Miaka 25 Jela Kwa Kuiba Chakula Kanisani

Friday, August 20, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani ambaye alihukumiwa kwenda jela miaka 25 baada ya kujaribu kuiba chakula kanisani, ametoka jela jana baada ya kutumikia miaka 13 jela.
Gregory Taylor, alijaribu kuganga njaa yake kwa kuzamia kwenye jiko la kanisa kwa nia ya kuiba chakula, kitendo chake hicho kiliyafanya maisha yake yaende mrama.

Taylor alikamatwa ndani ya jiko la kanisa na kufunguliwa mashtaka ya wizi ambapo alihukumiwa kwenda jela miaka 25.

Baada ya kutumikia miaka 13 jela, Taylor ameachiwa huru jana baada ya mahakama kuona kuwa adhabu aliyopewa ilikuwa kubwa sana kuliko kosa lenyewe.

Taylor alitupwa jela mwaka 1997 baada ya hakimu wa California kuitumia sheria inayosema kuwa mtuhumiwa anayekamatwa baada ya kufanya uhalifu mara tatu basi atupwe jela kuanzia miaka 25.

Kabla ya tukio la kujaribu kuiba chakula kanisani, Taylor alikuwa akikabiliwa na tuhuma za makosa mawili ya wizi, kosa la kwanza lilikuwa ni kumchomolea mtu pochi lake na kosa la pili lilikuwa ni kujaribu kumpora mtu mali zake.

Taylor alitoka kwenye jela ya wanaume ya mjini Los Angeles jana asubuhi na kulakiwa na ndugu na marafiki.

Taylor aliwaambia waandishi wa habari kuwa sasa amebadilika na anamshukuru mungu kwa kumpa chansi ya pili.

Alisema kuwa ana mpango wa kufanya kazi kwenye mgahawa wa kaka yake ili aweze kuwasaidia watu wengine wanaotafuta chansi ya pili katika maisha.


source nifahamishe

Afariki Baada ya Kulipukiwa na Simu ya Nokia

Thursday, August 19, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja nchini India amefariki dunia baada ya simu yake aina ya Nokia kumlipukia wakati akiwasiliana na mtu mwingine kwa kutumia simu hiyo.
Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Gopal Gujjar, mwenye umri wa miaka 23, alifariki dunia baada ya kupata majeraha makubwa shingoni, mabegani na masikioni.

Taarifa zinasema kuwa Gujjar mkazi wa jimbo la Rajasthan nchini India alikuwa akiwasiliana na mtu mwingine kwa kutumia simu yake aina ya Nokia wakati mlipuko mkubwa ulipotokea.

Mwili wake ulikutwa pembeni ya mabaki ya simu yake kwenye shamba lake lililopo kwenye kijiji cha Banda, limeripoti gazeti la The Times of India.

Polisi walithibitisha kupatikana kwa mabaki ya simu aina ya Nokia 1209 ya mwaka 2008.

Gazeti la The Times of India limesema kuwa tukio hili huenda likawa tukio la kwanza nchini humo kwa mtu kulipukiwa na simu ambayo haipo kwenye umeme ikichajiwa.

Mwezi januari mwaka huu, mwanamke mmoja nchini India mwenye umri wa miaka 27 alifariki dunia baada ya kulipukiwa na simu iliyotengenezwa China wakati akiongea huku akiichaji simu hiyo kwenye umeme.

Vifo vya watu kulipukiwa na simu vimekuwa vikiripotiwa mara nyingi nchini China, Korea Kusini na Nepal.

source nifahamishe

Amuuza Binti Yake Ili Apate Pesa za Pombe

Wednesday, August 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja nchini India, anashikiliwa na polisi baada ya kumuuza binti yake mwenye umri wa miaka sita ili aweze kupata pesa za kununulia pombe.
Mwanaume huyo chapombe mwenye umri wa miaka 40 aliyetajwa kwa jina la Krishnaiah, alimuuza binti yake mwenye umri wa miaka sita ili aweze kupata pesa za kununulia pombe.

kwa mujibu wa gazeti la The Times la India, Krishnaiah alikuwa na kiu ya pombe kali lakini alipoenda kwenye duka la jirani ambalo hununua pombe siku zote, alitolewa nduki kwakuwa alikuwa akidaiwa pesa na mwenye duka.

Ili aweze kukata kiu yake ya pombe, Krishnaiah aliamua kumuuza binti yake mtaani kwa bei ya kuanzia rupia 300 ambazo ni sawa na Tsh. 8000.

Hatimaye alifanikiwa kumuuza binti yake kwa rupia 1,000 ( Tsh. 28,000).

Polisi walipewa taarifa na walifanikiwa kumuokoa binti huyo aliyeuzwa na baba yake kabla ya mnunuzi hajatoweka naye.

Katika tukio hilo lililotokea katika jimbo la Kadapa, Krishnaiah alikamatwa na kutupwa rumande.

Mnunuzi wa binti yake alifanikiwa kukimbia kabla hajatiwa mikononi mwa polisi

source nifahamishe

Atakayemuonyesha Obama Matiti Yake Kulipwa Dola Milioni 1

Wednesday, August 18, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Bilionea mmoja wa nchini Marekani ameahidi kutoa zawadi ya dola milioni moja kwa mwanamke yoyote atakayejitokeza mbele ya rais wa Marekani, Barack Obama na kisha kumuonyesha matiti yake.
Bilionea Alki David ili kuitangaza tovuti yake ya "Battlecam" ameahidi donge nono la dola milioni 1 kwa mwanamke yoyote atakayekuwa wa kwanza kujitokeza mbele ya rais Obama na kisha kumuonyesha matiti yake huku akiwa amebandika lebo ya "Battlecam" kwenye kifua chake.

Sharti ya kushinda donge hilo nono ni kwamba tukio hilo lazima lionyeshwe LIVE kwenye tovuti ya Battlecam inayomilikiwa na bilionea huyo.

Awali bilionea huyo aliahidi kutoa zawadi ya dola laki moja lakini ameamua kuiongeza zawadi hiyo iwe dola milioni 1 baada ya watu kuona dola laki moja si donge nono.

"Watu wengi wanafikiria dola 100,000 hazitoshi kumfanya mtu azionyeshe sehemu zake nyeti kwenye hadhara, lakini dola milioni 1 ni pesa za kutosha kabisa", alisema bilionea Alki.

Alki alisema kwamba hadi sasa jumla ya watu 150 wameishajiandikisha kuwania zawadi hiyo.

Bilionea huyo alidai kuwa ameamua kumchagua Obama kwakuwa Obama ndiye kiongozi mkubwa wa dunia.

Bilionea Alki alizaliwa Lagos, Nigeria lakini anaishi Los Angeles, Marekani.

Ana nyumba tatu za kifahari nchini Uingereza na alitajwa kushika nafasi ya 45 katika listi ya matajiri waliopo Uingereza kwa mujibu wa gazeti la The Times la Uingereza.

source nifahamishe

Ajirusha Uchi Toka Ghorofa ya 11

Thursday, August 12, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Wakati China ikiendeleza kuombeleza vifo vya mamia ya watu kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo, mwanamke mmoja nchini humo amejaribu kujiua kwa kujirusha toka ghorofa ya 11 huku akiwa uchi wa mnyama.
Kufuatia mzozo na mumewe, mwanamke mmoja wa nchini China alijaribu kusitisha maisha yake kwa kujirusha toka ghorofa ya 11.

Katika tukio hilo lililotokea kwenye jimbo la Anhui nchini humo, mwanamke huyo alisababisha kizaazaa baada ya kuvua nguo zake zote na kupanda kwenye dirisha la nyumba iliyopo ghorofa ya 11 na kutishia kujiua kwa kujirusha chini.

Pamoja na jitihada za zimamoto na majirani kumsihi asijirushe, mwanamke huyo aliamua kujirusha ili kuhitimisha maisha yake.

Hata hivyo maisha ya mwanamke huyo yalinusurika baada ya kuangukia kwenye boya lililowekwa chini na zimamoto. Aliwahishwa hospitali kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Iligundulika kuwa sababu ya mwanamke kujaribu kujiua ni mzozo uliotokea usiku wa siku moja kabla ya tukio hilo.


source nifahamishe

Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500

Monday, August 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Msichana mmoja wa nchini Hungary ambaye aliinadi bikira yake kwenye mtandao ili apate pesa za kuisaidia familia yake, amepata mteja ambaye ameinunua bikira yake sawa na Tsh. Milioni 500.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19 anayejiita "Miss Spring" ameamua kuiuza bikira yake kwa mwanaume raia wa Uingereza ambaye atatoa paundi 200,000.

Msichana huyo alisema kuwa aliamua kuiuza bikira yake ili aweze kulipia gharama za masomo yake na pia aweze kulipa madeni ya mama yake.

"Familia yangu ina madeni na hatuwezi kuyalipa, mama yangu alikopa pesa ambazo alishindwa kuzilipa na kupelekea tupoteze nyumba yetu, nataka nilipe madeni yote", alisema msichana huyo.

"Pesa nilizopata sio nyingi sana kwani nitapoteza nusu yake kwenye kodi", aliongeza msichana huyo.

Msichana huyo alisema kuwa anajiandaa kwenda Uingereza ili aweze kumtunuku bikira yake mdau aliyetoa dau kubwa kuliko wote.

Mnada wa bikira ya msichana huyo ulianzia kwenye mtandao wa Ebay lakini ulimalizikia kwa njia ya email baada ya Ebay kuufutilia mbali mnada huo baada ya kugundua unahusisha uuzaji wa mapenzi.

"Nilikuwa nikiwasiliana na washindi wawili, mmoja raia wa Uingereza na mwingine raia wa Ireland, nimemchagua mwanaume wa Uingereza".

"Wote wanataka kunioa na kuitunza familia yangu lakini kwa sasa sifikirii kuishi maisha ya ndoa", alisema msichana huyo.

source nifahamishe

Nyota wa Uingereza Amhonga Kahaba Paundi 800 Kwa Usiku Mmoja

Monday, August 09, 2010 / Posted by ishak / comments (0)


Nyota wa Uingereza na timu ya Tottenham Hotspurs, Peter Crouch ameingia kwenye skendo kubwa sana baada ya kumsaliti mchumba wake na kumhonga kahaba paundi 800(Takribani Tsh. Milioni 1.8) kwa usiku mmoja.
Peter Crouch alikuwa kwenye vakesheni nchini Hispania pamoja na mchumba wake mwanamitindo, Abbey Clancy.

Siku mbili baada ya kumaliza vakesheni yake, Crouch alishindwa kujizuia kumsaliti mchumba wake kwa kununua penzi toka kwa kahaba mwenye umri wa miaka 19, anayejiita Monica Mint.

Crouch alimhonga kahaba huyo, paundi 800 ili afanye naye mapenzi mara mbili ndani ya usiku mmoja, mara moja kwenye taksi na baadae hotelini kwake.

Akitoboa siri ya tukio hilo, Monica aliliambia gazeti la News of the World la Uingereza kuwa Crouch hakujivunga hata kidogo kununua penzi lake kwa kiasi kikubwa cha pesa.

"Hakuhofia watu kutuona nyuma ya taksi, alisisitiza tufanye mapenzi ndani ya taksi wakati tukielekea hotelini", alisema Monica.

"Nilikuwa sijui kuwa ana mchumba, bado siamini amenunua penzi langu wakati ana mwanamke mrembo amemuacha nyumbani kwake", alimalizia kusema Monica.

source nifahamishe