda.
Epuka kabisa kusukumwa na mhemko wa mwili, usikubali kuwa mtumwa wa hisia kwani utajikuta umempa penzi mtu ambaye hata wenzako watashangaa jinsi ulivyoangukia pua.

UNAPOKUWA UMELEWA
Mazingira ya ulevi ni hatari sana, watu wengi hufanya ngono zembe bila kuangalia madhara yake wakati wakiwa wamelewa. Nashauri kwamba, unapokwenda baa jambo la kwanza kabisa unalotakiwa kulihifadhi kwenye akili yako ni kutojiingiza kwenye uhusiano mpya wa kimapenzi.

Katika maisha yangu ya ushauri nimekutana na watu wengi sana wakikiri kuambukizwa magonjwa ya zinaa walipokuwa wamelewa.
Nakushauri msomaji wangu kwamba, usikubaliane kabisa ulevi ukuingize kwenye masuala la kimapenzi. Acha starehe ya pombe pekee ikifurahishe, ukitaka vyote utaamka umefanya jambo la ajabu litakalokuhuzunisha maisha yako yote.

SIKU ZA UPWEKE
Nafahamu kuwa, harakati za kimaisha huwatengenisha wapenzi na kujikuta wakiwa wapweke kwa muda. Kipindi hiki kinaweza kuwa cha mwenza kwenda masomoni au safari ya kikazi. Ni kipindi cha kujaribiwa imani.

Jambo baya kabisa ni kuona, eti wapenzi waliotenganishwa na changamoto za kimaisha kujiona wapweke na kuamua kutafuta wachezaji wa nje wawasaidie kumaliza upweke.
Wapenzi wengi walijikuta kwenye majuto baada ya kujiingiza kwenye uhusiano na watu ambao kimsingi hawaendani nao ila kwa lengo moja tu la kuwaondolea upweke, matokeo yake kufumaniwa na jamii kuwashangaa kwa kutokuwa wavumilivu.

MSUKUMO WA MKUMBO
Ninaposema msukumo wa mkumbo namaanisha nyakati ambazo rafiki zako watakupitia kwenda disko, mkifika huko bila kupanga kila mtu anakuwa na wake, wewe unajikuta peke yako unalazimika kumkubali aliyebaki nawe kwa lengo la kuogopa kuonekana huna mtu wa kujirusha naye. Baadaye unajikuta kwenye majuto makubwa.


source globalpublishers