Miaka 20 Jela Kwa Kumtikisa Mtoto Wake Mchanga

Friday, August 27, 2010 / Posted by ishak /

Mwanaume wa nchini Marekani ambaye alichoshwa na vilio vya mtoto wake mchanga na kuamua kumnyamazisha kwa kumtikisa kwa nguvu mtoto wake huyo na kupelekea kuharibika kwa ubongo wake, amehukumiwa kwenda jela miaka 20.
Gerardo Espinosa mhamiaji holela nchini Marekani toka Mexico, amehukumiwa kwenda jela miaka 20 baada ya kupatikana na hatia ya kuuharibu ubongo wa mtoto wake mchanga kwa kumtikisa kwa nguvu wakati alipokuwa akilia.

Mwendesha mashtaka aliiambia mahakama kuwa Espinosa mkazi wa Nevada hakutaka vilio vya mtoto wake mchanga wa kike viingilie uchezaji wake wa video game kwenye televisheni.

Ili kumnyamazisha mtoto wake, Espinosa ambaye ana umri wa miaka 19, alimtikisa kwa nguvu sana mtoto wake na kupelekea kuharibika kwa ubongo wake.

Kitendo cha Espinosa kilipelekea mtoto wake apate vilema vya maisha, akipoteza uwezo wa kuona na kusikia huku akitembea kwa tabu sana.

Akiongea wakati wa kutoa hukumu, jaji Patrick Flanagan alilaani kitendo cha Espinosa na kusema kuwa kama sheria zingeruhusu angemhukumu Espinosa kwenda jela maisha.

Espinosa alihukumiwa kwenda jela miaka 20 pamoja na kujitetea kuwa majeraha ya binti yake yalitokana na kuanguka chini kwa bahati mbaya.

Mtoto wake alikuwa na umri wa wiki 11 wakati tukio hilo lilipotokea.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment