Unga Unawamaliza Wasanii wa Bongo Flava

Sunday, November 08, 2009 / Posted by ishak /


Muziki wa kizazi kipya Bongo Flava uko hatarini kutokana na kwamba mastaa wake wengi ambao wamewahi kutamba katika fani hiyo wanaanza kupotea mmoja mmoja baada ya kupata pesa na kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya.
Unga unaimeng’enya Bongo Flava
Mambo hayapo ok, Bongo Flava inazidi kumeng’enywa na nguvu kazi yake inapungua. Hapa ni gumzo kuwa vijana wengi wapo kwenye skendo ya kutumia dawa za kulevya.

Kuna maswali magumu; Kwanini baadhi ya wasanii wana-shine kidogo, wanakubalika kitaa na kiasi fulani maisha yao kuwa bora lakini ghafla tu madogo wanaonekana kitaa wamechoka na afya zimekuwa dhaifu.

Madai ya msingi ni matumizi ya dawa za kulevya a.k.a unga, kwamba madogo wengi wakishakubalika kitaa kwa njia moja au nyingine hujiingiza kwenye matumizi ya unga, wanabwia na wengine wanajidunga kabisa.

Its dangerous! The only gent on kundi marehemu la Wakilisha, Langa Kileo anaweza kuwa mfano hai, baada ya kukiri kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa iliyopita kuwa alikuwa anabwia unga lakini sasa amestop. Langa alisema kuwa alikuwa mbwiaji mzuri wa Cocktail kabla ya hivi karibuni kuugua typhoid, hivyo kukosa access ya kupata unga.

Alisema, alianza kama utani lakini baadaye alizidiwa na akawa hawezi kuacha, ingawa sasa hivi anamshukuru Mungu kwamba yamepita. Katika hilo, Langa alieleza kwamba angalau sasa anajisikia nafuu na afya imeanza kurejea. Hiyo ni kauli ya Langa kupitia session ya Crazy Friday, lakini ukweli ni kuwa madogo kibao wapo kwenye skendo ya kubwia.

Albert Mangwea ‘Ngwair’, Heri Samir ‘Blu’ Mark II B a.k.a Simba ni kati ya majina ambayo yanatajwa kwenye orodha ya wanaodaiwa kubwia unga. Hayo ni majina yanayotajwa lakini nyuma ya pazia ni wengi na hii inasababisha kizazi kipya kisiwe na afya standard. Madogo wanasimama vizuri lakini baadaye wanakuwa dhoofu l’hali. Hii ni hatari na sisi kama wadau tunalaani vikali matumizi ya dawa za kulevya.

source.nifahamishe

0 comments:

Post a Comment