Afungwa miaka 30 jela kesi ya wizi NBC Ubungo

Friday, January 15, 2010 / Posted by ishak /

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana iliwaachia huru washitakiwa tisa wa kesi ya kula njama na kuiba katika benki ya NBC Tawi la Ubungo,Dar es Salaam.

Mshitakiwa, Rashid Lembrisi, akihukumiwa kifungo cha miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya tuhuma hizo.

Walioachiwa huru ni Abdulrahman Dodo, Rahma Galos, Mashaka Mahengi, Philipo Mpoki, John Mdasha, Martine Mdasha, Jackson Sawangu, Lucas Aloyce na Ramadhan Abdulrahman.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na aliyekuwa Hakimu Mkuu Mkazi , Pelagia Khaday, ambaye hivi sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania.

Alitoa hukumu hiyo baada ya kupitia ushahidi wa pande zote mbili za mashitaka na utetezi ambapo alibainisha kuwa Lembrisi alionekana kuhusika zaidi na tuhuma hizo.

Wakili wa Upande wa Utetezi Magafu alimuomba Jaji huyo kumpunguzia adhabu mtuhumiwa huyo kwa madai kuwa ni kijana anayetegemewa na familia yake.

Jaji Khaday alisema, angetoa hukumu hiyo kwa kuzingatia aina ya kosa, uzito wa kosa na mazingira yake.

Watuhumiwa hao walikuwa wakidaiwa kuwa Februari 2, 2006 katika benki ya NBC tawi la Ubungo kwa pamoja walitumia silaha kuiba Sh milioni 168.5, dola za Kimarekani 16,128, na euro 50 mali ya benki hiyo.

source.habarileo.co.tz

0 comments:

Post a Comment