Kahaba Aishtaki Shule Yake Kwa Kumuachia Awe Kahaba

Friday, January 15, 2010 / Posted by ishak /


Mwanamke mmoja wa nchini Uholanzi ameifikisha kizimbani shule yake kwa kushindwa kumlinda asiangukie kwenye ukahaba.
Maria Mosterd ameifikisha mahakamani shule yake katika mji wa Zwole akiidai fidia kwa kushindwa kumlinda asiangukie kwenye ukahaba.

Maria mwenye umri wa miaka 20 ameandika kitabu kuhusiana na shughuli yake ya ukahaba akisema kuwa wafanyabiashara wa ukahaba walikuwa wakimchukua mbele ya shule na kwenda kumfanyisha ngono na wanaume kwa malipo.

Mama yake Lucie Mosterd alisema :"hali hii hutokea kwenye shule nyingi na hakuna mtu anayewajibishwa".

Mahakama katika mji wa Zwolle ilikataa kuikubali kesi hiyo ikisema kuwa shule yake ilijaribu kuwasiliana bila mafanikio na mama yake kuhusiana na mabadiliko ya tabia ya binti yake.

Mahakama iliiambia pia familia ya Maria kuwa wazazi ndio wenye majukumu ya kuwalinda watoto wao.

Familia ya Maria imesema itakata rufaa kuhusiana na maamuzi hayo ya mahakama.


source.nifahamishe

0 comments:

Post a Comment